Jumamosi, 27 Februari 2021

Kitabu chetu cha: MAMBO MUHIMU YA KUFANYA AU KUZINGATIA KUNAPOKUWA NA ADHABU YA KIUNGU INYOIJUMUISHA ENEO ULILOPO AU JAMII.

Na Mwalimu Oscar Samba 

Neno Kiungu huwakilisha kutoka kwa Mungu au Shetani, ujumbe huu ni sehemu ya hiki kitabu chenye mada na pwenti kadhaa, ila hapa nimezicha,bua mbili tu; #Corona #Covd19 #Tsunam #Majanga  #Kimbunga #magonjwayamlipuko  #tanzania

1. Lifanye Eneo Unloishi kuwa Ghosheni yako. 2. Ijue na Uitumie Damu ya Yesu ya Pasaka; 3. Mulize Mungu kama Daudi; 4. Litengenezee Kusudi la Mungu Kisafina kama Musa, ama Nuhu; 5. Jifunze Jambo kwa Mke wa Lutu;

6. Sadaka kama Ulinzi; 7. Sadaka kama Sehemu ya Rehema, Mfano ile ya Daudi kipindi cha adhabu ya Tauni, 8. Taka Kujua pigo Hilo au Adhabu hiyo Inataka nini ili Ujisalimishe kwa Bwana, Mfano Rahabu, na Epuka kosa la Farao.

 9. Yajue na Uyaombe Maombi ya Musa ya Kulitengeneza Boma, 10. Mtafute na Umuondoe Akani, 11. Jitenge na Kusanyiko, au Kiunganishi cha Kusanyiko ama Waadhibiwa, ondoa jina lako kwenye watu wanaotakiwa kupewa hiyo Adhabu kwa Damu ya Yesu.

 

12. Tafuta Maelekezo Maalumu ya Mungu juu yako, kama Isaka dhidi ya Janga la Njaa na Wazazi wa Yesu. 13. Unapoisikia Hofu Usiipuzie, Taaka Kujua ni Aina gani ya Hofu ala Uikabili..

 

14. Tafuta Kukumbuka kama Mungu Aliwahi Kukujuza hapo Awali na Hukumsikia Vyema au Hukumbuki. (Amosi 3:7 Hakika Bwana MUNGU hatafanya neno lolote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.) Sijui sana ni kwa nini kanisa la leo lina uzito kwenye hili,  nijualo ni kwamba uwezo wa kusoma alama za nyakati, au majira umekuwa ni adimu sana kwa kizazi cha leo! Nafahamu kuwa hali ya kupuzia ndoto, kutokutambua jinsi Mungu anavyoongea, na mafundisho manyonge kuhusu uhusiano wetu na Roho Mtakatifu ni miongoni mwa sababu ambatanishi.

 

Kama kuna mahali Shetani amefanikiwa leo ni kuondoa, ama kuzimisha kama sio kufifisha karama ya unabii, na huduma ya nabii, pamoja na neno la maarifa!

 

Na anatumia njia kuu kama mbili hivi, moja ni kuhakikisha kanisa linapoteza imani na manabii au wanaotumiwa na karama hizi, kwa kujiwekekea manabii wa uongo, ili kuwakatisha watu tamaa na kuwafanya wa waone hata wale wa Mungu nao ni kama hao wengine!

Pili analitumia kanisa lenyewe, kwa kufikia hatua ya kupinga, na kukataa, na kuzimisha huduma na karama hizi, na sababu zao ni nyingi ila hazina hoja timilifu kibiblia, maana kama kuna wimbi la mafundisho na huduma potofu, suluhu bado sio kuzima na kukataa ile ya kweli, bali wafunze watu namna ya kutambua kweli na uongo. Mchele ukiwa na chuya, dawa sio kukataza nyumbani wasipike tena mchele bali ni kuwafunza kuzitoa, na kama ni mcahanga basi watake kuwa makini kuchambua maana mawe mengine ni yale meupe, kwa hiyo yanafanana kwa karibu na mchele, lakini pia kama ni vigumu, wafunze kupembua au kuuchambua wakati wanauosha na maji, njia ambayo ni salama zaidi.

 

Maharage yakiwa na mchanga au mawe, hayamwagwi, bali huchambuliwa! Na wewe ukiona dosari katika hudumka na karama hizi, hakikisha unazikabili!

 

Maandiki yako wazi kabisa katika biblia kuwa tunatakiwa kujifunza na kuhakikisha kuwa tunasoma alama za nyakati, au tunajua mabadiliko kwa kuzitambua dalili zake, mkulima asipojua kusoma uso wa nchi, hakika atakuwa akipitwa na maamuzi dhabiti katika majira husika, wakati wengine wanandaa mashamba yeye atashindwa kufanya hivyo, ama atajikuta akiwacheka wengine, maana kwa wengine ili walime ni hadi waone mvua imenyesha bila kujua kwa kufanya hivyo ni gharama zaidi maana aridhi husumbua kwani kulima kwenye tope ni kugumu zaidi! Pia ipo hatari ya kushindwa kufanya vyema maana kuna uwezekano wa kunyeshewa! Kuna kuchelewa pia kupanda, maana wakati wa kuotesha wewe ndo kwanza unakwatua udongo.

 Hosea hufananisha jambo la kuukwatua udongo sawa na kuomba, maana husema tumtafute Mungu, akitangulia na kututaka kuukwatua udongo wa mashamba yetu! Kiroho kuna vipindi kama hivi! Kuna kipindi cha kumtafuta Mungu kabla ya adahabu haijaja! Ukichelewa gharama yake ni kubwa sana! Unaweza kujikuta umeshapoteza ndugu wengi, ama hasara kubwa imeshatokea!

 Mama yangu wakati ugonjwa huu unaingia au umeanza kushamiri, ndipo aliponitaarifu kuhusu ndoto aliyowahi kuiota! Japo hakuwa ameielewa kipindi hicho! Ila nataka ufahamu kuwa Mungu alikuwa ameshaongea naye!

 Elimu na ufahamu wa kuzijua nyakati ni muhimu sana, na ni kiroho kabisa, jihakikishie kwa watu hawa, ambapo hata leo makanisani wapo, na kama hawajafungwa