Jumanne, 12 Novemba 2019

USIFANYE HARAKA KUFUNGUA HUDUMA, KUHAMA KANISANI AMA KUACHA KAZI NA KUFUNGUA BIASHARA.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu ninachoendelea naho cha: NAFASI YA VIUNGO VYA MWILI WA MWANADAMU KATIKA ULIMWENGU WA ROHO.

Na Malimu Oscar Samba:
12. Uwe na Subira, Saburi ni kitu muhimu sana, kuna wakati unakuwa katika vita vya kumiliki na kutawala lakini unakuta eneo unalotaka kumiliki au kuweka maskani yako bado hakuna nafasi, usiwe na haraka, wala usifanye haraka, endelea kuwa na uvumilivu, jambo la kuwekwa kwa adui chini ya miguu yako ni swala la mchakato, sio la siku moja, na swala la kukuwekea mazingira ya kuishi katika miliki yako kiroho iwe ni kihuduma, kiuchumi ama kiutumishi na kindoa na kadhalika linahitaji muda !

Jumatano, 30 Oktoba 2019

NGUVU YA KUWA NA UTULIVU MOYONI UNAPOKUWA KATIKA MAZINGIRA MAGUMU.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu cha Mungu yu Pamoja Nawe, pwenti ya nne, karibu: Na Mwalimu Oscar Samba.
4. Uwe na Utulivu Nafsini Mwako, kukosa utulivu maana yake ni kuwa na mahangaiko moyoni, ni kuwa na wasiwasi au mashaka, ni hali ya kujisumbukia au kuhaha.

Hali hii ni mlango wa dhambi, maana ni adui wa imani, humuondolea mtu uwezo wa kumtegemea Bwana, maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari liwezalo kupelekwa huku na kule na upepo !

Kukosa utulivu ni kukosa raha, ni kupungukiwa kwa kiasi kikubwa na amani, ambayo hiyo amani ni njia ya Mungu kuongea, maana maandiko husema kuwa na amani ya Kristo iamuwe mioyoni mwenu, kwa hiyo hayo mazingira humzuilia Mungu kuamua ndani yako, lakini pia amani ni njia ya Mungu kukuongoza, sasa ikipotea maana yake hutaiona njia, ndio maana dalili kubwa ya mtu aliyekosa utulivu na matokeo yake ni kuwa kama mtu aliyeko njia panda asiyejua njia ya kuiendea !

Jumatatu, 14 Oktoba 2019

HISTORIA YA WOKOVU, AMA SIMULIZI ya Uamsho wa MASAMA MUDIO. Sehemu ya 6, Zamani Enzi za Askofu Imanueli Lazaro

Utapatapia Unabii wa Askofu kuhusu kufa kwa zao la Kawaha, na Pigo kwa Uchumi wa wanaume na kuhamia kwa Wanawake.
.
Kulia ni Mwandishi wa Makala hii Mwalimu Oscar Samba akiwa na Msimulizi wetu Mch. Theofilo
Inasimuliwa na Mzee na Mchungaji Mstaafu wa TAG huko Masama, THEOFILO BARTOMAYO KIMARO, huyu ni pacha au ndugu na Mchungaji Wilsoni Kimaro.
Tuanze simulizi yetu; Niliokoka mwaka wa 1962 January na Mungu kuniita mwaka huo huo, niliunganika na kanisa huko Mbuguni, ambako kanisa nililikuwa halijaanza huko, (la wokovu) nilipokoka tukaanza kushuhudia nyumba kwa nyumba kama vijana.

Nakumbuka kuna mama mmoja kipindi hicho alishikwa na kansa, huyu mama sikuwahi kumuona kanisani maana alikuwa mgonjwa na alikuwa amekonda sana,

Jumatano, 2 Oktoba 2019

UJUZO WA HISTORIA YA UAMSHO WA MASAMA KAMA INAVYOSIMULIWA NA Afuraeli Munisi, Sehemu ya 5.

Anasema kuwa sio kwamba kanisa la TAG lilianzia hapa, lilikuwa limeshaanza huko Mbea hapa lilifika huo mwaka 1959, walianza kuokoka huko ni Askofu Lazaro na Jakobo Ringo ni mpare kutoka Same, walikutana na Askofu huko Arusha na mmeshenari Paulo Brutoni. ( Kama tulivyojionea hapo awali !)

Sikumbuki tarehe wala mwezi ila ni mwaka huo baada ya wao kuanza kushuhudia huko Arusha kidogo,hapo awali alikuwa ni mshirika wa KKT, na mama yake na baba yake pia, baba alikuwa ni mzee wa kanisa mtunza hazina wa hiyo dini, anaendelea kusimulia Mzee Munisi ! ( Ambae kwa sasa ni mzee wa miaka 83 na mke wake ni 72, aitwae Anarabi Afuraeli Munisi, ambao kwa kweli wamezeeka na mzee hapa huongea kwa utulivu maana pia sio buheri sana wa afya.)
Tunaendelea !


Walipokuja ndo walikuja

Jumamosi, 28 Septemba 2019

UWEKEZAJI WA ULIMWENGU WA ROHO KATIKA KIZAZI AU UZAO.

Yoshua 4:21 Akawaambia wana wa Israeli, akasema, Watoto wenu watakapowauliza baba zao katika siku zijazo, wakisema, Mawe haya maana yake ni nini?
22 Ndipo mtakapowaarifu watoto wenu mkisema, Israeli walivuka mto huu wa Yordani, kwa njia ya nchi kavu.
Mahali: Kanisa la TAG Mudio Masama, {Jerusalem Temple} Kilimanjaro, ndilo liiloasisiwa na Askofu Lazaro na kuwa kitovu cha Uamsho maeneo mengi Tanzania:
Tarehe: 27 na 28/9/2019. Na Mwalimu Oscar Samba.

Utangulizi:
Unapoona neno uwekezaji maana yake ni kunuia kupata faida, au kuna kitu kinapandwa, au kuwekwa, chenye nia ya kuzalisha ili kumpatia mwekezaji faida.
Katika uwekezaji kuna mwekezaji, eneo, kitu kinachowekezwa/bidhaa, na soko au walaji, na alikadhalika kiroho wawekezaji ambao ni aidha Mungu au adui Shetani, wote hawa eneo lao ni duniani wakinuia kumpata mwanadamu.

Ijumaa, 27 Septemba 2019

HISTORIA YA UAMSHO WA MASAMA ENZI ZA ASKOFU LAZARO, Ikisimuliwa na Jereremia Balitomayo Kimaro, mdogo wake na mchungaji Wilson Kimaro, Sehemu ya 4.

Ni watatu kutoka kwake.
Kushoto ni mwandishi wa makala hizi Oscar Samba akiwa na msimulizi wa sehemu hii ya nne Jeremia B. Kimaro wakiwa nyumbani kwake Mudio au Modia kama inavyotamkwa na wenyeji eneo la Masama.

Anasimulia; Tulikuwa wadogo ila kumbukumbu tunayo, miaka ya 1959 na 60 ndo uwokovu ulianza, Lazaro Askofu aliupatia kutoka Arusha, na kuja na kumkuta baba yetu (Bartolome Kimaro) ambaye alikuwa ni mdhaifu au mlemavu kidogo, na baba aliukubali, Walutheri ndio waliotufanyia fujo sana.

Wengine walipigwa mfano Mzee Lazaro na Sikustaili, pamoja na Mch Robert ambae aliwahi kupigwa chuma ya kichwani kwenye paji la uso.

Fujo ilipozidi sana walikimbia, anaendelea kusimulia mzee Jeremia, anasema kuwa mmishenari aitwae Pauli Brutoni nae alikimbia na kwenda kuita polisi !
Walipokuja mimi nilimpowenti mmoja na kusema ni huyu, walimchukuwa na kumpeleka magereza, akakaa huko kama miaka miwili, na alipokuja alisema lazima atanifanyia kitu na kuja kuniua !

Alhamisi, 26 Septemba 2019

Wajuwe Mashujaa waliochochea Uamsho wa Injili au Wokovu Masama Mudio, yupo Askofu Emanueli Lazaro, pia Rev. Au Mchungaji Wilson Kimaro, Sehemu ya 3.

Hawa ndi ambao wametajwa au kuwekwa katika mnara maalumu kanisani hapo, na makala nyingine zijazo au dodoso zijazo zitaendelea kuwaibua wengineo ikiwemo Wamisheni !


Eneo hili la modio Masama kipondi hicho cha mwaka 1959 kuanzia mwezi wa 12 kuna maajabu makubwa ya kiroho yalitokea, (kama sehemu zijazo zinenevyo,) na hawa ndio washirika na watendaji wa mwazoni kabisa.



1. Askofu Imanueli Kundandumi Mwasha( Askofu Lazaro.)
2. Mrs. Evagrace Imanueli.
3. Rev. Wilson B. Kimaro.
4. Firyandian Kundandumi.
5. Nkira Aranya Bartolomayo

Jumanne, 24 Septemba 2019

TUNAENDELEA NA HISTORIA NA DODOSO LA WOKOVU KIPINDI CHA ASKOFU LAZARO HUKU MUDIO MASAMA. Sehemu ya 2.


Kumbuka kuwa hili ndilo eneo ambalo ni chimbuko la wokovu kwa makanisa megi kanda ya Kaskazini na chazo cha uzalishaji wa matumishi wengi kama sehemu yetu ya tatu ishuhudiavyo kwa nchi Nzima !

Jumatatu, 23 Septemba 2019

Udodoso wa Historia na Ueneaji wa Kanisa la Tag na Wokovu kipindi cha Askofu Imanueli Lazaro Mwasha. Sehemu ya 1

Hili Ndilo Kanisa la Kwanza Kabisa kujengwa na Askofu Emanueli Lazaro, hapa Masama Moshi Kilimanjaro, mzee nilie nae hapa Philipo Mwasha anasema kuwa hapa kulikiwa ni Nyumbani kwa Babu yake na Askofu aliyeitwa Lazaro.

NIPO MASAMA MOSHI KWA ASKOFU LAZARO NADODOSA HISTORIA YA KANISA LA TAG

Nipo na Mzee Philipo Mwasha, ndugu wa ukoo au jamaa ya Askofu Emanueli Lazaro Mwasha, ananipa historia ya mambo ya kale, nipo Masama Moshi alipozaliwa Askofu, mengi zaidi utayapata www.ukombozigospel.blogspot.com

Jumamosi, 21 Septemba 2019

MSAADA KWA WALIOWAI KUMWAGA DAMU YAANI KUUA:


Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu changu cha SABABU ZA DAMU YA YESU KUWA NA NGUVU ILIYO NAYO.

Kama uliwai kuua mtu, kwa kukusudia au bila kudhamiria, kwa njia ya ajli, au kutumia silaha, kutoa mimba, ukiwa kama mama wa mtoto, baba, dakitari, au kushiriki kiushauri ama kiuwezeshaji ama kwa njia yoyote ile.

Pia hata kama ulihusika katika mauaji ya mtu au watu, kwa njia yoyote, ikiwemo ya ushauri, kupanga mipango, au unafahamu fika na bayana kuwa damu ya mtu fulani ipo juu yenu, au juu yako, au katika eneo unaloishi njia hii itafanyika msaada kwako au kwenu Lakini pia hata kama wewe ni asikari, au mwanajeshi, na uliwai kumwaga damu, haijalisha uliona ina hatia au la,

Jumamosi, 14 Septemba 2019

BARAKA ZA KWENYE NDOA, FAMILIA AU UZAO

5 Bwana akubariki toka Sayuni; Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;
6 Naam, ukawaone wana wa wanao. Amani ikae na Israeli.

Bwana Yesu Asifiwe Mpendwa, mimi kama kuhani wa Bwana ninawiwa kumimina baraka juu ya uzao wako, ndoa, au familia yako, na hata kama bado hujaoa na kuolewa maombi haya fahamu ni akiba, au baraka hizi ziwe akiba kwako.

Amani yake Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na familia yako, uwe na watoto wenye afya njema na weledi wa akili, uzao wako ukamjue Mungu wa kweli na kumtumikia kiukamilifu na kwa nia ya kumkubali !

Jumatano, 11 Septemba 2019

Msihi Mungu Akupe ama Akugundishe Akili na Maarifa

Andiko hili linatupa uhalali wa kumsihi Mungu akupe ama akufundishe akili, na maarifa !
Yamkini wewe ni mwanafunzi msihi akupe za darasani, ni mfanya biashara msihi akupe za kiuchumi, yamkini ni mtumishi Mtumishi muombe akupe za kihuduma alikadhalika kiongozi au mwanasiasa mtake akupe za kiuongozi kama ilivyokuwa kwa mfalme Sulmani, pia uongozi huo waweza kuwa ni wa kitumishi kama shemasi au kiongozi wa idara, uchungaji alikadhalika uaskofu !

Zaidi tunacho kitabu cha NAFASI YA AKILI KTK KUKUFANIKISHA AU KUKUUFAISHA KIMAISHA, au kile cha MOYO WA UFAHAMU. Pia tembelea, www.ukombozigospel.blogspot.com
#MwalimuOscarSamba
#mwalimu
#yaelewemaandiko
#tanzania

Jumamosi, 7 Septemba 2019

MWAMBA UTOWE MAJI KWA AJILI YAKO.

                     
Wana wa Israeli walipokuwa wakisafiri kule jangwani na kuelekea Kanani walipita katika hali ngumu sana kiasi cha kuishiwa au kukosa maji ya kunywa, ila Bwana aliwafanyia mujiza kwa kuwatokezea maji huko jangwani !
Aliupasua mwamba napo maji yakawabubujikia; Zaburi 105:41 Akaufunua mwamba, kukabubujika maji, Yakapita pakavuni kama mto.

Nawe najua unapitia mahali pagumu, wala sio haba, ila huyu Mungu aliyetenda kwa Wana wa Israeli ni ombi langu atende na kwako siku hii ya leo, akufanyia mujiza kutokana na haja ya moyo wako, akufanyie maji, akupe mana yaani chakula cha mbinguni, wewe amini tu na umwamini Bwana maana Yeye ni mwaminifu wala hasemi uongo, atakutokelezea tu !

Ni ombi langu kwa Bwana maji yakutiririkie siku hii ya leo !


Alhamisi, 5 Septemba 2019

YESU KAMA MTULIZA MAWIMBI AU DHORUBA.

                                                  Na Mwalimu Oscar Samba #UgMinistry  #SHARE  #SAMBAZA Ili kueneza injili hii.
Siku moja wanafunzi wa Yesu walikuwa wakisafiri majini ama ziwani na walilenga kufika nga’ambo ya ziwa ili kufanya jambo fulani, lakini walipokuwa katika safari yao, Punde si Punde bahari ili kumbwa na Mawimbi makubwa yaliyoambatana na Upepo mkali.

Hali hiyo iliwapa hofu kubwa mno, Lakini katika mazingira yote hayo hawakukubali kukwama safarini bali walimwamsha Yesu aliyekuwa akipiga usingizi, Hii ina maana kubwa sana na hapo mbeleni nitaifafanua.

Tuyadodose maandiko ili kujionea jambo hili kiunaga ubaga, Soma Marko 4:35-41.  Marko 4:35 Siku ile kulikuwa jioni, akawaambia, “Na tuvuke mpaka ng’ambo.” 37Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi ya kakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji. 38 Naye mwenyewe alikuwapo katika Shetri, amelala juu ya mto; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu sii kitu kwako kuwa tunaangamia?” 39 Akaamka, akaukeme upepo, akaiambia bahari, “Nyamaza utuliye!” Upepo ukakoma, kukawa shwari kuu.
Hapo ninapata funzo kubwa naamini nawe unapata jambo la kushangaza sana; ya kwamba mtu huyu tuliye naye sio wakufananishwa kwani anaweza kutuliza mambo yaliyoonekana kuwa ni magumu maishani mwetu na wewe sasa jenga imani hiyo na usisite kumuamsha ili atulize yanayokusonga. Ili na kwako kuwe, “SHWARI KUU”

Maandiko hayo yanatuonyeshe dhairi shairi kwamba YESU alikuwa na malaka juu ya mawimbi, na upepo, na ukitazama kiumakini utagundua kuwa mamlaka hii tulishapewa tangu enzi za umbaji wa ulimwengu Mungu alipowaambia Adamu na Hawa kuwa amewapa uwezo wa kutawala ndege wa angani, (Mamlaka dhidi ya Anga), Samaki wa Baharaini, (Ni Mamlaka juu ya bahari), Na Wanyama wote wa Nchi kavu, (Ikiwa ni mamlaka juu ya Aridhi) pamoja na hayo mamlaka hiyo inaambatana na vitu vilivyopo sehemu husika.

Kwa hiyo adui mkubwa aliyewafanya wasiweze kuitumia hiyo mamlaka ni kwanza ni Uelewa wao, hawakulijua hili, maana walikuwa na Yesu, ni kweli ila hawakujua kama anauwezo wa kutuliza hadi mawimbi na upepo, ndio maaana baada ya mujiza huo wanashangaa,
“.. Wakaambiana, ‘Ni nani huyu, hata upepo na bahari humtii? ” Mariko 4:41. Fikiri kwa kina kwamba wapo na Yesu miaka ya kutosha ila bado hawakufahamu mamlaka/uwezo aliyo nao, kuhusu tatizo walilokuwa nalo.

Na wewe yamkini umeokoka ila hujafahamu uwezo wa Yesu kuhusu dhoruba zinazokukumba, usimwamshe Yesu katika mtazamo wa wale wanafunzi walio mwamsha ili wateseke wote na Yesu katika kupamba na ile hali kwani hawakutarajia YESU kutenda lile, ndio maana walimwambia hivi,
“..Sii, kitu kwako kuwa tunaangamia,” Mariko 4:38.  Katika Luka walitumia maneno; Bwana mkubwa huku wakiita zaidi ya mara moja. Usipotazama andiko hilo kwa jicho la uchunguzi hutaiona hii fikra ya wanafunzi, ila iinajidhirisha pale wanaposhangaa uweza wake mara baada ya mujiza kutendeka hali inayobainisha bayana ya kwamba kumuasha kwao hakukuwa na taraja ya mujiza ule bali kulikwa na mtazamo wa “tupambane sote.”
Nataka kukujengea Imanii ili utambue ya kwamba hilo unalolipitia Yesu analiweza kwa shabaha ya kukataka kuacha kuwatazama wanadamu ambao hawatakusaidia badala yake wengine wataishia kukusema ama kukusengenya hali itakayokukwamisha kiroho kwani maneno hayo yanatakumiza bure badala yake unapaswa kumtaza YESU huku ukitambua ya kwamba ndani yake ipo Mamlaka na itumiye kama alivyokupa ili utulize hayo mawimbi na upepo kwani Yesu aliukemea na wewe kemia hiyo misukosuko kwenye ndoa yako, uchumi familia au huduma sasa.

Jambo la pili lilikuwa ni WOGA, ukiogopa ni dhairi kwamba Imani yako itayumba hali itakayokufanya kushindwa kuitambua ama kuitumia mamlaka uliyopewa na Yesu Kristo juu ya hayo matatizo.
Tuone mafundisho haya ya Uoga kwenye ujumbe huu kama nilivyokudokezea kwenye kitabu changu cha Namna ya Kuishi Wakati wa Majaribu au Mapito katika Ukurasa ule wa 31 na kuendelea.

“….Natumai sasa utakubaliana nami vyema pale Yesu alipokuwa na wanafunzi wake katika boti na mawimbi ya kaja wakaogopa Yesu aliwauliza “Imani yenu iko wapi” Luka 8:25. Akiwa anamaanisha kuwa wameogopa na hofu ilimdhirishia Yesu kuwa tatizo ni Imani, katika swala hili;Tutazame tena Mathayo 8:26 Akawaambia “mbona mmekuwa waoga, enyi wa Imani haba” Waoga alafu wa Imani Haba , haba maana yake chache,Kwenye luka anataka kujua walipo iweka imani yao, hapa anawaambia kuwa Imani mliyo nayo ni chache, Joshu anawaambia “wala msiwaogope”

Twende kwenye Marko tuone Mfano ama stori hiyo hiyo ya dhoruba ziwani. Marko 4:40 Akawambia , “mbona mmekuwa waoga? Hamna imani bado ?”. Hapa Yesu anauliza Uwoga pili hamna Imani bado jumlisha na hoja ya luka na Mathayo changanya na hiyo ya Marko (“Imani yenu iko wapi” + “mbona mmekuwa waoga, enyi wa Imani haba” na “mbona mmekuwa waoga? +Hamna imani bado ?”)
Kuna kitu nilikuaidia kukudokezea hapa mbeleni nacho ni hiki, Yesu alipokuwa amelala sio kwamba hakujua kitakachotokea, La! Asha!! Alijua fika, ila alikuwa akihitaji kuona au kupima ama kufahamu kiwango cha wanafunzi wake kumjua, pili Uwezo wao wakukabilina na matatizo na tatu kiwango cha Imani yao. Ndiposa alipoamka aling’aka hali iliyoonyesha kuwa amekasirshwa na matokeo ya mtihani uliowakumba.

Nakudhibitisha hilo tazama kwa kina maneno yake katika vitabu vyote vitatu, 1. Imani yenu iko wapi 2. enyi wa Imani haba 3. Hamna imani bado ?”).
Kwa anayetazama mambo kwa jicho la tatu kama mimi, kuna kitu anajifunza hapo, na miongoni mwacho ni hiki cha kiwango cha Imani na Sehemu ilipowekwa, hali inayomaanisha kuwa ukimya wa Yesu ulikiwa ukiashiria usimamamizi wa Mtihani.

Walioenda shule walao hadi chekechea wanafahamu kuwa sura ya Mwalimu wakati anafundisha ni tofauti na ile wakati akiwa anasimamia mtihani, na ujio wa sura ya wakati wa kutoa matokeo unategemea na ujibuji au ufaulu wako wa mtihani. Ukifeli utaona mikunjo ya ndita na hamaki ila ukifaulu utaona furaha na tabasamu mwanana, linaloambata na jicho angavu .

Jumatano, 4 Septemba 2019

MADHARA YA KUTUMIKA KAMA NABII WA UONGO:

Tunaendelea na mfululizo wa jumbe za kinabii, katika kitabu chengu cha Wito na huduma ya Nabii, na leo tunatazama;
MADHARA YA KUTUMIKA KAMA NABII WA UONGO: Na Mwalimu Oscar Samba

1. Kutupwa pamoja na bwana zao katika hukumu ya Moto wa Milele: Ufunuo 20:10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele.
Nakutaka kuwa mkini sana mtu wa Mungu, hakuna faida yoyote ya kumtumikia  Ibilisi, tofautina kutupwa kwenye Jehanum ya moto au katika ziwa lile la moto, kwa hiyo ni yangu rai kukutaka kuachana na hiyo nia, au kuepuka na  kuwa makini naa jambo hili, wala usijihesabie haki kuwa mimi siwezi, wewe jiepushe na muombe Mungu akupe kuepuka jambo hili, wengi waliongea vivyo, lakini kwa kukosa udhabiti wa moyo, leo hii wanamtumikia Ibilisi, na hawajui kuwa ipo Ole kwa ajili yao;
Yuda 1:11 Ole wao! Kwa sababu walikwenda katika njia ya Kaini, na kulifuata kosa la Balaamu pasipo kujizuia, kwa ajili ya ujira, nao wameangamia katika maasi ya Kora.
Petro anatuambia kuwa kama Mungu hakuwaacha malaika wale waliaoasi, hakika na hawa pia watapokea hukumu yao;
2 Petro 2:4 Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu.
12 Lakini hao kama wanyama wasio na akili, ambao walizaliwa kama wanyama tu wa kukamatwa na kupotezwa, wakikufuru katika mambo wasiyoyajua, wataangamizwa katika maangamizo yao.
Hakika wataangamizwa: Yeremia 14: 15 Basi, kwa hiyo Bwana asema hivi, Kwa habari za manabii wanaotabiri kwa jina langu, wala mimi sikuwatuma, lakini husema, Upanga na njaa havitaingia katika nchi hii; Kwa upanga na njaa manabii hao wataangamizwa. Pia Yeremia 29:31-31, Ezekieli 13, na Zekaria 13.

Jumatano, 28 Agosti 2019

MSAADA WA KUTOKA KWENYE KIFUNGO CHA MADENI.

Kunamtu ameniandiki hivi, "Mtumishi Bwana Yesu asifiwe mnaendeleaje ss wazima mtumishi nina Hitaji tuombe niwezekupata hela ya kulipa madeni kwani ni nadaiwa sijui napata wapi pesa."
Nami kumjibu hivi:

Hatua ya kwanza ni kuvunja roho ya utumwa kupitia madeni,Mithali 22:7 Tajiri humtawala maskini, Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye.
Pili, lipa hayo madeni rohoni kwa Damu ya Yesu, tatu ndo kuomba milango ya fedha ifunguke ili uyalipe mwilini, 4, omba nidhamu ya Mungu ili fedha hiyo ikija uwe mwaminifu kulipa nasio kufanyia mambo mengine ! 5. Tumia hekima y

Jumamosi, 24 Agosti 2019

MAMBO MUHIMU KATIKA UINJILISTI:

Bwana Yesu aifiwe Mpendwa, leo tunageukia kitabu changu cha Wito na Huduma ya Uinjilisti, na tunaangazia kipengele kimoja;
 MAMBO MUHIMU KATIKA UINJILISTI:
Na Mwalimu Oscar Samba, wa Ug Ministry.
Kumbuka mada hii inahusiana na utendaji, maana yake namna ya kufanya unapokuwa shambani, au namna ya kujindaa kwa ajili ya kuingia katika eneo la mavuno, wala hapa sineni habari za mfumo, au tabia za Mwinjilisti kama huko awali.

Mambo haya yatake sana kuyajua ili uwekeze nguvu kubwa hapo katika maandalizi, maombi na hata wakati unahubiri:
1. Watu Kumuamini Yesu, 2. Kumkiri, na 3. Kumpokea kama Bwana.
Warumi 10.9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

Jumatatu, 19 Agosti 2019

#JE_WAJUA_KUWA_UKIFA_HUJAOKOKA_UTAENDA_MOTONI?


Awali ya yote pokea salamu zangu, leo ninataka kukufikirisha tu walau kwa kiduchu, kuwa maisha unayoishi leo ndio yenye hatima ya maisha yako ya baadae.
Kulikuwa na tajiri mmoja na masikini mmoja jina lake Lazaro, tajiri huyu hakumjua wala kumcha Mungu, ila Lazaro alikuwa ni mtu mwema.

Ikatokea siku wote wakafa, njia ambayo mimi na wewe ni shariti tuipitie, Lazaro alienda Mbinguni, na tajiri motoni;
Luka 16:22 Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

Alhamisi, 1 Agosti 2019

NAMNA YA KUMJUA NABII WA KWELI NA WA UONGO.   Mwalimu Oscar Samba wa Ug Minisry.
Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu changu cha Wito na huduma ya Nabii,
(a) WA UONGO:
1. Tazama Misingi yao ya Kihuduma, Hawana msingi wa neno, Hofu ya Mungu haipo pamoja nao, mambo muhimu ya kiroho kama Ubatizo, Toba ya dhambi, Ujazo wa Roho Mtakatifu, Msisitizo wa kudumu katika imani ya kweli, msisitizo katika maombi ya kufunga na kuomba katika Roho na Kweli, au matumizi ya jina la Yesu hayatakuwa yakitumika kama ilivyo amriwa, na kamwe hawezi kuitumia Damu ya Yesu.
Kumbuka hata akijifanya kujitahidi kubatiza, hataweza kutumia utatu mtakatifu au maji mengi, na kuwafunza watu wake katika Roho kuhusu huo ubatizo.
Mambo hayo yatazame sana katika huduma ambayo unaitilia shaka.
2. Chunguza Matunda yao, Yesu alituhusia na kutufahamisha kuwa tutawatambua kwa matunda yao, akibainisha kuwa mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, alikadhalika mti mbaya huzaa yaliyo mabaya.
Mathayo 7:15 Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?

Alhamisi, 11 Julai 2019

Mtu moja kauliza Hivi ! Hivi wakisema sisi hatupo chini ya sheria tupo chini ya Neema nini maana yake hasa?

Nami nimemjbu kwa kifupi sana, na kwa kirefu kipo kitabu chetu kiitwacho, YESU KAMA KWELI NA NEEMA, Jibu:
Ni kuongozwa na Roho Mtakatifu; Wagalatia 5:23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa RohMtu moja kauliza Hivi !
Hivi wakisema sisi hatupo chini ya sheria tupo chini ya Neema nini maana yake hasa?

Nami nimemjbu kwa kifupi sana, na kwa kirefu kipo kitabu chetu kiitwacho, YESU KAMA KWELI NA NEEMA, Jibu:

📖 Ni kuongozwa na Roho Mtakatifu; Wagalatia 5:23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.

Kazi moja wapo ya sheria ni kukujulisha lipi baya na jema, sasa neema inakujulisha baya na jema, na kukuwezesha au na kukupa nguvu ya kuepukana na baya , ukisoma Warumi tano hadi nane utaelewa zaidi !

Laini penye Roho Mtakatifu, pana sheria ! Ila utofauti yake ni kwamba ni katika Roho, ndiposa huitwa sheria ya Roho wa Uzima, ikimaanisha kuwa kuna neema ndani yake; Warumi 8:2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.

Jumatano, 3 Julai 2019

MUNGU ANAPOKAA KIMYA, WEWE FANYA YA FUATAYO, AMA TENDA HIVI:

Na Mwalimu Oscar Samba:

Wasomaji wa Biblia wanafahamu kuwa yapo maombi kadha wa kadha ambayo hayakuwahi kujibiwa, na mengine yalijibiwa lakini yalichukuwa muda mrefu tofauti na mtazamo wa wa husika ila Mungu alikuja kuyajibu.

Ibrahimu na mkewe ni kielelezo kikubwa katika hili, kwa hiyo, ikupe kufahamu kuwa wewe sio wa kwanza, sio hapo tu lakini twafahamu katika sura ya kutokujibiwa yapo hata maombi ya Yesu ambayo hayakujibiwa !
Alihitaji kikombe kimuepuke, na Mungu Baba kugoma kuyajibu ! Hadi alipobadili maombi, Musa na Yeremia nao wana orodha ya maombi ambayo hayakujibiwa !

Walijitetea kadri walivyoweza ili wasitumike lakini Mungu hakuzingatia hoja zao ! Kuna ndugu wa wiwili kipindi cha Yesu ambao ni wanafunzi wake, waliomba kuketi mkono wa kuume katika Ufalme wa Mbinguni ila maombi yao yalisogezwa

JINASUWE KWENYE ROHO AU VIFUNGO VYA KURITHI, FAMILIA, KABILA NA UKOO.

Ujumbe huu ni matokeo ya kiu ya kijana fulani anayesoma kidato cha Sita kunitaka nimfundishe maana amekuwa akisumbuliwa na mkuu wao wa ukoo ambaye humtokea na kumtangazia kumkwamisha kimasomo, japo yeye hamjui maana ni wa miaka mingi, ila hujitambulisha hivyo, na amekuwa akipitia wakati mgumu kitaaluma, hata kugubikwa na usingizi mzito mwalimu aingiapo darasani na kadhalika !
Pia ni nimeelezea jambo hili kiupana sio kitaaluma tu, natumai litakusaidia namna ya kujinasua kindoa, kiuchumi, na hata kimaisha, unapojiona umeokoka ila maisha yako yamekwama kama ndugu zako, una ugonjwa ambao husumbua jamii zako, unatatizo la kindoa kama nduguzo, unakataliwa na ndugu, huna kibali kwao, uwe na hakika hizi roho zipo kazini.

Jumamosi, 29 Juni 2019

MNGOJE BWANA KAMA MKULIMA ANGOJAVYO MAVUNO


Na Mwalimu Oscar Samba:
Kwenye pwenti ya kumngoja Bwana kwa Saburi; Mpendwa Mwenzangu katika Bwana ! Mwenye kungoja kwa Saburi huwa na taraja, ndani yake mna imani dhabiti, hana mashaka wala manongono, ni kama vile mkulima angojavyo mazao !
     ðŸ“œHana haraka, ana hakika yaja majira ya mavuno, kwanza hulikwatua ama huliandaa shamba hata kabla ya mvua kunyesha, hutia mbegu chini majira ya mvua ya kupandia, wakati wa palizi hana haraka ya kuvuna bali hufanya palizi, huwekea mbolea na kuyalinda dhidi ya wadudu, kisha huja wakati wa kuchanua, napo hana haraka, anajua kuna majira ya ngano au suke, ama mahindi yake kukomaa; Marko 4:26 Akasema, Ufalme wa Mungu, mfano wake ni kama mtu aliyemwaga mbegu juu ya nchi;

27 akawa akilala na kuondoka, usiku na mchana, nayo mbegu ikamea na kukua, asivyojua yeye.
28 Maana nchi huzaa yenyewe; kwanza jani, tena suke, kisha ngano pevu katika suke.
29 Hata matunda yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika.
Aina hii ya uvumilivu, ndio tunaotakiwa kuwa nao, ili kutuwezesha kuyafikilia mema yetu, mwisho wa maandiko nikupayo kuna onyo kuhusu manongono ! Hii ikupe kuwa makini na mwenendo huu, wenye ishara ya kukosa au kupungukiwa saburi, (Zakaria alimngoja Bwana kweli, ila kuna namna Saburi ilipungua ! Ni kweli ilikwepo

Alhamisi, 13 Juni 2019

Muongozo wa Maombi ya Kuombea aridhi

Ni ujumbe niliomtumia mtu kama "sms"

Mngoje Bwana


Mngoje Bwana, Jipe moyo, Usife Moyo
"Yeye aliyeahidi ni mwaminifu", kwa hiyo; hiyo ni sababu moja kubwa muhimu sana inayokupasa kumngoja !
Unajua mwanadamu haaminiki kwa asilimia zote, huweza kukwambia ningoje hapa, nisubirie hapa, na kisha asije kutokea, au akakwambia nilikwama, nilipitiwa, ila sio Mungu wetu, huyu Mungu ni mwaminifu, ni wa dhati na kweli.

Kuna heri, au ipo baraka kwa wanaomngoja Bwana ! Mithali 8:34 Ana heri mtu yule anisikilizaye, Akisubiri sikuzote malangoni pangu, Akingoja penye vizingiti vya milango yangu.
Hasemi siku moja, mbili, au tatu ! Hasemi mwezi mmoja, wala miaka miwili, bali husema siku zote !

Hili ni jibu kwa wenye swali la ningoje hadi lini ? Na kufuatiwa na maelezo kama kungoja kwa kweli nimengoja sana, nimesubiri sana, ila sijibiwi ! Ni hadi haki yako ichomoze kama mwangaza, na kufanywa sifa, na unapaswa kufanya hivyo siku zote, na ungoje kwenye vizingiti vya milango yake !

Jifunze Kuongeza au Ombea Imani yako ya Kupokelea Majibu

Aina za Imani katika Kuomba, na Mwalimu Oscar Samba
 ( Unapohisi imepungua, au itapungua, ingia kwenye maombi maalumu, ) awali ya yote nikufunze kuhusi imani ya kuomba, au aina ya imani ambayo hukusukuma au hukuwezesha kufanya maombi; Marko 11:23 Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake.
Wakati unaomba, unatakiwa kutokuwa na shaka, na uamini kile unachokihitaji, au kukiamrisha kiwe, kitakuwa, ama itakuwa kama vile ulivyokusudia au kunuia moyoni mwako. Ukisema ugonjwa huu toka, pona, uwe na hakika unachokihitaji kitakuwa, na ugonjwa utatoka. ( Hii ni imani inayotumika muda wa kuomba.)

Sasa ukishaomba, inakuja imani au inatakiwa iwepo imani ya kupokelea majibu, nikiwa na maana kwamba yale uyaombayo, au uliyokwisha kuyaomba, unatakiwa kuamini kuwa yamekwisha kuwa yako, pia imani hii itakusaidia kuendelea kushikilia wingu la maombi, na kukusaidia mara kwa mara kurejea katika imani ya kuomba, na kukuwezesha kuomba bila kukoma, ikiwa ni sehemu ya uhusiano uliopo kati ya aina ya kwanza na ya pili, na fahamu ya pili haiwezi kuja bila ya kwanza kufanya kazi yake.

Na sababu kubwa

Jumatatu, 10 Juni 2019

Upako ni Kulipa Gharama

Nimeandika hivi, katika kitabu chetu cha NGUVU YA KUOMBA BILA KUKOMA !
Najifunza kitu kisichochepesi kwa Elisha ! Natumai unajiuliza ni kipi tena hicho Mwalimu ! Ni hiki ! Elisha alikuwa na msimamo sana, maana Elia licha ya kumpa upinzani mzito ili kuuhakikisha moyo wake kama kweli umekusudia, kuna mthihani mwingine alimpa mara baada ya kuomba ombi lile !
2 Wafalme 2:10 Akasema, Umeomba neno gumu; lakini, ukiniona nitakapoondolewa kwako, utalipata; la hukuniona, hulipati.
Ni baada ya kuomba upako mara dufu, sasa Elia anampa shariti, kuwa akimuona saa anaondoka, atapokea, la hakumuona, hatapokea !
Huu ulikuwa ni mtihani muhimu sana, na kwa

Endelea Kumkumbusha Mungu, Kamwe Usiwe Kimya, Kaza Kuomba Bila Kukoma !

Kukaa kwako kimya kutamfanya Mungu nae kunyamaza, ila kuendelea kumzongazonga kwa maombi yako na sadaka ndiko kutakakomfanya kutokutulia, na kisha kukupatia majibu yako upesi !

Amejiaidia mwenye hapa ! Isaya 62:1 Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia, hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo.
:2 Na mataifa wataiona haki yako, na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha Bwana.

Daudi anatuambia kuwa katika taabu yake alimlilia Bwana, kisha naye akasikia kilio chake ! Sijui wewe katika taabu yako huwa unafanyaje ?

Alhamisi, 6 Juni 2019

Muhesabu Mungu kuwa ni Mwaminifu, ni katika kitabu cha NGUVU YA KUOMBA BILA KUKOMA.

Muhesabu Mungu kuwa ni Mwaminifu, ni katika kitabu cha NGUVU YA KUOMBA BILA KUKOMA.
Kwa hiyo, Mungu akikuaidia ni hakika atalifanya hilo kuwa jema, jambo muhimu kwako ni kumuhesabu kuwa ni mwaminifu, ukijuwa vyema kazi aliyoianza ni lazima ataimaliza tu ! Wafilipi 1:6 Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu.Kama amekupa mke au mume, uwe na hakika na mwana atakupa ! Kama ameweza kukupatia biashara, uwe na hakika na swala la wateja atalimaliza. Kama ameweza kukuleta ulimwenguni, basi na uponyaji ni haki yako.

Yamkini umeliombea jambo hilo kwa muda sasa, na imefika mahali limegeuka na kuwa jaribu ! Nikimaanisha sio hitaji la kawaida, maana limeanza kukuweka njia panda na kukufanya uanze kufikiri kwa upya kuhusu uhusiano wako na Mungu, au kuhusu uendelee kumngoja Bwana kwa saburi au umngoje katika hali ambayo akitenda sawa na asipotenda pia ni sawa, ili mradi wewe unachojua ukitwaliwa leo ni mbinguni mengine hutaki tena kuyajua !

Jumanne, 4 Juni 2019

Yajuwe Majina ya Mungu na Maana Zake, mfano Adonai maana yake ni Mungu mwenye Enzi, Mwanzo 15:2-3, Eli-Shadai ni Mungu Utoshalezae, Mungu Mwenyezi, Eli-Gibo, ni Mungu Mwenye Nguvu


Usiogope Adui MTAZAME MUNGU, NA TENDA KWA AKILI . Na Mwalimu Oscar Samba.


Zaburi 56:4
Aliinuka Sauli mfalme enzi za Biblia na kujaribu kupigana na shauri la Bwana akimuwinda Daudi aliyekuwa mfalme mtarajiwa kila kona lakini mwisho wake alijikuta akiishilia kwa mganga wa kienyeji na hatimae shauri la Bwana kushinda ndani ya Daudi !
Yamkini huyo anayepigana nawe hana hata cheo cha ubalozi wa nyumba kumi, na uwenda hakuwahi kuwa hata kiranja alipokuwa shule !

Sasa kwa nini uogope ! Ni kwa nini ukubali kutishwa na mwenye mwili wakati yupo awezae kuuzima kwa dakika ama sekunde moja na hata nusu sekunde !

Enzi za wakina Petro ama kanisa la kwanza aliinuka mtu mkoja aliyeitwa Herode, na kujipiga kifua mbele za Mungu wetu ila mwisho wake aliishilia kutafunwa na mdudu hadi kufa !
Farao alijifanya kupigana na taifa teule na mwisho wak

Jumatatu, 3 Juni 2019

Mtumaini Bwana Bila Wasiwasi !

Zaburi 26:1.
Na Mwalimu Oscar Samba.       Najua kuna mambo mengi kadha wa kadha umeyaombea ila bado hujaona majibu yake ! Yangu rai ni kukusihi kuwa Bwana yu malangoni, na ana heri yule amngojae hapo, ikiwa na maana kuwa amebarikiwa aliyeweka tumaini lake kwa Bwana.

Ni muhimu sana kufahamu sana kuwa imetupasa kumuomba Mungu bila kukata tamaa, hii iwe ndio dira yetu peke maana Mungu hujibu kwa wakati wake, na inatupasa kumuomba siku zote bila kuvunjika moyo, maana sisi wenye kumkumbusha Bwana twaambiwa tusiwe na kimya, anasema ameweka walinzi juu ya kuta zako, ambao hawatanyamaza usiku wala mchana , walinzi mpendwa ni aina ya waombaji !

Kwa hiyo Bwana amekusimamishia watu

Jumapili, 2 Juni 2019

HAWA NI WATU WALIOMDHIHAKI MUNGU NA KUPATWA NA SHIDA


1. JOHN LENNON (MUIMBAJI)
Wakati alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa habari wa gazeti la American alinukuliwa akisema hivi "Ukristo utakufa na kutoweka duniani, siwezi kuwa na wasiwasi na hilo kwa kuwa nina uhakika nalo. Mafundisho ya Yesu yalikuwa sahihi na wala sipingi hilo ila mafundisho yale yalikuwa mepesi sana ambayo mtu yeyote anaweza kuyafundisha. Hebu angalia leo, tumekuwa maarufu hata zaidi yake (Hapo alilitaja kundi lake la The Bettle). Ilikuwa mwaka 1966. Wiki moja baada ya kutamba kwamba yeye na kundi lake lilikuwa maarufu hata zaidi ya Yesu, akapigwa risasi sita na kufariki.
2. TANCREDO NEVES (RAIS WA BRAZIL)

Jumatano, 29 Mei 2019

Usifadhaike, Mungu anajua Unayohotaji.


Mathayo 6:8.
Nami nakuhakikishia kuwa ni Kweli na dhairi kuwa Mungu anajua unayoyahitaji, kwa hiyo huna sababu ya kufadhaika, kukata tamaa, kuhuzunika wala kujawa na wasiwasi, maana Mungu anajua unayoyahitaji, usijisumbukie, wala kupoteza muda mwingi kwa kuwazia adha uliyo nayo, Mungu anajua unayoyahitaji, hii ndio kauli yangu na ya dhati itokayo moyoni mwa Mungu wangu, maana andiko hilo, la dhibitisha hili !
Huna sababu ya kukosa usingizi, kushindwa kula, wala kukosa amani kisa una ukata, au ukwasi

Jumanne, 28 Mei 2019

WAPOLE WATAIRITHI NCHI.( Upole, Unyenyekevu kama Silaha ya Kivita.)

Na Mwalimu Oscar Samba


 WAPOLE WATAIRITHI NCHI.( Upole, Unyenyekevu kama Silaha ya Kivita.)
Ijumbe huu utaupata katika kitabu chetu cha #TEKATAWALANAUMILIKI
. Fahamu: Wapole Watairithi Nchi; Upole ama Unyenyekevu ni miongoni mwa silaha muhimu sana ya kivita, (fahamu sana kuwa upole unaotajwa kwenye maandiko sio wenye maana ya ule unaokuwa rathi kupokonywa haki yako, au kukosa ujasiri wa kujitetea, ama uzubaifu, la ! Ni upole kama tunda la Roho au kama tabia ya Rohoni, maana hata Yesu aliwahi kupinduapindua meza, kuvuruga gulio pale hekaluni akiitetea kweli ya Mungu, lakini bado alikuwa mpole, aliwahi pia kuwaambia nendeni kamwambie yule mbweha, akimlenga Herode aliyekuwa mtawala, pia aliwahi kumkaripia Petro vikali akimwambia rudi nyuma yangu Shetani, na kadhalika ila bado alikuwa mpole, twajifunza pia kwa Musa, alikuwa mpole lakini ifikapo swala la uhusiano na Mungu wake kuna namna upole ule haukuwa kikwazo maana ulikuwa ni tunda la Roho na sio hulika ya kawaida ya kibinadamu, au ule upole ambao ni matokeo ya "slow mindi" ama ufahamu uliopumbazika.
Mathayo 5:5

Alhamisi, 2 Mei 2019

SI MAPENZI YA MUNGU TUWE MASIKINI Na Mwalimu CHRISTOPHER MWAKASEGE


Utangulizi: (Namna ya mkristo kuishi katika hali ngumu ya uchumi bila kumkosea Mungu).
      Kati ya mambo yaliyotabiriwa kutokea katika siku hizi za mwisho ni dhiki katika mataifa, pamoja na hali ngumu ya uchumi. Soma mwenyewe katika Luka 21:25-26 na Ufunuo wa Yohana 6:5-6.

Pia, tunasoma kutoka katika biblia ya kuwa biashara na uweza wa kuuza na kununua utafuata mfumo fulani uliojaa dhuluma, ambao utatawaliwa na kundi fulani ulimwenguni. Watu hawatauza wala kununua bila ya kupatana na watu wa kundi hilo, na hasa kiongozi wao. Na asomaye na afahamu. Soma kitabu cha Ufunuo wa Yohana sura yote ya 13.
Si hivyo tu, bali biblia inaeleza wazi kabisa kuwa katika siku hizi za mwisho kutakuwa na uhusiano mkubwa sana kati ya utajiri na uasherati na pia kati ya biashara na uasherati. Soma kitabu cha Ufunuo wa Yohana sura za 17 na 18. Lakini pia unaweza kuwa na utajiri na ukafanya biashara bila kujihusisha na uasherati na mambo mengine yaliyo kinyume na maadili ya Mungu.

Muimbaji Faustin Munishi na Kilio cha Kushuka kwa au Kupoa kwa Moto wa Uinjilisti leo

Pichani NI MAKAMANDA WA YESU WALIOITIKISA TZ KWA INJILI.
  Ev Daudi Kuselya | Ev Emmanuel Lazaro | Ev Moses Kulola.

Ameyaeleza katika Mtandao wake wa kijamii wa Face book, unishi Muimbaji ameyasema haya ambayo kwangu leo ni changamoto, "NAKUMBUKA TULIKUWA DODOMA MWAKA 1982 KWENYE MKUTANO WA INJILI KANISA LA TAG LILILOKUWA LINAONGOZWA NA MCHUNGAJI MHINA

KABLA YA MKUTANO JIONI, NILIMWOMBA ASKOFU MOSES KULOLA WAKATI HUO MWINJILISTI WA TAIFA TAG TWENDE STUDIO TUCHUKULIWE PICHA HII.

Kushoto ni Mimi Mtumishi Faustin Munishi, Katikati ni Askofu Moses Kulola na kulia ni Aliyekuwa msaidizi wa Mwinjilisti Kulola wakati huo Mwinjilisti Emmanuel Mwasota Ambaye sasa ana Kanisa Dar.

Tulikuwa na ratiba iliyojaa kuzunguka Tanzania yote tukihubiri Injili.

Jumamosi, 27 Aprili 2019

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA.

Mahali: TAG Ushiri Rombo: Tarehe 28:2:2019. Na Mwalimu Oscar Samba.
Aliyeshika kipaza sauti (kushoto) ni mama mchungaji wa kania hili jia ni Paumelina B. Senkondo, na wengineo ni wanawake wakiimba shairi.

Mwalimu Oscar Samba

Washirika

Mwanzo 2:18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
Mwanamke ni msaidizi, andiko hilo lipo kabla ya dhambi kuingia ulimwenguni, hakukuwa na mfumo wa kanisa ama kuabudu kama leo, au kama baada ya dhambi, kusudio la ndoa, au familia ni ili liwe kanisa, yaani tuliumbwa kwa ajili ya ibada !
Kwa hiyo, kanisa, lina mukutadha wa ndoa, kwa hiyo, dhima ya mwanamke kindoa au kifamilia, ina mashabihiano na ile ya kikanisa !

Waefeso 5:23 Kwa maana

Jipatie maandiko mbali mbali ya Biblia kuhusu Damu ya Yesu, Shukurani, Ahadi za Mungu na kadhalika




KUNA MTU MMOJA MWENYE KESI AMENIOMBA NIMFUNZE NAMNA YA KUOMBA, NAMI NAKUMEGEA:

1. Omba Rehema, tubu bila kujihesabia haki, tumia Danieli 9, pia Warumi 3:25 ukiitaka Damu ya Yesu ifanye rehema, na Mathayo 26:28 kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.

2. Ifute hiyo Kesi kwa Damu ya Yesu, Waebr 9:22, futa hizo nakala/kopy za kesi ama mashitaka.

3. Gongomelea hzo hati za Mashitaka Msalabani, Wakolosai 2:14 akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;

Upole wako na ujulikane na kila mtu !

Bwana Yesu asifiwe,
Kuna Mtu aliniambia niseme Neno, nami nilisema ! Sasa nakumegea nilichomfunza !

    Upole ni Tunda la Roho, ambalo linadhima ya unyenyekevu ndani yake.

  Kazi na faida moja wapo ya upole ni kukupa majibu ya busara hata katika nyakati ngumu, haijalishi ni zenye kuuthi au kujeruhi, utajifunza kwa Yesu, na Yeremia pia, ila ona hapa;Mithali 15:1 Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.

Upole unakuwezesha kuepukana na mitego ya adui, inauonuia kukuyumbisha, ama kukukwamisha, au kukuvurugia masiha, maana upole umebeba unyenyekevu ndani yake ! Yeremia 11:19 Lakini mimi nalikuwa kama mwana-kondoo mpole, achukuliwaye kwenda kuchinjwa; wala sikujua ya kuwa wamefanya mashauri kinyume changu, wakisema, Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake, na tumkatilie mbali atoke katika nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.
Upole huu ndio uliomvusha Yesu ! Isaya 53:7 Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake.

Kuna wakati adui ananuia kabisa kukukwamisha mahali kwa kuibua changamoto, ama vikwazo, ila ukiwa nao huo upole, utanyamaza kimywa na adui anakosa mwanya wa kukudhuru au kukuangamiza !
Sasa sababu ya maandiko kututaka upole wetu ujulikane na kila mtu ni ili kuwa na maisha ambayo Tunda hili litakuwa active au hai, ili kutuwezesha kunufaika nalo, usisahau kuwa anamalizia nakusema Bwan yu karibu, ikiwa na maana kuwa unapokaribia mafanikio kama Yesu, au kukutana na majibu yako, adui haachi kuleta vikwazo, iwe kwa ndugu, marafiki, muajiri wako, wafanyakazi wenzako,walezi na kadhalika akinui kukuzuilia kukutana na Bwana, sasa upole utakuvusha kama Yesu na Yeremia ! Ona haya maandiko :
Anaanza na kututaka tufurai, akiwa na maana upole umebeba ama hukuwezesha kufurahi, maana mazingira ya huzuni, na uchungu hayawezi kuzaliwa penye upole ! Alafu amani huyoke, kumbuja amani pia ni Tunda la Roho !, pamoja na Furaha ! Sasa ukipata upole, hayo mengine ni rahisi sana kuchipuza !
Wafilipi 4:4 Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
:5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.

Katika somo hilo, tuna au una jigunza nini hapo ?

Natumai somo kuu, ni kwamba ukiwa mahali pagumu, huna majibu ya maswali yako, mazingira yanakuzalia ama hukutishia kukuzalia huzuni, au kukunyima amani, na furaha, masononeko na ukiwa zinakunyemelea! Basi upole ni dawa ! Ambapo utazaa Amani, na Furaha ! By Mwalimu Oscar Samba. Simu: +255759859287

NAMNA YA KUOMBEA ENEO, JAMII AU MTU FULANI.

Chimbuko la ujumbe huu ni kiu ya Mwanafunzi wangu mmoja aliyeniuliza maswali kadhaa majira haya, nami kumjibu, nami pia kupokea imizo la ndani yangu, kukumegea ama kukudodoselea majibu hayo, ila kwanza tazama kiu yake;
"Bwana Yesu Asifiwe Pastor
Kheri ya Pasaka.

Naomba mwongozo
Kama mtu unaguswa kuomba kwa ajili ya kumuombea au kuombea
1. Mtu binafsi analiyetakwa na nguvu za giza na yeye peke yake hawezi kujikomboa hatua zipi unapitia  ( Yaani mwongozo wa maombi kwa mtu huyu inakuwaje)

2. Kama unataka kuomba kwa ajili ya familia ulikozaliwa kwa ajili ya kuwakomboa uzao wa tumbo la mama yako ili Mungu aingilie kati unaendaj

Alhamisi, 28 Februari 2019

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Mahali: TAG Ushiri Rombo: Tarehe 28:2:2019. Na Mwalimu Oscar Samba.
 KANISA.

Mwanzo 2:18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.

  1. Mwanamke ni msaidizi, andiko hilo lipo kabla ya dhambi kuingia ulimwenguni, hakukuwa na mfumo wa kanisa ama kuabudu kama leo, au kama baada ya dhambi, kusudio la ndoa, au familia ni ili liwe kanisa, yaani tuliumbwa kwa ajili ya ibada !


Kwa hiyo, kanisa, lina mukutadha wa ndoa, kwa hiyo, dhima ya mwanamke kindoa au kifamilia, ina mashabihiano na ile ya kikanisa !

Waefeso 5:23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.
24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.

Kama ndivyo, mwanamke ameumbiwa kulichukulia kanisa kama anavyomchukulia mumewe, utendaji wa usaidizi kwa mume, ama kumuheshimu, uwe vivyo hivyo kwa kanisa, maana Kristo u kichwa huku.
Kumbuka hili Daima: Kuwa ni yule amchaye Mungu ndie asifiwaye: Mithali 31:30 Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa.

Jambo hili, likupe kuhakikisha una sifa ya uchaji, kama kweli unadhamiria kusifiwa na Kristo ambaye ndie kanisa, na hakika ukijipatia kibali au sifa njema kutoka kwa Bwana Yesu, ni umejipatia kutoka kwa kila mtu, jifunze kwa wakina Debora,Dorkasi, na wengine akiwemo yule Mariamu aliyempaka yale mafuta, hadi leo tukio hilo lingali likikumbukwa, sasa utafahamu kuwa utendaji wao mwema uliotokana na uchaji ndio uliopeleke kujizolea sifa hizo.

Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili ! Kwa hiyo ni hatari mno kujisifia vya mwilini, ila sifa zitokane na uchaji, ambao huzaa kazi njema !
MAJUKUMU YAKE KATIKA NAFASI KWENYE KANISA:

1.  Ni Mueneza Habari Njema, sifa njema kuhusu Mchungaji wake, kanisa lake, huduma ya kanisani, watumishi wa kanisani, na kila wasifu mzuri kulihusu.

Ni jukumu lake pia kumuelezea Kristo Yesu kwa wasio mjua, huyu ni mjumbe mzuri sana, maana mwanamke amepewa kinywa chenye uwezo wa kuzalisha maneno mengi, adui amekuwa akiwahi hili na kulitumia vibaya kwa umbea na misuto, ukizingatia pia amepewa uwezo wa kutoka mji huu ama nyumba hii na kwenda kwa ile, nia ni ili aeneze mema, ila adui amewatumia vibaya.

Mfano wa dhima hii kibiblia ni mwanamke yuke wa kisima cha Yakobo Msamaria: ( Yoh 4:7-42.)

Alipofahamu uzuri wa Yesu, moja kwa moja aliacha mtungi wake na kwenda kueneza wema wake!

Yohana 4:28 Basi yule mwanamke akauacha mtungi wake, akaenda zake mjini, akawaambia watu.

Kuna wakina mama au mabinti unakuta anafua nguo,au kukatakata kitunguu jikoni, ghafula huepua sufuria na kwenda mbio kwa jirani baada ya kusia umbea fulani, huku ni kukosa kujitambua ! Akisikia neno mbio ataaga na kutoka kanisani mapema utazani anawahi mtoto nyumbani, kumbe kuna sumu anaenda kumwaga kwa mpendwa ambaye hajaja kanisani.

Huyu Msamaria, kaacha mtungi, na kwenda kueneza habari za Yesu, wewe je unaacha na kwenda kueneza nini? Aibu ya kanisa, udhaifu wa mama mchungaji wako, udhaifu wa kiongozi wako wa idara, ama unapeleka madhaifu ya kikanisa kwa wapendwa na mbaya zaidi hata kwa wasio wapendwa yaani kwa watu wa mataifa ! Ila huyu, hakufanya hivyo!

Nisikilize, hakuna mtumishi aliyekamilika, wapo mbinguni, hakuna kanisa lililokamilika, hoja ni pale unapoona madhaifu unafanya nini? Unapaswa kuomba, ukiona doa kwenye koti langu, kachukuwe sabuni na maji uliondowe, sio kulipiga picha na kusambaza doa langu, hujanisaidia, na ukitangaza aibu ya mtumishi ni umeanika aibu ya Yesu, huko ni kulivua nguo kanisa, na kanisa ni Kristo, uwe na uhakika adhabu inakuhusu siku ile ya mwisho ! Jifunze sana kwa huyu mwanamke, nawe uwe ni mueneza habari njema kwa majirani zako, marafiki, usikubali kukaa nao na kujadili yasiyofaa, bali mjadili mema, mkiongea kumi kuhusu VIKOBA, na VIBATI, au mchezo wa fedha,basi wewe weka hapo mawili ya Yesu, anza tu stori kuwa nilipokuwa sijaokoka jamani nilikuwa na sumbuliwa na hili au lile, ila toka nimeokoka, naona nimepokea mujiza, usishangae jirani yako akikwambia, jamani nipelekeni na mimi hapo !

Ama, mchungaji wetu akikuombea, Mungu aliyeko ndani yake atakufungua haraka sana, hapo unafahamu kuna mgonjwa, hata kama hatatoa jibu muda huo uwe na hakika kuwa punde, au baada ya muda, Kuna siku atakutafuta tu, maana ulipanda mbegu, maneno ni mbegu !
(Mithali 6:19 Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.)

Sasa ikupe kujiuliza sana, huwa unapanda mbegu ipi uwapo kanisani, au na wapendwa, kama unamsema vibaya mchungaji, au kanisa, ama mpendwa, uwe na hakika, unapanda pando baya, na apandaye magugu ni mwana wa Ibilisi !

Tuendelee na utendaji wa mwanamke huyu, aliyemtengenezea Yesu mazingira mazuri ya kuifanya kazi yake !

Yohana 4:29 Njoni, mtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda. Je! Haimkini huyu kuwa ndiye Kristo?
Na wewe tafuta ulilotendewa na Yesu, lipo, ( Kila aliye na Mwana hakosi ushuhuda, kama huna, tazama vyema kiroho chako kama kweli unaye Mwana !)

30 Basi wakatoka mjini, wakamwendea.
39 Na katika mji ule Wasamaria wengi walimwamini kwa sababu ya neno la yule mwanamke, aliyeshuhudia kwamba, Aliniambia mambo yote niliyoyatenda.

40 Basi wale Wasamaria walipomwendea, walimsihi akae kwao; naye akakaa huko siku mbili.
:41 Watu wengi zaidi wakaamini kwa sababu ya neno lake.
42 Wakamwambia yule mwanamke, Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu; maana sisi tumesikia wenyewe, tena twajua ya kuwa hakika huyu ndiye Mwokozi wa ulimwengu.

Yesu alikuwa na kazi nyepesi sana huku, hakukuwa na haja ya kulipia matangazo ya mkutano, au kusambaza vipeperushi, maana kuna mtangazaji, na msemaji wake, alimtangulia, nawe una hiyo dhima, hakikisha unatumia vyema nafasi hii!

Kumbuka hili siku zote, kuwa Mungu asiponufaika na alichoweka ndani yako, basi adui atakitumia, huamini, acha kumsema Yesu, usipojikuta unawasema watu ! Kanisani utakuwa mkosoaji na kuchambua mabaya kana kwamba hakuna jema hata moja, kiongozi wa migomo baridi ni wewe, mbeba maneno utakuwa ni wewe, kwa nini, chai iliyopoa au supu, ndipo nzi hutua ! Kama kinywani mwako Yesu habebwi, Ibilisi atabebwa, utashangaa kila baada ya maneno yako unasema lakini tumuombee, lakini kiukweli huwa hauombi !

2. Ni Muombaji; Yohana 2:3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.
4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.
:5 Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.

Sijajua ni kwa nini, ila wanawake wamepewa nafasi ya maombi yao kuwa na wepesi na kibali cha haraka sana, labla kwa kuwa ndani yao uombolezaji ni mwepesi zaidi, ila ninachonuia kukwambia hapa ni kwamba uonapo tatizo au upungugufu kanisani, sio muda wa vikao, na kuchambua, bali ni muda wa kufanya maombi, au dua, ama toba, lishike hili siku zote !

3. Ni Chanzo cha Utatuzi wa Migogoro au Matatizo Sugu maana amepewa Busara na Hekima; Mfano 1, Abigaeli; ( 1 Samweli 25:4-35.)
1 Samweli 25:23 Ndipo hapo Abigaili alipomwona Daudi, alifanya haraka kushuka juu ya punda wake, akamwangukia Daudi kifulifuli, akainama mpaka nchi.

24 Akamwangukia miguuni pake, akasema, Juu yangu, bwana wangu, juu yangu mimi na uwe uovu; tafadhali mjakazi wako na anene masikioni mwako, nawe uyasikilize maneno ya mjakazi wako.

25 Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.

32 Naye Daudi akamwambia Abigaili, Na ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye amekuleta hivi leo kunilaki;

33 na ibarikiwe busara yako, na ubarikiwe wewe, uliyenizuia hivi leo nisimwage damu, wala kujilipiza kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.
Mfano 2, Kisa cha Seba aliyemuasi mfalme Daudi !

Baada ya tukio hili, Yoabu alinuia kuleta maangamizi makubwa kwa mji wao wote, na tayari alishaanza kuuvunja ukuta, nasi twafahamu huluka ya Yoabu, katika hiyo sura tu alikuwa ametoka kumuangamiza mtu kwa kukita upanga tumboni mwake, Abineli aliuawa naye, japo alikuwa ameshatengeneza, pia Absolum aliuawa, japo mfalme aliachilia rai ya kumtaka aishi ! Kwa hiyo, sio ajabu kuwa mji huo,ungedhuriwa !

Ila kwa hekima ya huyu mwanamke atwajaye kama mwenye akili, huku biblia nyingine za kingereza na zile za kiswahili rahisi kutumia neno mwenye busara,aliweza kuuokoa mji huo, sasa kanisa likiwa na mama mchungaji makini, na mumewe kujua kumtumia vyema, kwa kumsikiliza na kumpa nafasi, uwe na uhakika atafanikiwa kupindua maamuzi ambayo yangeweza kuleta madhara kwa kanisa, kama Abigaili na huyu waliweza, ni fika hata wewe wa weza !

Kuna ina fulani ya hekima, na busara, na uwezo wa ushawishi waliopewa wanawake, sasa adui akiuwahi, hapo huzalisha wakina Delila,ila Kristo kiuwahi, huzalisha wakina Abigaili, sijui wewe u wapi, au umempa nafasi adui au Kristo Yesu !
Tuuone mfano wetu :

2 Samweli 20:15 Na hao wakaja wakamhusuru katika Abeli wa Bethmaaka, wakafanya chuguu mbele ya mji, nayo ikasimama kuielekea ngome; na watu wote waliokuwa pamoja na Yoabu wakavunja-vunja ukuta, wapate kuubomoa.

:16 Ndipo akalia mwanamke mmoja mwenye akili toka mjini, Sikieni, sikieni; mwambieni na Yoabu, aje hapa karibu, niseme naye.
:17 Basi akamkaribia; na yule mwanamke akasema, Ndiwe Yoabu? Akajibu, Ndimi. Ndipo akamwambia Sikia maneno ya mjakazi wako. Akajibu, Mimi nasikia.

18 Kisha akanena, akisema, Watu hunena zamani za kale, wakisema, Wasikose kuuliza huko Abeli; ndivyo walivyomaliza shauri.
:19 Mimi ni wa hao wenye amani, walio waaminifu katika Israeli; wewe unatafuta kuuharibu mji, na mama wa Israeli; mbona wataka kuumeza urithi wa Bwana?

:20 Yoabu akajibu, akasema, Isiwe, isiwe kwangu, niumeze wala kuuharibu.
21 Neno hili silo hivyo; lakini mtu mmoja wa milima ya Efraimu, Sheba, mwana wa Bikri, jina lake, ameinua mkono wake juu ya mfalme, naam, Daudi, basi mtoeni yeye tu, nami nitaondoka katika mji huu. Basi yule mwanamke akamwambia Yoabu, Tazama, kichwa chake utatupiwa juu ya ukuta.

:22 Ndipo yule mwanamke akawaendea watu wote katika akili zake. Nao wakamkata kichwa Sheba, mwana wa Bikri, wakamtupia Yoabu huko nje. Ndipo akapiga tarumbeta, nao wakatawanyika kutoka mjini kila mtu hemani kwake. Naye Yoabu akarudi mpaka Yerusalemu kwa mfalme.

Mwanamke ! Mumeo akiwa mkali, akiwa na hasira kama simba, ni hatari wewe ukiwa kama mbuzi, ila ukiwa kama kondoo, utafanikiwa kuituliza, huyu mwanamke kama naye angeinuka na kujibizana, hakika angechochea ghadhabu ya Yoabu, ila alitumia busara, sasa wanawake wengine, nao hupanda juu, hawajui Mithali 15:1 husemaje ? Kuwa jibu la upole hutuliza hasira, ila la kinyume chake huchochea !
Biblia nyingi za kingereza zimetumia neno ulimi laini, au mzuri, kwa hiyo, ukitaka kutenda vyema, dhidi ya mumeo mwenye hulika kama ya Yoabu, hakikisha unakuwa na ulimi laini, maana hata vyuma bila mafuta husagika.

Akikuudhi na wewe ukisema naenda kwetu, usishangae akiwa wa kwanza kukutolea begi nje!

Sio kwamba hakupendi, ila umechochea ghadhabu, ndio maana ukiondoka, baada ya siku mbili tatu, anakufuata, hapo uwe na hakika, hasira imeisha ! Sasa unaweza kuituliza kwa akili, sio kwa kushindana, huyu mwanamke na Abigaili wawe ni somo tosha kwako !

Muone Ambaye anatumiwa na Ibilisi, ni Mvunjaji, ni mbomoaji, nyundo, huweza kujenga ikitumiwa katika dhamira hiyo, ila ikitumiwa vibaya hubomoa pia, kwa hiyo chombo hakina shida, mtumiaji ndie mwenyewe shida: Kwa hiyo kama kuna mwanaume anaoma huu ujumbe, ajuwe sasa kumuombea mwenzie ! Na kama ni mtumishi, ukiwa na wanawake waharibifu, jifunze kuwabadili au kubadili nia zao kupitia maombi na mafundisho !

Mithali 14:1 Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

Ona hapa:

Mithali 27:15 Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi, Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;

Oanisha na : Mithali 19:13 Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye; Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.

4. Hutunza Watumishi; 1. Yule Mshunami; 2 Wafalme 4:9 Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu wa Mungu.

10 Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa; na itakuwa, atujiapo, ataingia humo.

Kuna mzigo wa kipekee ambao Mungu ameweka kwa wanawake kuhusu kuwahudumia watumishi, na kanisa lenye wanawake wenye kujitambua kama hawa, moja kwa moja, hutimiza dhima hii vyema sana !

Mfano 2, Mwanamke wa Serepta, 1 Wafalme 17: 10-16.

Mfano 3, Enzi za Yesu, japo hata kwa Paulo Mtume ama kqnisa la kwanza walikweo wakina Lidia, tumuone Yesu;

Luka 8:2 na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3 na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.

Yesu alihudumiwa kwa mali zao, wewe jiulize, mtumishi wako unamuhudumia kwa mali zako ! Na Yesu wa leo ni huyo mlawi wako, ama mtumishi wake !

Na kama hujaokoka na unataka kufanya hivyo sasa tafadhli kwa imani kubwa nakuu kabisa fuatisha pamoja nami maneno haya, au sala hii ya toba ili uweze kuokoka, Sema;

BWANA YESU, NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NATUBU MBELE ZAKO LEO, NISAMEHE NA NINAKUOMBA UFUTE JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, TAFADHALI LIANDDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA, NINAKUKIRII NA KUKUPOKEA MOYONI MWANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, HAKIKA WEWE NI MUNGU NA ULIFUFUKA KATIKA WAFU, Amen.

Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, kwa maombi, sadaka kwa njia ya M-Pesa, kupiga simu au Wasats App, ni +25559859287. Tupo Arusha Tanzania.

Jumatano, 27 Februari 2019

MAANA YA MBEGU ILIYODONDOKA KANDO YA NJIA:

Mahali: TAG Ushiri, Rombo:     Tarehe 27/2/2019, Na Mwalimu Oscar Samba

Mathayo 13:3 Akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema, Tazama, mpanzi alitoka kwenda kupanda.
4 Hata alipokuwa akipanda, mbegu nyingine zilianguka karibu na njia, ndege wakaja wakazila;
( Luka, zikakanyagwa:Luka 8:5 Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake; naye alipokuwa akizipanda, nyingine zilianguka karibu na njia, zikakanyagwa, ndege wa angani wakazila.)
19 Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia.
Kwa hiyo, kutokulielewa neno, huifanya mbegu hiyo kukosa makao mazuri moyoni mwa muhusika, maana hapo huambiwa yule asikiaye, lakini asielewe yu sawa ama ndie aliyepandwa kando au pembezoni mwa njia, ambapo adui huja na kulitwaa hilo neno, ama kukanyagwa na kuharibiwa.
Maana ya Mbegu: Mbegu ni Neno la Mungu, mpanzi ni Muhubiri, ama Roho Mtakatifu moja kwa moja, au kumpitia mjumbe wake aliye Mtumishi wake;
Luka 8:11 Na huo mfano, maana yake ni hii; Mbegu ni neno la Mungu.
Shamba ni Moyo: Luka 8:12 Wale wa karibu na njia ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na kuokoka.
Kama huondolewa moyoni, maana yake lilipandwa hapo, kwa hiyo, kama mbegu ni neno, na moyo ni shamba, kwa mantiki hiyo mahubiri, au mafundisho hupandwa moyoni mwa muhusika.
Zile aina za mahali mbegu zilidondokea, yaani njiani, penye udongo mchache, penye miiba, na udongo mzuri, maana yake ni aina ya mioyo ya watu wanaolisikia neno la Mungu.
Mpanzi au mkulima apandapo, ili mbegu iwe imedondokea sehemu ipi, ni matokeo ya moyo ulio nao, kwa hiyo ukitaka kuwa na mafanikio, ni lazima kuhakikisha unajitengenezea moyo mzuri, ili neno lijapo, lidondoke mahali sahihi.
Kusudi la Mungu Kukutaka Mbegu yake Isipandwe kando ya Njia.
Kumbuka sana kuwa Mungu kama mkulima hataki au hapendi kupanda njiani, ila mazingira ya moyo wako ndio huifanya mbegu kuelekea hapo !
1. Ili Kuua na Kuuhuisha; Yohana 12:24 Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi.
25 Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa mikulala
26 Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.
Kitu neno hufanya ni kuua aina fulani ya maisha yasiyo ya Kiungu, na kuhuisha yaliyo sahihi, Warumi hutuambia vyema kuwa kufa kwa Yesu ni kuua mwili wa dhambi na kufufuka ndimo mlimo na mantiki ya kufufua utu mpya.
Mungu akitaka kuua visivyo vya kwake kwako, na kuhitaji kuhuisha vya kwake, huliachilia neno lake, au mbegu yake, sasa ikianguka mahali sahihi, ndipo hufanikiwa sana, unaposikia alikuwa mwizi na kuacha, maana yake, alipokea neno lililouwa wizi na kuhuisha uadilifu,ambao ni tunda la Kristo.
2. Kukufanya Uzae, na Huwezi zaa kama mazingira sio rafiki kwa uzalishaji, mfano wa mazingira rafiki;
Mathayo 13:23 Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathinhuu.
Kwa hiyo, ukihitaji kuwa na utumishi wenye mafanikio kwako, kuhakikisha kuwa unajiwekea mazingiira mazuri ya kupokea neno la Mungu linalonuia kukubadilisha kitumishi ni muhimu sana, ukihitaji kufanikiwa kimaisha, ni shariti moyo wako uwe na mazingira rafiki katika uzalishaji wa matunda na  hauwezi zaa, kama mbegu haijamea, ikidondoka njiani, haitamea, ya udongo haba au juu ya mwamba, itanyauka yakija mpito, na ile iliyosongwa haiwezi kuivisha kama Luka isemavyo.
Ujumbe huu ni jibu tosha na muhimu sana kwa yule anayehitaji kufanikiwa, au kustawi kihuduma, kimaisha, na kuwa mti mkubwa kama ufalme wa mbinguni ufafanuliwavyo, wengi hutamani sana kufanikiwa kihuduma, ila kuna mahali wamekwama, ambapo ni hapa, mfano utakaouona hapo mbeleni wa mti ulioanza na mbegu ndogo na kisha kupanuka na kuzaa,na ndege kukaa juu yake, ni muhimu kujua kuwa, asili yake ni mbegu, ila sio iliyodondoka njini, wala kusongwa, wala juu ya mwamba, bali ni ile ya udongo au moyo mzuri, kwa hiyo, nawe ukihitaji kufanikiwa katika jambo fulani ni lazima kujua au kuijua hii Kanuni !
Nakupa tena maandiko kuhusu dhima ya mbegu, katika kuuwa na kuhuisha kitu fulani, maandiko haya yakupe kuhakikisha unanufaika vilivyo na neno la Mungu, kama kuna vitu ndani yako huvitaki, na untaka vichipuke vya kiungu, maandiko haya hunena habari za nyakati za mwisho kuhusu kubadilishwa kwetu, ila hapa nataka ujionee thana ya mbegu, na ili iwe na matunda lazima ife, kufa ni kubadilika, kutoka katika mbegu, na kutoa mche, neno la Mungu lililopo kwenye biblia halina matunda hadi liingie moyoni mwako, na kuanza kuzalisha mabadiliko! Mbegu ambayo haijafa,ni mbegu, sasa hatutaki mbegu, tunataka matunda, na ili tuyapate ni lazima tupande, kisha imee, sasa wengi kiroho hutaka mbegu, ila kubadilishwa au kuiruhusu, ama kuipa nafasi ili iwabadilishe, kisha wawe na matunda hawataki, atakuwa ni mkulima wa ajabu sana ambaye ataishilia kununua mbegu, ila hataki mazao ! Na ndivyo wakristo wengi walivyo leo, husoma sana neno, huenda sana kanisani, ila hawairuhusu injili iwabadilishe! Usizini, usiibe, wahi kanisani, uwe mtoaji, toa zaka kamili, ila bado wako pale pale, hawaruhusu neno hilo, kuingiza mabadiliko mapya ndani yao, tujionee maandiko !
(1 Wakorintho 15:35 Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani?
36 Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa;
:37 nayo uipandayo, huupandi mwili ule utakaokuwa, ila chembe tupu, ikiwa ni ya ngano au nyingineyo;
:38 lakini Mungu huipa mwili kama apendavyo, na kila mbegu mwili wake. )
Kumbuka/ Fahamu: Mungu ni Mpanzi, na Shetani naye ni Mpaanzi, kwa hiyo moyo wako usipopandwa mbegu njema, utapandwa mbaya, na nia ya mbegu njema, ni Ufalme wa Milele;
(1 Petro 1:23 Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele. )
Mungu alipoiumba dunia, alipanda pando jema, adui akaja, baada ya kulala kwa Adamu, akapanda pando baya, hii ikupe kuenenda kwa umakini humu ulimwenguni;
Mathayo 13:24 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
:25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
:26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
Ukindelea mbele ya hayo maandiko utapata kujua kuwa magugu yanatakiwa kuachwa hadi siku ya mavuno, kwa hiyo inawezekana nawe katika kwaya, au utumishi ama kanisani u gugu, ila bado umeachwa haimaaniishi parapanda ikilia nawe utakuwa mawinguni, la!
Bali utaingia jehanum ya moto, hekima ya kuachwa kwa magugu haikupi kuingi mbinguni, maana siku ya mavuno, itachambuliwa ngano na kufungwa matitamatita, kisha kuwekwa ghalani, na magugu nayo yatafungwa, ila yatatupwa motoni, na huko ndimo mlimo kilio na kusaga meno, sasa hii ikupe kutengeneza na Bwana, yaani uruhusu mbegu njema, ambapo mimi kama mpanzi kwa uweza wa Mpanzi Mkuu, ninanuia kupanda moyoni mwako leo, au majira haya, ili sasa pando jema liwe ndani yako, na kuuwa kila pando baya, yaani ufisadi, ulafi, uasherati, wizi, matukano, kiburi, dharau na kadhalika.
3. Kumbuka Hauwezi Kufika Hapa kama Mbegu yako haikupandwa Sehemu sahihi; Mathayo 13:31 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake;
32 nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake.
Ni dhairi kuwa ukihitaji kuinuliwa, au kupanuka kimaisha na kiroho, na kihuduma, ni lazima kuhakikisha kuwa moyo wako una mazingira sahihi katika kulipokea, na kulitunza neno la Mungu, mkulima makini huliandaa shamba vyema na kulitilia mbolea, nawe kama Mkristo makini, hakikisha moyo wako ni uliopondeka.
Isaya 66, hutuambia kuwa mtu ambaye akilisikia neno la Bwana hutetemeka, huyo ndiye Mungu humuangalia, kwa maana kwamba huyu mtu moyo wake, u na mazingira mazuri, akionywa huonyeka, akihaswa huzingatia, iwe hivyo kwako !
Madhara ya Kupandwa Kando ya Njia, au Nia ya Adui Anapoweka Mazingira moyoni mwa mtu ili Neno lipandwe kando ya Njia:
Kuna vijitabia ambavyo Shetani huvitumbukiza ndani ya moyo wa mtu, na wengi hawajui ni kwa nini ! Nia yake ni kumuwekea muhusika mazingira ya mbegu au neno alisikialo lisidondoke sehemu sahihi !
Mathalani kiburi, huyu mtu asikii maonyo, asikii mahusia, maana njia yake imenyooka machoni pake mwenyewe, ikiwa na maana kwamba kile akiwazacho, akionacho, akipangacho hukiona ni sahihi hata kama atashauriwa, kwenye kiburi kuna upumbvu, pia ujinga, ukija katika Obadia 1:3-4, utagundua kuwa kiburi pia hudanganya, yaani hupotosha, kwa hiyo kitamuaminisha kuwa njia hii ni sahihi, wazo hili ni sahihi, kama ilivyokuwa kwa mfalme Sauli, maana kiburi kilimpa kujiamini hata kama Mungu atakuwa amemuacha, maana kii na mbinu na tabia ya kudanganya, mtu hujiona yu salama kumbe sivyo !
Mazingira mbayo ni hatarishi sana kwa Neno kuweza kuchipusha linalotakiwa kuhipusha !
1. Ili Aweze Kuinyakuwa, au kuiharibu, ama Kuizuilia Isichipuke: Luka 8:12 Wale wa karibu na njia ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na kuokoka.
Unapohubiri na mtu kusema ananisema, au moyoni mwake kuwa na mawazo mengine, kimawazo kuwa mbali ama kiakili,ama anapofanikiwa kubana akili ama fikra zake, au ufahamu wake ili asielewe, uwe na uhakika kuwa baada ya mahubiri, au neno hilo, adui huja na kulinyakuwa, ama hukanyagwa !
2. Ananuia Kukuzuilia Kunufaika na Kile Kilichokusudiwa na Mpanzi; Yohana 12:40 Amewapofusha macho, Ameifanya mizito mioyo yao; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakafahamu kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya..
Wakati wakina Bartomayo kipofu wakipokea miujiza yao, Mafarisayo, haikuwa hivyo kwao, hakuna mahali wananufaika na injili yaa Yesu isipokuwa Nikodemu aliyejua kuweka kiburi cha kidini na elimu pembeni na kukubali kunyenyekea, sio kwamba hawakuwa na mahitaji la! Walikuwa nayo, ila tatizo ni mioyo yao kugoma kuipokea hiyo mbegu !
Sasa maandiko hayo hutuambia kuwa ni ili wasije wakapokea nuru ama mwanga kisha kuweza kuponywa na Kristo Yesu, kwa hiyo, unapohubiri na watu kutema chakula, maana yake, adui amefanikiwa kuwazuilia kubadilishwa na hilo neno, dalili kubwa ya mtu ambaye mbegu haijadondoka njiani ni mabadiliko yake, ukiwa na mshirika asiyebadilika, kuwa makini na shamba upandalo mbegu, kama hana kiburi, sio mwenye madharau, na mkataa maonyo, basi ombea ufahamu wake, maana kuna namna umefungwa,katika mpanzi huambiwa kuwa mtu anapolisikia hilo neno na kushindwa kulielewa hapo ndipo huja adui na kulinyakuwa, kwa hiyo adui akifanikiwa kuzuilia au kubana uekewa wako ama wake uwe na uhakika amezuilia jambo kubwa sana.
Katika kitabu chetu cha IJUWE HUDUMA YA UINJILISTI, nimewataka wainjilisti kuhakikisha kuwa wanaombea hii mioyo, yaani wanaandaa hili shamba vyema, ila katika upandaji, waweze kupanda mahali sahihi, hakuna mpanzi atakaye kupanda njiani, ama mahali pasipo mzalia matunda !
Sasa wachungaji, na wale wanaombea ibada, ni lazima sana kujifunza kuelewa usikiaji wao, fahamu zao, kama akikamata fikra, ama mioyo yao na kuitia uzito hufanikiwa kuwazuilia kupata wokovu, basi wewe ombea hizo fikra ziangushe hizo ngome za mawazo mbaya, na kila fikra zijiinuazo kinyume na elimu ya Kristo, kisha zitiishe, hii ni siri kubwa sana,hakikisha unaombea usikiaji wao, maana hapo ndipo adui huwekeza sana, ndiposa wakati wa ibada hujitahidi sana kupambana na usikiaji wao, asipoamisha mawazo, basi atafinya hata mtoto ili aliye, kwa nia ya kuondoa usikivu !
3.
Mazingira Rafiki na Hatarishi kwa Mbegu:
1. Roho na Tabia ya Kupuzia Maonyo, au Mahubiri, ama Mafundisho, ama Makaripio: Mithali 1:28 Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione.
29 Kwa kuwa walichukia maarifa, Wala hawakuchagua kumcha Bwana.
30 Hawakukubali mashauri yangu, Wakayadharau maonyo yangu yote.
31 Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao, Watashiba mashauri yao wenyewe.
32 Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.
33 Bali kila anisikilizaye atakaa salama, Naye atatulia bila kuogopa mabaya.
Kuna Hatari ya Kupotea, na hata Kufa: Mithali 5:23 Atakufa huyo kwa kukosa maonyo, Naye atapotea kwa wingi wa ujinga wake.
Suluhu lake: Tilia Moyoni, Luka 2:49 Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?
50 Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia.
:51 Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
Mamaye na Yesu, hakuwa kama wengine, alitilia moyoni, hapo ukiniuliza sababu ya wengine kutokutilia moyoni, nitakwambia i katika huo mstari wa 50, kwamba hawakuelewa, sasa utaniele ni kwa nini adui huhakikisha kuwa watu wakisoma biblia hawaelewi, wakisikiliza mahubiri hawaelewi, huishilia kusema kile kitabu ni kizuri, somo alihubiri visuri, ila mulize alichoambulia hapo, hana! Anachokumbuka ! Labla kichekesho ama kitu kilichomfanya ama kuwafanya kucheka! Hii ni hatari sana.
Sasa ikupe kuhakikisha unapoonywa, unapokatazwa, unatilia moyoni unayoambiwa, unaposikiliza neno na kugundua dosari yako hapo, kinachotakiwa kufuata ni mabadiliko, ukisikia injili ya onyo kwa wasiotoa zaka,moja kwa moja anza kutubu, kisha msihi Mungu akuumbie tabia na mwenndo mpya, sasa huyu ndiye anayeitwa kuwa humfurahisha Mungu, ama ndiye mtu ambaye Mungu humtazama, tumuejionea kwenye Mithali hapo juu kuwa wapo wamuitao, ama wamtafutao kwa bidii ila hawamuoni, maana wamekataa maarifa, na sababu ni kudharau monyo, sasa leo tuna waombaji wazuri sana, wanataka kumuona Mungu kwenye jambo fulani, ila hawajui kuwa ameshagoma kuwasikiliza maana alinyoosha mkono hawakuutazama, wanamtafuta kwa bidii ila kauficha uso wake kwa maana walikwepa maonyo !
( Kutilia Moyoni ni Kuhifathi: Mwanzo 37:11 Ndugu zake wakamhusudu; bali baba yake akalihifadhi neno hili.)
Ona Mukutadha wa Kutokutilia Moyoni hapa: Isaya 42:18 Sikilizeni, enyi viziwi; tazameni, enyi vipofu, mpate kuona.
19 Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu? Au aliye kiziwi, kama mjumbe wangu nimtumaye? Ni nani aliye kipofu, kama yeye aliye na amani? Naam, kipofu kama mtumishi wa Bwana?
20 Unaona mambo mengi, lakini huyatii moyoni; masikio yake ya wazi, lakini hasikii.
Pili Kubali kuonywa; Kusudi la Maonyo ni Kukugeuza: Mithali 1:23 Geukeni kwa ajili ya maonyo yangu; Tazama, nitawamwagia roho yangu, Na kuwajulisheni maneno yangu.
24 Kwa kuwa nimeita, nanyi mkakataa; Nimeunyosha mkono wangu, asiangalie mtu;
:25 Bali mmebatilisha shauri langu, Wala hamkutaka maonyo yangu.
Nia na kusudio kubwa la maonyo ni kukugeuza, kama huo mstari wa 23 uanzavyo, ni sawa na mtu anayetaka kuelekea uwanja wa ndege wa KIA, ila kapanda gari la kuelekea Dar es salam, na kashafika Tanga, anaulizwa na mtu unaenda wapi, KIA, anaambiwa kuwa umepeotea, geuka,anagoma, sasa ni sawa na mtu anayeonywa, kuwa ukitaka kufanikiwa kielimu, achana na ngono, ukitaka kufaulu, acha kiburi, ila bado ni jeuri, baada ya muda, hujikuta amepotea, ila akisiliza, hugeuka, na hapo huelekea njia iliyo salama !
Kuna mahali maonyo hukuelekeza na kukuwezesha kufika, maana ni njia;
Mithali 6:23 Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru, Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.
Maonyo kuna kitu yamebeba, ukiyakubali, huweza kunufaika na kilichobebwa nayo, mfano hekima; Mithali 29:15 Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.
Na kama hujaokoka na unataka kufanya hivyo sasa tafadhli kwa imani kubwa nakuu kabisa fuatisha pamoja nami maneno haya, au sala hii ya toba ili uweze kuokoka, Sema;

BWANA YESU, NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NATUBU MBELE ZAKO LEO, NISAMEHE NA NINAKUOMBA UFUTE JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, TAFADHALI LIANDDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA, NINAKUKIRII NA KUKUPOKEA MOYONI MWANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, HAKIKA WEWE NI MUNGU NA ULIFUFUKA KATIKA WAFU, Amen.

Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, kwa maombi, sadaka kwa njia ya M-Pesa, kupiga simu au Wasats App, ni +25559859287. Tupo Arusha Tanzania.