Ijumaa, 30 Julai 2021

UPENDO WA MUNGU KWAKO NI WA MILELE, HAUFUNGWI NA MSIMU WALA MUDA

Na Mwalimu Oscar Samba

Ujumbe hu ni Sehemu ya Kitabu chetu cha MUNGU ANAKUPENDA. Kitabu kinachonuia kukusaidia kuliona pendo lake hata kama upo wakati mgumu, ukifahamu kuwa haupitii kwa sababu Mungu amekuacha, hakupendi ama amekukatataa.

Yeremia 31:3-7

Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.
 Mara ya pili nitakujenga, nawe utajengwa, Ee bikira wa Israeli mara ya pili utapambwa kwa matari yako, nawe utatokea katika michezo yao wanaofurahi. Mara ya pili utapanda mizabibu juu ya milima ya Samaria; wapanzi watapanda, nao watayafurahia matunda yake.
Maana kutakuwa siku moja, ambayo walinzi watalia juu ya vilima vya Efraimu, Inukeni, tukaende Sayuni, kwa Bwana, Mungu wetu.
Maana Bwana asema hivi, Mwimbieni Yakobo kwa furaha, mkampigie kelele mkuu wa mataifa, tangazeni, sifuni, mkaseme, Ee Bwana, uwaokoe watu wako, mabaki ya Israeli.

 

Msatari wa 8 anazungumza kuhusu kurejeshwa kwao, anaongelea habari za watu mbalimbali kurejea.

Hiki ni kipengele cha ajabu sana, ya kwamba Mungu anazungumza na wana wa Israeli ya kuwa amewapenda kwa upendo wa milele, yaani upendo usiokuwa na mwisho, upendo usio na mipaka, upendo usiofungwa na muda wala umbali, upendo usiofungamana na misimu mbalimbali waliyokuwa wakiipitia.

Katikati ya utumwa na mateso ya watu waliokuwa wamewachukuwa mateka Mungu analidhiirisha pendo lake, na kuwapa tena ahadi ya kupanda mizabibu ama kurejea kwa uchumi na maisha ya neema kwenye maisha yao, anatanguliza neno kuwa upendo wake ni wa milele!

Sijui unapitia mahali pagumu kiasi gani ila ninachofahamu ni kwamba upendo ama pendo la Mungu juu yako ni la milele, halikuwahi kupunguka au kukuacha kwa sababu ya ugumu ulionao. Inawezekana marafiki wamekuacha, yamkini hata mume ama mke amekaa mbali nawe, ila fahamu kuwa Mungu hajakuacha.

Wakati Yusufu akiwa katika shimo huko nako pendo la Mungu lilimfuata, alipoingia kwa Potifa na kuishi kama mtumwa huko nako lilikuwa pamoja naye; Mwanzo 39: Bwana akawa pamoja na Yusufu, naye akasitawi; naye alikuwa katika nyumba ya bwana wake, yule Mmisri.

Ndugu zake walimuuza sawa, ila katikati ya machungu ya kuuzwa, na kufanywa mtumwa Bwana Mungu wetu hakumuacha, alikuwa pamoja naye, baba yake alimpenda sana ila hakuweza kuwa pamoja naye, alithania kuwa mwana wake amefariki.

Kama hapo haitoshi alisingiziwa na kutupwa jela, huko nako Bwana alikuwa pamoja naye!

Yamkini ninazungumza na mtu ambaye anasema moyoni mwake lakini Mwalimu Oscar nimepakaziwa, wewe fahamu kuwa Bwana yu pamoja nawe, alikuwa pamoja na kijana huyu wa Yakobo, uwe na hakika yu nawe pia, ni kweli uko jela ya uchumi, uko jela ya ndoa yako, uko jela ya utumishi wako, na ukitazama karibia kila mtu ni kama vile amekususa ama kukuwekea ukuta, wewe usife moyo la muhimu fahamu kuwa Bwana yu pamoja nawe maana pendo lake halifungamani na ubinadamu, halina umbali wala mipaka, linapenya hadi gerezani, upendo wake u nawe hata katika wakati huo mgumu.

Haijalishi marafiki zako hawapokei simu, wapo mbali nawe ila wewe fahamu kuwa Bwana yu pamoja nawe.

19-20 Ikawa bwana wake aliposikia maneno ya mkewe aliyomwambia, akisema, Mtumwa wako amenitendea mambo kama haya, hasira yake ikawaka. Bwana wake akamtwaa Yusufu, akamtia gerezani, mahali walipofungwa wafungwa wa mfalme, naye akawamo humo gerezani.

 

Inawezekana ni fika na bayana kuwa na wewe mwangalizi wako amesikia maneno waliyokusingizia, askofu wako bila uchunguzi wa kina amewasikiliza, ama ni mchungaji wako na umejikuta upo mahali pabaya kazini kutokana na bosi ama mwajiri wako kuwasikiliza wafanyakazi wengine, na bila udadisi ukajikuta unahukumiwa! Sauti yako ya kujitetea; ni kama vile umezibwa kinywa, mimi ni kwambie tu ya kuwa Bwana yu Pamoja nawe!


2-23 Lakini Bwana akawa pamoja na Yusufu, akamfadhili, akampa kibali machoni pa mkuu wa gereza.

 Mkuu wa gereza akawatia mkononi mwa Yusufu watu wote waliofungwa, waliomo gerezani; na yote yaliyofanyika humo ndiye aliyeyafanya.
 Wala mkuu wa gereza hakuangalia neno lililoko mkononi mwa Yusufu; kwa kuwa Bwana alikuwa pamoja naye. Bwana akayafanikisha yote aliyoyafanya.

 Upendo wa Mungu haukuzuiliwa na makomeo ya jela, ni kweli ndugu na jamaa huweza kuzuiliwa na milango migumu na mizito ila sio kwa Mungu wetu! Walipomfunga Petro upendo wa wapendwa ulizuiliwa na uzio wa gereza, nao kwa hofu wakajikuta wanaminywa zaidi katika kudhiirisha pendo lao, wakajifungia na kumuombea, nawe wapo wanaoogopa kukufuata ili wasije kuonekana kuwa wapo pamoja nawe, japo wanjua fika hakutenda kaosa, ila kw ahofu ya wakuu wamekkaaa mbali nawe, maadamu wanakuombea, wewe usiwahesabu kama maadui, fahamu tu pendo la Mungu linapenya hadi gerezani, ndiposa Petro akatolewa kwa mkono wa Bwana akitumia malaika zake.

 Paulo na Sila waliligundua hili, ndio maana katikati ya kifungo walichapa pambio na kuomba, sijui wewe! Nikutie moyo, kuwa katikati ya hiyo dhiki na adha, wewe chapa zako pambio, imba umeuona mkono wa Bwana, hapo utamfanya Mungu kujifunua kwa haraka na ampema zaidi.

 Fahamu sana kuwa pendo la Mungu ni la milele! Inawezekana kuwa wakati huu uliomaliza nao shule wana maisha mazuri, ndugu zako wanachanua kimaisha, lakini kwako wewe hali ni ngumu kupita maelezo!

Usife moyo, wewe mtazame Yesu.

Maana wakati Yusufu anatupwa kwenye shimo, yupo utumwani, na hatamae jela, ndugu zake waliendelea kusherekea na kufurahi, wakati yeye yu mbali na wazazi wake, nduguze waliendelea kuishi maisha ya furaha pamoja nao.

 Epuka kujiuliza maswali ya kwa nini mimi! Maana Yusufu ili aweze kubeba jukumu lilopo mbele ni lazima andaliwe kitofauti. Inawezekana na wewe ulioanza nao huduma wameonyesha kuchanua kuliko wewe, wameonyesha kupanuka kuliko huduma yako, uliomaliza nao darasa moja kwenye chuo cha biblia wana mana mafanikio makubwa kukupita, nawe ukitazama unaumia maana ulikuwa nayo sema vita fulani vya kuonewa vimekuvuta shati, na kuna mahali umekwama!

 

Usife moyo, fahamu tu kuwa pendo la Mungu halina msimu, maana wakati mafanikio yako yakiwa katika msimu wa maandalizi, na wengine wakisherekea, uwe na hakika kuwa upendo wa Mungu ulipo juu ya wanaocheka ndio ulipo ju yako wewe unayelia leo, maana unakuandaa kufurahi siku moja.

 kama hujaokoka na umeusoma ujumbe huu na kufahamu jinsi pendo la Kristo lilovyokubwa kwako, na unataka kumpa Yesu maisha yako, basi nikupongeze na hongera kwa hatua hiyo, nakutaka kufuatisha nami maneno haya ya sala hii ya toba kw aimnai, na badaa ya hapo utakuwa umeokoka:

 sema, MUNGU BABA, NINAKUPENDA, NINAKUTAKA UINGIA NDANI YANGU, ILI UFANYIKE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINAAMINI KUWA YESU NI MUNGU, ALIKUFA NA KUFUFUKA, TAFADHALI FUTA JINA LANGU KWENYe KITABU CHA HUKUMU, NA ULIANDIKE SASA KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Amen.

 Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, kwa maombezi, ushauri na mahuburi au maswali wasiliana nasi kwa Simu namba: +255759859287, Emaili: ukombozigospel@gmail.com au tembelea www.ukombozigospel.blogspot.com

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni