Ijumaa, 28 Agosti 2020

Utangulizi wa Kitabu chetu cha UTUMISHI NA MTUMISHI

Mwalimu Oscar Samba

Luka 10:20 Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.
Ni kweli kabisa maandiko yanasema kuwa mtawatambua kwa matunda yao! Na mti mbaya au mwovu hauwezi kuzaa matunda mema, kwani tini huzaa tini wala zabibu haiwezi kuzaa michongoma, au kwa lugha nyingine huwezi kuchuma embe kwenye mti wa mchongoma au mchicha katika mbigili!
Lakini ukweli na uhalisia ni kwamba andiko hilo lina mukutadha wake na undani wake! Wengi wamekuwa wakiyatumia ili kuficha uhalisia wao bila kujua kuwa hawamdanganyi Mungu bali ni wanadamu wenzao, na hawa ni wale wasiojali sana hatima zao, yaani kwao maisha baada ya kufa sio kipaumbele chao kikuuu!
Kitabu hiki mpendwa kimebeba nia na kusudi la kuwasaidia watumishi, ili wasije kubweteka na utumishi walio nao, au wakifikiria kuwa utumishi ni tiketi au kibali cha kuwapeleka mbinguni, ni vyema kufahamu kuwa pasipo huo utakatifu haiwezekani kumuona Mungu!
Utumishi na Mtumishi maana yake ni kwamba hakuna uhusiano kati ya utumishi ulionao na wewe kumuona Mungu! Kuingia mbinguni kigezo kikubwa ni utakatifu au wokovu na sio jinsi gani unatumiwa na Mungu! Na kitabu hiki pia kitawasaidia wale watu ambao wanateseka na kuumia na kujiuliza maswali yasiyo na majibu kuwa inakuaje mtu anatumiwa na Mungu kwa ishara na miujuza, au kwa neno ambalo linawasaidia wengine na wengi kuokoka ama kufunguliwa lakini maisha yake mwenyewe binafsi ni machafu!
Sikatai kuwa kuna mapungufu, ambayo mtu huzidi kukamilishwa, au kuna kuanguka au kukosea kama Daudi alipolala na mke wa mtu, na kumua mumewe, au jinsi Musa na Haruni walivyokorofishana na Mungu, ama mapungufu kadha wa kadha ambayo pia tunayona kwa Petro!
Hapa ninanena habari za watu walioharibika mioyo kabisa, au ambao wapo katika kuharibika lakini kwa kuwa Mungu anajithiirisha kwao au kwa kuwa bado wamejaa Roho basi wanabweteka na hali hiyo, na kudhania kuwa Mungu hachukizwi na kosa au mwenendo wao!
Kuna muda utakatifu unaenda pamoja na utumishi! Ila kuna muda utumishi au mapenzi (kusudi maalumu) ya Mungu hutimizwa hata na chombo ambacho sio kisafi! Tutajionea kwa Balaamu, mtu mchawi aliyetumiwa kiunabii na kukamilisha makusudi ya Mungu, ila alikuwa mchawi na utumishi haukubadili maisha yake, lakini pia tutajionea kwa watu kama yule mganga wa kienyeji alivyo mpandisha Samweli nabii kutoka Ahera au kifuani mwa Ibrahimu, (Paradiso) lakini alikuwa ni mpunga pepe!
Nakutaka sana kuhakikisha kama kweli unataka kwenda mbingunbi basi unjitahidi kuulinda utakatifu! Na hii ilikuwa ni shabaha kubwa sana ya Paulo mtume, kuwa alilinda asije akawa wa kuwahubiria wengine na kisha yeye kuachwa! Nawe uwe makini, pepo kutoka sio kigezo cha wewe kuiona mbingu!
Ndio maaana furaha ya wanafunzi wa Yesu kuhusu ishara na ambao yaliyotokea haikuwa kipimo au kigezo chawao kuiona mbingu, bali furaha yao iliyopaswa kupimwa ni kwa kuwa majina yao yameandikwa mbinguni! Kuupata ulimwengu wote, kujaaa karama na kutenda miujiza hakuna faida kwako kama utapata hasara ya nafsi yako! Mathayo 16: Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake? 27 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
Kilio chako kikubwa, na haja yako kubwa isiwe ni huduma yenye miujiza, ishara na umaarufu wa kiutumishi, bali utakatifu kwanza! Tafuta kumpendezesha Mungu kwanza!
Nayanena haya maana tumekuwa na watumishi ambao wapo tayari hata kutumia ushirikina ili tu wahakikishe wanapata nafasi fulani kwenye dini au dhehebu lake! Wapo ambao hutumia rushwa, na hata kampeni chafu ili tu kupata vyeo, wapo ambao hutumia hila wakifanya miujiza bandia ili tu wapate umaarufu na kadhalika!
Utakatifu kwanza, kisha vingine baadae! Tumekuwa na watumishi ambao hukandamiza vipawa au huduma za wengine kwa hofu ya kupinduliwa kiutumishi, na hata kuwatengenezea tuhuma au hila mabaya ili tu kuwachafua wengine kwa nia ya kulinda mkate!
Wapo ambao huhakikisha wanawaaribia wengine kwa lengo la kuchua nafasi walizo nazo! Wengine hutimia vibaya mahusioano yao na waangalizi, maaskofu au watu wenye dhamana husika ili kuwataka wamuondoshe ama wampe uhamisho mtumishi fulani kwa lengo la wao kukaa kwenye hiyo nafasi! Hii ni dhambi kama nyingine! Fahamu sana kuwa haki ni tabia ya Mungu, kutenda haki ni sehemu ya utakatifi!
Wapo viongozi ambao huonea wengine, wakikosewa au wakiona hawajatendewa sawa hata kama muhusika yupo sahihi basi kinachofuata ni wao kumuadhibu kwa kumuamisha au kumuondoa kwenbye vyeo fulani fulani! Huyu naye hatambua kwamba anapaswa kuhakikisha jina lake li mbinguni kwa kuwa mtu wa haki!
Mshirika! Kitabu hiki ni muhimu kwako pia! Maana unapaswa kuhakikisha kuwa unazingatia mambo ya adili au maadili ya kiroho kwanza na sio vinginevyo! Maana Yesu alisema kuwa napenda adili kwanza! Na katika Agano la Kale akasema anataka rehema kwanza! Kwa maana kwamba kuna vitu vya msingi ambavyo Mungu anavitazama, ili kukuhesabia haki!
Epuka sana mambo fulani fulani yakaonekana mema ila wewe ukakataliwa! Mungu alimkubali Habili, na sadaka yake, kwa hiyo angeweza kuikubali sadaka ya Habili, ila asimkubali Habili! Kwa Korinerio aliikubali sadaka yake/zake na kumkataa Korinerio! Kisha akahakikisha anamtuma Petro ili sasa sio sadaka tu zikubalike bali na kiroho cha Korinerio kikamilishwe! Sasa kwa Kornerio ilikuwa ni kesi tofauti! Kwako wewe uliyeijua kweli yote, ukiteleza/haribika hakika utakuwa kama Kaini, ambaye sadaka yake ilikuwa mbovu, ikakataliwa, na maisha yake yalikuwa mabaya pia nayo yakakataliwa! Sasa wewe usiishilie tu kuwa na sadaka njema, kuwa mfanya usafi mzuri kanisani, kumjali mchungaji wako na kusahau roho yako ! Ambapo hayo yatakubalika! Bali hakikisha na kiroho chako kipo vyema! Kwa hiyo kwa moyo mkunjufu ninakukaribisha humu kitabuni!
Kitabu kikitoka kitafute!
Hongera kwa kusoma ujumbe huu, nakutia moyo kuzidi kumtazama Mungu, na pia uwenda hujaokoka, yaani Yesu sio Bwana na mwokozi wa maisha yako! Nakutia moyo pia kuokoka sasa! Yamkini ni uchumi, fedha, hazipatikani, unazingirwa na nuksi na mikosi, kila unalofanya haliendi, unakabwa na mapepo, ! Wewe njoo kwa Yesu na hayo yote yatapita kabisa ! Sasa natumi u tayari!
Sema; MUNGU BABA, NINAKUPENDA, ASANTE KWA KUNIPENDA KWANZA, LEO NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NA NIPO TAYARI KUOKOOKA, TAFADHALI INGIA NDANI YANGU, SAMEHE DHAMBI ZANGU, NA FUTA JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKU, NA ULIANDIKE SASA KATIKA KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Ameni.
Kwa kufanya hiyo umekwisha kuokoka sasa, na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka lililopo karibu nawe ukasali, hapo, waambie kuwa umeokoa hivi karibuni, ili wakulee vyema kiroho.
Mawasiliano yetu, kwa M-Pesa au Simu: +255 759 859 287, barua pepe: ukombozigospel@gmail.com

PENDO LA KRISTO JUU YAKO NI LA MAFANIKIO


 Mpendwa nikutie tu moyo kuwa Yesu anakupenda, anakuwazia mawazo yaliyo mema, ni Mawazo ya Amani, Furaha, ana mipango mizuri juu yako, ni Mipango ya Kuinuliwa, Kufanikiwa, kama ilivyo nia yake katika 1 Yohana 3:2, kuwa anataka ufanikiwe kimwili au kifya na katika kila eneo la maisha yako ikiwemo uchumi, ndoa, huduma na kadhalika kama vile roho au nafsi yako ifanikiwavyo:

Hali ya mapito unayokutana nayo leo ni muhimu sana kufahamu kuwa ni ya muda tu! jangwa lipo ili kukufundisha na kukutengenezea mazingira mazuri zaidi kwa ajili ya Kanani yako! wana wa Israeli walipita hapo ili waweze kuishi vyema kwenye nchi ya Maziwa na Asali!
Nawe nchi yako ya maziwa na asali yaja ndiposa u ukipitishwa hapo!
La muhimu ni kuhakikisha imani yako haiyumbi, wana wa Israeli waliofia jangwani ilikuwa ni matokeo ya kutokuchanganya ile ahadi na imani kama maandiko yafunzavyo:
Lakini ukija katika Waebrania 3 na 4 utauona uapo wa Mungu pale kuwa aliwapia hawataingia rahani mwake kwa sababu ya kupungukiwa imani, na katika ile Hesabu 14 Mungu anamwambia Musa kuwa watu hawa watanidharau hadi au hata lini! Ikiwakilisha kuwa jambo la wewe kuogopa adui zako au vitisho katika safari yako ya kiroho kwa Mungu ni kumdharau ni sawa na kutokuliheshimisha jina lake!
Nikutie moyo kuwa kama wakina Yoshua na Kalebu na Musa na Haruni walivyosimama upande wa Mungu na kulitetea jina lake pale wakiwasihi wenzao wasimwasi Mungu wala wasiogope, na wewe hakikisha haumuasi Mungu nami ninakwambia kuwa usiogope maana uvuli uliokuwa juu yao umondolewa!
Jikaze kiume, jikaze viuno kama maandiko yatufunzavyo, kisha songa mbele! Mema yako yapo. majibu yako yapo. Ushindi wako upo, la muhimu ni wewe kujipa moyo!
Fahamu sana kuwa Yesu anakupenda, na anakuwazia yaliyo mema, mapito ni ishara ya upendo huo, wala sio mateso, maana askari mzuri ni yule aliyeandaliwa vyema, na Mungu anataka uwe askari mzuri!
kama hujaokoka na umeusoma ujumbe huu na kufahamu jinsi pendo la Kristo lilovyokubwa kwako, na unataka kumpa Yesu maisha yako, basi nikupongeze na hongera kwa hatua hiyo, nakutaka kufuatisha nami maneno haya ya sala hii ya toba kw aimnai, na badaa ya hapo utakuwa umeokoka:
sema, MUNGU BABA, NINAKUPENDA, NINAKUTAKA UINGIA NDANI YANGU, ILI UFANYIKE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINAAMINI KUWA YESU NI MUNGU, ALIKUFA NA KUFUFUKA, TAFADHALI FUTA JINA LANGU KWENYe KITABU CHA HUKUMU, NA ULIANDIKE SASA KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Amen.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, kwa maombezi, ushauri na mahuburi au maswali wasiliana nasi kwa Simu namba: +255759859287, Emaili: ukombozigospel@gmail.com au tembelea www.ukombozigospel.blogspot.com

YESU ANAKUPENDA!

 Na Mwalimu Oscar Samba

Sijui kama unajua kuwa Yesu anakupenda! Ni hatari kujaribu kusema kuwa mbona ninateseka, mbona maisha ni magumu, sasa inawezekanaje Yesu anipende wakati huu ni mwaka wa .. sijapona?

Ukweli ni kwamba Yesu anakupenda, na kuteseka kwako ni wewe tu bado hujatambua unachotakiwa kufanya ili kukubaliana na pendo hili! Unajua ndugu yangu acha nikwambie ukweli huu, nikuweke wazi katika viwango hivi vya uwazi! Mungu ili afanye kazi kwenye maisha yako ni lazima wewe umpe nafasi!

 

Mungu ni tofauti sana na Shetani, Shetani huweza kulazimisha, anaweza kutumia hila na mbinu batili ili kufanya jambo kwenye maisha yako, ila ili Mungu akusaidie wewe unapaswa kumruhusu!

 

Mfano, kuna mama mmoja alitokwa na damu kwa muda wa miaka 12; kwenye biblia tunajuzwa hili jambo, muda wote huo alikuwa akiwaendea waganga wa kienyeji na matatibu wa dunia hii! Ila siku alipoamua na kudhamiria moyoni mwake kwa kulishika pindo la vazi la Yesu hapo hapo alipokea uponyaji, wake!

Sasa jionee! Ni kwamba kupona kwake, kulitokea pale ambapo aliamua, alidhamiria kumuendea Yesu; Luka 8:43  Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote, 44  alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma.

 

Hapo pendo la Kristo linadhibitika ndani yake! Uponyaji unatokea, lakini sio kwamba Yesu alianza kumpenda alipomponya la! Upendo ulikwepo ila huyu mama alipoamua kukubaliana na pendo hilo ndipo alipopona!

 

Yesu alitupenda na alimpenda huyu mama hata kabla hajavaa mwili yaani hajaja humu ulimwenguni, na pendo hili linadhibitishwa na Uungu wote; Yohana 3:16  Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

 

Dhambi ilipoingia ulimwenguni pendo la namna hii ililijidhiirisha mara! Halikuanzia katika kuzaliwa kwa Yesu, bali hata Agano la mlima Sinai ni ishara ya hili pendo, Mungu alipochinja mnyama na kuwavika wakina Adamu nguo ilikuwa ni sehemu ya utendaji wa hili pendo! Mahali pengine kwenye biblia hujulikana kama neema, unapoona neema, uwe na hakika huwakilisha pendo la Kristo, tumeokolewa kwa neema tu, ama tumeitwa kwa neema tu, uwe na uhakika ni pendo lake!

 

Pendo hili haliwezi kujifunua kwako wakati ukiwa na shida unaenda kwa waganga wa kienyeji, ukiwa na mahitaji humulezi Yesu unawaeleza watu tu na kuishia hapo! Hutaki kwenda kanisani, maana huyu mama alimfuata Yesu kwenye kusanyiko, na penye kusanyiko maana yake ni penye uwepo wa Mungu, sasa kwenye ibada ndipo alipo Kristo!

 

Usiende kanisa ni kanisa, usiende kusanyiko ni kusanyiko, maana siku hizi watumishi wengi wa uongo wameibuka, tafuta kanisa la watu walio hai kiroho, mahali ambapo kiukweli hata akili na ufahamu wako wa kawaida unatambua hapo Mungu yupo, epuka mbwe mbwe za Shetani, na misisimko isiyo na Mungu ndani yake.

 

Yawe ni maombi yako na ni maombi yangu pia kuwa Mungu afunguwe macho yako ya ndani ili uweze kujua sehemu sahihi itakayokuwezesha kukutana na Yesu wa kweli, maana siku hizi kuna ma-yesu wengi wa uongo, hawamuhubiri Yesu mwenye kukemea dhambi, kwao dhambi ni sehemu ya ibada, hapo kimbia!

 

Ukiona huduma isiyokemea dhambi, hiyo imepotoka, ukiona huduma ambayo wazinzi na walevi wamo humo humo na ni watumishi, hapo kimbia wala usiage! Ukiona mtumishi anawataka washirika wake kimapenzi ujue huyo ni “ajenti” ama wakala wa kuzimu, na ukimkubalia atakuunganisha na kuzimu moja kwa moja, kwani mashariti yao moja wapo ya kuwaunganisha ni kulala na watu! Hususani wenye nyota ambazo zitawasaidia kuvuta watu makanisani! Epuka na kimbia hili!

 

Unajua kuna watu wanaenda kanisani ili kuirithisha nafsi yao kuwa nao wapo kanisani! Hii ni hatari sana, ni sawa na kunywa maji machafu ili tu uwe umekunywa maji! Ni sawa na kula mkapi au vyakula vibovu ili tu kukidhi hitajio la kula! Ukifikia hapo upo mahali pagumu sana!

 

Maana baada ya muda afya yako itakongoroka tu! Wengine huabudu kwa kufuata mkumbo! Yaani ni mtumishi yupi anawika sana mjini siku za leo, akipoa au akiona ushabiki umempungua basi hufikiri kuhama hapo! Akiibuka mwingine mjini, humfuata!

 

Watoto hata! Shetani huwa naye anahubiri, tena ni muhubiri mzuri tu! Ukipinga muendee Yesu kwenye Mathayo na Luka 4, utamuona Yesu akihubiriwa na Shetani pale, na maandiko anamsomea, kuwa akiwa ndie Mwana w aAdamu ageuze jiwe kuwa mkate, na alimuonyesha hata utajiri alionao akimpa na kanuni kuwa akimsujudia atampatia!

 

Sasa usitishike na injili za mafanikio, maana hawakuanza wao alianza Shetani, na kupata fedha au mafanikio kutoka kwao sio jambo la kigeni, maana hata Yesu angemsujudia hakika angepewa, maana ni muhimu kujua nao huwa wanamsujudia nani!

Kusoma maandiko na kuyafafanua siyo kipimo, kwani hata Shetani alimsomea Yesu, maana ni kweli yapo kwenye biblia! La muhimu na jambo zuri kuliko yote ni wewe kuhakikisha kuwa ndani yako unapata amani ya Kristo, maana wapo ambao Mungu anawakosesha amani na mtu husika ila kwa ushabiki huzidi kugandamana naye! Huku ni kupotea!

 

Injili ambazo jina la Yesu limewekwa kando, msisitizo wa maombezi sio katika jina la Yesu na Damu yake kwenye uhalisia, ama nguvu za Roho Mtakatifu, bali ni katika viambatanishi, au visaidizi, kama mafuta ambayo yamesingiziwa kuwa ya upako, na wengi hawataki kujua kama ni upako upi unaotajwa hapo, maji ya upako au maji ya baraka, wengine wanagawa hadi bangili za upako, pete za upako, nasikia siku hizi kuna keki za upako,  hii ni hatari sana!

 

Najua wana wa upotevuni ni wepesi sana kukinzana na ukweli huu, na wana hoja nyingi sana wakitumia maanadiko, ila mioyoni mwao wanaujua ukweli, maana sifa zipo kwenye mafuta na maji yakaniponya, Yesu amekuwa kama ni msaidizi!

 

Nisikilize, ukitaka kuliona pendo la Kristo likikusaidia maishani mwako ni muhimu sana kuhakisha kuwa unaambatana na Yesu kama alivyo, waepuke wanaokupa maji machafu, katika Yohana 7:38-39 Yesu anaita akiwataka wale wenye kiu waje au waende kwake ili awape maji!

 

Maji yake ni safi, alimwambia yule mama kwenye kisima cha Yakobo katika Yohana 4 kuwa kiyanywa hayo maji ya Yesu hataona kiu tena! Sasa wamekupa Yesu na bado kiu ya ulevi ipo, wamekupa Yesu na bado una kiu ya kuiba waume za watu! Ukimuona mume wa mtu mate yanakutoka kama fisi na mfupa! Wamekupa Yesu angali bado una kiu ya dogo-dogo, ukimuona kijana “handsame” ama binti mrembo, hata kama ni umri wa mwanao jicho linakutoka kama vile fundi simu aliyedondosha nati, maana nati zake ni ndogo kwa hiyo asipotoa macho hawezi kuziona kirahisi, huu akiwa na hofu usikute imepotea!

Unasema eti umeokoka, au unamependa na una Yesu, sawa sikataii! Lakini mbona hajaondoa kiu ya dhambi nadani yako! Bado ni mwizi, unazini kwa siri, nyumba ndogo kuacha umeshindwa! Hakika huna Yesu aliyehai una yesu marehemu! Wala usinikunjie ndita, ila ukweli ndio huo!

 

Anasema hivi; Yohana 4:13  Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena.

Yesu akiingia nadani yako, na kiu ya mambo ya dunia ispoondoka, uwe makini, rejea msalabani upya!

Neno la Mungu ni maji, sasa injili kama inahubiriwa haibadilishi maisha yako, kuna mambo mawili hapo makuu, wewe mwenyewe u na moyo mbovu, ama injili unayopewa ni maji machafu, ni maji yasiyo na uwezo wa kukausha kiu ya dhambi, na tamaa zake, swala la upinzani wa Shetani hili ni la maombi tu! Ila hatuwezi au maombi hayawezi kukusaidia sana kama wewe mwenyewe hujakaa eneo salama, maana pepo mchafu amtokapo mtu na akipata mwanya mwingine hurejea, maandiko husema mmekuwa safi kwa lile neno, neno hukuweka kuwa safi, na mapepo hayakai maeneo ambayo yamesafishwa kwa Damu ya Yesu!

Huwa nasema kuna yesu aliyekufa, na kuna Yesu aliye hai, unaposema nataka kumuona Yesu, nina haja na Yesu, uwe makini maana wakina Pilato wapo hapo kukupa yesu aliyekufa kama Yusufu wa arimathayo, huyu alipewa Yesu/yesu ila mfu, aliyempatia alihakikisha kuwa amekwisha kufa! Na aina hii ya Yesu hawezi kuleta mabadiliko kwenye maisha yako!

 

Unasema una Yesu lakini hatuoni badiliko la ndani; ndani yako, una sema una Yesu lakini hatuoni matokeo ya wewe kuhuishwa hata kidogo! Yesu aliye hai, hukushindia dhambi, huhuisha utu mpya na kuua ule utu wa kale, hawezi kuchangamana na dhambi! Ukiona unajiita una Yesu lakini hakuna badiliko la dhambi au la kiroho ndani yako uwe na hakika kuwa kuna shida ipo mahali, utakuwa wamekupa yesu aliyekufa siyo Yesu aliye hai kama Yule aliyefufuka siku ya tatu, maana kuna dini zina yesu sawa, ila ni yesu marehemu!  

Wanahubiri habari za Yesu, Lakini wao wenyewe ni wazinzi, ni walevi, hawawezi kusimama madhabahuni bila kunywa pombe kidogo, hawawezi kukaa bila kutongoza washirika! Ni mzee wa kanisa ila sigara anavutia chooni!

 

Ona hapa; Marko 15:44  Lakini Pilato akastaajabu, kwamba amekwisha kufa. Akamwita yule akida, akamwuliza kwamba amekufa kitambo. 45  Hata alipokwisha kupata hakika kwa yule akida, alimpa Yusufu yule maiti.

Kuna dini, zimehakikisha kuwa yesu waliye naye amekwisha kufa, ndio maana wamekupa wewe! Maji yao siyo yale halisi yenye uwezo wa kuondoa kiu ya dhambi, ndio maana wamekupa wewe!

 

Huwa ninaweka sana angalizo hili, kuwa unapokuwa na kiu ya kutaka kumjua Yesu, unapokuwa na kiu ya kutaka kukoka, unapaswa kuwa makini tena mno, maana ukisema nina kiu, moja kwa moja uwe na hakika kuwa wapo watu ambao hawaachi kukuletea maji, ambayo kwa kweli siyo sahihi, ndio maanaYesu kwenye ile Yohana akapaza sauti aksema kila mwene kiu na aje kwangu, aje anywe, hakusema na aje achote maji ila alisema na aje kwangu, kwa hiyo jifunze kumtafuta Yesu kwanza, na sio maji kwanza , kama wengi wafanyanvyo! (Maana ukiwa na Yesu, atakwambia haya maji uliyopewa siyo yangu.)

Najifunza sana kwa Yesu mwenyewe, alipokuwa pale msalabani na alipopatwa na kiu, alisema naona kiu, na badala ya kumletea maji walimletea siki! Uwe na hakika na wewe ukisema nina kiu, wapo na watu ambao nao watakuletea siki ama maji machafu!

 

Ukisema nataka kuokoka, ninamtaka Yesu watakwambia usiondoke kwenye dini yetu maana na huku pia watu wanaokoka, kuna vikundi huku nako vya uaomsho, uwe na hakika ni uamsho bandia, maana kuna na moto bandia, ambao hufananishwa na ule wa Roho Mtakatifu!

 

Namtaka Yesu, wanakuletea Yesu ambaye amekufa, hawezi kuondoa dhambi! Ndio maana adui ameweka utitiri wa madhehebu na makanisa mapya na watumishi wengi, ni ili kuwapoteza watu, maana ma-yesu wafu wamejaa sana humu duniani! Umakini unahitajika sana!

Asante kwa kunisikiliza (nafsini mwako), ama kunifuatilia kwa njia ya usomaji huu wa hii makala, nina amini kuwa kuna kitu umekipata hapa, Yesu anakupenda, ila kama hujakutana na pendo lake uwe na hakika kuna dosari ipo mahali, chukua hatua mapema mnoo!

Pia anasema kwamba mtu akimpenda atazishia amri zake, kwa hiyo kama kweli umedhamiria, mpende kwa kuzishika amri zake, epuka michanganyo, epuka kuuzoelea wokovu, asante na Mungu akubariki mno; Yohana 14:23  Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake. 24 Mtu asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalolisikia silo langu, ila ni lake Baba aliyenipeleka.

Hongera kwa kusoma ujumbe huu, nakutia moyo kuzidi kumtazama Mungu, na pia uwenda hujaokoka, yaani Yesu sio Bwana na mwokozi wa maisha yako! Nakutia moyo tena kuokoka sasa! Yamkini ni uchumi, fedha, hazipatikani, unazingirwa na nuksi na mikosi, kila unalofanya haliendi, unakabwa na mapepo, ! Wewe njoo kwa Yesu na hayo yote yatapita kabisa ! Sasa natumi u tayari!

Sema; MUNGU BABA, NINAKUPENDA, ASANTE KWA KUNIPENDA KWANZA, LEO NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NA NIPO TAYARI KUOKOOKA, TAFADHALI INGIA NDANI YANGU, SAMEHE DHAMBI ZANGU, NA FUTA JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKU, NA ULIANDIKE SASA KATIKA KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Ameni.

 

Kwa kufanya hiyo umekwisha kuokoka sasa, na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka lililopo karibu nawe ukasali, hapo, waambie kuwa umeokoa hivi karibuni, ili wakulee vyema kiroho.

Mawasiliano yetu, kwa M-Pesa au Simu: +255 759 859 287, barua pepe: ukombozigospel@gmail.com

pia temnbelea: www.ukombozigospel.blogspot.com .