Alhamisi, 31 Machi 2022

Sehemu ya Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA, Kuna na Ushuhuda wa Mwalimu Oscar, Nia ya Ujumbe ni Kukutana Unipe Moyo Usikate Tamaa

 Na Mwalimu Oscar Samba

Ujumbe huu ni shehemu ya Kitabu chetu cha CHAKUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA, katika mada ya Kwanza inayohusu aina ya Imani inayohitajika Ukiwa Njia Panda. Kumbuka ni kitabu chenye kuelezea mazingira ya mtu aliyegubikwa na maamuzi zaidi ya moja ikiwa ni matokeo ya mahali anapopitia. Yaani Njia panda ya kiroho au Kifikra na hapa ni katika pwenti ya pili

2. Tazama Nguvu Zako. Kwanza fahamu mtu anapokata tamaa, hususani katika kiwango cha kuwa radhi kuachana na mapenzi ya Mungu hata kama anayajua dhairi, au kufikia kiwango cha kutamani kufa; ni nguvu zimemuishia! Kwa kifupi amelemewa na aina ya dhiki aliyonayo;

Maana ndugu, hatupendi, msijue habari ya dhiki ile iliyotupata katika Asia, ya kwamba tulilemewa mno kuliko nguvu zetu, hata tukakata tamaa ya kuishi. 2 Wakorintho 1:8

Nguvu zao zilizidiwa, kilichofuata ni wao kukta tamaa ya kuishi! Sasa utaelewa ni kwa nini Elia alijiombea kufa katika ile 1Wafalme 19! Wengi wanashangaa na kukosa majibu maana huku nyuma tu katoka kufanya tukio kubwa na la kushangaza! Ni kwamba vita viliibuka upya, na nguvu hakuwa nayo!

Imani haikai hewani, kuna mahali inakaa. Eneo moja wapo ni kwenye nafsi, na inategemea sana nguvu zilzizopo kwenye nafsi yako. Ndio maana Yesu alipoishiwa nguvu alianza janja ya kutaka kukwepa mapenzi ya Baba yake! Sio kwamba alikuwa hajui umuhimu wake, la! Alijua sana tu. Ila nguvu zilipunguka.