Jumamosi, 27 Aprili 2019

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA.

Mahali: TAG Ushiri Rombo: Tarehe 28:2:2019. Na Mwalimu Oscar Samba.
Aliyeshika kipaza sauti (kushoto) ni mama mchungaji wa kania hili jia ni Paumelina B. Senkondo, na wengineo ni wanawake wakiimba shairi.

Mwalimu Oscar Samba

Washirika

Mwanzo 2:18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
Mwanamke ni msaidizi, andiko hilo lipo kabla ya dhambi kuingia ulimwenguni, hakukuwa na mfumo wa kanisa ama kuabudu kama leo, au kama baada ya dhambi, kusudio la ndoa, au familia ni ili liwe kanisa, yaani tuliumbwa kwa ajili ya ibada !
Kwa hiyo, kanisa, lina mukutadha wa ndoa, kwa hiyo, dhima ya mwanamke kindoa au kifamilia, ina mashabihiano na ile ya kikanisa !

Waefeso 5:23 Kwa maana

Jipatie maandiko mbali mbali ya Biblia kuhusu Damu ya Yesu, Shukurani, Ahadi za Mungu na kadhalika




KUNA MTU MMOJA MWENYE KESI AMENIOMBA NIMFUNZE NAMNA YA KUOMBA, NAMI NAKUMEGEA:

1. Omba Rehema, tubu bila kujihesabia haki, tumia Danieli 9, pia Warumi 3:25 ukiitaka Damu ya Yesu ifanye rehema, na Mathayo 26:28 kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.

2. Ifute hiyo Kesi kwa Damu ya Yesu, Waebr 9:22, futa hizo nakala/kopy za kesi ama mashitaka.

3. Gongomelea hzo hati za Mashitaka Msalabani, Wakolosai 2:14 akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;

Upole wako na ujulikane na kila mtu !

Bwana Yesu asifiwe,
Kuna Mtu aliniambia niseme Neno, nami nilisema ! Sasa nakumegea nilichomfunza !

    Upole ni Tunda la Roho, ambalo linadhima ya unyenyekevu ndani yake.

  Kazi na faida moja wapo ya upole ni kukupa majibu ya busara hata katika nyakati ngumu, haijalishi ni zenye kuuthi au kujeruhi, utajifunza kwa Yesu, na Yeremia pia, ila ona hapa;Mithali 15:1 Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.

Upole unakuwezesha kuepukana na mitego ya adui, inauonuia kukuyumbisha, ama kukukwamisha, au kukuvurugia masiha, maana upole umebeba unyenyekevu ndani yake ! Yeremia 11:19 Lakini mimi nalikuwa kama mwana-kondoo mpole, achukuliwaye kwenda kuchinjwa; wala sikujua ya kuwa wamefanya mashauri kinyume changu, wakisema, Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake, na tumkatilie mbali atoke katika nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.
Upole huu ndio uliomvusha Yesu ! Isaya 53:7 Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake.

Kuna wakati adui ananuia kabisa kukukwamisha mahali kwa kuibua changamoto, ama vikwazo, ila ukiwa nao huo upole, utanyamaza kimywa na adui anakosa mwanya wa kukudhuru au kukuangamiza !
Sasa sababu ya maandiko kututaka upole wetu ujulikane na kila mtu ni ili kuwa na maisha ambayo Tunda hili litakuwa active au hai, ili kutuwezesha kunufaika nalo, usisahau kuwa anamalizia nakusema Bwan yu karibu, ikiwa na maana kuwa unapokaribia mafanikio kama Yesu, au kukutana na majibu yako, adui haachi kuleta vikwazo, iwe kwa ndugu, marafiki, muajiri wako, wafanyakazi wenzako,walezi na kadhalika akinui kukuzuilia kukutana na Bwana, sasa upole utakuvusha kama Yesu na Yeremia ! Ona haya maandiko :
Anaanza na kututaka tufurai, akiwa na maana upole umebeba ama hukuwezesha kufurahi, maana mazingira ya huzuni, na uchungu hayawezi kuzaliwa penye upole ! Alafu amani huyoke, kumbuja amani pia ni Tunda la Roho !, pamoja na Furaha ! Sasa ukipata upole, hayo mengine ni rahisi sana kuchipuza !
Wafilipi 4:4 Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
:5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.

Katika somo hilo, tuna au una jigunza nini hapo ?

Natumai somo kuu, ni kwamba ukiwa mahali pagumu, huna majibu ya maswali yako, mazingira yanakuzalia ama hukutishia kukuzalia huzuni, au kukunyima amani, na furaha, masononeko na ukiwa zinakunyemelea! Basi upole ni dawa ! Ambapo utazaa Amani, na Furaha ! By Mwalimu Oscar Samba. Simu: +255759859287

NAMNA YA KUOMBEA ENEO, JAMII AU MTU FULANI.

Chimbuko la ujumbe huu ni kiu ya Mwanafunzi wangu mmoja aliyeniuliza maswali kadhaa majira haya, nami kumjibu, nami pia kupokea imizo la ndani yangu, kukumegea ama kukudodoselea majibu hayo, ila kwanza tazama kiu yake;
"Bwana Yesu Asifiwe Pastor
Kheri ya Pasaka.

Naomba mwongozo
Kama mtu unaguswa kuomba kwa ajili ya kumuombea au kuombea
1. Mtu binafsi analiyetakwa na nguvu za giza na yeye peke yake hawezi kujikomboa hatua zipi unapitia  ( Yaani mwongozo wa maombi kwa mtu huyu inakuwaje)

2. Kama unataka kuomba kwa ajili ya familia ulikozaliwa kwa ajili ya kuwakomboa uzao wa tumbo la mama yako ili Mungu aingilie kati unaendaj