Jumatatu, 12 Februari 2024

Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha IMANI SAHIHI, Katika Mada ya Misingi na Tabia za Imani Sahihi.

 


Mwalimu Oscar:

Mwl OSCAR SAMBA ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu: #Usiogope
 Lengo la kitabu hiki ni kukuwezesha kuijua au kuitambua imani ya kweli, na kuzifahamu hila za adui Shetani katika imani potofu; ikiwemo namna ya kuzitofautisha na ile ya kweli na jinsi ya kuzishinda.

Misingi na Tabia za Imani Sahihi
Maana ya Imani. Katika Biblia na hata maisha yetu ya kawaida, neno imani limegawanyika katika maana zaidi ya moja, na huweza kuwa na maana kuu mbili. Mosi ni ile imani kama kuwa na hakika ya jambo unalolitarajia ambalo bado hujalipata ama kuliona ila unamatumaini nalo. Waebrania 11:1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
Unganisha na hili andiko; Warumi 8:24 Kwa maana tuliokolewa kwa taraja; lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana, hakuna taraja tena. Kwa maana ni nani anayekitarajia kile akionacho?

Maana ya Pili ya Neno Imani: Ni mfumo au "settings" ya mambo muhimu yenye kunuia kuunda aina fulani ya njia ya mtu; kimtazamo, fikra na hatimaye kimatendo, (kiimani "faith:") yenye kufuma namna ya kuabudu kwake, kusali, miiko fulani na maadili muhimu ya kuishi hapa