Jumamosi, 3 Juni 2017

NAMNA YA KUJINASUA KWENYE VIFUNGO VYA PEPO MAHABA. Sehemu ya 4.

 Na Mwalimu Oscar Samba wa Ug Ministry.
 Kwa tabasamu Mubashara ninakukaribisha tena katika mfululizo wa makala yetu hii ikiwa leo ni sehemu ya 4 na kama hukusoma zilizotangulia ni vyema ukazisoma ili tuweze kwenda sanjari, pia kumbuka ujumbe huu ni sehemu ya kitabu changu cha NGUVU YA NDOTO KWENYE ULIMWENGU WA ROHO.
(8) Kusikiliza au kufwatilia Hadithi zenye elementi au chembe chembe za pepo mahaba.
Sikio ni malango wa rohoni tena hatarishi kama utatumiwa na adui. Elifazi aliota ndoto ambayo Shetani alitumia mlango wa sikio kupenyeza mathara kathaa ikiwemo hofu, kutetemeka mifupa na hata nywele kusisimka. Mstari ule wa 12 anasema kuwa alisikia na kusikia huko ndiko kulikoruhusu hayo mathara. Ona katika kitabu kile cha Ayubu 4:12-16. Na wewe kusikiliza hadithi zenye “elementi”/chembechembe za jini Mahaba kutakufanya kumfungulia mlango maana tayari masikio yameshamruhusu kupenya hali itakayompa uhalali wa kukutembelea ndotoni.

Kusoma hadithi hizo kutampa mlango maana unachokisoma chaweza ingia nafsini au moyoni. Na huko ndiko kuliko na lango la kiroho pia fahamu mtu wa ndani na ndiye anayeota ndoto kama hizi.
Namna ya Kumshinda Pepo Mahaba.
Katika ulimwengu wa roho ukiwaona mabinti waliovalia nguo za rangi nyekungu na kwa nadra waweza vaa za rangi ya zambarau ambazo zipo kama gauni ila lenye mpasuo mrefu na huonyesha utupu wao, jua ni jeshi la pepo mahaba. Mapepo haya yanakitengo chao kwa ajili ya kupigana vita ndio maana ni vigumu kuyashinda bila kanuni stahiki na kiongozi wao Mkuu ni Mama wa Makahaba wa Babeli ama Mama wa Machukizo ya nchi. Soma Ufunuo wa Yohana 17:1-18.
1. Muombe Mungu akujulishe milango/mlango alioutumia.
2. Bada ya kuujua mlango, Omba rehema kwa mlango huo kufunguka. Epuka kujihesabia haki punde ujuapo kuwa huku husika ama huna hatia iliyofanya mlango huo kufunguka. Rehema ya kumng’o Pepo huyu inapaswa kuwa kubwa kwani huwa na tabia ya kuwa king’ang’anizi, ndio maana watu wengi hushindwa kupambambana naye. Rehema hiyo yapaswa ifanyike katika maombi ya kufunga na kuomba na ya muda mrefu huku yakiwa na mfumo wa maombolezo.
3. Futa uhalali wa Shetani kuutumia huo mlango kwa kutumia Damu ya Yesu ile imwagikayo ubavuni na mikononi. Omba kwa kumaanisha na kuzama.
4. Funga mlango huo kwa Maombi ya muda mrefu na yenye ujazo wa Roho.
5. Fanya maombi malumu ya kufunga mlango huo kabla ya kulaa. Anza na rehema, pili funga mlango. Pia taja kila lisaa kwa kukemea na kufunga kuanzia muda unaolala hadi utakapo amka, ukifika muda ambao mara nyingi huota ndoto hiyo, kemea ama ombea muda huo kwa mzigo zaidi. Mara nyingi mapepo haya hutumia lango la muda au siku fulani, ndio maana ni muhimu kuandika au kujua muda ambao mara nyingi huota ndoto za aina fulani. Pia huweza kubadilika baada ya muda fulani. Kwa mfano ukijua ni saa tisa au saa kumi na moja, wengine huwa ni saa moja kasoro, muda huo uombee kwa kasi na nguvu zaidi.
6.  Unapoamka hakikisha unajiombea na kuwaombea wale ambao huweza kufungua mlango wako wa ndoto kwa siku hiyo wasifanye hivyo, pia jitenge nao rohoni kama watafanya hivyo. Jiombe ili Shetani asipate nafasi ya kuyatumia macho yako kutamani au mawazo yako kutafakari upumbavu hali itayomuwezesha kupata nafasi. (Zaidi soma kipengele cha Usimpe Ibilisi nafasi kilichopo kwenye kitabu changu cha Namna ya Kuishi wakati wa Majaribu au Mapito)
Katika kuomba tumia sana Damu ya Yesu na Silaha ya moto, pia na Upanga. Ukisoma sura ya 17 nzima ya kitabu kile cha Ufunuo wa Yohana, utaona jinsi walivyo mshinda kwa Damu za watakatifu na ya Mwanakondoo pamoja na moto. Ufunuo 17:14 Hawa watafanya vita na Mwanakondoo, na Mwanakondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Bwana, na Mfalume wa Wafalume; na hao waliopamoja nao ndio walioitwa, na wateule na waaminifu. Hapa tunapata pia Silaha nyingine ya Bwana wa Mabwana, na Mfalume wa Wafalume. Tumia majina hayo katika kumpinga na kupigana naye, ila kufuta uhalali changanya hapo na Damu ya Yesu.                                                                        
7. Vunja hiyo ndoa kwenye ulimwengu wa roho, Mapepo haya huwa yanafunga ndoa na wahusika kwa hiyo baada ya hatua hizo hapo tangaza kimaombi kuivunja hiyo ndoa. Pia Vua vitu ambavyo ni alama ya mapepo ulivyovikwa rohoni, mfano pete mikononi na miguuni, vikuku na hereni na hata mavazi. Fanya maombi hayo kwa ishara na kwa kumaanisha na yawe maombi ya vita.                                                                       8. Futa alama za mapepo mahaba ambazo hukaa mwilini, kuna mwanaume mmoja wakati anafanya haya maombi Mungu alimuonyesha kwenye mguu wake eneo la chini kwenye kiungo cha ubavu kuna alama ya uke. Ikiwa na maana kila aridhi atakayoikanya yenye mapepo haya ni rahisi kuvamiwa au kutekwa nayo ama kumtumia ndotoni kwani mguuni kuna malango. Wengine huwa na Ume/Uke wa kimapepo katika sehemu zao za siri ama popote mwilini, alama hii ni hatarishi kwani mtu kama huyu huweza kuwaka hisia kwa haraka sana na wengi wao huwa na vitendo vya kujichua/“punyeto” ama ushoga na usagaji na akiota huweza kuota anazini na mtu wajinsia yake kwani kwenye ulimwengu wa roho ana alama ya jinsia ningine. Na alama kama hizi zikiongezeka za jinsia tofauti na kukomaa kwa muda mrefu muhusika kama ni wakike huweza kuwa namuonekano au tabia kama za kiume na kama ni wakiume huweza kuwa na tabia kama za kike. (Taadhari: Sio kila mwenye tabia hizo ana tatizo hili kwani wengine ni matatizo ya kihomo za kibaolojia, au jinsi alivyojiweka; ingawaje na huyu ni matatizo ya kihomoni kiroho.) Siku moja nilimuota mtu mmoja mwanaume mwenye maziwa/matiti ya kike kifuani mwake, na ni ishara ya kwamba mapepo haya yamemkali na huwa mwepesi wa kuzini bila hiyari yake. Zote zifute na kabla huja zifuta anza na maombi ya rehema ili kuondoa uhalali wake na kisha futa kwa alama hizo Damu ya Yesu.
NB: maombi haya yafanye kwa muda mrefu, hata ukiona hali hiyo imeisha usikubali kuacha hadi Mungu akuakikishiye maana Pepo hili huwa na tabia ya kutulia kwa muda ili usahau na kisha hurudi tena. Ama huweza kuamua kuamia kwa ndugu yako, watoto au mwanandoa mwenzako pia huwa na utamaduni wakulipiza kisasi. Kwa hiyo funga pia roho za kisasi na mashambulizi.
Kwa watumishi, Watumishi wa Mungu wanaokemea mtu mwenye mapepo kama haya wanapaswa kufuga roho za visasa na wao kuishi maisha matakatifu kwani mara nyingi hupenda kulipiza kisasi kwenye ndoa zao au watoto pia hata ndugu. Ndio maana watoto wengi wa watumishi hujikuta wakianguka kwenye Uzizi na bathi ya wake za watumishi hujikuta wakitoka kwenye ndoa zao. Na watumishi wengi wanaoanguka kiroho husumbuliwa sana na dhambi hii ikiwa ni matokeo ya kisasi.
Kwenye ndoa, Hakikisha unamuombea mwanandoa mwenzako kila wakati dhidi ya roho hii ili isimvae. Fungua nami kitabu kile cha Zaburi, Zaburi 22:20 Uniponye nafsi yangu na upanga, mpenzi wangu na nguvu za mbwa. Watu wa kiroho wanafahamu kuwa kiwakilishi cha roho ya umalaya na ukahaba ama mapepo mahaba kwenye ulimwengu wa roho ni mbwa. Na kwa kulifahamu hili mtunga Zaburi anamuombea mpenzi wake alindwe na Mungu dhidi ya nguvu za mbwa. Maana yake ipo nguvu kwa Pepo Mahaba iwezayo kumdhuru mwenzako. Ona pia Zaburi 35:17.
Na kama ndoa yako imeshavamiwa kwa mujibu wa dalili tajwa hapo juu, ya kupasa kuipeleka kwenye maombi ili ipone na usikubali makwazo ya mwanandoa mwenzako kukuzuia maana Shetani huyaleta ili kukupa uchungu utakao kunyima kumuweka kwenye maombi. Zaidi, fwatilia somo langu liitwalo Hatari ya Pepo Mahaba.
Hongera wa kutufwatilia hadi kufikia hatua hii, na kwa mfululizo kutoka kwenye kitabu chetu hapo ni mwisho ila kesho nitakupa mwendelezo ambao ni wa ziada sio kwepo kwenye kitabu na hapo nitatanua matamvua yangu kifikra zaidi ili kukupatia mambo muhimu yasiyokwemo humu maana ujumbe huo kwa kiasi fulani ulizingatia maudhui na shabaha ya kitabu ambayo ililenga kwenye nyanja ya Pepo Mahaba. Tuonane kesho na kusanya Uwezo na Nguvu wakutanabaishwa vyema.
Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigospel.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,   
PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              

Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa                                                                          2 DAY SKY: https://www.2daysky.com/home

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni