Jumatano, 22 Februari 2023

Fahamu ni Sababu za Mungu Kukutaka Uendelee Kuvumilia hilo Pito au Jaribu

 

Na Mwalimu Oscar Samba
Ujumbe huu ni Sehemu ya #Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA. Tunaendelea kidogo plae tulipoishia katika Makala iliyopita, kisha ttutatazama jambo la Kwanza; Karibu:

Ikifika mahali ukiona msisitizo uliopo ndani yako sio kumtwisha tu Mungu mzigo wako, sio Mungu tu kukutia nguvu. Bali swali lako ni kwamba sawa nitavumilia, ila Mungu atanijibu lini? Uwe na hakika kuwa unahitaji msaada mkubwa zaidi.


Maana kuna mambo mawili hapo. Mosi ni la kuchoka na pili ni la kuhoji uaminifu wa Mungu kwamo?

Kwamba huna shaka, hata sasa ukimuita akutie nguvu anweza, ila hoja ni kamba huu ni mwaka wa tano sasa, kumi au miaka naho inaenda, unakaribia 40 na hata 50 sasa ila bado hajakutokea. Ndio maana ukinielewa hapa hutaacha kuyaelewa maandiknya Zabuti kuhusu uaminifu. MUNGUkuna.mahali unasoma na unaona jinsi mtunga Zabuti anavyopitia sehemu ngumu, kisha anataja uaminifu wa Mungu.

KANUNI
1. Fahamu ni Kwanini Mungu Anataka Bado Uendelee Kuubeba au Uendelee Kupitia. Waliowahi kusoma kitabu kile cha Isaya 55 utabaini kuwa watu wale kuna namna walikuwa wamepishana na mipango ya Mungu maishani mwao. Ndio maana Mungu anafika hatua ya kuwaambia kuwa mawazo yenu sio mawazo yangu, wala njia zenu sio njia zangu. Anawapa na kipimo husika, kwamba kama vile mbingu zilivyo mbali na aridhi; ndivyo mimi nanyi tunavyopishana.

Najua unajua kuwa Mungu ana akili kuliko wewe. Ufahamu wake ni mkubwa kukuzidi. (Ikupe kujiuliza kwa nini kakuacha.) Na kubwa zaidi ni kwamba anakupenda kuliko unavyo mpenda. Na kile kitabu chetu cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO LAKO kinafunza kiunagaubaga kuhusu kusudi la Mungu kukupitisha hapo.

Jumamosi, 18 Februari 2023

NENO LA LEO Zaburi 90:12

 Neno la Leo


Zaburi 90:12 Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima.



‭‭Psalms‬ ‭90:12‬ ‭NIV‬‬

[12] Teach us to number our days, that we may gain a heart of wisdom.


Yawe ni Maombi yako, Omba Hekima; Bali Omba Akugundishe Kuzihesabu Siku ili Uweze Kuwa na hiyo Hekima


Uvumilivu na Kuwa Mtu wa Kujifunza kila Uchwao ni Miongoni Mwa Maana ya Kuzihesabu Siku...


Tembelea pia www.ukombozihospel.blogspot.com

Jumanne, 14 Februari 2023

kitabu chetu cha: CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu cha: CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA.

Hiki sii kitabu cha kawaida wala si somo tu bali ni ujumbe. Najua kila ujumbe ni somo katika mukutadha wa mafundisho na ufundishaji. Japo sio kila somo ni ujumbe.

Ujumbe huu ni matokeo ya mahali ninapopapitia ambapo mwaka jana palinipatia vitabu kama viwili hivi. Mosi ni kile cha  HAKUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA. Na pili ni kile cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO LAKO.

Kwa lugha nyingine unaweza kusema kuwa sii jumbe za kawaida. Bali ni maelekezo. Mfano wa ujumbe kibiblia ni pale mfalme Nebukaddeza alipoota ile ndoto na kisha kujikuta hana tafsiri yake na kuomba msaada kwa Danieli nabii wa Mungu. Tukiachana na yote pale, yale maneno, "Danieli 4:27 Kwa sababu hiyo, Ee mfalme, shauri langu lipate kibali kwako; ukaache dhambi zako kwa kutenda haki, ukaache maovu yako kwa kuwahurumia maskini; huenda ukapata kuzidishiwa siku zako za kukaa raha."


Kwa hiyo, kama Mungu amekupa kukisoma kitabu hiki, moja kwa moja fikra zako zielekeze kwenye ujumbe uliopo ndani yake. Ambao unanuia kumsaidia kwa kumpa mtu husika maelekezo muhimu ya kufanya ili kuendelea mbele na pito au jaribu analolipitia.

Ni matoke ya mimi katika jana ya leo, baada ya kuzungumza na kiongozi wangu mmoja juu ya pito ninalolipitia na majibu ya Mungu juu yangu. Majibu hayo yalinitaka niendelee kuvumilia. Na aliniambia hadi nimalize masomo. Nikauliza je nikimaliza Mungu ndo atanijibu?

Akaniambia hata yeye hajui kama atanijibu au la, ila alichoambiwa ni kwamba kwa wakati huu usijaribu kubeba mambo mawili. Kwa mujibu wa mukutadha wa hekima ile ni kwamba inaonekana maamuzi yangu dhidi ya pito husika nyuma yake hayana mapenzi makamilifu ya Mungu.