Alhamisi, 11 Julai 2019

Mtu moja kauliza Hivi ! Hivi wakisema sisi hatupo chini ya sheria tupo chini ya Neema nini maana yake hasa?

Nami nimemjbu kwa kifupi sana, na kwa kirefu kipo kitabu chetu kiitwacho, YESU KAMA KWELI NA NEEMA, Jibu:
Ni kuongozwa na Roho Mtakatifu; Wagalatia 5:23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa RohMtu moja kauliza Hivi !
Hivi wakisema sisi hatupo chini ya sheria tupo chini ya Neema nini maana yake hasa?

Nami nimemjbu kwa kifupi sana, na kwa kirefu kipo kitabu chetu kiitwacho, YESU KAMA KWELI NA NEEMA, Jibu:

📖 Ni kuongozwa na Roho Mtakatifu; Wagalatia 5:23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.

Kazi moja wapo ya sheria ni kukujulisha lipi baya na jema, sasa neema inakujulisha baya na jema, na kukuwezesha au na kukupa nguvu ya kuepukana na baya , ukisoma Warumi tano hadi nane utaelewa zaidi !

Laini penye Roho Mtakatifu, pana sheria ! Ila utofauti yake ni kwamba ni katika Roho, ndiposa huitwa sheria ya Roho wa Uzima, ikimaanisha kuwa kuna neema ndani yake; Warumi 8:2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.

Jumatano, 3 Julai 2019

MUNGU ANAPOKAA KIMYA, WEWE FANYA YA FUATAYO, AMA TENDA HIVI:

Na Mwalimu Oscar Samba:

Wasomaji wa Biblia wanafahamu kuwa yapo maombi kadha wa kadha ambayo hayakuwahi kujibiwa, na mengine yalijibiwa lakini yalichukuwa muda mrefu tofauti na mtazamo wa wa husika ila Mungu alikuja kuyajibu.

Ibrahimu na mkewe ni kielelezo kikubwa katika hili, kwa hiyo, ikupe kufahamu kuwa wewe sio wa kwanza, sio hapo tu lakini twafahamu katika sura ya kutokujibiwa yapo hata maombi ya Yesu ambayo hayakujibiwa !
Alihitaji kikombe kimuepuke, na Mungu Baba kugoma kuyajibu ! Hadi alipobadili maombi, Musa na Yeremia nao wana orodha ya maombi ambayo hayakujibiwa !

Walijitetea kadri walivyoweza ili wasitumike lakini Mungu hakuzingatia hoja zao ! Kuna ndugu wa wiwili kipindi cha Yesu ambao ni wanafunzi wake, waliomba kuketi mkono wa kuume katika Ufalme wa Mbinguni ila maombi yao yalisogezwa

JINASUWE KWENYE ROHO AU VIFUNGO VYA KURITHI, FAMILIA, KABILA NA UKOO.

Ujumbe huu ni matokeo ya kiu ya kijana fulani anayesoma kidato cha Sita kunitaka nimfundishe maana amekuwa akisumbuliwa na mkuu wao wa ukoo ambaye humtokea na kumtangazia kumkwamisha kimasomo, japo yeye hamjui maana ni wa miaka mingi, ila hujitambulisha hivyo, na amekuwa akipitia wakati mgumu kitaaluma, hata kugubikwa na usingizi mzito mwalimu aingiapo darasani na kadhalika !
Pia ni nimeelezea jambo hili kiupana sio kitaaluma tu, natumai litakusaidia namna ya kujinasua kindoa, kiuchumi, na hata kimaisha, unapojiona umeokoka ila maisha yako yamekwama kama ndugu zako, una ugonjwa ambao husumbua jamii zako, unatatizo la kindoa kama nduguzo, unakataliwa na ndugu, huna kibali kwao, uwe na hakika hizi roho zipo kazini.