Jumatano, 28 Agosti 2019

MSAADA WA KUTOKA KWENYE KIFUNGO CHA MADENI.

Kunamtu ameniandiki hivi, "Mtumishi Bwana Yesu asifiwe mnaendeleaje ss wazima mtumishi nina Hitaji tuombe niwezekupata hela ya kulipa madeni kwani ni nadaiwa sijui napata wapi pesa."
Nami kumjibu hivi:

Hatua ya kwanza ni kuvunja roho ya utumwa kupitia madeni,Mithali 22:7 Tajiri humtawala maskini, Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye.
Pili, lipa hayo madeni rohoni kwa Damu ya Yesu, tatu ndo kuomba milango ya fedha ifunguke ili uyalipe mwilini, 4, omba nidhamu ya Mungu ili fedha hiyo ikija uwe mwaminifu kulipa nasio kufanyia mambo mengine ! 5. Tumia hekima y

Jumamosi, 24 Agosti 2019

MAMBO MUHIMU KATIKA UINJILISTI:

Bwana Yesu aifiwe Mpendwa, leo tunageukia kitabu changu cha Wito na Huduma ya Uinjilisti, na tunaangazia kipengele kimoja;
 MAMBO MUHIMU KATIKA UINJILISTI:
Na Mwalimu Oscar Samba, wa Ug Ministry.
Kumbuka mada hii inahusiana na utendaji, maana yake namna ya kufanya unapokuwa shambani, au namna ya kujindaa kwa ajili ya kuingia katika eneo la mavuno, wala hapa sineni habari za mfumo, au tabia za Mwinjilisti kama huko awali.

Mambo haya yatake sana kuyajua ili uwekeze nguvu kubwa hapo katika maandalizi, maombi na hata wakati unahubiri:
1. Watu Kumuamini Yesu, 2. Kumkiri, na 3. Kumpokea kama Bwana.
Warumi 10.9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

Jumatatu, 19 Agosti 2019

#JE_WAJUA_KUWA_UKIFA_HUJAOKOKA_UTAENDA_MOTONI?


Awali ya yote pokea salamu zangu, leo ninataka kukufikirisha tu walau kwa kiduchu, kuwa maisha unayoishi leo ndio yenye hatima ya maisha yako ya baadae.
Kulikuwa na tajiri mmoja na masikini mmoja jina lake Lazaro, tajiri huyu hakumjua wala kumcha Mungu, ila Lazaro alikuwa ni mtu mwema.

Ikatokea siku wote wakafa, njia ambayo mimi na wewe ni shariti tuipitie, Lazaro alienda Mbinguni, na tajiri motoni;
Luka 16:22 Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

Alhamisi, 1 Agosti 2019

NAMNA YA KUMJUA NABII WA KWELI NA WA UONGO.   Mwalimu Oscar Samba wa Ug Minisry.
Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu changu cha Wito na huduma ya Nabii,
(a) WA UONGO:
1. Tazama Misingi yao ya Kihuduma, Hawana msingi wa neno, Hofu ya Mungu haipo pamoja nao, mambo muhimu ya kiroho kama Ubatizo, Toba ya dhambi, Ujazo wa Roho Mtakatifu, Msisitizo wa kudumu katika imani ya kweli, msisitizo katika maombi ya kufunga na kuomba katika Roho na Kweli, au matumizi ya jina la Yesu hayatakuwa yakitumika kama ilivyo amriwa, na kamwe hawezi kuitumia Damu ya Yesu.
Kumbuka hata akijifanya kujitahidi kubatiza, hataweza kutumia utatu mtakatifu au maji mengi, na kuwafunza watu wake katika Roho kuhusu huo ubatizo.
Mambo hayo yatazame sana katika huduma ambayo unaitilia shaka.
2. Chunguza Matunda yao, Yesu alituhusia na kutufahamisha kuwa tutawatambua kwa matunda yao, akibainisha kuwa mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, alikadhalika mti mbaya huzaa yaliyo mabaya.
Mathayo 7:15 Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?