Mada ya 2 ya Mambo Mengine ya Kufanya au Kuepuka Ukiwa Njia Panda.
Na _Mwl. Oscar_ Samba
Pointi ya 3. Ingia kwenye Maombi ya Muda Mrefu. Yanaweza pia yasiwe
ya muda mrefu, ila yakawa ya kina na mazito au yenye mzigo mzito.
Lakini imizo la maombi ya muda mrefu sio la kupuuza, ni muhimu sana
kulizingatia. Yanaweza kuwa ya siku tatu kavu, masaa 24, au ya wiki
moja. Huweza kuwa katika mfumo wa masaa 12 au 24 kwa 24 ama
masaa 36 na kadhalika. Ni kadri Roho wa Bwana atakavyo kuongoza.
Kuna baba mmoja alikuwa akipitia mahali pa gumu sana, aliingia ubia
wa kibiashara na mtu ambapo ilimbidi aweke dhamana mali zake
muhimu. Na Yule mtu baadae akajakukimbia na ile fedha; alifikia hatua
ya kutaka kujiua. Maana ilikuwa ni fedha nyingi, mkewe alimshauri
asijidhuru badala yake wa mgeukiye Bwana.
Aliamua kuingia kwenye maombi ya siku tatu, alipokuwa kwenye hayo
maombi alisikia sauti ya Roho Mtakatifu ikimwmabia sio siku 3 bali ni
siku 90. Lilikuwa jambo gumu sana kwake, alimueleza wazi kuwa
kwake hata maombi ya siku 21 yale yanayotangazwaga kanisani
kufunga kwa ufanisi ni tatizo. Kwa ujumla alikuwa; ni mdhaifu kwenye
hilo eneo, alimuomba amtie nguvu lakini pia amuinulie watu. Ghafula
akaanza kusikia kutoka kwa watu asiyowajua kwamba wamepewa
mzigo wa kuomba naye, huyu wiki na yule muda kadhaa.
Wakiwa na baada ya maombi alipokea majibu makubwa sana kutoka
kwa Mungu. Biashara zake zilifunguka na mipango mingine ya
kibiashara ilifana sana. Akajikuta anapata fedha za kulipa ule mkopo,
jambo lililonusuru kuuzwa kwa mali zake muhimu alizoziweka kama
dhamana.
Alikuwa katika njia panda ambayo sio kwamba ilitishia tu uhai wake
wa kiroho ama mahusiano yake na Mungu; bali alitaka kujidhuru hata
mwilini! Bahati nzuri alimgeukia ama alimtafuta Bwana.
Yesu alipokuwa katika njia panda ya kuamua aende msalabani au
akwepe! Aliamua kuingia kwenye maombi mazito. Maombi haya ni
aina au ni moja ya maombi ambayo mbingu na nchi haziwezi
kuyasahau kabisa. Maana yalibeba hatima ya ukombozi wetu!
Kumbuka njia panda yoyote ile imewekwa ili kukupa kuamua maamuzi
yatakayo beba hatima yako ya baadaye. Ndio maana ni hatari kuamua
kuolewa kiholela kwa sababu tu ya kungoja mchumba kwa muda bila mafanikio! Matokeo au madhara yake ni makubwa sana, jaribu kufikiri
nini kingetokea kama Yesu angekwama kwenye njia panda ile! Ni
hakika tusingalikuwa na ukombozi hivi leo!
Mathayo 26:39 Akaendelea mbele kidogo, akaanguka
kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana,
kikombe hiki kiniepuke;..
Kitu kimoja wapo maombi haya hufanya ni kukutia nguvu, kuna watu
wamefikia hapa sio kwamba mioyo yao imeharibika au imegeuka ila ni
matokeo ya wao kuishiwa nguvu kabisa. Mioyo imezimia na haipo tayari
kusonga mbele; lisikie Neno la Bwana ndugu yangu! Wazimiao watapokea
nguvu mpya, nao watapanda juu kama tai, wala hutachoka tena! Hiyo ni
Isaya 40, maana ndivyo Mungu anavyotuambia. Hali inayoashiria kuwa swala
la kuchoka na kuzimia au kufa moyo; kupo ila yupo mtoa nguvu, na mombi ya
mzigo ndiyo yatakayokupa uweza huo!
Kwa Yesu hili lilitokea; 22: Malaika kutoka mbinguni akamtokea
akamtia nguvu.
44 Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; hari
yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchini.]
Luka 22:43-44.
Kutiwa nguvu kupo, ila tatizo linakuja katika nia ya mtu, ukichoka na
kufikia hatua ya kugoma kuhitaji msaada wa kutiwa nguvu; hilo ni
tatizo tena kubwa! Ni sawa na mgonjwa nayekataa dawa. Na baya zaidi
akataa na kula chakula na kunywa maji!
Maana kuna muda mwili unapambana au unajipambania maana
kibaolojia umepewa kutengeneza kinga yakujihami na kushambuliana
na magonjwa! Sasa kama haupewi chakula na maji ni hatari sana! Kama
huwezi hicho ni kitu kingine, tatizo ni nia, ndio maana hospitalini kuna
kutundikiwa maji ya dawa, au yenye nguvu ama maji kama maji.
Kuongezewa damu na kwa wengine hata kulishwa kwa njia ya mpira!
Lakini kama hutaki, uwe na hakika ukipata nguvu kido tu
utaishimamisha hiyo “dripu” au utaichomoa! Maana hutaki kuishi tena!
Hapa sio swala la mwili kuwa dhaifu tu; bali ni mtu kuwa na nia ya
kutokutaka tena msaada kwa kiwango kikubwa.
Nampenda sana Elia, maana alipokuwa amechoka katika ile 1 Wafalme
19 alikimbilia chini ya Mretemu. Huu ni mti wenye kivuli kizuri. Na ukizingatia ilikuwa ni jangwani, jua ni kali, hakukubali kujiweka penye
jua. Na alipoletewa chakula au ku ndaliwa na malaika. Alikubali kula,
akalala bado alipoamshwa au kuimizwa tena alikula. Na baada ya hapo
alikubali sasa kuuendea au kuendelea na mpango wa Mungu juu yake.
Ukiona umechoka kiroho, na hutaki msaada, ukiwaona wapendwa
unawakwepa., hutaki kupokea hata ya simu ya mchungaji wako.
Ukimuona mama mchungaji unajifanya kama vile hujamuona! Uwe na
hakika u sawa na mgongwa anayeikwepa hospitali! Mgonjwa anaye
mkimbia “nesi” badala ya kumkimbilia.
Ukiedelea utagundua kuwa baada ya haya maombi, Yesu anawaambia
wanafunzi wake laleni sasa! Ikiwa na maana kuwa vita amefanikiwa
kuvimaliza.
Tutajionea kwa mfalme Hezekia, na Yehoshefathi, walipokuwa kwenye
kipindi kigumu cha kivita, adui zao waliwatishia. Maana walikuwa na
uwezo mkubwa kuliko wao; ila waliamua kumkimbilia Mungu. kwani
adui waliwatengenezea mazingira magumu ya kujisalimisha; walikuwa
na njia kuu mbili mbele yao. Kusisalimisha kwa adui au kumtazama
Mungu! Na kwa hila adui alijitutumua mbele yao kana kwamba ana
guvu kuliko wao na Mungu wao. Ndio maana walitaja ukuu wa miungu
yao. Hususani huyu aliyekuwa akipamba na Hezekia, alijigamba sana.
Na kueleza jinsi miungu yake ilivyompigania; akiwataka Wayahudi
wasimuamini mfalme wao akiwa na nia ya kuwafanya wabadilike
kimtazamo. Bali walikaza katika kumtazama Bwana kimaombi na
kiimani na hatimaye Bwana aliwapigania.
Kama Hujaokoka, Nikutie Moyo Kufanya hivyo Sasa, Sema BWANA YESU MIMI NI MWENYE DHAMBI NAKUOMBA UNISAMEHE SASA; Amen.
Tafadhali Tafuta Kanisa la Watu Waliokoka Ukasali Hapo... Àsante...Tuandikie pia katika namba hapo chini ili tukutumie Kitabu cha Kuukulia Wokovu... Asante..
Usikose Mfululizo Ujao wa 7 katika pointi isemayo Tafuta Ushauri Sahihi..kwa mfuluzo huo na mingine tangulizi usiache kuifuatilia Channeli yetu hii: ..
Karibu Sana Katika Channel Yetu Hii
*Ni Maalumu kwa Ajili ya Mafundisho ya Neno la Mungu.*
Tufolo; https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h
Tafadhali Tembelea na Hufuma Zetu Nyingine
BIBLIA TAKATIFU
https://whatsapp.com/channel/0029Vb6yb822f3EB3Zfbep3z
BARAKA ZA MUNGU
https://whatsapp.com/channel/0029VbBZGFZ1CYoaefQvAa12
Kwa Maombi: +255759859287
http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL
UWE NA AMANI
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni