Ijumaa, 29 Desemba 2023

Mwalimu Oscar Samba FIKRA SAHIHI KATIKA SHAMBA LA BWANA Kitabu cha Kiroho Kipakuwe Bure free download

Mwalimu Oscar Samba FIKRA SAHIHI KATIKA SHAMBA LA BWANA Kitabu cha Kiroho Kipakuwe Bure free download 




Sabato Maana Yake ni Nini ? MAANA YA SABATO KIBIBLIA Ielewe Sabato ya Kweli

 


Na Mwl Oscar Samba

#FaidayaJaribu: #Usiogope

Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha MAANA YA UZIMA, NA UZIMA WA MILELE. Pwenti ya Pumziko Kuu.

Kwenye Kipengele cha Taswira ya Uzima wa Milele

Pumziko Kuu; Yaani Sabato Kukuu. Watu wengi hawajui ya kuwa Sabato maana yake ni pumziko katika kilele cha uzima wa milele yaani wakati huu hapa ulimwenguni kwa kuokoka, (kupumzika katika Kristo Yesu kama mtua mizigo ya dhambi na kila mateso.) Na pili kama sehemu ya kupumzika kutoka katika dunia iliyopo chini ya umiliki wa Shetani kama mungu wa dunia hii, na pamoja na dunia yenye pigo la laana la kosa la Adamu na Hawa. 

Unapookoka ni umeingia katika Sabato. Kwa hiyo, msabato halisi ni mtu aliyeokoka. Kama hujaokoka wewe sio Msabato, maana bado upo chini ya utumwa wa Shetani. Wokovu unakupa pumziko. Kanuni na sheria zile za Agano la Kale hususani sabato na taratibu zake zote, zilinuia kutufikisha hapa kwenye wokovu na hatimaye katika Sabato kamilifu ile ya Mbingu Mpya na Nchi Mpya.

Ndiposa Yesu alipokuja, mkazo wa sheria za kisabato ule wa Agano la Kale haukwepo tena. Maana amekuja Sabato Mwenyewe. Ndio maana alijibu hivi; Marko 2:27 Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato. 28 Basi Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia. ( Kwa hiyo kama utaendelea kusingizia kumsikiliza mjumbe wa Sabato Musa na kumuacha Bwana wa Sabato; basi utakuwa umekwama sana.

Mathayo 12:5 Wala hamkusoma katika torati, kwamba siku ya sabato makuhani hekaluni huinajisi sabato wasipate hatia? 6 Lakini nawaambieni, kwamba hapa yupo aliye mkuu kuliko hekalu.

7 Lakini kama mngalijua maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka, msingaliwalaumu wasio na hatia. 8 Kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.

Tuone kisa kingine:

Jumapili, 17 Septemba 2023

Kila Jaribu Lina Mlango wa Kutokea JIPE MOYO

 

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu:

1 Wakorintho 10:9 Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

:11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

:12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.

:13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.

http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL

Nikutakie Siku Njema

Jumamosi, 16 Septemba 2023

Neno la Leo #Nenola Leo #NenolaMungu #NenolaBiblia #Ujumbe waSiku

 

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu:

Waebrania 4:2 Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu halikuchanganyika na imani ndani yao waliosikia.

:6 Basi, kwa kuwa neno hili limebaki kwamba wako watu watakaoingia humo, na wale waliohubiriwa habari ile zamani walikosa kuingia kwa sababu ya kuasi kwao,..

:7 aweka tena siku fulani, akisema katika Daudi baada ya muda mwingi namna hii, Leo; kama ilivyonenwa tangu zamani, Leo,kama mtaisikia sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu.

Usiufanye Mgumu Moyo Wako..(Safari ya Wokovu Ni Kila Siku) Hakikisha Unafanya Matengenezo Kila Uonapo Dosari Maishani Mwako..ikihubiriwa Injili Usiikatae, na Usiseme Wananisema... Shinda Vikwazo Ili Uingie Rahani Mwake Yesu..

http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL

Nikutakie Siku Njema

Ijumaa, 8 Septemba 2023

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar ) #FaidayaJaribu: Waebrania 5 inatupa Kufahamu Umuhimu wa Aina ya Chakula cha Kiroho

 

Waebrania 5:12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu.

:13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga.


:14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.

Kama Nilivyokuhaidia Jana, ni Kwamba Aina ya Chakula Unachokula Ndicho Kinachoamuwa kama Uendelee kuwa Mwanafunzi au Mwalimu. Na kwa mujibu wa Jana Washindi Wana Aina Yao ya Vyakula, (Mana Iliyofichwa.)

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Kwa Maombi +255759859287 

Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/Mafun

Alhamisi, 7 Septemba 2023

Neno la Leo: MANA ILIYOFICHWA KWA ASHINDAYE

 

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu:

Ufunuo wa Yohana 2:17 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea.

Kuna aina ya Viwango vya Kiroho Vinavyoamua Upewe Chakula Gani cha Kiroho, Kutokana na Kushinda Kwako Majaribu..Kwa Wahubiri; Ukihitaji Kuwa na Mafundisho Tofauti yasiyoyakawaida, Huna Budi Kushinda Vikwazo ili Upewe Mana Isiyo ya Viwango vya Kawaida. (Natumai Kesho Utanielewa Zaidi..)

http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL

Nikutakie Siku Njema

Jumanne, 29 Agosti 2023

Faida ya Jaribu na Dhima ya Utoaji au Kumtunza Mtumishi wa Mungu ( soma sura yote ya Wafilipi 4 )


 Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )

#FaidayaJaribu:

Wafilipi 4:8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.

:9 Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea, na kuyasikia na kuyaona kwangu, yatendeni hayo; na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.

:10 Nalifurahi sana katika Bwana, kwa kuwa sasa mwisho mmehuisha tena fikira zenu kwa ajili yangu, kama vile mlivyokuwa mkinifikiri hali yangu lakini hamkupata nafasi.


:19 Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.

(Baraka Hizi za Paulo Zinakuja Baada ya Hawa Watu Kusimama Kwenye Nafasi Yao)

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Jumanne, 22 Agosti 2023

Faida ya Majaribu au Mapito ( Mtazame Yesu )


 Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )








 Faida ya Jaribu :

Waebrania 12:3 Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.


:4 Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi;


Tunapewa Nasaha za Kumtazama Yesu Aliyestahimili Mambo Magumu kwa Ajili Yetu, Hata Akautoa Uhai wake..Mimi Na wewe Hatujafikia Kipimo Hicho cha Kuimwaga Damu...Nasi Hatuna Budi Kuyastahimili kama Yeye Alivyofanya kwa Ajili Yetu..Nasi Tufanye kwa Ajili Yake..


http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD


Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk


Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Kwa Maombi +255759859287 


Nikutakie Siku Njema

Jumatano, 16 Agosti 2023

SEMINA KKKT MWANZA 2016. NA MWL CHRISTOPHER MWAKASEGE KOSA LA SABA. 7.YESU AKIAMUA KUTOITULIZA DHORUBA USIMKASIRIKIE BALI ENDELEA KUOMBA NA KUFUATA MAELEKEZO YAKE.

 7⃣SOMO:JIEPUSHE NA MAKOSA YAFUATAYO UKITAKA KUVUKA KWA USHINDI MWAKA HUU


Hili ni eneo ambalo unahitaji kulielewa sana kwa sababu si kila mtu atapita mahali ambako pako shwari.

Kila mtu anapita kwenye dhoruba yake na si kila dhoruba ni mbaya.

Warumi 8:28.
28 Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.

Simama kwenye kusudi la Mungu shetani hawezi kukuzamisha atajaribu kila namna lakini atashangaa ukisimama kwa upya.

Kuna matatizo mengine Mungu anayaruhusu kwa ajili ya kukujengea msuli wako kwa ajili ya mambo yaliyopo mbele yako.

Yesu aliomba “kikombe hiki kiniepuke” alikuwa anajua kabisa angeweza kuamuru jeshi la malaika kumtetea na kumpigania, angeweza kuwatoroka, lakini Biblia inasema mbigu zilinyamaza kwa sababu Mungu hakuwa na mpango wa kumwondolea msalaba,kwa sababu msalaba ungeondolewa hakuna mahala tungekombolewa.

Mungu akinyamaza usikasirike, endelea tu kuomba kwa sababu inawezekana ni jambo bado majira yake.

Tatizo tunambea katika majira ambayo tunahisi tunapopata matatizo tunahisi tumepungukiwa imani lakini kumbe hatujajua ni sehemu ya safari au sehemu ya maisha.

Hakuna mtu hapa Duniani atayekuambia matatizo ni mazuri. Lakini tunapotembea hapa Duniani hakuna mtu yeyote ambaye hatakutana na matatizo, kwa hiyo usijaribu kuishi na mawazo kwamba hautakutana na matatizo.


 Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )


Yakobo 5:10 Ndugu, watwaeni manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa uvumilivu.

:11 Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287

Nikutakie Siku Njema

Jumanne, 15 Agosti 2023

BWANA ANA HAJA NAWE


Na Mwl Oscar Samba 

Duniani hatukuja kwa bahati mbaya, lipo kusudio la kuumbwa kwetu. Kama vile mtu anavyomuajiri mfanyakazi na kisha kuwa na malengo naye katika eneo analohitaji asaidiwe kazi, ndivyo na Mungu wetu alivyotuumba akiwa na kusudio maalumu la uumbaji wake kwetu.

Nimfano wa mtu aliyenunua chombo chake cha usafiri! Hapana shaka huyu mtu huwa na malengo katika matumizi fulani ya hicho chombo. Mimi na wewe ni chombo cha Mungu. Mungu hakutuumba kwa bahati mbaya, wala hukuzaliwa kwa bahati yoyote kama vile wengineo huweza kuzania. Kila mtu amezaliwa kwa kusudi la Mungu lililo kamili kabisa.

Wasomaji wa kitabu kile cha Zekaria wanajuwa kuna unabii ulitolewa kuhusu punda ambaye Yesu alikuja kumtumia miaka kadhaa mbele katika Agano Jipya. Najuwa kuna jinsi jambo kama hili huweza kuonekana kuwa ni dogo, lakini lilishatabiriwa au kuangaziwa toka miaka mingi yenye oroda ya mamia ya miaka ama mlolongo wa karne nyingi.

Usipojuwa unaweza kuliona hili tukio kuwa ni la kawaida ila kiuhalisia lilishaandaliwa; Marko 11:2 akawaambia, Nendeni mpaka kile kijiji kinachowakabili; na katika kuingia ndani yake, mara mtaona mwana-punda amefungwa, asiyepandwa na mtu bado; mfungueni, kamleteni.

3 Na mtu akiwaambia, Mbona mnafanya hivi? Semeni, Bwana anamhitaji na mara atamrudisha tena hapa.

Luka 19.33 Na walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe waliwaambia, Mbona mnamfungua mwana-punda? 34 Wakasema, Bwana ana haja naye.

Sasa jaribu kufikiia kama punda anaandaliwa hivi kwa ajili ya tuko la siku moja tu! Je, wewe sii Zaidi? Ambaye unatarajiwa kutumika miaka na miaka! 

Jumatano, 9 Agosti 2023

Neno la Leo, Kufurahia Pito au Majatibu, kwa Ajili ya Injili au Kristo

 

Neno la Leo (Nasaha za Mwl Oscar)

Mathayo 5:11 Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.

:12 Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.

*Kesho nitakupa Mfano wa Watu Waliofurahia Mateso na Dhiki ikiwemo Kupigwa kwa Ajili ya Yesu au Injili..Unapaswa Kufurahia Kufukuzwa Kazi, Kuonewa na Hata Kubaguliwa ama Kuchukiwa kwa Ajili tu Wewe Umeokoka...Kila Dhaa kwa Ajili ya Imani Yako, Kwako Lifurahie Maana Malipo Yake ni Mkaubwa Mbinguni... Maana Bila Hayo Taji Yako ni Ndogo* ...

www.ukombozigospel.blogspot.com

Jiunge na Kundi Letu la Telegram

https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Kwa Maombi: +255759859287

Uwe na Siku Njema


Jumatano, 2 Agosti 2023

Neno la Leo, Amani na Maendeleo

 

Neno la Leo (Nasaha za Mwalimu Oscar)

Maombolezo 3:17 Umeniweka nafsi yangu mbali na amani; Nikasahau kufanikiwa.

*Kumbe Amani Ikitoweka na Mafanikio nayo Hupotea au Huwa Adimu..! Kwa hiyo; Hakikisha Amani Haipotei Moyoni Mwako ili Kulinda au Kuchunga na Kudumisha Mafanikio...Tazama Toka Uchungu, Hasira na Msongo wa Mawazo Vilipokukabili..Utakuta na Kasi ya Mafanikio Imepungua na Hata Mambo ya Msingi km Ujenzi na Biashara Kukwama* ..

www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi Letu la Telegram

https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Nikutakie Siku Njema


Alhamisi, 27 Julai 2023

Neno la Leo, Amani Moyoni

 

Neno la Leo

Zaburi 119:165 Wana amani nyingi waipendao sheria yako, Wala hawana la kuwakwaza.

*Jifunze Kupendezwa na Sheria au Neno au Maelekezo Yenye Kukutaka Kutokutenda.. ama Kutenda yaliyo ya Mungu. Ukifanya hivyo ndipo Amani Yake Itakukalia...Kwa hiyo; Ukiona Unafanya Jambo na huna Amani, jitazame km Moyoni Mwako Umependezwa nayo..*

www.ukombozigospel.blogspot.com

Nikitakie Siku Yenye Baraka na Amani Nafsini..


Jumanne, 25 Julai 2023

Neno la Leo AMANI NA FURAHA KATIKA MAGUMU Zaburi 4:7, 8.

 

Neno la Leo

Zaburi 4:7 Umenitia furaha moyoni mwangu, Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai.

:8 Katika *amani* nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama.

*Katika Yote Hakikisha Una Amanj ya Kristo, Usitazame wingi wa Vita na ukubwa wa Maadui, bali Tazama Amani ya Kristo ndani yako..ilinde hiyo..Amani yake ni Ishara ya Uwepo wake...Kujibizana na Maadui na Manung'uniko huondoa Amani.. Amani Huleta Utulivu..*

Uwe na Siku Njema


Jumamosi, 15 Julai 2023

Neno la Leo Ujira waKahaba au Fedhaa ya Sadaka Isiyo Halali

 Neno la LEO


Kumbukumbu la Torati 23:18 Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili.


 *Sadaka Ambayo Mapato Yake Siyo Halali Haikubaliki Mbele za BWANA na ni Machukizo*


Nikutakie Umakini ktk Utoaji


Pia na Siku Njema


Alhamisi, 20 Aprili 2023

Jana tulianza Mkutano wetu hapa KWA TOKORA katika Kijiji cha MACHAME ALENI Keni Rombo Kilimanjaro Tanzania

 Umenza tarehe 19 hadi 23 (jumatano hadi jumapili) 2023


Ujumbe: UFALME WA MBINGUNI UMEKARBIA. Mathayo 3:2


Hivi Ndivyo Tulivyoitimisha Mkutano wa Injili Katika Zahanati ya Mokala Rombo Klimamnjaro Tarehe 12 hadi 16 Aprili Mwaka 2023

 Ujumbe wa Mkutano huu ulikuwa ni UPENDO WA MUNGU KWA MWANADAMU 

Tukuongozwa na Andiko la Yohana 3:16.

Tazama Baadhi ya Picha za Matukio

Picha hii na Zifanazo na hii ni Watu Waliotoka kwa Ajili ya Kuokoka na Maombezi




Picha hii na hiyo tangulizi hapo juu ni Waimbaji wakiimba Wimbo wa Kichaga na Kucheza "Iriingi".

Naomba NiRepost NDOA NI ZAIDI YA UPENDO

Naomba NiRepost

#VIJANA_NISIKILIZENI_Haya_Nayo_Ni_Maneno_ya_Mwenye_Hekima


Moyo Unaweza Kumpenda Mtu Bila Kuwa na Sababu Yoyote ya Msingi ila Usikubali Kuoana na Mtu Asiyetosheleza Vigezo Vya Ndoa kwa Viwango Fulani.



Moyo wa mwanadamu kuna muda unavutiwa na mtu bila hata kukupa sababu zenye mashiko kwanini umempenda. Utamsikia mtu akisema basi nimepanda tu! Ni kweli ni jambo jema, na hatuwezi kuweka sababu kwa kila mtu au maamuzi ya moyo kupenda.

Ndiposa wengine wakasema mapenzi ni upofu, ikiwa na maana kwamba kuna mambo ya msingi mtu anaweza  kuya_overloock ama kuyapuuza ifikapo swala la kupenda. Hapa napo sina shinda napo.


Ila msemo huu ndio unaonipa shida; kipendacho roho hula nyama mbichi! Ndugu yangu, nyama mbichi huvimbisha matumbo, huleta kuharisha sanjari na hatari ya magonjwa ya minyoo.

Jumatano, 22 Februari 2023

Fahamu ni Sababu za Mungu Kukutaka Uendelee Kuvumilia hilo Pito au Jaribu

 

Na Mwalimu Oscar Samba
Ujumbe huu ni Sehemu ya #Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA. Tunaendelea kidogo plae tulipoishia katika Makala iliyopita, kisha ttutatazama jambo la Kwanza; Karibu:

Ikifika mahali ukiona msisitizo uliopo ndani yako sio kumtwisha tu Mungu mzigo wako, sio Mungu tu kukutia nguvu. Bali swali lako ni kwamba sawa nitavumilia, ila Mungu atanijibu lini? Uwe na hakika kuwa unahitaji msaada mkubwa zaidi.


Maana kuna mambo mawili hapo. Mosi ni la kuchoka na pili ni la kuhoji uaminifu wa Mungu kwamo?

Kwamba huna shaka, hata sasa ukimuita akutie nguvu anweza, ila hoja ni kamba huu ni mwaka wa tano sasa, kumi au miaka naho inaenda, unakaribia 40 na hata 50 sasa ila bado hajakutokea. Ndio maana ukinielewa hapa hutaacha kuyaelewa maandiknya Zabuti kuhusu uaminifu. MUNGUkuna.mahali unasoma na unaona jinsi mtunga Zabuti anavyopitia sehemu ngumu, kisha anataja uaminifu wa Mungu.

KANUNI
1. Fahamu ni Kwanini Mungu Anataka Bado Uendelee Kuubeba au Uendelee Kupitia. Waliowahi kusoma kitabu kile cha Isaya 55 utabaini kuwa watu wale kuna namna walikuwa wamepishana na mipango ya Mungu maishani mwao. Ndio maana Mungu anafika hatua ya kuwaambia kuwa mawazo yenu sio mawazo yangu, wala njia zenu sio njia zangu. Anawapa na kipimo husika, kwamba kama vile mbingu zilivyo mbali na aridhi; ndivyo mimi nanyi tunavyopishana.

Najua unajua kuwa Mungu ana akili kuliko wewe. Ufahamu wake ni mkubwa kukuzidi. (Ikupe kujiuliza kwa nini kakuacha.) Na kubwa zaidi ni kwamba anakupenda kuliko unavyo mpenda. Na kile kitabu chetu cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO LAKO kinafunza kiunagaubaga kuhusu kusudi la Mungu kukupitisha hapo.

Jumamosi, 18 Februari 2023

NENO LA LEO Zaburi 90:12

 Neno la Leo


Zaburi 90:12 Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima.



‭‭Psalms‬ ‭90:12‬ ‭NIV‬‬

[12] Teach us to number our days, that we may gain a heart of wisdom.


Yawe ni Maombi yako, Omba Hekima; Bali Omba Akugundishe Kuzihesabu Siku ili Uweze Kuwa na hiyo Hekima


Uvumilivu na Kuwa Mtu wa Kujifunza kila Uchwao ni Miongoni Mwa Maana ya Kuzihesabu Siku...


Tembelea pia www.ukombozihospel.blogspot.com

Jumanne, 14 Februari 2023

kitabu chetu cha: CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu cha: CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA.

Hiki sii kitabu cha kawaida wala si somo tu bali ni ujumbe. Najua kila ujumbe ni somo katika mukutadha wa mafundisho na ufundishaji. Japo sio kila somo ni ujumbe.

Ujumbe huu ni matokeo ya mahali ninapopapitia ambapo mwaka jana palinipatia vitabu kama viwili hivi. Mosi ni kile cha  HAKUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA. Na pili ni kile cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO LAKO.

Kwa lugha nyingine unaweza kusema kuwa sii jumbe za kawaida. Bali ni maelekezo. Mfano wa ujumbe kibiblia ni pale mfalme Nebukaddeza alipoota ile ndoto na kisha kujikuta hana tafsiri yake na kuomba msaada kwa Danieli nabii wa Mungu. Tukiachana na yote pale, yale maneno, "Danieli 4:27 Kwa sababu hiyo, Ee mfalme, shauri langu lipate kibali kwako; ukaache dhambi zako kwa kutenda haki, ukaache maovu yako kwa kuwahurumia maskini; huenda ukapata kuzidishiwa siku zako za kukaa raha."


Kwa hiyo, kama Mungu amekupa kukisoma kitabu hiki, moja kwa moja fikra zako zielekeze kwenye ujumbe uliopo ndani yake. Ambao unanuia kumsaidia kwa kumpa mtu husika maelekezo muhimu ya kufanya ili kuendelea mbele na pito au jaribu analolipitia.

Ni matoke ya mimi katika jana ya leo, baada ya kuzungumza na kiongozi wangu mmoja juu ya pito ninalolipitia na majibu ya Mungu juu yangu. Majibu hayo yalinitaka niendelee kuvumilia. Na aliniambia hadi nimalize masomo. Nikauliza je nikimaliza Mungu ndo atanijibu?

Akaniambia hata yeye hajui kama atanijibu au la, ila alichoambiwa ni kwamba kwa wakati huu usijaribu kubeba mambo mawili. Kwa mujibu wa mukutadha wa hekima ile ni kwamba inaonekana maamuzi yangu dhidi ya pito husika nyuma yake hayana mapenzi makamilifu ya Mungu. 

Jumatatu, 2 Januari 2023

Rombo

#Mkutano #Mkutano #Mkutano Wiki hii; 4-8/1/2023 Katika Viwanja vya Zambia, Mengeni Chini Rombo . Muhubiri: Mwalimu Oscar Samba Walete wagonjwa na wenye mateso mbalimbali na Yesu Mtenda miujiza Atawaponya. Karibu Umsikie Mungu Akisema na Maisha Yako. Tafadhali watakatifu na Wengine