Alhamisi, 1 Juni 2017

NAMNA YA KUJINASUA KWENYE VIFUNGO VYA PEPO MAHABA. Sehemu ya 2.

Karibu tena katika muendelezo wa makala hii ya kiroho na leo tunaendelea na dalili za mtu anayesumbuliwa na Mapepo Mahaba ikiwa ni somo lenye dhima ya kukunasuma na mateso hayo na nisehemu ya kitabu chang cha NGUVU YA NDOTO KWENYE ULIMWENGU WA ROHO.Pia kama hujasoma sehemu ya kwanza jitaidi uisome ili kujua tutokapo na tuendapo.
Kushindwa kujizuia, kutazama au kufwatilia kitu chenye kushawishi kufanya ngono. Aliyetawaliwa na Roho wa Mungu huwa mwepesi kufwatilia mambo ya Kiungu. Alikadhalika aliyevaliwa na roho ya mpira pia huwa mwepesi wa kufwatilia na hushindwa kujizuia kuacha kufwatilia maswala ya kimpira. Na hii ni matokeo ya roho hizo kukamata uwezo wa maamuzi yao, fahamu kuwa uwezo wa maamuzi upo kwenye nafsi, na nafsi ndiyo inayoratibu shuhuli na matendo ya mtu kwa kivuli cha moyo.

Kwa hiyo mtu aliyekaliwa na Mapepo Mahaba hujikuta akilazimika kutizama picha za Utupu, Maumbile ya yatamanishayo ama sehemu zake kwa mshichana/mvulana.
Hata kutizama baadhi ya miziki kwa lengo la kuona hayo maumbile ama kukodolea macho magazeti au majarida yenye picha za mapepo za watu walio katika mkao wa kimapepo mahaba.
Hutamani hata kushika mkono na mtu aliyemtamani, au kuongea naye huku akiwa hana hoja ya msingi, ama kuingia gharama yoyote ile ikiwemo kununua vocha na kumpigi ama kuwasilia na mtu kwa dhumuni la kupiga hadithi za kimahaba bila kujali gharama atakayo itumia na kulinganisha na uwezo wake kiuchumi, ndio maana wengine hufanya kazi za sulubu na kupata kipato kidogo lakini huweza kuishia kuhonga bila kufanya jambo la msingi na fedha hiyo. Miongoni mwa tabia ya Pepo Mahaba ni kuleta Umasiki/Utumwa kifikra au kimaisha.
Unakuta mtu anafwatilia hadidhi kama hizi aidha kwenye intanenti au jarida fulani ama filamu au tamfilia kwa gharama kubwa na kwa kupoteza muda mwingi. Utumwa huu ni mbaya maana hupoteza muda, fedha na huathiri uwezo wa mhusika kufikiri huku ukifungua milango ya dhambi na ndoto za kishetani.
Kuwa mwepesi wa kifkra za kimahaba hata kwa jambo au mambo yasiyoendana. Maandiko kwenye kitabu kile cha Mithali hutamka bayana kuhusu jambo hili, Mithali 23:7a maana aonavyo nafsini mwake ndivyo alivyo.. Bibilia ya kingereza imetumia neno afikirivyo (think) badala ya neno aonavyo, kwa huyo liweke hapo ilo neno na usome kwa upya msatari huo. “maana awazavyo/afikirivyo nafsini mwake ndivyo alivyo”. Kwa mantiki hiyo ni kwamba nafsi ya mtu iliyovaliwa na Mapepo Mahaba, hufikiri kimapepo mahaba ama kufikiri kwa huyu mtu ni matokeo ya Pepo huyu kukaa ndani yake.
Unaweza ukatoa maneno ambayo hayahusiani na mahaba ila unashangaa mtu fulani akicheka au kutabasamu na ukichunguza unakuta alifikiria jambo jingine. Uonapo hilo jua ndani yake ipo kambi ya Jini Mahaba.
Mfano unaweza kuzungumzia juu ya tunda la mti wa katikati ya Edeni ila yeye fikra zake huenda kwenye maeneo ya katikati ya mwili.
Ugumba au Utasa, Mapepo haya huwa na tamaduni za kumzuia mtu kupata mtoto ingawaje kibaolojia huweza kuwa na uwezo huo. Kumbuka kila pepo mahaba humkalia mtu akiwa na shabaha fulani na miongoni mwayo yaweza kuwa hii ya utasa ama ugumba.
Matatizo katika siku za mwezi, Pia mapepo haya huusika katika kuleta maumivu yasiyo ya kawaida katika siku za hethi ama mwezi kwa mwanamke. Ya weza kuwa maumivu ya kiuno, kichwa ama tumbo. Pia kwa wengine hushidwa kuziona siku zao kabisa ama kupitiliza nje ya sababu za kibaolojia. Kumbuka swala la mwezi la weza kusumbua kikawaida ila hapa silizungumzii kwa taswira hiyo.
Ndoa:
108
UNYUMBA HUSUMBUA, NDOA YENYE PEPO HUYU HUSUSANI MWANANDOA ALIYEINGILIWA HUWA NA UTAMADUNI WA KUKOSA LADHA NA TENDO HUSIKA NA KUKINAI MAPEMA HUKU MWENZAKE AKITESEKA KWA KUKOSA TENDO HILO AU KUPATA USHIRIKIANO ULIO DUNI. KUKOSEKANA KWA TENDO LA NDOA HULETA MAATHIRIKO MAKUBWA SANA YA KISAIKOLOJIA NA KUIFANYA NDOA KUWA NA UPWEKE HUKU IKIMUNG’UNYUA AU KULA POLE POLE TUNDA LA UPENDO. TENDO HILI WANASAIKOLOJIA HUSEMA KWAMBA HUIMARISHA NDOA KWA ASILIMIA KUMI NA TANO (15%) LIKIPATIKA VYEMA NA LIKIKOSEKANA HUVUNJA NDOA AMA HUWA SABABU YA NDOA KUVUNJIKA KWA ASILIMIA THEMANINI NA TANO, (85%).
Unaweza ukaona taswira hiyo kwamba Mapepo haya yana mathara makubwa kiasi gani katika kusambaratisha ndoa za watu.
Namna ya kuishi na Mwanadoa mwenzako mwenye Pepo Mahaba.
Inakupaswa wewe unayenyimwa kuwa mvumilivu huku ukilifanyia maombi swala hilo. Sehemu sahihi zaidi ni kwa Mungu. Pia kama mwenzako ni muelewa kwamba hiyo siyo hali ya kawaida bali inahitaji maombi ili mshirikiane kwa pamoja. Mapepo haya pia huweza kumfanya hata mwenzako kutokupika au kufua, yaani kutimiza wajibu wake kama mwanandoa na ukimuliza huwa mkali na mwenye majibu ya umizayo, ingawaje baadaye hujijutia ila hurudia tena. Na kwa mwanaume huweza kuwa mkali bila sababu ya msingi kumpiga mke, kumtukana au kuchelewa kuja nyumbani na pia kupoteza mvuto mkewe. Lakini katika kupoteza mvuto au upendo huweza kuchangiwa na matendo ya mwezake kama ndiye mwenye mapepo hayo. Zaidi soma kipengele cha Dalili ya ndoa yenye mapepo mahaba kilichopo kurasa zinazofwatia.
Mara baada ya kuota hujikuta unamchukia mwenzako bila sababu za msingi. Jini Mahaba huwa na tabia ya wivu sana na hii ndiyo inayochangia kumfanya mhusika kuwa na chuki kuu kwa mwenzi wake.
Kutamani kufanya tendo hilo na mtu mwingine angali mwenzako yupo. Pepo hili huwa na tabia za kumtamani mtu yeyote limpendalo na huambukiza au hutumia mwili wa aliyeukalia. Utamkuta mtu ana upendo  wakipepo kwa mtu fulani wakati ndani mwenzake yupo. Na hata sio mwanandoa hujikuta akitamani watu ambao sio utashi wake kufanya hivyo
Kuishiwa nguvu au hamu ya kufanya tendo hilo na mwenzako. Kuna mwanaume mmoja aliyekuwa na hali hii ambayo kiungo chake husika kilishindwa kuwa katika hali ya tendo. Ila mke wake alikuwa ni mtu wa kiroho na kusema “hali hii sii ya kawaida”. Alikishika na kufanya maombi, mara baada ya muda hali ikarejea na kuwa kawaida.
Ikimkuta mwanamke hali hii huweza kumfanya kutokuwa na ladha na tendo husika na pia kumuona mwenzake kama anamsumbua au kumpotezea muda. Hali hii ikiongezeka au kukomaa huweza kusababisha ugomvi wakati wa tendo au mmoja wapo anapohitaji na Pepo hili likikomaa ndani ya mtu muhusika huweza kumtharau mwingine au kumtusi kwa maneno.
Pamoja na Utasa ama Ugumba, Kumekuwa na kilio kikubwa kwa wanandoa kukosa watoto na mara nyingi tatizo hilo huwa ni matokeo ya ndoa hiyo ama mwanandoa kutawaliwa na Pepo mahaba. Linaweza kupata uwalali kwa njia nitakazokujuza kwenye kipengele kijacho ama kwa mtu kumwendea mwenzake kwenye njia za kishirikina ili kumfunga ikiwemo kwa waganga wakienyeji ama kumloga. Katika hayo yote ipo Damu ya Yesu iwezayo kumkomboa huyu mtu na kumbuka katika sehemu yangu ya kwanza ya makala hii nilimtaka mlengwa anayesumbuliwa na Mapepo haya kuokoka kwani ni njia kuu ya ukombozi na kama ameshaokoka ya mpasa kusimama kiroho na kupambambana kimaombi. Pia nitakuelekeza namna ya kuomba ndio maana nikakwambia ni somo la NAMNA AYA KUJINASUA.
MLANGO UNAOWEZA KUIFUNGUA NDOTO YA MAPEPO MAHABA.
(1) Uhalali wa kuridhi, Kitovu chako hakikukatwa, wala kuoshwa kwa maji na kutiwa chunvi, maana yake ipo nguvu ya kurithi inayoyasumbua maisha yako. Kwani kitovu huwakilisha hali ya kuridhi maana mtoto hulishwa na mamaye kupitia kitovu. Na maji ni utakaso wa Roho Mtakatifu na chunvi huondoa mapooza. Kwa hiyo kama nyumbani kwenu kuna tatizo litokanalo na Pepo mahaba ama roho ya Pepo huyu inakalia jamii ya kwenu ama kabila au eneo ulilopo ni fika adui huyu huweza kukusumbua ndotoni na mlango mkubwa ikiwa ni hali hii.
Dalili/Ishara zitakazokujulisha uwepo wa Pepo Mahaba kwa njia ya Uridhi. (….Tuonane Kesho)
Pasina shaka umependezwa na kujengwa na ujumbe huu katika sehemu hii ya pili, kipengele nilichokudokezea hapa mwishoni ndiho tutakacho anza nacho kesho katika sehemy ya 3 ya ujumbe huu. Kwa hiyo hakikisha unatufwatilia. Na Mungu akubariki.

Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigospel.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              

Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa                                                                          2 DAY SKY: https://www.2daysky.com/home

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni