Jumamosi, 23 Mei 2026

. Chuki Ina Nguvu Kama Mauti. Kati ya jambo la ajabu sana nililojifunza na ningependa ulifahamu; ni hili la nguvu ya chuki. Ni hakika chuki ina nguvu sawa na roho ya mauti. Lakini pia chuki hutenda kazi kama ilivyo roho ya mauti. Sio jambo jepesi kulielewa kama halijawahi kukuta ama kama hujawahi kujifunza somo hili kwa sura ya namna hii. Na Mwl Oscar Samba Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu Chetu cha IMANI INAPOJARIBIWA; Karibu... Walipomchukia Yusufu na kumuuza; ni wazi alishakufa ndani ya mioyo yao. Katika kujifunza hili somo nilijikuta nawaza hivi ilikuaje wakati Yakobo analia na kuomboleza wale ndugu wakawa kimya sana, na wakamuacha baba yao akiwa analia siku zote na kukaa hali ya ukiwa? Liliwezekanaje jambo hili! Yaani katika maombolezo makuu namna hii hawa ndugu bado wapo kimya tu! Tazama; Mwanzo 37:34 Yakobo akararua mavazi yake, akajivika gunia viunoni, na kumlilia mwanawe siku nyingi. 35 Wanawe wote, na binti zake wote, wakaondoka wamtulize, lakini akakataa kutulizwa, akasema, La! Nitamshukia mwanangu, nikisikitika, hata kuzimu. Baba yake akamlilia. Maneno kama haya, waliyashuhudia: "Nitamshukia mwanangu, nikisikitika, hata kuzimu. Baba yake akamlilia." Katika kumtuliza baba yao nao hao waliomuuza walikwepo. Huo mstari anaposema binti na wana, uwe na hakika Biblia ya Kingereza imetumia neno "sons" ikiwakisha wana wa kiume. Nao wanahusika katika kumtuliza, angali ndio waliomuuza; Mwanzo 37:35 Wanawe wote, na binti zake wote, wakaondoka wamtulize, lakini akakataa kutulizwa, akasema, La! Nitamshukia mwanangu, nikisikitika, hata kuzimu. Baba yake akamlilia. And all his sons and all his daughters rose up to comfort him; but he refused to be comforted; and he said, For I will go down into the grave unto my son mourning. Thus his father wept for him. (Neno wote limetumika.) Nalijiuliza sana huu ujasiri ulitoka wapi; Mwanzo 37:32 Wakaenda nayo ile kanzu ndefu, wakamletea baba yao, wakasema, Tumeona hii; basi, utambue kama kanzu hii ni ya mwanao, ama siyo. 33 Akaitambua, akasema, Ndiyo kanzu ya mwanangu, mnyama mkali amemla; bila shaka Yusufu ameraruliwa. Baada ya kufikiri sana mahali huo ujasiri ulipotoka, ndipo nilipokuja kutambua ya kwamba, chuki ina nguvu kama mauti. Kwa maana kwamba, waliposema tumue, alikuwa ameshakufa kwanza kwenye mioyo yao. Wanasaikolojia wanasema hivi; kabla mtu hajamua mtu, anaanza kuiuwa dhamiri yake kwanza, ndipo auwe mtu. (Kifo cha kukusudia.) Yusufu ni kweli alishakufa kwenye mioyo yao. Hapa ilikuwa ni madhiirisho tu! Tazama; Mwanzo 37:20 Haya, twende, tukamwue na kumtupa katika birika mojawapo, nasi tutasema, Mnyama mkali amemla; kisha tutaona zitakuwaje ndoto zake. Ndio maana waliweza kumuuza na wakamsahau kabisa. Haya ni majibu ya swali nililokuwa najiuliza, ya kwamba ilikuaje wakamuuza sawa; ila wakaweza kumsahau kabisa kwa muda wa miaka 27? Na "actually" walishamsahau kabisa, kabisa. Maana kama asingalisimama mbele yao wakati wamekimbilia Misri, bado kumbukumbu lake lisingali kwepo. Kumuuza ni sawa, labla ni matokeo ya kughafilika tu; lakini kumsahau kabisa, kabisa! Hili sii jambo dogo hata kidogo. Tena ndugu wa damu! Nilikuwa nawaza mimi binafsi ya kwamba hawa watu ni kweli wamenifukuza kazi, tena bila kunisikiliza au kupewa nafasi ya kujibu mashitaka yao...lakini wanawezaje kunisahau namna hii! Sizioni hata fadhili za kanisa, ni kama vile sikuwahi kusimama mbele yao kabisa kabisa. Ndipo Roho Mtakatifu akanisemesha kwa ndani; chuki ina nguvu kama mauti. Kwenye moyo wao ulishakufa. Haiwezekani kumsahau Yusufu kana kwamba kweli kafa, kumbe angali hai. Ukiona hivyo, ndani yao ni kweli amekufa. Nilijifunza pia chuki ina tabia ya kukua na kuambukizwa. Sasa eneo la kuambukizwa sitalisemea, maana kuna wengine wanashiriki kukuchukia angali hukuwahi kuwakosea lolote. Nataka kukugusia eneo la kukua. Hapo awali walikuwa wanamchukia kwa kiwango fulani, lakini hapa; chuki ilizidi kukua. Maana chuki inayolandana na mauti, ni chuki yenye kiwango kikubwa kabisa. Na kwangu tukio la kuoa, lilikuza chuki kwa kiwango kikubwa sana. Usiniulize kwa nini? Kwa Yusufu ni hili hapa; Mwanzo 37:5 Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia. Hiyo ndoto ilileta chuki, hapana shaka kabisa ilikwepo ikaongezeka. Lakini mstari ujao linaongezeka neno na maneno yake. Ina maana wazi kabisa Yusufu kwa kuwa alikuwa na ujuzi wa kutafsiri ndoto, aliwapa na tafsiri yake. Kitu kilichokuza chuki zaidi, na zaidi. Mwanzo 37:8 Ndugu zake wakamwambia, Je! Kweli wewe utatumiliki sisi? Nawe utatutawala sisi? Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake, na kwa maneno yake. Ndoto ya pili iliongeza au ilikuza tena kiwango cha chuki; Mwanzo 37:11 Ndugu zake wakamhusudu; bali baba yake akalihifadhi neno hili. Watu wengi hawajui ya kuwa azimio na kikao rasmi cha kumua Yesu kilizaliwa au kuja mara baada ya muujiza wa kufufuka kwa Lazaro. Ni kweli awali walikuwa wakimuwinda, ila hapa ndipo chuki ilipokuwa na kufikia ukomo. Hatua isiyovumilika kabisa kabisa. Sifa ya chuki iliyofikia hatua hii, ni mtu kuwa radhi kufanya lolote ili tu akuangamize. Hatajali hatima yako, maana mauti ina tabia za namna hiyo. Tazama; Yohana 11:45 Basi wengi katika Wayahudi waliokuja kwa Mariamu, na kuyaona yale aliyoyafanya, wakamwamini. 46 Lakini wengine wakaenda zao kwa Mafarisayo, wakawaambia aliyoyafanya Yesu. 48 Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu. 49 Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote; 50 wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima. Chuki kwa Daudi ilikwepo, lakini ilikua zaidi kutoka kwa Sauli mfalme, kwa sababu ya tukio hili; 1 Samweli 18:6 Hata ikawa, walipokuwa wakienda, hapo Daudi aliporudi baada ya kumwua yule Mfilisti, wanawake wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda. 7 Nao wale wanawake wakaitikiana wakicheza, wakasema, Sauli amewaua elfu zake, Na Daudi makumi elfu yake. 8 Basi Sauli akaghadhibika sana, na maneno haya yakamchukiza; akasema, Wamempa Daudi makumi elfu, na mimi wamenipa elfu tu; kuna nini tena awezayo kupata, isipokuwa ni ufalme? 9 Sauli akamwonea Daudi wivu tangu siku ile. 10 Ikawa siku ya pili yake, roho mbaya kutoka kwa Mungu ikamjilia Sauli kwa nguvu, naye akatabiri ndani ya nyumba. Basi Daudi alikuwa akipiga kinubi kwa mkono wake kama siku zote; naye Sauli alikuwa na mkuki mkononi mwake. 11 Mara Sauli akautupa ule mkuki; maana alisema, Nitampiga Daudi hata ukutani. Daudi akaepa, akatoka mbele yake, mara mbili. Shetani ana tabia ya kupanda chuki ndani ya moyo wa mtu pole-pole, anajua anachokifanya. Kuna siku anafahamu itakuwa, na kisha kubeba mimba, itazaa mwana tu. Kiufupi ni kwamba, chuki ina tabia ya kupasuka kama nyongo. Nimepita mikononi mwa wachunguji na viongozi kadhaa. Mkuu wangu akinichukia huwa na mpa muda tu. Najua asipotumbua hilo jipu na kukamua mapema; litakuja kupasuka tu. Ndio maana nimekuwa nikiishi kama mgeni katika mazingira ya namna hii. Hili ni jambo nililojifunza tangu awali. Kuwa makini sana na mtu anayekuchukia. Huwa nasema hivi, kuna watu wakikosa uchafu chumbani kwako; wanaenda kwenye "dustbin" au chombo cha takataka cha hapo ndani ama nje na kupekua. Wakikosa na hapo huwa wanaenda jalalani, kisha wanachukua uchafu na kuja kuumwaga sebleni kwako. Wanapiga picha na kusema ushahidi huu hapa tunao kumuhusu huyu mtu. Epuka sana watu wanaokaa kikao cha kuuwa, kisha ndipo wanatafuta makosa yako. Sio kosa linawasukuma kukuuwa, bali ni chuki. Kisha hiyo chuki inahalalishwa kwa makosa waliojiokotea. Ndivyo ilivyokuwa kwa Yesu. Yaani, unahukumiwa kabla hata ya kukutwa na kosa. Na ndivyo viongozi wetu wengi wa kidini walivyo. Lakini ashukuriwe Mungu ambaye hatuachi tuwe mateka wa adui zetu. Wanandaa mauti, lakini Bwana anaigeuza na kuwa ushindi. Ingawaje ni kweli majira haya yanaumiza sana. Ila ndio njia ambayo mashujaa wengi hupita. Nimejikuta nikimuomba Mungu awaondoe moyoni mwangu kama walivyoniondoa wao. Anipe kuwasahau kama walivyo nisahau. Wafe kwenye nafsi yangu, kama nilivyotangulia kufa ndani yao. Maana nikifikiria jinsi nilivyojitoa, moyo unaumia kama ule wa Daudi katika Zaburi. Maana sio jambo la kawaida hata wazee wa kanisa kwa umoja wao waseme tumjuliye hali mchungaji, jamani hata mashemasi nao! Mshirika mmoja akaniambia baba, nimeambiwa eti hapa ndio utamaduni wetu ya kwamba mchungaji akishaondoka ndo ameondoka, hairuhusiwi hata kumpigia simu! Ninachojua ni kwamba chuki imewaambukiza lakini kila penye chuki kuna sheria. Ukishangaa sheria kwenye chuki nenda katika Danieli, mashujaa watatu na Danieli wenyewe ilibidi ipitishwe sheria ili kuwatia hatiani. Lakini sheria ya kulinda chuki utaikuta kwa Mafarisayo, walishatangaza kuwatenga watu na sinagogi kama watamkiri Yesu kama Masihi na kadhalika. Na kweli hata sasa watu huwa katika kundi fulani kama wataambana na mtu ambaye mkuu kwa hila zake mwenyewe kaamua kumchukia. Sauli alipomchukia Daudi, alisababisha ufa mkubwa. Kukawa na kundi la Daudi na la Sauli. Watu walilazimika kujipendekeza kwa mfalme ili kulinda ugali wao. Kuna sheria za "wananzengo" (kwa kanda ya ziwa ni wana jamii wa mtaa mmoja,) ya kwamba mtu akitengwa na "nzengo" alafu wewe ukashirikiana naye, au ukaenda kwake; na wewe unatengwa. Hii ni tabia ya roho ya chuki. Ikusaidie kukujibu mbona hadi fulani na fulani nao wamenichukia! Nimemuomba Mungu pia ya kwamba, nafsi yangu iweze kutambua ya kuwa Bwana ameshanitenga nao. Hii itanisaidia kuniondolea maumivu na kutokuwatazama tena moyoni mwangu. Hakiki hapa kuhusu nguvu ya chuki kimauti: nikuonye tena; kuwa makini na mtu anayekuchukia; 1 Yohana 3:15 Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji: nanyi mnajua ya kuwa kila mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake

Kati ya jambo la ajabu sana nililojifunza na ningependa ulifahamu; ni hili la nguvu ya chuki. Ni hakika chuki ina nguvu sawa na roho ya mauti. Lakini pia chuki hutenda kazi kama ilivyo roho ya mauti. Sio jambo jepesi kulielewa kama halijawahi kukuta ama kama hujawahi kujifunza somo hili kwa sura ya namna hii. Na Mwl Oscar Samba Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu Chetu cha IMANI INAPOJARIBIWA; Karibu... Walipomchukia Yusufu na kumuuza; ni wazi alishakufa ndani ya mioyo yao. Katika kujifunza hili somo nilijikuta nawaza hivi ilikuaje wakati Yakobo analia na kuomboleza wale ndugu wakawa kimya sana, na wakamuacha baba yao akiwa analia siku zote na kukaa hali ya ukiwa? Liliwezekanaje jambo hili! Yaani katika maombolezo makuu namna hii hawa ndugu bado wapo kimya tu! Tazama; Mwanzo 37:34 Yakobo akararua mavazi yake, akajivika gunia viunoni, na kumlilia mwanawe siku nyingi. 35 Wanawe wote, na binti zake wote, wakaondoka wamtulize, lakini akakataa kutulizwa, akasema, La! Nitamshukia mwanangu, nikisikitika, hata kuzimu. Baba yake akamlilia. Maneno kama haya, waliyashuhudia: "Nitamshukia mwanangu, nikisikitika, hata kuzimu. Baba yake akamlilia." Katika kumtuliza baba yao nao hao waliomuuza walikwepo. Huo mstari anaposema binti na wana, uwe na hakika Biblia ya Kingereza imetumia neno "sons" ikiwakisha wana wa kiume. Nao wanahusika katika kumtuliza, angali ndio waliomuuza; Mwanzo 37:35 Wanawe wote, na binti zake wote, wakaondoka wamtulize, lakini akakataa kutulizwa, akasema, La! Nitamshukia mwanangu, nikisikitika, hata kuzimu. Baba yake akamlilia. And all his sons and all his daughters rose up to comfort him; but he refused to be comforted; and he said, For I will go down into the grave unto my son mourning. Thus his father wept for him. (Neno wote limetumika.) Nalijiuliza sana huu ujasiri ulitoka wapi; Mwanzo 37:32 Wakaenda nayo ile kanzu ndefu, wakamletea baba yao, wakasema, Tumeona hii; basi, utambue kama kanzu hii ni ya mwanao, ama siyo. 33 Akaitambua, akasema, Ndiyo kanzu ya mwanangu, mnyama mkali amemla; bila shaka Yusufu ameraruliwa. Baada ya kufikiri sana mahali huo ujasiri ulipotoka, ndipo nilipokuja kutambua ya kwamba, chuki ina nguvu kama mauti. Kwa maana kwamba, waliposema tumue, alikuwa ameshakufa kwanza kwenye mioyo yao. Wanasaikolojia wanasema hivi; kabla mtu hajamua mtu, anaanza kuiuwa dhamiri yake kwanza, ndipo auwe mtu. (Kifo cha kukusudia.) Yusufu ni kweli alishakufa kwenye mioyo yao. Hapa ilikuwa ni madhiirisho tu! Tazama; Mwanzo 37:20 Haya, twende, tukamwue na kumtupa katika birika mojawapo, nasi tutasema, Mnyama mkali amemla; kisha tutaona zitakuwaje ndoto zake. Ndio maana waliweza kumuuza na wakamsahau kabisa. Haya ni majibu ya swali nililokuwa najiuliza, ya kwamba ilikuaje wakamuuza sawa; ila wakaweza kumsahau kabisa kwa muda wa miaka 27? Na "actually" walishamsahau kabisa, kabisa. Maana kama asingalisimama mbele yao wakati wamekimbilia Misri, bado kumbukumbu lake lisingali kwepo. Kumuuza ni sawa, labla ni matokeo ya kughafilika tu; lakini kumsahau kabisa, kabisa! Hili sii jambo dogo hata kidogo. Tena ndugu wa damu! Nilikuwa nawaza mimi binafsi ya kwamba hawa watu ni kweli wamenifukuza kazi, tena bila kunisikiliza au kupewa nafasi ya kujibu mashitaka yao...lakini wanawezaje kunisahau namna hii! Sizioni hata fadhili za kanisa, ni kama vile sikuwahi kusimama mbele yao kabisa kabisa. Ndipo Roho Mtakatifu akanisemesha kwa ndani; chuki ina nguvu kama mauti. Kwenye moyo wao ulishakufa. Haiwezekani kumsahau Yusufu kana kwamba kweli kafa, kumbe angali hai. Ukiona hivyo, ndani yao ni kweli amekufa. Nilijifunza pia chuki ina tabia ya kukua na kuambukizwa. Sasa eneo la kuambukizwa sitalisemea, maana kuna wengine wanashiriki kukuchukia angali hukuwahi kuwakosea lolote. Nataka kukugusia eneo la kukua. Hapo awali walikuwa wanamchukia kwa kiwango fulani, lakini hapa; chuki ilizidi kukua. Maana chuki inayolandana na mauti, ni chuki yenye kiwango kikubwa kabisa. Na kwangu tukio la kuoa, lilikuza chuki kwa kiwango kikubwa sana. Usiniulize kwa nini? Kwa Yusufu ni hili hapa; Mwanzo 37:5 Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia. Hiyo ndoto ilileta chuki, hapana shaka kabisa ilikwepo ikaongezeka. Lakini mstari ujao linaongezeka neno na maneno yake. Ina maana wazi kabisa Yusufu kwa kuwa alikuwa na ujuzi wa kutafsiri ndoto, aliwapa na tafsiri yake. Kitu kilichokuza chuki zaidi, na zaidi. Mwanzo 37:8 Ndugu zake wakamwambia, Je! Kweli wewe utatumiliki sisi? Nawe utatutawala sisi? Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake, na kwa maneno yake. Ndoto ya pili iliongeza au ilikuza tena kiwango cha chuki; Mwanzo 37:11 Ndugu zake wakamhusudu; bali baba yake akalihifadhi neno hili. Watu wengi hawajui ya kuwa azimio na kikao rasmi cha kumua Yesu kilizaliwa au kuja mara baada ya muujiza wa kufufuka kwa Lazaro. Ni kweli awali walikuwa wakimuwinda, ila hapa ndipo chuki ilipokuwa na kufikia ukomo. Hatua isiyovumilika kabisa kabisa. Sifa ya chuki iliyofikia hatua hii, ni mtu kuwa radhi kufanya lolote ili tu akuangamize. Hatajali hatima yako, maana mauti ina tabia za namna hiyo. Tazama; Yohana 11:45 Basi wengi katika Wayahudi waliokuja kwa Mariamu, na kuyaona yale aliyoyafanya, wakamwamini. 46 Lakini wengine wakaenda zao kwa Mafarisayo, wakawaambia aliyoyafanya Yesu. 48 Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu. 49 Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote; 50 wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima. Chuki kwa Daudi ilikwepo, lakini ilikua zaidi kutoka kwa Sauli mfalme, kwa sababu ya tukio hili; 1 Samweli 18:6 Hata ikawa, walipokuwa wakienda, hapo Daudi aliporudi baada ya kumwua yule Mfilisti, wanawake wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda. 7 Nao wale wanawake wakaitikiana wakicheza, wakasema, Sauli amewaua elfu zake, Na Daudi makumi elfu yake. 8 Basi Sauli akaghadhibika sana, na maneno haya yakamchukiza; akasema, Wamempa Daudi makumi elfu, na mimi wamenipa elfu tu; kuna nini tena awezayo kupata, isipokuwa ni ufalme? 9 Sauli akamwonea Daudi wivu tangu siku ile. 10 Ikawa siku ya pili yake, roho mbaya kutoka kwa Mungu ikamjilia Sauli kwa nguvu, naye akatabiri ndani ya nyumba. Basi Daudi alikuwa akipiga kinubi kwa mkono wake kama siku zote; naye Sauli alikuwa na mkuki mkononi mwake. 11 Mara Sauli akautupa ule mkuki; maana alisema, Nitampiga Daudi hata ukutani. Daudi akaepa, akatoka mbele yake, mara mbili. Shetani ana tabia ya kupanda chuki ndani ya moyo wa mtu pole-pole, anajua anachokifanya. Kuna siku anafahamu itakuwa, na kisha kubeba mimba, itazaa mwana tu. Kiufupi ni kwamba, chuki ina tabia ya kupasuka kama nyongo. Nimepita mikononi mwa wachunguji na viongozi kadhaa. Mkuu wangu akinichukia huwa na mpa muda tu. Najua asipotumbua hilo jipu na kukamua mapema; litakuja kupasuka tu. Ndio maana nimekuwa nikiishi kama mgeni katika mazingira ya namna hii. Hili ni jambo nililojifunza tangu awali. Kuwa makini sana na mtu anayekuchukia. Huwa nasema hivi, kuna watu wakikosa uchafu chumbani kwako; wanaenda kwenye "dustbin" au chombo cha takataka cha hapo ndani ama nje na kupekua. Wakikosa na hapo huwa wanaenda jalalani, kisha wanachukua uchafu na kuja kuumwaga sebleni kwako. Wanapiga picha na kusema ushahidi huu hapa tunao kumuhusu huyu mtu. Epuka sana watu wanaokaa kikao cha kuuwa, kisha ndipo wanatafuta makosa yako. Sio kosa linawasukuma kukuuwa, bali ni chuki. Kisha hiyo chuki inahalalishwa kwa makosa waliojiokotea. Ndivyo ilivyokuwa kwa Yesu. Yaani, unahukumiwa kabla hata ya kukutwa na kosa. Na ndivyo viongozi wetu wengi wa kidini walivyo. Lakini ashukuriwe Mungu ambaye hatuachi tuwe mateka wa adui zetu. Wanandaa mauti, lakini Bwana anaigeuza na kuwa ushindi. Ingawaje ni kweli majira haya yanaumiza sana. Ila ndio njia ambayo mashujaa wengi hupita. Nimejikuta nikimuomba Mungu awaondoe moyoni mwangu kama walivyoniondoa wao. Anipe kuwasahau kama walivyo nisahau. Wafe kwenye nafsi yangu, kama nilivyotangulia kufa ndani yao. Maana nikifikiria jinsi nilivyojitoa, moyo unaumia kama ule wa Daudi katika Zaburi. Maana sio jambo la kawaida hata wazee wa kanisa kwa umoja wao waseme tumjuliye hali mchungaji, jamani hata mashemasi nao! Mshirika mmoja akaniambia baba, nimeambiwa eti hapa ndio utamaduni wetu ya kwamba mchungaji akishaondoka ndo ameondoka, hairuhusiwi hata kumpigia simu! Ninachojua ni kwamba chuki imewaambukiza lakini kila penye chuki kuna sheria. Ukishangaa sheria kwenye chuki nenda katika Danieli, mashujaa watatu na Danieli wenyewe ilibidi ipitishwe sheria ili kuwatia hatiani. Lakini sheria ya kulinda chuki utaikuta kwa Mafarisayo, walishatangaza kuwatenga watu na sinagogi kama watamkiri Yesu kama Masihi na kadhalika. Na kweli hata sasa watu huwa katika kundi fulani kama wataambana na mtu ambaye mkuu kwa hila zake mwenyewe kaamua kumchukia. Sauli alipomchukia Daudi, alisababisha ufa mkubwa. Kukawa na kundi la Daudi na la Sauli. Watu walilazimika kujipendekeza kwa mfalme ili kulinda ugali wao. Kuna sheria za "wananzengo" (kwa kanda ya ziwa ni wana jamii wa mtaa mmoja,) ya kwamba mtu akitengwa na "nzengo" alafu wewe ukashirikiana naye, au ukaenda kwake; na wewe unatengwa. Hii ni tabia ya roho ya chuki. Ikusaidie kukujibu mbona hadi fulani na fulani nao wamenichukia! Nimemuomba Mungu pia ya kwamba, nafsi yangu iweze kutambua ya kuwa Bwana ameshanitenga nao. Hii itanisaidia kuniondolea maumivu na kutokuwatazama tena moyoni mwangu. Hakiki hapa kuhusu nguvu ya chuki kimauti: nikuonye tena; kuwa makini na mtu anayekuchukia; 1 Yohana 3:15 Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji: nanyi mnajua ya kuwa kila mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake

Jumatano, 6 Mei 2026

KUUJENGA UKUTA KUNA GHARAMA na Shujaa Hushinda Vita

Nehemia alighamua nia ya yule nabii mke na mwovu na alichonuia kukifanya. Alitaka kumjengea hofu kwa kupitia aina fulani ya maneno ili aweze kumuondoa katika kusudi. Adui Shetani alipoona wakina Tobia na Sanbalati wameshindwa kuzuia ukuta kwa njia mbalimbali, aliamua moja kwa moja kutumia njia hii. Lazima ujifunze hatari ya maneno unapokuwa unavikabili vita. Yawe yanatoka kwa adui au mtu mwingine. Na yakitoka kwako huwa mabaya zaidi. Maana Shetani atakufanya kama kiwanda cha kuzalisha hofu itokayo ndani mwako. Mawazo ya kushindwa yatakutawala nawe utazungukwa na kushindwa muda wote. Tazama; Nehemia 6:11 Nami nikasema, Je! Mtu kama mimi nikimbie? Naye ni nani, akiwa kama nilivyo mimi, atakayeingia hekaluni ili kuponya maisha yake? Sitaingia. 12 Nikatambua, na tazama, siye Mungu aliyemtuma; lakini amefanya unabii huu kinyume changu; nao Tobia na Sanbalati ndio waliomwajiri. :13 Kwa sababu hii aliajiriwa, ili mimi niogope, nikafanye hivyo na kutenda dhambi, kisha wao wawe nazo habari mbaya, ili wanishutumie. 14 Uwakumbuke, Ee Mungu wangu, Tobia na Sanbalati sawasawa na hayo matendo yao, na yule nabii mke Noadia, na hao manabii waliosalia, waliotaka kuniogofya. 15 Basi huo ukuta ukamalizika siku ya ishirini na tano ya mwezi wa Eluli, katika muda wa siku hamsini na mbili. 16 Ikawa adui zetu wote waliposikia, ndipo makafiri wote waliotuzunguka wakaogopa, nao wakakata tamaa sana machoni pao wenyewe; maana waliitambua kazi hiyo ilivyotendwa na Mungu wetu. Alitumwa mjumbe, mwenye ujumbe! Sii kila maneno unapaswa kukubaliana nayo. Shujaa huwa makini sana anapokuwa vitani. Sii kila mwanajeshi aliyevaa nguo na zenye nembo kama yako unapaswa kumuamini! Wengine wameajiriwa na wakina Sanbalati ili wakuogofye. Nia yao ni kukutia hofu. Wanajifanya wana mpango mzuri wa kukusaidia, kumbe ni baada ya wao (kama Sanbalati) kukwama katika kukuzuilia kuujenga ukuta. Watakupa maneno mengi ya kwamba huyu ana misimamo mingi sana; ni mtu wa misimamo mikali...wewe usijali. Mimi huwa nasema ya kwamba asiye na misimamo ni maiti pekee. Lakini baadae nafikiria nakusema hata maiti ina misimamo maana imeshachagua upande wa kufa. Na uzima sio sehemu yake tena. Ukiumaliza ukuta ndipo watakapokuja kukuelewa. Usilazimishe kueleweka mapema na kila mtu. Unajua, anayeona unakoelekea ni wewe mwenyewe; kwa hiyo epuka kuwalazimisha wasiona waone kama wewe. Kama kila mtu atafanikiwa kuona kama unavyoona wewe basi hayo sio maono tena. Maono sifa yake moja wapo ni aidha mtu mmoja ama watu wachache kuona kwa niaba ya wengine. Na usikubali wasiona wakalie nafasi ya maamuzi yako. Wengine ni kweli uko nao ila ni wakina Tobia na Sanbalati, hili lazima ulielewe daima. Ukiona mtu unakataa ushauri wake na anakukasirikia au anakuwa mkali kama pilipili; uwe na hakika haukuwa ushauri bali yalikuwa ni maamuzi au maelekezo aliyokuwa anakupatia. Na inapendeza sana kama ukifanikiwa kujua roho iliyo ndani yake kama Nehemia dhidi ya Noadia nabii mke. Maana kama ingelikuwa ni ushauri kusingekuwa na haja ya yeye kukasirika. (Kuna watu fulani waliwahi kunifanyia fitina, moyoni mwangu nikajisemea wanafikiri mimi ni dhaifu kiasi hicho. Ningekuwa dhaifu nisingefika hapa). Nehemia asingekaza katika kusudi ukuta usingejengwa. Utakutana na Ujumbe Huu Katika Kitabu Chetu Kipya cha KUJARIBIWA KWA IMANI

Ijumaa, 10 Aprili 2026

Falsafa ya Mwalimu Oscar Samba ya Kuwa Marehemu Anayeishi

Kijana Mmoja Akaniuliza; Mwalimu Nini Siri ya Mafanikio Yako ? Nataka Kuwa Mwalimu Mzuri Kama wewe. Nami Nikamjibu, "Mimi ni Marehemu Anayeishi." Kuna Watu Wengine Ukiishi Nao, Ukiwa Hai, Watakuuwa: Suluhu Ni Kuwa Marehemu Anayeishi.

Alhamisi, 26 Machi 2026

Aina za Upako

Pichani ni Mwl. Oscar Samba, akiwa anatoka Shambani akijikinga mvua kwa njia ya Asili: anatumia jani la gimbi kujifunika.
 Huku ikisadifu maudhi haya kwa kutuonyesha alipokuwa anapitia. Ambapo utapaelewa katika kitabu chake cha IMANI INAPOJARIBIWA na Kile cha KWA NINI MUNGU ANATUTAKA TUSIJILIPIZIE KISASI?.

 #AINA ZA #UPAKO

1. Upako Unaotokana na Mahali Unapopitia

2. Upako Unaotokana na Maombi

3. Upako Unaotokana na Neema au Karama. Au Unao ambatana na Wito ama Mafuta. (Ingawa kuna ambaye ana Mafuta ya Wito 'kila aliyeitwa hupewa.' Na kuna yule mwenye mafua hayo pamoja na neema ya ziada ambapo huitwa Karama.

4. Upako Unaotokana na Utii wako kwa Mungu katika Maelekezo aliyokupatia. Mfano aina ya ujumbe, kibali cha kuhudumu eneo au mahali husika na kadhalika. (Mapenzi Makamilifu ya Mungu.)

5. Upako Unaotokana na Kuombewa, au Kubandikwa Mikono na Muhubiri au mtumishi fulani. Paulo anamueleza Timotheo ya kwamba kuna aina ya mafuta aliyapata kwa kuwekewa mikono na wazee. (Uwe makini sio kila mzee amebeba roho sahihi.) 

Aina Nyingine

 6.Tukio Maalumu la Kutembelewa na Nguvu za Mungu Katika Ibada. 

7. Uwezo wa Kufuata Maelekezo Maalumu Yanayokuja Saa hiyo hiyo Unapokuwa Madhabahuni.

Jumatano, 28 Januari 2026

Karibu katika Mfululizo Wetu wa 1, wa Kitabu Chetu Hiki Kipya cha #KUJARIBIWA KWA IMANI katika Mada ya Cha Kufanya #Unapotupwa Kwenye Shimo, Pointi ya 1.

Na Mwl Oscar Samba

1. Cha Kufanya Unapotupwa Kwenye Shimo

1. Uwe Utayari na Ufahamu ama Akili ya Kukubali Kuishi Katika Shimo. Lugha ya kutupwa katika shimo ina maana ya kushushwa au adui kunuia kukuua. Ni aina ya pigo la kukung'oa au kukuangamiza kabisa kabisa. Mfano vijana wale wa tatu wa Yuda alipotupwa katika tanuru la moto; Meshack, Shedraka na Aberinego. Danieli katika shimo lenye simba wakali. Alikadhalika Yusufu gerezani, maana alitolewa katika maisha ya utukufu, na kisha kushushwa chini ghafla. Alikadhalika pia alipotupwa katika shimo na nduguze, na kisha kuuzwa utumwani. Maisha ya utumwa kwake bado yalikuwa ni kama shimo, maana anatolewa katika familia ya

Jumatatu, 26 Januari 2026

Karibu Katika Mfululizo Wetu wa 10, katika Kitabu Chetu Hiki cha CHA #KUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA. Pointi ya 8-10

Mwl. Oscar Samba

8. #Uwe na Utulivu Moyoni. Nimekujuza kuwa kama hujui cha
Kufanya usifanye chochote, ila na hapa nakutaka pa kuhakikisha ya
kuwa unakuwa na utulivu moyoni. Ukapata kibali cha kusoma kitabu
chetu kinacho uelezea nafasi ya mwili wa mwandamu au viungo vyake katika kumtumikia Mungu; kuna jambo muhimu sana utalipata
pale.

Jambo hilo lipo katika tukio la Nuhu akiwa katika Safina. Alimtuma
kunguru na kugundua kuwa muda bado wa kutoka safinani. Mara
baada ya muda kadhaa kupita, akamtuma njiwa: mara ya kwanza na
alirudi na jani la mti bichi. Napo kuna kitu aligundua ya kwamba bado
hakujakauka. Mara ya mwisho akamtuma na hakurudi tena; ndipo
alipogundua ya kuwa nchi imekauka!

Hakuwa na haraka, hakuchukua maamuzi hadi alipojiridhisha; sio

Jumatano, 21 Januari 2026

Karibu katika Mfululizo wa 9 wa Kitabu Chetu cha CHA KUFANYA UKIWA NJIA PANDA . Katika Pointi ya 7. Na Mwl Oscar Samba 7. Kama Hujui cha Kufanya Usifanye Chochote

 Watu wengi wamejikuta wakiwa katika njia isiyo sahihi mara baada ya kupitia 

kipindi cha ukimya wa Mungu. Kuna kipindi Mungu huwa kimya kama 

sehemu ya jaribu kwetu. Ikiwa imani yetu kwake inapimwa, jambo la 

sabra na hata nidhamu, utii na hofu kwake; ni kwamba ni kweli 

tunamtegema na kumtumaini Yeye! 

Japo wakati mwingine anaongea lakini hatuelewi, na pia kuna muda 

anaona hata akiongea hatutamuelewa. Usisau pia ukimya wake, huweza 

kuwa ni matoke ya hasira yake juu yetu. Maana hata mfalme Sauli kuna 

wakati Mungu hakusema naye; baada ya kukorofishana naye, na 

kujikuta akigeukia msaada kwa mganga wa kienyeji. Na alilalamika 

kuwa Mungu hasemi naye hata kwa ndoto.

Sasa, Nisikilize; Mungu anapokua kimya, au unapofikia katika hatua 

Jumamosi, 17 Januari 2026

Usiogope Na Uwe Mwaminifu Hadi Kifo

Uwe Mwaminifu hadi kifo maana yake uwe na msimamo ambao utakuwa tayari kulipa gharama yoyote ile.

Pia tunaambiwa ya kuwa, ukishinda kuna madhara utaepukana nayo; hii inatupa kufahamu bayana ya kuwa, zipo faida za ushindi.

 Tazama Andiko : Ufunuo wa Yohana 2:10 Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima. 

11 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili. 

Ninalowiwa kukupatia Majira haya ni kukutia moyo ya kwamba USIOGOPE na nikutake kuwa Mwaminifu huku ukijua mwisho wake kuna ushindi tele.

Maumivu nyakati kama hizi ni muhimu, ila mwisho wake umejaa mafanikio tele...kuna majira unalazimika kuingia gharama kwa ajili ya kulinda kile ulichokibeba ....

Jumatano, 14 Januari 2026

Karibu Katika Mfululizo wa 8 wa Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UKIWA NJIA PANDA, Pointi ya 5.

 Na Mwl. Oscar Samba

 5. Omba Mpenzi ya Mungu Yatimie.* Unajua maana yake ni nini?

Ni kwamba, umefikia mahali ambapo kwa akili na fahamu zako, 

hujui mpango wa Mungu, ama unajua lakini huna ujasiri na uwezo 

wakuukukabili! Sasa mwambie Mungu sio kama mimi nitakavyo bali 

mapenzi au mpango wako, ama njia yako ndiyo niiendee, sio njia 

nyingine. Yaombe haya kwa mzigo mkubwa sana, na kwa kumaanisha 

kwa viwango vikubwa mno.

22:41 Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba, 

42 akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; 

walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. 

Jumanne, 13 Januari 2026

Jifunze Kubariki na Kubarikiwa Katika Swala la Uzao, na Kuoa au Kuolewa

Watu wengi hawaijui hii siri...ndio maana sio wepesi wa kuzidai baraka hizi iwe ni kutoka Madhabahuni, (kwa watumishi wa Mungu) Wazazi na Kadhalika...

Hata wao wanaopaswa kuzitoa wengi wao hawana weledi wa kutosha kuwahusu au kuzihusu....

Nikiwa katika mkoa ambao hivi sasa nipo, nimejikuta nashangaa kuona sherehe za SendOff hata za watu walio okoka zisizokuwa na ibada ndani yake.

Sherehe hizo unakuta nyingine zinaudhuriwa hata na wachungaji na zinafanyikia kanisani ama mazingira hayo...lakini hata muda wa neno la Mungu haupo...(Hawajui kilichotokea kwa Rebeka saa anaagwa).

Jumapili, 11 Januari 2026

#Muamshe Yesu Kwenye Maisha Yako*

Sikatai ya Kwamba Yesu Unaye, Nakubali Kabisa...

Ila Umemfanya Kukosa Chakukufanyia Kiasi cha Yeye Kutulia au Kunyamaza Kimya...

Ni sawa na wewe kualikwa ugenini alafu mwenyeji wako akawa anafanya kila kitu...hali hiyo inakufanya kukosa jambo la kufanya...

Na unajikuta umekaa mkao wa kusubiri kuambiwa walau nisaidia kukatakata mboga ama kufagia hapo nje...hii ikupe kuhakikisha unamfanya Yesu Kutokutulia katika Maisha Yako...

Siku moja wanafunzi wa Yesu wakapaswa kuvuka  kutoka ng'ambo moja na kuelekea Gerasi...katika boti Yesu hakupewa chakufanya...akalazimika kulala....walipokutwa na Dharuba Majini Ndipo Walijikuta Wakimuamsha....hapo ndipo alipoingia kazini na kuwasaidia....jifunze kitu hapo..

Jumamosi, 10 Januari 2026

Mfululizo wa 7, Katika Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UKIWA NJIA PANDA, Pointi ya 4.

Na _Mwl. Oscar Samba_ 

 4. Tafuta Ushauri Sahihi.

Hapo juu nimekupa mfano wa huyu baba ambaye alifikia mahali

pagumu sana kimaamuzi, ila mkewe alimshauri asimwache Mungu.

Badala yake waombe, nukuu moja wapo inamtaja au inamkariri huyu

baba akiwa anasema kuwa, Mungu amempa mke mzuri sana maana

alimshauri vyema!


Katika nyakati kama hizi ni muhim kujua umhimu wa namna ya

kukabiliana na shauri mbalimbali, maana wapo marafiki wataabishaji

ambao hawataacha kuja kwa nia ya kukuyumbisha kiushauri.

Kwenye fikra zako ni alzima kuwa na akiba ya hekima na maraifa ya

namna ya kukabilina na mamabo au amsuari au hali amahizi;

Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na

Jumanne, 23 Desemba 2025

Mfululizo wa 6 Katika Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UKIWA NJIA PANDA.

Mada ya 2 ya Mambo Mengine ya Kufanya au Kuepuka Ukiwa Njia Panda.

Na _Mwl. Oscar_ Samba 

Pointi  ya 3. Ingia kwenye Maombi ya Muda Mrefu. Yanaweza pia yasiwe 

ya muda mrefu, ila yakawa ya kina na mazito au yenye mzigo mzito. 

Lakini imizo la maombi ya muda mrefu sio la kupuuza, ni muhimu sana 

kulizingatia. Yanaweza kuwa ya siku tatu kavu, masaa 24, au ya wiki 

moja. Huweza kuwa katika mfumo wa masaa 12 au 24 kwa 24 ama 

masaa 36 na kadhalika. Ni kadri Roho wa Bwana atakavyo kuongoza.

Kuna baba mmoja alikuwa akipitia mahali pa gumu sana, aliingia ubia 

wa kibiashara na mtu ambapo ilimbidi aweke dhamana mali zake 

muhimu. Na Yule mtu baadae akajakukimbia na ile fedha; alifikia hatua 

ya kutaka kujiua. Maana ilikuwa ni fedha nyingi, mkewe alimshauri 

asijidhuru badala yake wa mgeukiye Bwana.

Jumatatu, 22 Desemba 2025

3⃣ SERA YA UFALME WA MBINGUNI KUHUSU UJENZI WA NYUMBA YA KUISHI KWA “RAIA” WAKE WALIOKO DUNIANI 🖊 Mwl.CHRISTOPHER MWAKASEGE.

Bwana Yesu asifiwe sana!

Masomo ya wiki mbili mfululizo zilizopita, juu ya Sera ya ufalme wa Mungu kuhusu ujenzi wa nyumba za kuishi, yamezaa maswali kadha kutoka kwa wasomaji.


Maswali hayo yalihusu kupata ufahamu zaidi, juu ya sera hii ya ufalme wa Mungu. Tumeyapokea hayo maswali, ingawa si rahisi tukayajibu yote, kwa sababu ya “ufinyu” wa nafasi ya kufanya hivyo.

Lakini kwa leo tunataka tujibu swali moja, kati ya maswali mengi yaliyoulizwa, – na tunaamini majibu hayo yataongeza ufahamu zaidi juu ya utekelezaji wa sera hii.

Swali lenyewe lenyewe liliulizwa hivi: “Je, unatushauri kuweka wakfu au kuitakasa ardhi kabla ya sijajenga?”

Majibu yake ni haya:

Kuna tofauti kati ya kutakasa kitu,

Alhamisi, 18 Desemba 2025

Mfululizo wa 1 wa Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UNAOOKUWA NJIA PANDA

Tunaanza na Utangulizi (kinapatikana Google Bure)

 Na Mwl. Oscar Samba

 Utangulizi

Kitabu hiki kimenuia kumsaidia mtu ambaye yupo katika mazingira

magumu ya kimaamuzi, na mbele yake kuna aina zaidi ya moja ya

maamuzi ambayo anahatarishwa kuyachukuwa au yanayomkabili,

inawezekana lililo hatari ni moja, au salama ni moja ila kuna zaidi ya

aina mbili au moja na kadhalika.

Kitabu hiki ni matokeo ya sehemu ninayopitia sasa kuhusu ndoa yangu.

Ikumbukwe sasa ni mwaka unaokaribia wa nane toka mwenzangu

tuoane na kujikuta ananiacha kwa talaka mahakamani hali inayonipa au

kunipelekea kuwa njia panda. Njia panda yangu inaweza isiwe na tija

sana kwako ila la muhimu ni wewe kufahamu mazingira ya kitabu

hiki ili kikusaidia. (Wakati nakitoa, imetimia miaka 10/11, “2015-

2015”.)

Unaweza usione umuhimu wake kwa leo ila nikuhakikishie kuwa

chakula hiki ni kama akiba, kuna muda tunakula leo lakini chakula

hicho kinatusaidia kesho; sio kwamba tuliingia kwenye mfungo la! Bali

homa ya ghafula imetukuta na kutunyima hamu au uwezo wa kula. Ila

kwa akiba ya jana ambayo hatukuwa hata na wazo la kula tumevuka leo

salama!

….Nikikuongezea ni kwamba, mara baada ya kuandika

utangulizi huu, na nikiwa tayari nimeshaanza kukiandika hiki

kitabu, njia panda nyingine ilijitokeza kama sio moja basi ni

zaidi, licha ya swala la ndoa, lakini pia limeibuka swala la

kusimamishwa masomo chuoni. Kumbuka nipo katika chuo cha

Biblia Dodoma cha CBC; mara baada ya kutofautiana na

kiongozi wangu mmoja wapo katika swala fulani, nilijikuta

nikipewa adhabu ya kusimamishwa masomo mwaka mmoja.

Nikiwa tu nimetoka kuchukuwa barua zangu, (ikiwa moja yangu na ya

mchungaji wangu kingozi,) ndipo nilipokutana na mchungaji mmoja wa

dhehebu jingine akiniambia kuwa nihamie kwake. Maana huku

kumekuwa kugumu kwangu na katoa sababu kadhaa: zingeweza

kuonekana ni zenye mashiko maana nyuma ya pazia jambo langu

limeonekana ni matokeo ya mimi kuwa na tabia ya kutetea na kudai haki. Pamoja na kusema ukweli pale ambapo ninapoona mambo

hayajaka sawa.

Wazo hili halikwepo kabisa kichwani mwangu, maana nilishapitia

mahali kama hapa mara baada ya uongozi wangu wa sehemu huko

Arusha kutofautina nami na kunichukulia mamuzi ambayo sikuyapenda

maana sikusikilizwa kimapana!

Jumanne, 11 Novemba 2025

Jifunze Kuidharau Aibu #mwalimuoscarsamba


 Kuna Mafanikio ili Uyafikie; Lazima Ujifunze Kuidharau Aibu.

By Mwalimu Oscar Samba

#nukuuyamwalimuoscarsamba MVUVI na Mvua

 


#nukuuyamwalimuoscarsamba KUMUA MAREHEMU



 

Ufunuo Dhidi ya UTAWALA

Mimina Kitasa yaani Pigo Juu ya Utawala, au Ufalme Usioutaka yaani Uliodhalimu...

Ufunuo wa Yohana 16:1 Nikasikia sauti kuu kutoka hekaluni, ikiwaambia wale malaika saba, Enendeni, mkavimimine vile vitasa saba vya ghadhabu ya Mungu juu ya nchi. 

10 Na huyo wa tano akakimimina kitasa chake juu ya kiti cha enzi cha yule mnyama; ufalme wake ukatiwa giza; wakatafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu.

Waombaji Wana nafasi Kubwa Sana ya Kuleta Mabadiliko Ktk Mifumo ya Uongozi Kwenye Maeneo Mbalimbali.

Heri Alitunzaye Vazi Lake

Uwokovu ni Vazi. Je, Unautunza Wokovu wako?

Nikuite Moyo hivi Leo kutokuendelea kucheza na Dhambi. Tunza wokovu, linda vazi lako. Yesu yu karibu kuja. Anakuja kulinyakuwa kanisa lake..

Ufunuo wa Yohana 22:13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. 

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. 

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.