Ijumaa, 16 Juni 2017

Mwalimu Oscar Samba, MBINU TEULE ZA KUTOKA KWENYE UMASIKINI KWA WATU WALIOKOKA, 5.

Mwalimu Oscar Samba akifundisha katika semina
 jana hapa Morombo Arusha Tanzania
Na Mwandishi wetu, Ug Ministry.
Ninakukaribisha katika jina la Yesu Kristo Bwana wetu na Mwokozi wetu katika sehemu hii ya 5 ya ujumbe wetu kama alivyofundisha Mwalimu jana kwenye semina inayofanyika hapa mkoani Arusha kwenye viwanja ya Morombo nchini Tanzania.

Kama ilivyo ada alianza kwa kutoa msisitizo kwa watu kuutafuta kwanza ufalume wa mbinguni na haki yake na kisha hayo mengine ikiwemo ya uchumi ama utumishi watazidishiwa.

Mwalimu wetu alitoa utangulizi uliyolenga kuwakumbusha wanafunzi wake mahali aliponzia tangu siku ya kwanza na kusema ya kwamba alitamani kugusia somo la Agano la Chumvi ili kuwasaidia watumishi wa Mungu maana ni Agano la kitumishi ila kwa jana hakupata kibali ila siku ya mwisho ya semina huenda akakipata na ikumbukwe kuwa hasemi jambo kwa akili zake bali hunena lile ambalo Roho anataka alinene kwa wakati gani na sehemu gani.


Jana alizungumzi mbinu moja teule nayo ni MALANGO au LANGO, aliwataka watu kuvuta taswira ya mlango au geti ambalo lina kuwa na dhima ama jukumu la kumruhusu mtu kuingia au kutoka na pia ukifungwa humzuilia kuingia au kutokuingia. Alikadhalika kwenye ulimwengu wa roho ndivyo ilivyo ili Baraka za kiuchumi zimfikiliye mtu ni lazima zipitiye katika mlango wa rohoni. Alisema zaidi kuhusu swala hili waweza kutafuta kitabu chake cha MALANGO KWENYE ULIMWENGU WA ROHO, punde kitokapo.

Alibainisha kwamba yapo malango ya aina mbili, ya kwanza ni yale ya dhambi na ya pili ni ya Baraka ambayo ndiyo aliyoyazungumzia kimapana zaidi jana. Ya dhambi alitoa mfano kwa Kaini pale Mungu alipomwambia kuwa dhambi inakuotea mlangoni ya kupasa uishinde, na maandiko kwenye kitabu kile cha Waefeso 4:27 wala msimpe Ibilisi nafasi.
Maana yake kubwa hapo nikutokumpa Shetani mlango maana kabla Yuda hajamsaliti Yesu maandiko yanasema ya kwamba alitafuta nafasi, yaani alitafuta mlango, kwa hiyo kwa Yesu kuna mlango uliokuwa wazi uliyompa nafasi Yuda ya kufanya jambo lile ama Shetani kupitia Yuda. Alibainisha ya kwamba Yuda mwenyewe alikuwa ni nafasi, maana likuwa ni mtumishi ama mtu wa karibu kwa Yesu. Ndio maana kwenye ndoa mwanandoa mwenzako anapokutamkia neno baya kama la kutokufanikiwa huwa na nguvu maana yeye ni mlango na ametumika kama lango la dhambi au uaribifu, ndio maana pia ni hatari sana kama mtumishi atakuwa na watumishi wasaidizi na mmoja wapo akawa kinyume naye, maana yake anafanyika lango kwenye ulimwengu wa roho lilola uaribifu, kama Yuda.

Tuingiye sasa katika lango la Baraka ambalo ndilo kiini cha somo letu siku ya leo, Ili Mungu kukubariki ni lazima lango lako liwe wazi na kama limefungwa lifunguwe kwa maombi.

Tuyaone malango kibibilia kabla ya kukujuza mifano ya hayo malango; Isaya 60: 11 Malango yako nayo yatakuwa wazi daima; Hayatafungwa mchana wala usiku; Ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa, Na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.

Maana yake utajiri unapaswa kupitia kwenye hayo malango, Fungua nami kitabu kile cha Mwanzo 22: 17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;

Umeona hilo jambo hapo, anasema kuwa uzao wako utamiliki malango ya adui zako, kwa hiyo ili kuwa tajiri mtu uliyeokoka yakupasa kumiliki malango ya adui zako.

Andiko jingine ni lile la Rebeka mkewe na Isaka wakati anaagwa, (Send-off, kwa lugha ya leo), wazazi wake na jamaa yake walimtamkia baraka tele ikiwemo ya kumiliki malango ya adui zake. Ndiposa Mwalimu akasema ni jambo la muhimu sana kumtamkia baraka binti yako ama mwanao wakati wakumuaga maana ukimuaga na manung’uniko yataambata naye na wasipojua kuyatangua rohoni huweza kuwasumbua daima. Na jambo hilo ni la kweli maana kama kwa Rebeka maneno ya mwisho ya wazazi na nduguze yalikuwa na nguvu hiyo ni fika kwamba hata mabaya huwa hivyo.

Tutazame maneno hayo na ninataka upate uwakika ya kwamba malango yapo kiroho kweli, Mwanzo 24: 60 Wakambarikia Rebeka, wakamwambia, Ndugu yetu, uwe wewe mama wa kumi elfu, mara elfu nyingi, na wazao wako waurithi mlango wa hao wawachukiao.

Kwenye Isaya tumeona malango kuwa wazi, kwa Ibrahimu kumiliki ya adui, na kwa Rebeka tunaona ya kuridhi malango ya adui.

Huu ulikuwa ni unabii wa kuja kuimili Kanani na utajiri wake, kwa hiyo ni fika ya kwamba umekubaliana na Mwalimu ya kwamba ni kweli malango yapo.

Tuyadodose hayo Malango sasa,  Lango la kwanza ni Urithi, tumeona watoto wengi wa viongozi nao wakiwa viongozi, wa wafanya biashara nao wakiwa wafanya bisahara, kwa bahati mbaya kwa lango baya wale wa kahaba nao wapo wanaokuwa makahaba.

Ukiona hivyo jua ni swala la urithi, Isaka na hatimaye Yakoo walirithi Baraka, yule mwana mpotevu alirithi Baraka kutoka kwa wazi wake. Hata kama wazi wako wasipokupa mali ama hawapo, lango hili hukurithisah kitu kilichopo ndani yao.

Lango jingine ni NDOA, maisha ya mtu kabla hajaoa na baada ya kuoa kwake huwa tofauti, kwani lango hili hupitisha Baraka kama litakaa salama, ndio maana hata afya yake, uchumi wake na maisha kwa ujumla hunawiri. Ila kama ndoa hiyo ikiingiliwa na migogoro shetani huligeuza lango hili na kupitishia hapo balaa na mikosi ndio maana wanandoa wakigombana kila kitu kinagoma ikiwemo uchumi, ukiona hivyo jua fika ni kwamba Shetani ameligeuza nakulitumia kama lango la dhambi laana au uaribifu kama nilivyokujuza aina hiyo lango hapo awali.

Katika lango la Baraka ukisoma maandiko ya Isaka wakati anaona, tunamuona Ibrahimu akimbariki Isaka na kumrithisha mali yake baada ya Isaka kuoa, maana yake lango hili ndilo lilopitisha Baraka zake. Ndio maana kabla ama wakati wakuoa Shetani huleta vita kwa watu, hapa Shetani hana shida na Ndoa yako bali ana shida na Lango hili maana anajua litapitisha nini. Ndio maana akishindwa kuwazuia kuoana atahakiksha anapenyeza migogoro kwenye hiyo ndoa ili alitumie lango hili kama la uaribifu.

Lango lingine ni WAZAZI, wanayo nguvu kubwa sana katika kuyabariki maisha yako, wapo watu wanaoishi maisha magumu kwa sababu ya kutokupata Baraka za wazazi. Tazama maisha ya Yakobo, na Esau, yalikuja kuwa tofauti na nduguye kwa sababu ya kuzipata Baraka za wazazi. Na wewe hakikisha unawaendea wazazi na ukiweza andaa sadaka ama zawadi kisha piga wagoti mbele yao waombe msamaha kwa lolote ulilowai kuwakosea yamkini ukiwa mdogo kisha waombe wakuwekee mikono ya Baraka.

Jingine ni ARIDHI,Lango hili ni la ajabu sana na ni wachache wanajua kulitumia, sehemu unayofanyia biashara ina nguvu kubwa sana ama kazini kwako. Na hata nyumbani, hiyo aridhi ikifungwa ni dhairi kwamba hata uchumi wako utafungwa. Ndio maana wachawi wakija hunena maneno kwenye hiyo aridhi ama wanaoenda kwa waganga huelekezwa kuchota udongo hapo ama kuchimbia hapo vitu. Lango hili likiwa limefungwa lifunguwe kwa maombi ya rehema kisha tangua maneno na ufute na kuangamiza kila kilicho cha kipepo hapo.

Musa aliitajika kuisogelea aridhi ambayo Mungu anaiita ni Takatifu, Mungu angeweza kuzungumza naye akiwa mbali maana kama aliweza kuisikia sauti ya vua viatu ni fika angeweza kusikia maelekezo ya Wito wake, ila Mungu alimtaka aisogelee ile Aridhi ambayo kiroho ilikuwa ni Lango, maana tayari ni Takatifu na lango hilo ndilo lilokuwa na nguvu ya kupitisha kile ambacho Mungu alikusudia ndani yake kipite.

Na wewe hunabudi kuhakiksiha aridhi unayofanyia biashara ama kuishi inakuwa takatifu ili Mungu awezekupitisa Baraka ama riziki zako kwa siku ya leo kesho na kadhalika.

Lago jingine la mwisho kama alivyofundisha Mwalimu jana ni MBINGU AMA ANGA , Mwalimu Samba alisemakuwa kama Anga lako limefunwa ni hakika hutaweza kupokea Baraka zako. Kwani Danieli wakati anatia nia ya maombi, alishapewa majibu yake, anaingia kwenye maombi tayari akiwa na majibu yake, ila hayakumfikia kwa sababu mkuu wa uajemi alikuwa amekaa kwenye lango hili na malaika mwenye majibu alishindwa kupenya ama kupita hapo mlangoni kwa sababu ya mlango kufungwa. Ila Danieli alifanya maombi ya sku 21, yaliyolenga kufungua Anga lake.

Alitoa mfano wake ya kwamba kuna siku alikuwa anapita mahali pa gumu sana kimaisha na aliona njozi akiwa ndani kwake kwamba kuna ndege anapasua dari “silingbodi,” na alikuwa na kitu cheupe mdomoni: Alifahamu fika ya kwamba ile ametumia nguvu kupenya kuna shida kwenye Anga lake. “Na wewe ukina hivyo yakupasa ulifnguwe.” Mwalimu alifafanua.

Alisoma maandiko kwenye kitabu cha Zaburi yaliyosadifu dhairi shairi ujumbe huo,
Zaburi 78: 23 Lakini aliyaamuru mawingu juu; Akaifungua milango ya mbinguni;
24 Akawanyeshea mana ili wale; Akawapa nafaka ya mbinguni.
25 Mwanadamu akala chakula cha mashujaa; Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.

Tunaonah apo ili Mungu kuwapa chakula wana wa Iziraeli walikuwa jangwani ilimbidi ayaamuru Mawingi, ikiwa na maana yalikuwa na nguvu fulani, kisha akaifungua milango ya Mbinguni, maana yake Angani ama Mbinguni ipo milango, na ikifungwa hutaweza kupitishiwa Baraka au riziki kwenye biashara yako kama atakavyo Mungu.

Baada ya Mungu kuifungua, mstari unaofwata tunaona matokeo yake ikiwa ni watu hawa kupata chakula, kwa hiyo milango hiyo ilipitisha MANA, Soma tena hiyo mistari… Natumai umenata taswira halisi hapo.

Kwa hiyo kuna wakati tunamlaumu Mungu kwa kutokutubariki kumbe tatizo sio kwake kwani alisha achilia baraka kama ilivyokuwa amekwisha kuachilia majibu kwa Danieli ila wakuu wa anga wakipepo wamekaa kwenye hilo lango na Baraka haziwezi kupenya. Kwa hiyo ni wangu wito kukutaka kuwa mwepesi wa maombi ya vita ili kufungua anga lako ikiwezekana ombea malango yako ya Baraka kila siku. Lango jingine ambalo jana hakulitaja Mwalimu ni lile la juzi ambalo ni Agano, alisema jana kwamba Agano huweza kufanyika lango la Baraka ama dhambi au uaribifu na huwa hivyo kama ni la kipepo ila la kimungu kama lile la Ibrahimu ni lango la Baraka kwetu.

Usikose kutazama video yake kwenye YouTube Channel yetu ya Ukombozi Gospel, pia jana Mwalimu alibainisha pasipo kificho ya kwamba ni vyema kuokoka, na fahamu somo hili ama mbinu hizi teule za kutoka kwenye umasikini haiziwezi kuwa halisi kwako kikamilifu kama huja okoka, kwa hiyo yakupasa kuokoka ili ukifa pia leo uweze kwenda Mbinguni.


Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigospel.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,  
 PAGE: https://www.facebook.com/ugukombozigospel/
Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa
2 DAY SKY: https://www.2daysky.com/home

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni