Jumanne, 23 Januari 2024

KUSAMEHE, MSAMAHA Na Christopher Mwakasege

 Felix Mbwanji:

SAMEHE NA KUSAHAU (BY MWL, C.MWAKASEGE)

                            

TABIA YA MUNGU YA KUSAMEHE NDANI YAKO

         Ulipompokea Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako, ulipokea tabia ya aina gani?

"  Bali wote waliompokea (Kristo) aliwapa uwezo wa  kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu." (Yohana 1:12,13)


         Ulipozaliwa mara ya pili kwa Neno la Kristo ulifanyika kuwa mtoto wa Mungu.

Watoto wa Mungu wana tabia ya namna gani?

         Kwa kuwa wamehamishwa toka ufalme mwingine na uzazi mwingine, na kuingizwa katika ufalme wa Mungu na uzazi wake (Wakolosai 1:13); watoto hawa wanatakiwa wawe na tabia nyingine.


          Kabla ya kuzaliwa mara ya pili, kabla ya kumkiri Kristo ya kuwa ni Bwana: ulikuwa na tabia ya dunia hii iliyoongozwa na mfalme wa dunia hii ambaye ni shetani.

          Ulipozaliwa mara ya pili na kuukiri wokovu katika Kristo, ulipokea tabia mpya inayoongozwa na Mungu mwenyewe aliye ndani yako.


"  Kwa kuwa uwezo wake wa Uungu umetukirimia  vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa (Utakatifu), kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno; za thamani,ili kwamba kwa hizo mpate kuwa Washirika wa TABIA YA UUNGU, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa." (2 Petro 1:3,4)

Jumatatu, 8 Januari 2024

NDOTO ZA UZINIFU au MAPEPO MAHABA, ama Kuota Unazini Ndotoni Maana yake ni Nini?

Na Christopher Mwakasege_


 Leo nataka tujifunze juu ya “Mwongozo wa kutafakari na kuombea ndoto zenye UZINIFU AU UASHERATI ndani yake”.

Maneno haya ‘uzinifu na uasherati’ yanahusu ufanyikaji wa tendo la ndoa usio halali kibiblia. Uzinifu linatumika zaidi wakati tendo la ndoa limefanywa na mtu ambaye hajaoa au hajaolewa. ‘Uasherati’ linatumika zaidi wakati tendo la ndoa limefanywa nje ya ndoa na mtu ambaye ameoa au ameolewa.


Mtu anayepata ndoto zenye mambo hayo, huwa zina madhara makubwa sana ya kiroho, na ya kimwili – kwa aliyeota ndoto hizo!

Kumbuka kwamba: Neno la Mungu la biblia, kwa kushirikiana na Roho Mtakatifu, linatuongoza kujua namna ya kutafsiri na kuziombea ndoto za aina yo yote – ambazo ni pamoja na hizi zenye mambo ya uzinifu au uasherati ndani yake.

Jumatano, 3 Januari 2024

Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha MAANA YA UZIMA, NA UZIMA WA MILELE. Pwenti ya 2, katika mada ya pili ya Uzima wa Milele

 Mwl OSCAR SAMBA ( #NasahazaMwlOscar )

#FaidayaJaribu: #Usiogope

Na Mwl. Oscar Samba

Kwenye Kipengele cha Faida za Uzima wa Milele

2. Tunakula Matunda ya Mti wa Uzima. Huu ni mti wa ajabu sana. Kumbuka mti huu ndio uliowafanya Adamu na mkewe kuondolewa kwenye bustani ya Edeni. Mimi na wewe leo hatupo hapo bustanini kwa sababu ya hii dhambi. 

Mungu alihofia wasije wakala na kisha wakaishi milele. 

Ufunuo wa Yohana 2:7 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu. (Nikutie moyo pia kuhakikisha unashinda vita, majaribu, maana mbingu ni mji wa washindi! Sio sehemu ya walioshindwa! Hili lijue na ulifikiri daima maana ni taswira halisi unayopaswa kuwa nayo kwenye fahamu zako.) 

Tujione Siri hii muhimu kule Edeni:

Mwanzo 3:22 Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele; 23 kwa hiyo Bwana Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa.

24 Basi akamfukuza huyo mtu, akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya Edeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima.

Kilichowafanya kuondolewa sio uzuri wa bustani! Sio kwamba wameshafanya dhambi kwa hiyo hawastaili tena kuendelea kula mema ya hiyo bustani, la! Bali ni kwa sababu ya uwepo wa huu mti. Ndiyo sababu kubwa Mungu anayoitoa anapowaondosha hapo.