Jumamosi, 3 Juni 2017

NAMNA YA KUJINASUA KWENYE VIFUNGO VYA PEPO MAHABA. Sehemu ya 3.

Na Mwalimu Oscar Samba #Ug Ministry  
Dalili/Ishara zitakazokujulisha uwepo wa Pepo Mahaba kwa njia ya Uridhi. (..Mpendwa Kesho ya jana ni leo, na ahadi ni deni kama waswahili wanenavo, nami sina budi kuendelea pale nilipo ishia jana. Kumbu hii ni sehemu ya 3 kwa hiyo kama uipitwa na zilizopita zitafute ili tuweze kwenda sanjari)
1. Wazazi au babu zako watakuwa na mafarakano kwenye ndoa, yaani migogoro au kutokuelewana na hali hiyo huwa kwa ndoa za ndugu zako pia.
2. Baathi ya ndugu wa kwenu kuwa na watoto wa nje ya ndoa. Ukiona mama au baba alikuwa na tabia hiyo na hatimaye watoto/mtoto kuiridhi jua roho hii ipo miongoni mwao.
3. Wanandoa kutengana, huyu kuishi huku na yule kule ni dalili kubwa sana ya Pepo Mahaba, na jambo hilo kuwa katika jamii husika.

4. Wazazi kugawana watoto, unakuta katika familia kuna watoto wa wapendwao zaidi na baba na wale wa mama. Na jambo hili huwa katika familia za kwenu yaani zaidi ya moja. Dalili hii imejificha sana na kwa bahati mbaya wengi hawaitambui kuwa ni ya uwepo wa Pepo Mahaba.
Hatua za kuchukuwa: Nimekwisha kukuorotheshea mbinu kadhaa za kumshinda huyu pepo kwenye kipengele kilichopo hapo mbeleni ila hapa ninakutaka kufanya ya fwatayo.
Zipo njia kuu mbili za kufanya.                                        
 Ingawaje wataalamu ama wa mambo ya kuvunja madhabahu ama kujinasua katika matatizo kama haya hupendekeza kwa anayetaka kutumia njia zote kuanza na ya pili ili kujikomboa yeye kwanza na kisha kuwakomboa wengine kwa madai kwamba mfungwa ni ngumu kumkomboa mfungwa ama ni vigumu kusukuma gari angali ukiwa upo ndani ni shariti ushuke kwanza nami ninakubaliana nao.
(a) NI ILE YA KUVUNJA MADHABAHU. Faida yake: Ni kwamba utawakomboa ndugu zako wote ama watu wote waliopo chini ya hiyo madabahu, aidha ni ukoo au kabila ama eneo fulani.
Gharama yake: Maombi yake ni magumu na huchukuwa muda mrefu.
(b) NJIA YA PILI, KUJITENGA NA MADHABAU. Njia hii ni pale muhusika atakapofwata hatua zote za kuvunja madhabahu ila maombi yake hayata lenga kuivunja bali kujitenga yeye na huweza kuitenga pia na familia yake au kikundi kidogo cha watu. Hufananishwa na kukata tawi la mti huku yale ya kuvunja madhabahu yakifananishwa na kung’oa mti. Kwa mfano huo natumai utaelewa utofauti wake. Pia unaweza kulitoa jina lako kwenye maagano ama viapo ulivyoingizwa aidha na mababu, wazazi ama mtu yeyote aliyekuwa na uhalali huo ikiwemo viongozi wakimila, kabila, jadi ama kisiasa/kiseikali.
Gharama yake: Huchukuwa muda mfupi kulinga na bidii ya muombaji.
Hasara yake: Jamii iliyosalia itaendelea kuteseka na madhabahu hiyo huku wewe ukiwa salama ila kuna baadhi ya vitu hutavipata kwa haraka au ukamilifu hususani vile vya kurithi vilivyo vizuri yaani Baraka za wazazi au zilizopo kwenye eneo husika ambavyo ni halali yako kuvipata kwa mujibu wa bibilia.
Katika namna ya kuvunja madhabahu fwatilia mbinu hizo kwenye kitabu changu cha Namna ya Kuishi wakati wa Majaribu au Mapito kwenye mada ya kujitia nguvu, kipengele cha huzuni mada ndogo ya kuifunga dhambi katika madhabahu.
Naguswa kukupa mfano wa njia hizo mbili za kujikomboa. Mfano wa njia (a), Nilikuwa katika maombi ya kuvunja madhabahu kipindi fulani na niliota ndoto ya kuwa nimeung’oa mti mkubwa uliopo kijijini kwetu, ila bado ulikuwa hai na ulikuwa upo chini huku ukiwa na uhalisia wa mtu na sura ya miongoni mwa babu yetu mmoja wa kale aliyekwisha kufariki. Kung’oa mti maana yake ni kuvunja madhau na kuendelea kuwa hai angali ukiwa chini umeng’olewa maana yake ni kwamba hatua za kuharibun kuangamiza/kuteketeza zinaitajika, kwani kuung’oa ni ishara ya kung’oa na kubomoa, kama lisemavyo hili andiko: Yeremia 1:10.
Katika mfano (b) wa kujitenga, kuna rafiki yangu mmoja aliye mtumishi mwenzangu alinisimulia kuwa wakati akifanya maombi fulani mlimani yaliyomgarimu miaka kama miwili, aliona dhairi kwamba kuna kisu kimempita na kwenda kukata tawi fulani la mti na tawi lile kudondoka chini. Kisha Mungu akamwambia kuwa “tawi hilo ni wewe”. Maana yake mtu huyu alikuwa kwenye maombi ya kujitenga na roho za kwao kwani pia Mungu alimwambia mti huo ni ukoo wa kwao na tawi ni yeye. Kwa hiyo yeye yupo salama ila ndugu zake bado wapo hatarini/matesoni. Tuendele na mlango mwingine;
(3) Vitendo vya Uzizi/Uasherati. Dhambi hii maandiko yanatamka bayana ya kwamba hufanyika nje na ndani ya mwili wa mwanadamu. Nje ni kwa huu mwili na ndani humuwakilisha Mtu/Utu wa ndani na mtu wa ndani ndiye anayeota ndoto. Nikiwa na maana nafsi yako, roho na moyo. Kwa hiyo ufanyapo hivyo ni dhairi kwamba mapepo haya hupata nafasi ya kuweka makao kwako na kuketi panapo mlango wa ndoto ambao upo kwenye nafsi. Kumtoa pepo aliyepenya kwa njia hii kuna hitaji maombi ya rehema makubwa na yale ya utakaso wa nafsi na moyo pamoja na upatanisho wa nafsi ambao hufanywa kwa Damu ya Yesu na Ujazo wa Roho Mtakatifu.
(3) Kutizama Picha za Utupu/Uchi. Macho ya mfalume Daudi alipomtizama yule mwamke aliyekuwa katika pozi la kuoga na ndani yake yaani kwenye ulimwengu wa roho Pepo Mahaba ilipata nafasi, na kupitia dhambi ile maisha yake na ya Taifa lake yaliyumba mno. 2Samweli 11:2 Ikiwa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari la jumba la mfalume; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wakupendeza macho. Kupitia Macho Daudi alianguka dhambini, kwani mistari inayofwata anaanza kupeleleza habari za huyo mwanamke, na wewe unayetazama  picha za utupu kupitia macho utaanza kupeleza kutenda dhambi na hapo hapo mapepo yatakupeleleza ili kukupata na madamu mlango huu wazi yataingia na kufunga ndoa nawe rohoni.
Kumbuka kupitia macho yako waweza fungua mlango kwa adui huyu kuingia ndani yako na kukuvuruga kupitia ndoto. Kitendo cha kutizama picha hizo kina mpa Shetani nafasi kwa kufungua mlango kwani macho yako na mawazo yako moyoni ni mlango.
(4) Kutamani Mke/Muwe wa Mtu ama Binti/Mvulana (Tamaa ya Ngono). Katika kitabu kile cha Kumbukumbu la Torati 5:21 Wala usimtamani mke wa jirani yako.. Mungu alijua fika ya kwamba kutamani kwa aina hii hufungua mlango kwa Pepo Mahaba na kwa njia hiyo huweza kukusumbua ndotoni.
Ukisoma mada ile ya Usimpe Ibilsi nafasi na ya Namna ya kuifunga dhambi kwa kamba madhabauni kwenye kitabu changu cha Namna ya Kuishi wakati wa Majaribu au Mapito nimeelezea jinsi ya kujinasua na kukwepa jambo hili. Ila hapa ninakudokezea kwa kifupi.
Jitaidi sana kuchunga macho yako kwa kumsihi Mungu pia akusaidiye, Ayubu 31:1 “Nimefanya agano na macho yangu: basi nawezaje kumuangalia msichana? Na Daudi aliomba hivi; Zaburi 119:37 Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, unihuishe katika njia yako. Mungu akishageuza macho yako mwambiye pia avifanye viungo vyako kupita katika njia yake kama Daudi aombavyo, “unihuishe katika njia yako
(5) Mwanandoa mwenzako kupoteza uaminifu, Natuma tupo pamoja nisemapo kuwa mtu mke na mtu mume waliowana ni mwili mmoja. Kama ndivyo basi rohoni pia ndoa yao hutumia mlango mmoja. Kosa la mwanadoa mmoja linaweza kufungua mlango kwa Pepo Mahaba na akija atakaa juu ya ndoa yenu na akikaa hapo atawavuruga sana. Ila mmoja wapo akiwa yupo vizuri kiroho na kwa kujua jinsi ya kufunga mlango, Pepo huyu hawezi kukaa juu ya ndoa hiyo badala yake atakaa kwa mhusika aliyefungua mlango au aliyedhaifu kiroho. Yaani anaweza kufungua mlango mume na akatubu na kuendelea vyema kiroho ila Pepo likakaa kwa mke ambaye hakufungu mlango ila amelega kiroho maana ameshindwa kulifukuza.
Tutazame jinsi pepo linavyoweza kukaa juu ya ndoa kwakutizama mfano huu wa jinsi lilivyo wai kukaa juu ya Taifa la Iziraeli. 1Mambo ya Nyakati 21:1 Tena Shetani akasimama juu ya Iziraeli, akamshawishi Daudi kuwahesabu Iziraeli.
Ukifwatilia kisa hiki utaona jinsi Mungu alivyokasirika na kuachilia adhabu yake kwa Taifa hili. Nataka utizame nami hapo kwa akili za rohoni: Ni kwamba Shetani amekaa juu ya Iziraeli na matokeo yake akapata nafasi ya kumshawishi mfalume Daudi na kumtumbukiza dhambini. Na kwenye ndoa yako akikaa juu ya hiyo ndoa ni hakika hakuna namna mtakavyoweza kuelewana na mwenzako au wote mnaweza kujikuta mnatafuta “nyumba ndogo” na kufanya vitendo visivyofaa.  Na kupoteza uaminifu kwa mwanandoa mwenzako kwa weza kuwa kwa kutoka nje ya ndoa, kumtamani mtu wingine kingono na kadhalika.
(6) Mahusiano ya Uchumba Bubu au “Uboyifrendi/Ugelifrendi”, ama Ahadi ya kukuoa/Kuolewa nawe.
Kupitia pia ahadi ya mtu aliyewai kukutamkia kukuoa au kuolewa na wewe na jambo hilo kutokutimia, huweza kufanyika mlango kwa pepo huyu. Ndio maana baada ya muda ukiota unafanya tendo hilo unaiona sura ya huyo mtu. Ni jambo la hatari kwa vijana kujihusisha kwenye mapenzi kabla ya wakati wake nikiwa na maana “Uboyifrendi” na “Ugelifredi” ni dhambi pia uchumba usio na lengo la kuoana ni dhambi pia. Maandiko yanaunga nami dhairi bila kificho, Wimbo uliobora 3:5 Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, kwa paa na kwa ayala wa porini: msiyachoche mapenzi, wala kuyaamsha, hata yatakapoona vyema yenyewe.
Kuona vyema yenyewe maana yake mahusiano ya kimapenzi yana wakati wake. Kwa hiyo kufanya hivyo kabla ya wakati wake ni hatari ndio maana punde ufanyapo hivyo Shetani anapata mlango wakuyavuruga maisha yako na miongoni mwa vitu anavyopenyeza ni ndoto. Na njia hii ni miongoni mwa njia kuu zinazowasumbua wengi hususani wanandoa na watumishi, maana Shetani ni ngumu kuipata njia nyingine kwako kwa hiyo hulazimika kuifwatilia historia yako ya zamani ili kukutesa leo.
(7) Miziki/Nyimbo za kidunia. Bibilia huziita nyimbo za upuzi, Amosi 6:5. Nyimbo hizi zimeingiliwa na kutawaliwa na Mapepo Mahaba ndio maana “staili” zao za kucheza na mavazi yao walio wengi hususani wanawake ni yakimapepo mahaba. Watacheza kama watu wanaofanya tendo la ndoa au kuchezesha viungo vya mwili vyenye mvuto kimapenzi na kuvaa mavazi ya nusu na hata uchi kamili.
Mauthui ya nyimbo zao walio wengi huwa ya kimapepo mahaba. Utakuta wanaimba mapenzi na kuhimiza au kusifia jambo hilo kwa shabaha za kuwadondosha wengi katika dhambi hiyo. Muonekano wa waimbaji baathi ya wakiume huchocheoa vitendo vya Ushoga kwani wapo waimbaji wakiume wanaovaa hereni na kufunga suruali chini ya kiuno. Hizo zikiwa ni alama za Ushoga. Pia kwa wanawake wapo wanaoonyesha vitendo vya kuchochea usagaji kwa kucheza kwao na hata kuvionyesha atharani. Unapo tazama ama kusikiliza nyimbo kama hizo ni fika una fungua mlango kwa mapepo hayo kukuingia kwani nyimbo huweza kuimba moyoni kwa muda mrefu na picha hizo kukaa katika macho ama nafsini kwa muda. Epuka hili kwa gharama yoyote ile na kumbuka ni dhambi kwa aliyeokoka kuimba au kutiza na hata kucheza nyimbo hizo.
(8) Kusikiliza au kufwatilia Hadithi zenye elementi au chembe chembe za pepo mahaba.
Sikio ni malango wa rohoni,… (..Tuonane tena Kesho). Nakusihi kuendelea kunifwatilia tena kesho na panapo majaliwa tutaendelea na kipengele hiki na vinginevyo. Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigospel.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              

Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa                                                                          2 DAY SKY: https://www.2daysky.com/home

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni