Jumamosi, 17 Juni 2017

Mwalimu Oscar Samba: MBINU TEULE ZA KUTOKA KWENYE UMASIKINI KWA WATU WALIOKOKA 6.

Na Mwandishi wetu wa Ug Ministry.
Ninakukaribsha katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana na Mwokozi wa maisha yetu katika safu hii ya ujumbe wa Semina ya Neno la Mungu ikiwa ni siku ya sita kama ilivyofundishwa jana na Mwalimu.

Mwalimu alianza kwa msisitizo kwamba ili kufanikiwa Kiroho na kiuchumi ama kufikia mafanikiao ya kutajirika kiuchumi katika Kristo Yesu yatupasa kuutafuta kwanza Ufalume wa Mbinguni na Haki yake na kisha hayo tunayaoyahitaji tutayapata.

Jana alifundisha mbinu moja nayo ilikuwa ni KULIJUA KUSUDI LA MUNGU LA KUKUTAJIRISHA, katika mbinu hii Mwalimu aliwataka walio matajiri kufahamu jambo hili na kuliishi huku akiwafundisha wale wenye nia au kiu ya kutajirika kupitia mfumo wa kimbingu kuhakikisha wanalifahamu na kuliisha kusudi hili ili Mungu awatajirishe na akisha kuwatajirisha wahakikishe wanalitimiza hili kusudi ili mali ama fedha zisiwatowe kwake.


Mwalimu aliendela kubainisha ya kwamba siku hizi kumekuwa na tatizo kubwa sana siku za leo ya kwamba watu kabla hawajawa matajiri au kipindi wakiwa hawana kazi walikuwa wakijitoa mbele zake kwa kufanya usafi makanisani au kuwa wana maombi ila mara baada ya mafanikio hali hiyo imeyayuka ndani yao.
Tulitazame hilo kusui, Ni 1Timotheo 6:17 Walio matajiri wa ulimwengu wa sasa uwaagize wasijivune, wala wasiutumainie utajiri usio yakini, bali wamtumaini Mungu atupaye vitu vyote kwa wingi ili tuvitumie kwa furaha.
18 Watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo;
19 huku wakijiwekea akiba iwe msingi mzuri kwa wakati ujao, ili wapate uzima ulio kweli kweli.
Kwa mujibu wa hayo maandiko tunapata ya kwamba jambo la kwanza Mungu anawataka WASIJIVUNE, Maana yake utakapokuwa na mali haikupasi kujivuna ama kuiringia hiyo mali. Pili Kutokuutumaini huu Utajiri, Mwalimu alisema ya kwamba wapo watu walioweka tumaini lao kwenye utajiri ama mali zao ndio maana wakisikia duka limeungua ama gari limepata ajali nao hupata presha ama kushindwa kuendelea vyema na maisha, na alisema athari yake kubwa likija jaribu na kupiga hizo mali hakika utamwacha Mungu au hutaweza kupita hapo.

Ayubu alishinda kwa sababu aliweka tumaini lake kwa Mungu ndio maana kuna mahali anasema kama alizitumainia hizo dhahabu, nalitokee jambo fulani akiwa na maana hakuutumainia utajiri wake na kwako ikiwa hivyo likija jaribu utasema Bwana Ametoa Bwana Ametwaa, Jina lake lihimidiwe.
Jambo la tatu ni kuvitumia kwa furaha, sio kusudi la Mungu la kutupa fedha kisha sisi tushindwe kuzitumia hizo fedha kwa furaha, bali ni kusudi lake tuzitumiye bila masikitiko, haifai kuwa tajiri huku watoto au jamaa yako ikiishi maisha magumu.
Nne watende Wema, Wawe Matajiri kwa kutenda wema, wema ya kwanza hapo ni ya tajiriri binafsi na ile ya pili ni kutenda wema kupitia utajiri wake. Wewe kama mtu binafsi unapaswa kuhakikisha unakuwa mwema, Ukiona jambo jema lifanye ukiona uhitaji wa tendo la kiungwana mahali litende kama wewe. Pili kukiwa na uhitaji wa tendo lolote linalohitaji fedha wewe litendo katika wema.

Tano, Unapaswa kuwa tayari kutoa mali zako, utoaji ndilo kusudi kuu la Mungu katika kukubariki na anahitaji ufanye hivyo kwa ajili ya kuitegemeza kazi yake na kuwasaidia wenye uhitaji mbali mbali. Kuna watu walimuomba Mungu magari kisha akawapa ila magari yao hayakuwai kubeba hata kipaza sauti kwa ajili ya kuhubiri injili, huku wakishindwa hata kuandika neno YESU ANAOKOA nyuma ya magari yao.

Wengine walimuomba vyombo vya Injili cha ajabu havitumiki katika kumtukuza Bwana badala yake vinapiga miziki isiyofaa kwenye masherehe ya kidunia huku vikitumika kuwapeleka watu jehanamu ya moto.
Sita, Washirikiane na wengine kwa Moyo, hapo maandiko yanawataka matajiri kuwa na ushirika na watu wote bila kubagua au kuchagua tena kwa moyo wala sio kwa kuigiza ama kujionyesha kwenye magazeti au mbele ya waandishi wa habari bali jambo hilo la paswa kufanywa kwa moyo wakupenda na wakujitoa. Shiriki misiba, wenzako wakichimba kaburi na wewe chimba.

Saba ni ili wajiweke akiba kama msingi mzuri wa baadaye, kumbuka katika siku za awali ya kwanza ama ya pili tulichambua jambo hili la akiba kiundani sana na ndiposa Mwalimu akakutaka kumuiga chungu ama kujifunza kwa sisimizi ambaye Mithali 6:6-8 ina mataja kama ni mwenye akili na hujiwekea akiba kwa ajili ya majira ya njaa, na wewe kukutaka kufanya hivyo huku akitaja aina nyingine ya akiba kuwa ni ile ya wema au ukarimu, na kusema unapokarimu wengine ndiposa na Mungu atakukarimu na wewe hata kama yule uliyemkarimu hata kuwepo muda huo Mungu atakuinulia mtu mwingine ikiwa ni matokeo ya wewe kutumia hiyo akiba. Akiba nyingine ilikuwa ni ile ya Sadaka, alifafanua vyema ya kwamba unapotoa Sadaka unajiwekea akiba Mbinguni kusiko haribika, kwa nondo wala hakuna kutu na jambao hilo ni la msingi sana.

Shabaha kuu ya Mungu kuyafanya hayo yote ni ili wewe upate Uzima Kweli Kweli, hapo zipo kweli mbili, ya kwanza ni ile ya kuhesabiwa haki kulingana na utajiri wako na ya pili ni ile ya wewe kuurithi ufalume wa Mbinguni mara baada ya kufa yaani kuwa mwana wa Mungu na kuepukana na ile falisafa ya kwamba ni ngumu matajiri kuurithi ufalume wa Mbinguni.

Awali ya kukupa mbinu hiyo teule  na kisha kukutaka kulitumia au kuliisi hilo kusudi la Mungu la kukutajirisha Mwalimu Oscar alikutaka kufahamu kuwa usipolijua kusudi hilo la Mungu ni rahisi sana kukumbwa na mambo ya fwatayo;

Fungungua nami kitabu hicho cha 1 Timotheo 6:9 Lakini hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu.
Pia sio hilo tu bali, Mstari wa 10,  6:10 Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.
Katika hayo yote alitoa sababu kubwa inayopatikana kwenye mfano ule wa Mpazi tafsiri ya aliyepandwa kwenye miiba ni mtu aliyekuwa yupo vizuri kiroho na kisha Shuhuli nyingi, taama na udanganyifu wa mali vikamsonga. Maana yake mali ni roho ndio maana huweza kumdanganya mtu. Na ili uishinde yakupasa kulifahamu vyema hilo kusudi la Mungu.
Ni Matahayo 13: 13.22 Naye aliyepandwa penye miiba, huyo ndiye alisikiaye lile neno; na shughuli za dunia, na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno; likawa halizai.
 Katika kuhitimisha kwa maombi ya Baraka Mwalimu na Mwinjilisti aliyekuwa ni mtumishi Mgeni Sixmoni, aliwataka wapendwa kutokuwa wasikiaji tu wa Neno bali wawe pia ni watendaji wa hilo Neno.

Na kabla hajamkaribisha Mtumishi huyo Mgeni ili kufunga ibada kwa maombi, Mwalimu Oscar aliwataka wale ambao hawajaokoka kuhakikisha wanafanya hivyo kwani hawajui ni lini watakufa na wakifa katika hali hiyo ya dhambi ni fika wataenda jehanamu ya moto maana bado hawajampokea Bwana na wale wanaotaka kutajirika kibibilia kupitia mfumo huu wanapaswa kuliishi jambo hili kiusahihi zaidi, na ili kufanya hivyo hawana budi kuokoka ili Roho Mtakatifu awasaidiye kutimiza jambo hilo.
Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigospel.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,  
 PAGE: https://www.facebook.com/ugukombozigospel/
Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa
2 DAY SKY: https://www.2daysky.com/home

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni