Jumapili, 27 Septemba 2020

MUNGU ANAKUPENDA KWA SABABU AMEANDAA MPANGO WA KUKUTOA KWENYE HILO JARIBU AU PITO.

Basi, Bwana ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, na kuwaweka wasio haki katika hali ya adhabu hata siku ya hukumu. 2 Petro 2:9.

Wakati wana wa Israeli wanalia, wanalalamika, wanaumia ama wanaonyesha hisia zao kutokana na ugumu wa mateso yale ya nchi ya utumwa wa Misri, Mungu kwa upande mwingine alikuwa akitekeleza mipango ya kuwaokoa kwenye ile nchi!

Hakuna mtu aliyekuwa akiona, kutambua, au kufahamu kuwa upande wa pili Mungu alikuwa akimpatia Musa maelekezo ya namna ya kuwatoa kwenye ile ncchi!

Na hata kabla ya hapo, Mungu alikuwa akimuandaa Musa kwa ajili ya swala hilo, sio kwamba tu alilifanya hilo wakati Musa akiwa Midiani, bali hata kabla ya Musa kukimbilia huko Mungu alishamuandaa, ndio maana yale mahubiri yake kwenye kitabu kile cha Matendo ya Mitume yanaelelezea vyema kuwa Mungu alimuandaa huyu, ila hakumuelewa mapema, na wana wa Isreali hawakulielewa lile ndio maana walimkataa kwa wakati ule!

 

Jumamosi, 19 Septemba 2020

Kitabu cha USIFIE JANGWANI Mwalimu Oscar Samba Pdf

#Tangazo, Tunamshukuru Mungu kwa kufanikiwa kutoa kitabu hiki kwa njia ya Pdf, kwa hiyo kinaweza kusomwa kwenye Simu yako au Komputa, ukikihitaji utakipata kwa shilingi 50,000/ths. Tumia namba zifuatazo kufanya mawasiliano na malipo kwa M-Pesa, +255 (0) 756293767, jina ni Oscar Samba. Mwalimu Oscar Samba Tunajianda pia kukipeleka Amazon