Jumanne, 12 Novemba 2019

USIFANYE HARAKA KUFUNGUA HUDUMA, KUHAMA KANISANI AMA KUACHA KAZI NA KUFUNGUA BIASHARA.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu ninachoendelea naho cha: NAFASI YA VIUNGO VYA MWILI WA MWANADAMU KATIKA ULIMWENGU WA ROHO.

Na Malimu Oscar Samba:
12. Uwe na Subira, Saburi ni kitu muhimu sana, kuna wakati unakuwa katika vita vya kumiliki na kutawala lakini unakuta eneo unalotaka kumiliki au kuweka maskani yako bado hakuna nafasi, usiwe na haraka, wala usifanye haraka, endelea kuwa na uvumilivu, jambo la kuwekwa kwa adui chini ya miguu yako ni swala la mchakato, sio la siku moja, na swala la kukuwekea mazingira ya kuishi katika miliki yako kiroho iwe ni kihuduma, kiuchumi ama kiutumishi na kindoa na kadhalika linahitaji muda !