Jumamosi, 3 Juni 2017

NAMNA YA KUJINASUA KWENYE VIFUNGO VYA PEPO MAHABA. Sehemu ya 5.

Na Mwalimu Oscar Samba wa Ug Ministry.
Hakika ni jambo la fanaka kukutana tena katika safu hii ya makala za kiroho na ikiwa ni sehemu yetu ya mwisho ya mfululizo wa makala hii, leo nimekuandalia mambo kadhaa kuhusu hadhari za huyu Pepo mahaba na ni ombi langu Mungu akupe kibali cha kukuletea ujumbe kama huu katika sura nyingine maana hakika Mungu amenipa hazina ya maarifa kuhusu roho hii hatarishi.
Moja kwa moja nianze kwa kukujuza ya kwamba hii ni miongoni mwamambo ama roho inayoitessa dunia mno. Ikumbukwe kuwa katika historia ya Bibilia Mungu aliwai kuiangamiza dunia kwa maji kipindi cha Nuhu na kwa moto mji ule wa Sodoma na Gomora na sababu kubwa ikiwa ni roho hii.
Utumishi wa Daudi na Samsoni uliingia doa na sababu kubwa ikiwa ni roho hii. Ilimtesa pia Musa na Joshua sanjari na Kalebu kule Jangwani. Kumbuka baada ya matokeo yale ya upelelezi ya nchi ile ya ahadi Mungu anasema ya kwamba wamefanya uzizi na aina inayotajwa pale sio ya kukutana kimwili bali ni taswira nyingine ya utendaji kwa upande waibada za miungu na imani inayotajwa kiroho na lipo somo litakalo gusia taswira hiyi nami nimekuonjesha mwishoni mwa makala hii. Tuone adhari moja wapo ya roho hii.
HUTIA JERAHA, KUKUVUNJIA HESHIMA, Kitabu kile cha Mithali kimebainisha jambo hili vyema. Mithali 6: 32 Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake. 33 Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika.
Kwa mantiki hiyo unapotenda dhambi hii ni fika kwamba unaijerui nafsi yako na kwenye nasi kuna vitu vikuu vifwatavyo, 1. Hisia, utajikuta uwezo wako wakumwambudu Mungu katika roho na kweli unatoweka huku ukipoteza upendo kwa Mungu na kwa mwanandoa wenzako ama mchumba maana Upendo ni matokeo ya hisia itokayo katika Nafsi. 2. Akili, hiki ni kitua muhimu sana na hakipatikani kwenye ubongo bali ni kwenye nafsi, na jambo hili linaudhibitisho kibibilia katika kitabu changu cha SAIKOLOJIA YA MTU WA NDANI, nitalidadavua zaidi. Kwa hiyo
unapotenda hiyo dhambi akili zako zinadhoofika ndio maana utamkuta mtu akiwa radhi kuwalisha watoto wake dagaa ama kisamvu  pamoja na mkewe huku nyumba ndogo wakila nyama choma. Yuko tayari watoto warudishwe ada huku hawara akila vizuri. Ukiona hivyo jua ni akili zimeshaharibiwa, ndiposa pia hilo andiko likasema ya kwamba hana akili mtu huyu.
3. Makusudi, Pia yamo kwenye nafsi. 4. Dhimiri, Tunafahamu kuwa jambo hili huusika sana katika kutoa ama kuachilia hukumu kwenye moyo na ndiposa Roho Mtakatifu akihitaji kumgeuza mtu huugua kupitia Dhamiri, ila dhambi hii inaiadhiri na kuifanya ife kwa haraka zaidi. Mtu aliyemzizi ama mwasherati huwa na moyo mgumu sana kutubu. Au kujinyeyekesha.
5. Nia, Yesu alitutaka tuwe na nia ile ile kama aliyokuwa nayo yeye, katika kitabu kile cha Wafilipi. Nia ni kama kiini cha uhai wa jambo fulani katika maisha ya mwanadamu na ndicho huzalisha , Malengo, mikakati na hatimaye kufanikisha maono ama jambo fulani na kwa ujumla huweza kuziita njia. Maandiko yanapotutaka tuwe na nia moja tusitangetange katika nia mbili pia yanatutaka kwa tafsiri rahisi tuwe na nia moja maana vitu hivyo vilivyopo kwenye nia huitwa njia kwenye ulimwengu wa roho, sanjari na mawazo huzalishwa ama aina fulani ya Nia huzalisha mawazo ya aina yake na ndiyo huunda aina fulani ya moyo na yakipanuka huadhiri makusudi katika moyo, ambayo huwa na madhara katika njia za mtu. Ukiona mahali pameandikwa ya kwamba acheni njia zenu mbaya maana yake anza kwanza kubadili Nia na kisha mambo yaliyomo ndani yake. Ukimkuta mtu anahubiri Injili ili watu waokoke lakini ndani yake analenga kupata fedha jua huyo yupo kwenye utumishi wa Mungu na Nia isiyokuwa ya Kristo. Ba Nia yake  ni kupata fedha. Ili kumbadilisha ni msaada wa maandiko yafwatayo.
Wafilipi 2:.5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

Pia Yakobo na mistari yote hii imebeba kanuni kuhusu namna ya kujikwamua hapa ikiwemo Kumpinga Shetani aliyekamata hiyo Nia, Kumtii Mungu ili kuifwata Nia yake, Kuusafisha Moyo, Kutakasa Mikono ikiwa na tafsiri ya kazi ama mambo uyafanyayo. Huku Mungu akielekeza namna ya kuomba na anatuambia kuwa ni maombi ya Kuomboleza, Kulia, pamoja Kujinyenyekesha, hii pia inapatika katika kitabu hicho cha Wafilipi na ukitaka picha kamili endelea na maandiko yanayoendelea hapo utamuona jinsi Yesu alivyojishusha na kuikubali hata mauti ya msalaba huku akiiacha Mbingu. Jambo hili ni Muhimu sana kwako maana kwa Mtumishi kuwa na Nia mbli (Double Mind), Ni jambo hatarishi sana na ni matokeo ya kukosa unyeyekevu. (Zaidi fwatilia Somo langu la Nia ama kitabu cha Saikolojia ya Mtu wa Ndani kikitoka)
Bila iyana nakufungulia maandiko hayo; Yakobo 4:7 Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. 8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.
9 Huzunikeni na kuomboleza na kulia. Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa hamu. 10 Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza.

Kwa mantiki hiyo ni kwamba dhambi hii huweza kuugeuza moyo wako na kukujengea nia isiyotoka kwa Mungu na kujikuta unakuwa na utumishi tofauti na ule uliyoanza nao hapo awali.
Alikadhalka katika maisha ya kawaida dhambi hii huweza kubadili Nia ya muhusika ambayo hapo awali ilikuwa ni kununua viwanja, kuipenda familia ama kuwa na Nia njema kuhusu nduguze na mara baada ya kuanza jambo hili anabadilika na kuwa mtu mwingine na unashangaa anavaliwa na Nia ya ukali, hasira na kadhalika.
6. Maamuzi, uwezo wa maamuzi wa huyu mtu unabadilika, Samsoni alipokubali kukaa kwenye mapaja ya Delila kilichomtokea ni maamuzi yake kujikuta yakitekwa. Mtu anayefanya dhambi hii huwa na maamuzi yasiyokuwa shupavu na mara nyingi hutawaliwa na roho hii.
Ni fika na bayana ya kwamba nalitamani kuendele na somo hili katika sehemu ya 6, ila tukutane siku nyingine katika ujumbe kama huu kwenye somo liitwal HATARAI YA PEPO MAHABA. Na hapo nitakujuza kiunaga ubaga jinsi roho hii inavyofanya kazi hadi kwenye siasa na dini na mtaji wangu mmoja wapo utatoka kwenye kitabu kile cha Ufunuo wa Yohana sura ya 17 anapomtaja yule mwanamke kahaba wa Babeili mwenye jina la siri la Babeli Mkuu mama wa makahaba na machukizo ya nchi pia anahusika na maangamivu.

Anasema wafalume wamezini naye na kujipatia utajiri na kadhalia. Nitakufafanulia sababu za andiko hilo kusema kuwa alilewa, na nafasi ya Damu ya Yesu katika kupigana naye ambayo husimama sehemu kama ya mvinyo umleweshao na namna ya kutumia kikombe cha gadhabu ili kupigana naye ambacho maandiko husema ya kwamba ni kikombe chenye kulevywa na fahamu kikombe hicho ni Agano. Ndiposa katika Luka 22 Yesu akatanaibasha ya kwamba kikombe hiki ni Agano Jipya, (22.20 Kikombe nacho vivyo hivyo baada ya kula; akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu.]) Sasa nitakuelekeza namna ya kuchukuwa KIKOMBE+AGANO kama silaha.
Na fahamu pia maandiko yanasema waliokaa juu ya nchi wamelewa kwa mvinyo wake wa uasherati, ndiposa miziki ya dunia yenye kubeba roho hii inawabamba wengi. Pamoja na uvaaji wa mavazi ya roho hii ambayo mitindo yake hutoka kuzimu moja kwa moja yakiratibiwa na kitengo ama idara hii pamoja na “staili” za kucheza kwenye miziki yao na maudhui ya filamu zilizo nyingi ndiposa nyingine hazikamiliki bila kuonyesha vitendo vya kikahaba na miziki yao na bila mavazi ya kimalaya huku kanisa likijikuta likiiga mavazi na uchezaji wao na kwa upofu wachungaji wamefumbia macho uchezaji huo na uvaaji huo kwa kuwa na Falsafa zilizokufa kiroho za “Eti atuangalii mwili bali ni roho”, NINANI ALIYE WALOGA HAWA? Paulo Mtume anasema ya kwamba sisi ni barua, na maandiko hututaka tuvae mavazi ya Staha ama yatusitirio huku wanaume wakivaa mavazi ya kiume na wanawake wakivaa mavazi ya kike.
(Tafadhi naona Upako wakiinjilisti unatiririka, tukutane kwenye programu yangu mpya ya Tv on Line ikiwa ni Mwanzo wa Ug Tv, ambayo itagusia maswala haya na nitavaa pia kofia ya kiinjilisti.)
Nitajibu pia hoja ya watu wanaodai kwamba walipokuwa watumishi na kujikuta wamaetoka kwenye mstari wa Mungu kwa kuhitaji nguvu za kihuduma kwa upande wa shetani walijikuta wakiwa baharini na kuhitajika kuzini na mwanamke aliyetoka baharini (Kwenye maji, na andiko hilo la Ufunuo humtaja Mama huyu wa Machafuko kuwa anatoka majini: Hakiki jambo hili,
Ufunuo wa Yohana
17.1 Akaja mmoja wa wale malaika saba, wenye vile vitasa saba, akanena nami, akisema, Njoo huku, nitakuonyesha hukumu ya yule kahaba mkuu aketiye juu ya maji mengi;) na nitakwambia ni huyu au jirani yake. Na hapo hapo nitakupa jibu la kiumbe kiitwacho Nguva na siri ya wanamuziki na waigiza filamu ama watu wakisirikina kutumia picha za wanawake warembo wakiwa baharini na namna ishara ya samaki inavyomuwakilisha Pepo Mahaba, na nitagusia kitengo ama idara ya vita ama jeshi la Pepo Mahaba linavyofanya kazi kwenye ulimwengu wa roho.
Langu jina ni mwalimu Oscar Samba wa Ug Ministry mtoto wa pili wa Mama Flora wa Mzee Samba. Tukutane kesho kwenye makala nyingine iliyo Murwa na hakika itakujenga vilivyo.

Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa Upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.
Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigospel.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              
Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni