Tunaanza na Utangulizi (kinapatikana Google Bure)
Na Mwl. Oscar Samba
Utangulizi
Kitabu hiki kimenuia kumsaidia mtu ambaye yupo katika mazingira
magumu ya kimaamuzi, na mbele yake kuna aina zaidi ya moja ya
maamuzi ambayo anahatarishwa kuyachukuwa au yanayomkabili,
inawezekana lililo hatari ni moja, au salama ni moja ila kuna zaidi ya
aina mbili au moja na kadhalika.
Kitabu hiki ni matokeo ya sehemu ninayopitia sasa kuhusu ndoa yangu.
Ikumbukwe sasa ni mwaka unaokaribia wa nane toka mwenzangu
tuoane na kujikuta ananiacha kwa talaka mahakamani hali inayonipa au
kunipelekea kuwa njia panda. Njia panda yangu inaweza isiwe na tija
sana kwako ila la muhimu ni wewe kufahamu mazingira ya kitabu
hiki ili kikusaidia. (Wakati nakitoa, imetimia miaka 10/11, “2015-
2015”.)
Unaweza usione umuhimu wake kwa leo ila nikuhakikishie kuwa
chakula hiki ni kama akiba, kuna muda tunakula leo lakini chakula
hicho kinatusaidia kesho; sio kwamba tuliingia kwenye mfungo la! Bali
homa ya ghafula imetukuta na kutunyima hamu au uwezo wa kula. Ila
kwa akiba ya jana ambayo hatukuwa hata na wazo la kula tumevuka leo
salama!
….Nikikuongezea ni kwamba, mara baada ya kuandika
utangulizi huu, na nikiwa tayari nimeshaanza kukiandika hiki
kitabu, njia panda nyingine ilijitokeza kama sio moja basi ni
zaidi, licha ya swala la ndoa, lakini pia limeibuka swala la
kusimamishwa masomo chuoni. Kumbuka nipo katika chuo cha
Biblia Dodoma cha CBC; mara baada ya kutofautiana na
kiongozi wangu mmoja wapo katika swala fulani, nilijikuta
nikipewa adhabu ya kusimamishwa masomo mwaka mmoja.
Nikiwa tu nimetoka kuchukuwa barua zangu, (ikiwa moja yangu na ya
mchungaji wangu kingozi,) ndipo nilipokutana na mchungaji mmoja wa
dhehebu jingine akiniambia kuwa nihamie kwake. Maana huku
kumekuwa kugumu kwangu na katoa sababu kadhaa: zingeweza
kuonekana ni zenye mashiko maana nyuma ya pazia jambo langu
limeonekana ni matokeo ya mimi kuwa na tabia ya kutetea na kudai haki. Pamoja na kusema ukweli pale ambapo ninapoona mambo
hayajaka sawa.
Wazo hili halikwepo kabisa kichwani mwangu, maana nilishapitia
mahali kama hapa mara baada ya uongozi wangu wa sehemu huko
Arusha kutofautina nami na kunichukulia mamuzi ambayo sikuyapenda
maana sikusikilizwa kimapana!