Jumatano, 24 Machi 2021

Ujumbe huu ni sehemu ya #kitabu chetu cha MTUMIKIE MUNGU, UKubali #Wito, #Kuna Faida katika Kumtumikia Mungu, na Kuna Hasara za Kukaidi Wito.

Na Mwalimu Oscar Samba

Usipoelewa jambo hili, huwezi elewa ni kwa nini Mungu aliamua kumfuata Yona baharini! Angeweza kuamuacha na kuinua mtu mwingine!

Anayefahamu swala hili kwa kina sio mwepesiwa kuimba ule wimbo wa “usifaye mchezo na Yesu na watu wengi! Wengine wanapanda na wengine anshuka!”
Japo ni kweli kabisa, ila kuna wakati mukutadha wake unagoma!
Hivi unajua ilimgharimu Mungu miaka mingapi kumuinu mbadala wa mfalme Sauli!
Ni rahisi sana kushangilia Mungu kumkataa Sauli! Ila fahamu iligharimu muda mrefu sana hadi kuja kutawala kwa mfalme Dudi!
Daudi hawezi kutawala kama muda hajaimarika, hajamaliza darasa la uongozi, hajafikia vigezo vya ufalme wa mbinguni.
Ndio maana hata baada ya Sauli mfalme kukataliwa na Mungu aliendelea kutawala hadi wakati ulipofika, na hata alipofariki bado Dauli hakuruhusiwa kutawala Israeli yote! Kwa hiyo bado kuna maeneo tena eneo kuba sana lilikuwa halina utawa ambao Mungu anautaka.

Jumamosi, 6 Machi 2021

Muombee Elia ama Yusufu wako, Ni Msaada wa kutoka kwenye Majanga kama ya Corona. #Corona #Covd19

 nA mWALIMU oSCAR sAMBA

Ujumbe huu ni sehemu ya #kitabu chetu cha MAMBO MUHIMU YA KUFANYA AU KUZINGATIA KUNAPOKUWA NA ADHABU YA KIUNGU INYOIJUMUISHA ENEO ULILOPO AU JAMII

18. Muombee Elia ama Yusufu wako; Kuna mtu MUNGU amemuweka ili kukuvusha ama kulivusha taifa na hata dunia kwa ujumla! shida kubwa ya wapendwa ni kwamba katika mambo kama haya kuomba kwa maarifa kumekuwa ni tatizo kubwa sana kwao! Wamisri walivushwa kutokana na akili, na hekima, pamoja na Roho wa Bwana ndani ya Yusufu kama Farao anavyokiri kwenye ile Mwanzo 41, kuwa hapana mtu mwenye akili, hekima na Roho wa Bwana ndani yake kama Yusufu! Ina maana gani! Kama Misri na dunia ya kipindi kile ilivushwa katika janga la njaa kutokana na sifa hizo zilizopelekea uwekaji wa akiba, basi na wewe muombee mtu ambaye mbingu zimemuandaa au kumtazamia kama sehemu ya majibu ya janga husika, kama ni la njaa, sawa, kama la kijografia pia sawa. Mfano kama ni la ugonjwa, ambao tena hauna dawa au kinga, waweza muombea Mungu ampe maarifa zaidi, na uwezo zaidi ama kuwaombea wanasayansi wapate maarifa zaidi ya kuwawezesha kugundua chanjo sahihi, na yenye uwezo stahiki, na isiyo na madhara katika mwili wa mwanadamu. Pili wagunduwe dawa, au tiba, huku ukiombea na viwanda vunavyotengeneza au vitakavyotengeneza dawa hizo, na vifa ambazo pia hutumika kipindi kama hiki, pamoja na kuwaombea madakitari na wauguzi ulinzi maalumu, maana nini kitatokea kama ukienda hosipitalini na kukuta madakitari na wauguzi wote hawapo ama wamaelemewa na wagonjwa kuiasi cha kushindwa kukusaidi na sababu ni baadhi yao kufariki!
Waombee pia wafadhili wataojitoa kwa fedha zao ili kuwezesha upatikana wa dawa hizo na vifaa pamoja na kuchangia gharama ili watu wengine wazipate, na huku sio kupungukiwa na imani bali ni kiroho kabisa. Kuweka akiba kwa Yusufu ni jambo la mwilini, na dawa pia ndivyo ilivyo, sayansi ni kiroho kabisa. Sasa tumekuwa na injili ambayo huiita injili makorokocho, kuwa hata chanjo ni pepo, hususani za ambao unaendeleao sasa, kuwani njama za watu wa mataifa fulani wanaotaka kutuua! Unafikiria mwenye fikra kama hizi ataombea sayansi isaidie kupembana na tatizo kweli! Maelekezo ya Paulo mtume kwa Timotheo kutumia mvinyo ilikuwa ni sayansi, maana kuna tiba hapo! (Sasa sina maana na kwako ufanye hivyo la!) Ila ninataka uione nafasi ya sayansi katika mambo kama haya! Tunajua kwa Yesu kumpaka mtu tope na kumtaka akanawe na Isaya kutumia makate wa tini ilikuwa ni ufuno sawa, ila sayansi nayo ni kiroho, waombee wafunuliwe dawa!