Ijumaa, 30 Julai 2021

UPENDO WA MUNGU KWAKO NI WA MILELE, HAUFUNGWI NA MSIMU WALA MUDA

Na Mwalimu Oscar Samba

Ujumbe hu ni Sehemu ya Kitabu chetu cha MUNGU ANAKUPENDA. Kitabu kinachonuia kukusaidia kuliona pendo lake hata kama upo wakati mgumu, ukifahamu kuwa haupitii kwa sababu Mungu amekuacha, hakupendi ama amekukatataa.

Yeremia 31:3-7

Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.
 Mara ya pili nitakujenga, nawe utajengwa, Ee bikira wa Israeli mara ya pili utapambwa kwa matari yako, nawe utatokea katika michezo yao wanaofurahi. Mara ya pili utapanda mizabibu juu ya milima ya Samaria; wapanzi watapanda, nao watayafurahia matunda yake.
Maana kutakuwa siku moja, ambayo walinzi watalia juu ya vilima vya Efraimu, Inukeni, tukaende Sayuni, kwa Bwana, Mungu wetu.
Maana Bwana asema hivi, Mwimbieni Yakobo kwa furaha, mkampigie kelele mkuu wa mataifa, tangazeni, sifuni, mkaseme, Ee Bwana, uwaokoe watu wako, mabaki ya Israeli.

 

Jumatano, 21 Julai 2021

KAWIA UFIKE

 Na Mwalimu Oscar Samba

Ni kweli ngoja ngoja huumiza matumbo, au fahamu pia simba mwendapole ndie mla nyama! Maana mtaka yote kwapupa hukosa yote! Hawakuwahi kukosea waliosema kuwa subra yavuta heri!

 Ni hakika haraka haraka haina baraka! Maana hata waingereza ama wenye kingereza chao husema kuwa, njia ya kato siku zote ni njia isiyo sahihi.

 Kuna watu wengi wamjejikuta wakiingia hasara maishani mara baada ya kutaka mafanikio kwa haraka! Wamejikuta wakipoteza ama wakiharibikiwa kimaisha, ni kweli ni tajiri ila kapoteza mke na woto kwa sababu ya mashariti ya mganga! Ni kweli ana fedha sawa na elimu sawa ila ni muadhirika wa UKIMWI! Kapenda chipsi hatimae ni mjamzito na ndoto za kusoma zimakomea hapo!

 Ni heri ukawie lakini ufike uendako, kuliko kukimbia ukajikuta unakimbia hadi unasahau nyumbani ama unashindwa kuangalia taadhari ya alama za barabarani na hatimae ukaingia katika kusababisha ama kujisababishia ajali!

Narudia tena na tena kuwa kawia ufike, pole pole ndio mwendo! Unaonaje mkulima akapanda mbegu leo na kutaka kuvuna siku hiyo hiyo! Kama kwa mkulima haiwezekani uwe na uwakika kuwa na katika safari ya mafanikio ndivyo ilivyo.   

Embu tujionee jinsi maandiko mtakatifu ya Biblia yanavyotufunza katika kitabu kile cha Yakobo: 5:5 Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.

8 Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia.9 Ndugu, msinung'unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.

 

Jumamosi, 3 Julai 2021

Mwalimu Oscar Samba KUMFANANIA KRISTO Mkimbizi Iringa Ibada ya 1

Mwalimu Oscar Samba THAMANI YA KUMKABITHI MUNGU MAISHA YAKO YA BAADAE na...

Nilipata nafasi ya Kuwafundisha wanafunzi wahitimu wa Chuo Kikuu cha Mipango Dodoma CASFETA
Ujumbe huu utakusaidia uliye mwanafunzi na usie mwanafunzi kujua umuhimu wa kumshirikisha Mungu katika kila hatua muhimu ya maisha yako ikiwemo ile ya mawazo ama upangaji wa mipango