Jumatano, 14 Juni 2017

Mwalimu Oscar Samba: MBINU TEULE ZA KUTOKA KWENYE UMASIKINI KWA WATU WALIOKOKA, 3.

Mwalimu Oscar Samba akifundisha  

NA Mwandishi Wetu, Ug Ministry.
Leo ni siku ya tatu ya ujumbe wetu huu Mubashara kama ulivyofundishwa na Mwalimu wetu kwenye Semina ya Mkutano wa Neno la Mungu inayoendelea ikiwa ni siku 8, hapa Mkoani Arusha nchini Tanzania kwenye viwanja vya Morombo.
Jana Mwalimu alianza kwa msisitizo kwenye andiko ambalo Mungu ametupa kutembea nalo kwenye semina hii nzima la kuutafuta kwanza Ufalume wa Mbinguni na Haki yake na kisha hayo mengine yote tutazidishiwa. Ni Mathayo 6:33.
Alisema kuwa inampasa kila mwana wa Nuru kuutafuta kwanza Ufalume wa Mbinguni na haki yake kisha Mungu atamzidishia akirudia mfano wa Mfalume Sulemani wa kumtafuta kwanza Mungu kwa kumuomba Moyo wa Hekima, Akili, Maarifa na kisha Mungu kumpatia hivyo vyote huku akimpa na Fedha. Kwa sababu alitafuta kanuni au mbinu teule ilizomuwezesha kutoka kwenye umasikini.


Mbinu aliyoanza nazo jana mara baada ya utangulizi huo ilikuwa ni Mbinu ya 3, “FANI” au UJUZI, Alibainisha, “Fani au Ujuzi ni kitu muhimu sana ambacho humsaidia mtu kupata fedha ama kujikwamua kutoka kwenye umasikini”

Alielezea kiini cha pwenti hiyo; “Msingi mkubwa wa pwenti hii ni siku moja nilikuwa innatoka kanisani, jirani ama karibia na kufika nyumbani, nilimuona fundi umeme akiwa amevaa varoli lake, ndipo Roho Mtakatifu akaniambia, ‘Mwanangu huyu mtu anaishi mjini kwa fani yake ya ufundi umeme’, nilitulia kimya ili kujua nini Roho ananiambia, alisema; ‘Tatizo watoto wangu hawalitambui hili. Wakisha okoka wanataka kuishi kwa imani, bila kujua imani bila matendo imekufa’. Mara baada ya ujumbe huo sikupoteza muda bali nilichukua kalamu na dafutari kisha kuanza kuandika ujumbe ule na kuweka kwenye kitabu changu”

Aliwataka watu waliokoka kuhakikisha ya kwamba wanakuwa wepesi wakuwa na fani au ujuzi ili uwawezeshe kujikwamua kimaisha.
Alisema ujuzi waweza kuwa ni udakitar, udereva, ama ufundi wowote ule. Ilikuwa ni rai yake kuwataka vijana kutokupoteza muda na wazazi wao pia bali wawasomeshe watoto kama Mithali inavyowataka kumshika sana elimu. Alitoa pia mfano wa Paulo mtume aliyekuwa mtumishi wa Mungu wa madhabauni ila alikuwa na fani ya kushona mahema, iliyomsaidia. Na katika hili aliwataka hata wale wenye wito wa kumtumikia Mungu kuhakikisha wanakuwa na ujuzi kwani utawasaidia. Alitanabaisha kwamba unaweza kuitwa 2010 ila Mungu akataka utumike 2030, na kuhoji hapo katikati utakuwa ukila nini?.
Onyo lake lilielekea kwa wale wanaosikia kuitwa nakutaka kuacha Shule, huku akiwaambia ni kosa bali watafute hekima ya Mungu katika hilo.

Mbinu nyingine ya 4, ni KIPAWA/KARAMA au KIPAJI, Mwalimi alisisitiza sana ya kwamba mafanikio ya mtu yamefungwa kwenye kipawa ama kipaji au karama ambayo Mungu amempatia. Alisoma maandiko yafwatayo.

Mithali 17: Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; Kila kigeukapo hufanikiwa.
Pia aliambatanisha na hili hapa; Mithali 18: Zawadi ya mtu humpatia nafasi; Humleta mbele ya watu wakuu.

Alisema ya kwamba kipaji au kipawa humuwezesha mtu kukaa na watu wakuu, kama Yusufu alivyokaa na Farao Mfalume wa Misiry, humpatia nafasi ikiwa na maana ya cheo, alikadhalika humpatia mafanikiao katika maisha yake.
Alitoa ufafanuzi ya kwamba neno zawadi ni sawa na kipaji ama kipawa ambapo Bibilia ya kingereza ya KJV imetumia neno moja katika kipawa na zwadi ambalo ni “Gift”, Yaani zawadi.

Alitoa mfano wa Mwimbaji wa nyimbo za Injili Rose Muhando, na Bonyi Mwaitege, Pia Mwalimu Mwakasege, wanatambulika kwa mujibu wa karama ama vipaji vyao. Na wanaishi kwavyo. Pia alisema wanaishi mjini kwa hivyo vipawa.
Alitoa mfano wa mgunduzi wa mtandao wa Facebook, anaishi na amefanikiwa kwa mujibu wa ubunifu wake, waliobuni vyombo vya muziki wananufaishwa kwa ubunif huo. Ndiposa aliwataka watu kutumia vipawa vyao vyema ili kujikwamua kimaisha.
Alisoma habari za Yusufu aliyekuwa gerezani ila alitoka kwa sababu yakutumia vyema kipawa chake cha kutafsiri ndoto, na kusema na wewe unaweza kutoka kwenye hiyo taabu kwa kutumia vyema kipawa ulicho nacho.
Pia alibainisha inawapasa wale ambao hawajaokoka kuhakikisha ya kwamba wanamjua Mungu iliwatumie vipawa vyao katika kuhubiri Neno la Mungu, maana wasipookoka wanaweza kutumia vipaji hivyo kubuni vitu vitakavyo wapeleka watu jehanamu kama Pombe na kadhalika.

Sanjari na hayo alifafanua kwamba ipo garama ya kutumia kipawa chako hususani kwa watu waliokoka kwani shetani hulipinga sana jambo hilo. Alitoa mfano wa Yusufu aliyechukiwa na ndugu zake kwa sababu ya ndoto zake, hatimaye kuuzwa, kuwa “houseboy”, kupelekwa gerezani pasina hatia yoyote ile, na hiyo ilikuwa ni garama ya kutumia kipawa chake.

Alikadhalika kwa watu waliokoka mambo hayo yapo ila yawapasa kuyashinda. Zaidi tazama video yake kwenye Chaneli yetu ya Youtubu ya Ukombozi Gospel. Ama tembelea www.ukombozigospel.blogspot.com
Ila Mwalimu alimalizia kwa maombezi kwa watu wote lakini pia kabla ya maombezi aliwataka watu ambao hawajaokoa kufanya hivyo ili waweze kutumia vyema vipawa vyao maana wasipokuwa na Roho ya Mungu ndani yao, (alitoa mfano wa Yusufu pale ambapo Farao alisema Roho ya Mungu inakaa ndani yake na kumuita ni mwenye Akili). Ya kwamba ni vigumu kuwa na ufanisi katika kipaji chako maana kama ni muimbaji utaimba nyimbo za dunia na jambo hilo litakuwa ni hatari kwa wewe maana ukifa utaenda jehanamu ya moto.

Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigospel.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,
PAGE: https://www.facebook.com/ugukombozigospel/
Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa
2 DAY SKY: https://www.2daysky.com/home










Hakuna maoni:

Chapisha Maoni