Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Matangazo. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Matangazo. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 6 Mei 2026

KUUJENGA UKUTA KUNA GHARAMA na Shujaa Hushinda Vita

Nehemia alighamua nia ya yule nabii mke na mwovu na alichonuia kukifanya. Alitaka kumjengea hofu kwa kupitia aina fulani ya maneno ili aweze kumuondoa katika kusudi. Adui Shetani alipoona wakina Tobia na Sanbalati wameshindwa kuzuia ukuta kwa njia mbalimbali, aliamua moja kwa moja kutumia njia hii. Lazima ujifunze hatari ya maneno unapokuwa unavikabili vita. Yawe yanatoka kwa adui au mtu mwingine. Na yakitoka kwako huwa mabaya zaidi. Maana Shetani atakufanya kama kiwanda cha kuzalisha hofu itokayo ndani mwako. Mawazo ya kushindwa yatakutawala nawe utazungukwa na kushindwa muda wote. Tazama; Nehemia 6:11 Nami nikasema, Je! Mtu kama mimi nikimbie? Naye ni nani, akiwa kama nilivyo mimi, atakayeingia hekaluni ili kuponya maisha yake? Sitaingia. 12 Nikatambua, na tazama, siye Mungu aliyemtuma; lakini amefanya unabii huu kinyume changu; nao Tobia na Sanbalati ndio waliomwajiri. :13 Kwa sababu hii aliajiriwa, ili mimi niogope, nikafanye hivyo na kutenda dhambi, kisha wao wawe nazo habari mbaya, ili wanishutumie. 14 Uwakumbuke, Ee Mungu wangu, Tobia na Sanbalati sawasawa na hayo matendo yao, na yule nabii mke Noadia, na hao manabii waliosalia, waliotaka kuniogofya. 15 Basi huo ukuta ukamalizika siku ya ishirini na tano ya mwezi wa Eluli, katika muda wa siku hamsini na mbili. 16 Ikawa adui zetu wote waliposikia, ndipo makafiri wote waliotuzunguka wakaogopa, nao wakakata tamaa sana machoni pao wenyewe; maana waliitambua kazi hiyo ilivyotendwa na Mungu wetu. Alitumwa mjumbe, mwenye ujumbe! Sii kila maneno unapaswa kukubaliana nayo. Shujaa huwa makini sana anapokuwa vitani. Sii kila mwanajeshi aliyevaa nguo na zenye nembo kama yako unapaswa kumuamini! Wengine wameajiriwa na wakina Sanbalati ili wakuogofye. Nia yao ni kukutia hofu. Wanajifanya wana mpango mzuri wa kukusaidia, kumbe ni baada ya wao (kama Sanbalati) kukwama katika kukuzuilia kuujenga ukuta. Watakupa maneno mengi ya kwamba huyu ana misimamo mingi sana; ni mtu wa misimamo mikali...wewe usijali. Mimi huwa nasema ya kwamba asiye na misimamo ni maiti pekee. Lakini baadae nafikiria nakusema hata maiti ina misimamo maana imeshachagua upande wa kufa. Na uzima sio sehemu yake tena. Ukiumaliza ukuta ndipo watakapokuja kukuelewa. Usilazimishe kueleweka mapema na kila mtu. Unajua, anayeona unakoelekea ni wewe mwenyewe; kwa hiyo epuka kuwalazimisha wasiona waone kama wewe. Kama kila mtu atafanikiwa kuona kama unavyoona wewe basi hayo sio maono tena. Maono sifa yake moja wapo ni aidha mtu mmoja ama watu wachache kuona kwa niaba ya wengine. Na usikubali wasiona wakalie nafasi ya maamuzi yako. Wengine ni kweli uko nao ila ni wakina Tobia na Sanbalati, hili lazima ulielewe daima. Ukiona mtu unakataa ushauri wake na anakukasirikia au anakuwa mkali kama pilipili; uwe na hakika haukuwa ushauri bali yalikuwa ni maamuzi au maelekezo aliyokuwa anakupatia. Na inapendeza sana kama ukifanikiwa kujua roho iliyo ndani yake kama Nehemia dhidi ya Noadia nabii mke. Maana kama ingelikuwa ni ushauri kusingekuwa na haja ya yeye kukasirika. (Kuna watu fulani waliwahi kunifanyia fitina, moyoni mwangu nikajisemea wanafikiri mimi ni dhaifu kiasi hicho. Ningekuwa dhaifu nisingefika hapa). Nehemia asingekaza katika kusudi ukuta usingejengwa. Utakutana na Ujumbe Huu Katika Kitabu Chetu Kipya cha KUJARIBIWA KWA IMANI

Jumatano, 28 Januari 2026

Karibu katika Mfululizo Wetu wa 1, wa Kitabu Chetu Hiki Kipya cha #KUJARIBIWA KWA IMANI katika Mada ya Cha Kufanya #Unapotupwa Kwenye Shimo, Pointi ya 1.

Na Mwl Oscar Samba

1. Cha Kufanya Unapotupwa Kwenye Shimo

1. Uwe Utayari na Ufahamu ama Akili ya Kukubali Kuishi Katika Shimo. Lugha ya kutupwa katika shimo ina maana ya kushushwa au adui kunuia kukuua. Ni aina ya pigo la kukung'oa au kukuangamiza kabisa kabisa. Mfano vijana wale wa tatu wa Yuda alipotupwa katika tanuru la moto; Meshack, Shedraka na Aberinego. Danieli katika shimo lenye simba wakali. Alikadhalika Yusufu gerezani, maana alitolewa katika maisha ya utukufu, na kisha kushushwa chini ghafla. Alikadhalika pia alipotupwa katika shimo na nduguze, na kisha kuuzwa utumwani. Maisha ya utumwa kwake bado yalikuwa ni kama shimo, maana anatolewa katika familia ya

Jumatano, 21 Januari 2026

Karibu katika Mfululizo wa 9 wa Kitabu Chetu cha CHA KUFANYA UKIWA NJIA PANDA . Katika Pointi ya 7. Na Mwl Oscar Samba 7. Kama Hujui cha Kufanya Usifanye Chochote

 Watu wengi wamejikuta wakiwa katika njia isiyo sahihi mara baada ya kupitia 

kipindi cha ukimya wa Mungu. Kuna kipindi Mungu huwa kimya kama 

sehemu ya jaribu kwetu. Ikiwa imani yetu kwake inapimwa, jambo la 

sabra na hata nidhamu, utii na hofu kwake; ni kwamba ni kweli 

tunamtegema na kumtumaini Yeye! 

Japo wakati mwingine anaongea lakini hatuelewi, na pia kuna muda 

anaona hata akiongea hatutamuelewa. Usisau pia ukimya wake, huweza 

kuwa ni matoke ya hasira yake juu yetu. Maana hata mfalme Sauli kuna 

wakati Mungu hakusema naye; baada ya kukorofishana naye, na 

kujikuta akigeukia msaada kwa mganga wa kienyeji. Na alilalamika 

kuwa Mungu hasemi naye hata kwa ndoto.

Sasa, Nisikilize; Mungu anapokua kimya, au unapofikia katika hatua 

Jumanne, 11 Novemba 2025

Heri Alitunzaye Vazi Lake

Uwokovu ni Vazi. Je, Unautunza Wokovu wako?

Nikuite Moyo hivi Leo kutokuendelea kucheza na Dhambi. Tunza wokovu, linda vazi lako. Yesu yu karibu kuja. Anakuja kulinyakuwa kanisa lake..

Ufunuo wa Yohana 22:13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. 

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. 

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya. 

Jumanne, 29 Julai 2025

AKILI ZILIZO MACHO KATIKA UFALME WA MBINGUNI Mathayo 24:45

Ujumbee huu ni Sehemu ya Kitabu Chetu Kipya Cha: KILI ZILIZO MACHO KATIKA UFALME WA MBINGUNI

Mathayo 24:45

Na Mwalimu Oscar Samba 

Utangulizi
Kulala Usingizi, Kupoa kiroho, au Kifo cha Kiroho = Ni sawa sawa na:- (Hufananishwa na Hali ya Mtu Asiye na Akili ama Mwenye Tatizo hilo Katika Ulimwengu wa roho. 

Hiyo ni picha muhimu unayopaswa kuwa nayo, wakati huu unapoelekea kukisoma kitabu hiki. Ni muhimu sana kufahamu ya kuwa maana moja wapo ya Yesu ya kututaka tusilale usingizi yaani tuwe macho; ama tukeshe ililenga eneo la akili zetu.

Tazama mfano ule wa Wana Wali watano wenye Busara na watano Wapumbavu. Ndipo utakapotambua ya kuwa upumbavu unaotajwa pale, ni unaotokana na hali ya kutokujua ni nini cha kufanya katika nyakati kama hizi.

Malengo ya Kitabu:

1. Kuyafumbua Macho ya Aliyefumbwa, Kuziamsha Akili za Asinziaye ili Aweze Kuwa na Utayari wa Kutumika Kiusahihi (kama impasavyo), Katika Kulielekea Kusudi Aliloitiwa Kinyakati.

2. Kumpatia Ufahamu, Utakaotumika Vyema na Akili Zake, ili Kujua Ni Nini Kimpasacho Kukifanya Katika Majira Husika.

1 Mambo ya Nyakati 12:32 Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.

3. Kumjengea Fikra za Kumuwezesha Kuzitambua Hila za Adui Shetani; Katika Mpango wa Kumnyamazisha au Kutaka Kumpoozesha Kiroho na Kiutumishi, (au Kiutumishi/Kiroho.) 2 Wakorintho 2:11 Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikra zake.

4....


Lengo Kuu: Kukujengea Fikra za Kiuamsho, Ili Kuibua Hari na Kuamsha .... Kukuumbia Nia ya Kiuamsho Ndani Yako. (Penye Nia, Pana Utayari).

.....,....

1. Maonevu na Migogoro Katika Kanisa, Ama Baina ya Watumishi, au Washirika: Ni Ishara ya Kujisahau Kiroho. Watu waliopoteza kusudi, au kulisahau ama walioshindwa kujitambua ndio pekee huweza kuanza kuumana. Unapoona

Ijumaa, 25 Aprili 2025

Ishara na Miujiza Kwa Mkono wa Musa: MIUJIZA HUITAMBULISHA HUDUMA.

 Ujumbe huu ni Sehemu ya Kitabu Chetu Kipya cha MOTO WA UAMSHO KATIKA BIBLIA (Tunachambua kila Kila Tukio Lenye Uamsho ktk Biblia Nzima).

Na Mwl Oscar Samba 

Kitabu cha Kutoka ... na Yoshua Sura ya 3 na 4, pia Yohana 2:7-11.

Somo la ....: Ishara na Miujiza Kwa Mkono wa Musa: MIUJIZA HUITAMBULISHA HUDUMA.

Shalom mtu wa Mungu, tumekutana tena katika somo jingine. Hapa kwa pamoja tunaangazia nafasi ya ishara na miujiza katika kuitambulisha huduma au mtumishi husika. 

Tukiwa tungali katika wito wa Musa kwenye kitabu hiki cha Kutoka; Musa alipoitwa, na kukabidhiwa majukumu kadhaa, alionyesha hali ya kutokukubalika. Alikuwa na mashaka au wasiwasi kama atapata kibali kutoka kwa watu. Jibu la Mungu lilikuwa ni jepesi tu kwake, Mungu alimpatia ishara kadha wa kadha. Na kumwambia ya kuwa, watamuamini kwa kupitia hizo.

Alhamisi, 3 Aprili 2025

Moto wa Uamsho Katika Biblia

 

Ujumbe huu ni Sehemu ya Kitabu Chetu Kipya cha; MOTO WA UAMSHO KATIKA BIBLIA
(Mwanzo Hadi Ufunuo.)
Na Mwalimu Oscar Samba 
Utangulizi:
1.Kitabu hiki kimenuia kukusaidia kuona mbinu, kanuni, au matukio na matendo ya Kiungu ya kiuamsho katika Biblia.

2. Kina muwezesha Mkristo kwa muhubiri, kuisoma Biblia yote kwa sura ya kiuamsho.

3. Kinanuia kuibuisha tena kusudio la Kiungu lakuleta uamsho, au kuturejesha katika viwango vya kiroho.

4. Kinanuia kuunga mkono na kivitendo ajenda ya kanisa la nchi ya Tanzania na Afrika na baadhi ya makanisa ya nchi nyinginezo: inayohusu uamsho.

5. Ni muongozo wa Kibiblia wa kujifunza uamsho.

Alhamisi, 18 Julai 2024

MAFANIKIO KWA KANISA LA KWANZA

 


Nina *Mshukuru Mungu* kwa Kufanikiwa Kukamilisha Kitabu Changu Kipya cha Uchambuzi wa Kitabu cha Matendo ya Mitume. Kitabu kinaitwa SIRI YA *MAFANIKIO KWA KANISA LA KWANZA* ( *kanisa la Mitendo ya Mitume) By Mwl Oscar Prospa Samba mwana wa Flora Samba

Kipakiwe Bure Kitabu hiki Free Download Pdf 

Bonyeza Hapa Mwalimu Oscar Samba SIRI YA MAFANIKIO KWA KANISA LA KWANZA (Kanisa la Matendo ya Mitume)

Jumatatu, 12 Februari 2024

Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha IMANI SAHIHI, Katika Mada ya Misingi na Tabia za Imani Sahihi.

 


Mwalimu Oscar:

Mwl OSCAR SAMBA ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu: #Usiogope
 Lengo la kitabu hiki ni kukuwezesha kuijua au kuitambua imani ya kweli, na kuzifahamu hila za adui Shetani katika imani potofu; ikiwemo namna ya kuzitofautisha na ile ya kweli na jinsi ya kuzishinda.

Misingi na Tabia za Imani Sahihi
Maana ya Imani. Katika Biblia na hata maisha yetu ya kawaida, neno imani limegawanyika katika maana zaidi ya moja, na huweza kuwa na maana kuu mbili. Mosi ni ile imani kama kuwa na hakika ya jambo unalolitarajia ambalo bado hujalipata ama kuliona ila unamatumaini nalo. Waebrania 11:1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
Unganisha na hili andiko; Warumi 8:24 Kwa maana tuliokolewa kwa taraja; lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana, hakuna taraja tena. Kwa maana ni nani anayekitarajia kile akionacho?

Maana ya Pili ya Neno Imani: Ni mfumo au "settings" ya mambo muhimu yenye kunuia kuunda aina fulani ya njia ya mtu; kimtazamo, fikra na hatimaye kimatendo, (kiimani "faith:") yenye kufuma namna ya kuabudu kwake, kusali, miiko fulani na maadili muhimu ya kuishi hapa

Alhamisi, 7 Septemba 2023

Neno la Leo: MANA ILIYOFICHWA KWA ASHINDAYE

 

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu:

Ufunuo wa Yohana 2:17 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea.

Kuna aina ya Viwango vya Kiroho Vinavyoamua Upewe Chakula Gani cha Kiroho, Kutokana na Kushinda Kwako Majaribu..Kwa Wahubiri; Ukihitaji Kuwa na Mafundisho Tofauti yasiyoyakawaida, Huna Budi Kushinda Vikwazo ili Upewe Mana Isiyo ya Viwango vya Kawaida. (Natumai Kesho Utanielewa Zaidi..)

http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL

Nikutakie Siku Njema

Jumatano, 16 Agosti 2023


 Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )


Yakobo 5:10 Ndugu, watwaeni manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa uvumilivu.

:11 Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287

Nikutakie Siku Njema

Jumatano, 2 Agosti 2023

Neno la Leo, Amani na Maendeleo

 

Neno la Leo (Nasaha za Mwalimu Oscar)

Maombolezo 3:17 Umeniweka nafsi yangu mbali na amani; Nikasahau kufanikiwa.

*Kumbe Amani Ikitoweka na Mafanikio nayo Hupotea au Huwa Adimu..! Kwa hiyo; Hakikisha Amani Haipotei Moyoni Mwako ili Kulinda au Kuchunga na Kudumisha Mafanikio...Tazama Toka Uchungu, Hasira na Msongo wa Mawazo Vilipokukabili..Utakuta na Kasi ya Mafanikio Imepungua na Hata Mambo ya Msingi km Ujenzi na Biashara Kukwama* ..

www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi Letu la Telegram

https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Nikutakie Siku Njema


Alhamisi, 20 Aprili 2023

Naomba NiRepost NDOA NI ZAIDI YA UPENDO

Naomba NiRepost

#VIJANA_NISIKILIZENI_Haya_Nayo_Ni_Maneno_ya_Mwenye_Hekima


Moyo Unaweza Kumpenda Mtu Bila Kuwa na Sababu Yoyote ya Msingi ila Usikubali Kuoana na Mtu Asiyetosheleza Vigezo Vya Ndoa kwa Viwango Fulani.



Moyo wa mwanadamu kuna muda unavutiwa na mtu bila hata kukupa sababu zenye mashiko kwanini umempenda. Utamsikia mtu akisema basi nimepanda tu! Ni kweli ni jambo jema, na hatuwezi kuweka sababu kwa kila mtu au maamuzi ya moyo kupenda.

Ndiposa wengine wakasema mapenzi ni upofu, ikiwa na maana kwamba kuna mambo ya msingi mtu anaweza  kuya_overloock ama kuyapuuza ifikapo swala la kupenda. Hapa napo sina shinda napo.


Ila msemo huu ndio unaonipa shida; kipendacho roho hula nyama mbichi! Ndugu yangu, nyama mbichi huvimbisha matumbo, huleta kuharisha sanjari na hatari ya magonjwa ya minyoo.

Jumanne, 14 Februari 2023

kitabu chetu cha: CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu cha: CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA.

Hiki sii kitabu cha kawaida wala si somo tu bali ni ujumbe. Najua kila ujumbe ni somo katika mukutadha wa mafundisho na ufundishaji. Japo sio kila somo ni ujumbe.

Ujumbe huu ni matokeo ya mahali ninapopapitia ambapo mwaka jana palinipatia vitabu kama viwili hivi. Mosi ni kile cha  HAKUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA. Na pili ni kile cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO LAKO.

Kwa lugha nyingine unaweza kusema kuwa sii jumbe za kawaida. Bali ni maelekezo. Mfano wa ujumbe kibiblia ni pale mfalme Nebukaddeza alipoota ile ndoto na kisha kujikuta hana tafsiri yake na kuomba msaada kwa Danieli nabii wa Mungu. Tukiachana na yote pale, yale maneno, "Danieli 4:27 Kwa sababu hiyo, Ee mfalme, shauri langu lipate kibali kwako; ukaache dhambi zako kwa kutenda haki, ukaache maovu yako kwa kuwahurumia maskini; huenda ukapata kuzidishiwa siku zako za kukaa raha."


Kwa hiyo, kama Mungu amekupa kukisoma kitabu hiki, moja kwa moja fikra zako zielekeze kwenye ujumbe uliopo ndani yake. Ambao unanuia kumsaidia kwa kumpa mtu husika maelekezo muhimu ya kufanya ili kuendelea mbele na pito au jaribu analolipitia.

Ni matoke ya mimi katika jana ya leo, baada ya kuzungumza na kiongozi wangu mmoja juu ya pito ninalolipitia na majibu ya Mungu juu yangu. Majibu hayo yalinitaka niendelee kuvumilia. Na aliniambia hadi nimalize masomo. Nikauliza je nikimaliza Mungu ndo atanijibu?

Akaniambia hata yeye hajui kama atanijibu au la, ila alichoambiwa ni kwamba kwa wakati huu usijaribu kubeba mambo mawili. Kwa mujibu wa mukutadha wa hekima ile ni kwamba inaonekana maamuzi yangu dhidi ya pito husika nyuma yake hayana mapenzi makamilifu ya Mungu.