Jumatatu, 5 Juni 2017

ATHARI ZA KULA VYAKULA VYA FUTARI VYA DINI FULANI, VYA MAAGANO, SHEREHE ZA KIPEPO, MILA NA KISICHO SALAMA KIROHO.

 Na Mwalimu Oscar Samba wa Ug Ministry.
Kwa kifupi ujumbe huu hulenga kukupa mathara ya kula vyakula visivyosalama kiroho, kwani wapo wakristo ama watu waliookoka ambao hubugia ama hula kila kitu kilichopo mbele yao ama huwa na mazoea ya kula vyakula ambayo ni matokeo ya ibada fulani ama huambatana na ibada ya dini fulani. Na hufaya hivyo bila kujua athari zake. Leo Bwana amenituma kukupa mathara hayo.

Kwa dini za wenzetu vyakula ni ibada, kabla ya kupika na wakati wakupika huvunenea na pia muda wa kula. Hata kwetu ndivyo ilivyo, ndiposa Yesu alikuwa akifanya hivyo mara kwa mara, kumbuka ile mikate na samaki alishukuru na kuiombea.

Pia katika Luka 22 kabla ya kuumega ule mkate na kunywa maji ya mzabibu alishukuru na kisha kuwagaiwa wanafunzi wake. (Luka 22.19 Akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, [Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.)

Na kwa wale wanaofanya matambiko pia hufanya hivyo hivyo, kwani hata uchinjaji wao ni kwa mujibu wa taratibu za mila zao yaani kipepo. Mfano wachaga, humnyonga hadi kufa kwanza huyo mfugo ndiposa wamchinje, wengine humtemea mate na wapo wanaompa chakula cha aina fulani. Hata ipo dini ambayo huchinja kwa sheria zao na kuna aina fulani ya maneno hutamka.
Sasa unapokula vyakula vyao unajiingiza katika uharibifu wa nafsi yako ama hali yako ya kiroho kwenye ulimwengu wa roho na kuna hatari pia yakuingia kweye maagano ya kipepo, na kesho nitakuwekea somo kuhusu jambo hili la maagano ya kipepo kupitia chakula.

Kuna mtu mmoja aliniambia ya kwamba aliwai kula chakula cha dini fulani kilichokuwa ni chaibada ama sherehe au sikuku fulani na baada ya hapo hali yake ya kiroho ilibadilika. Kwa bahati nzuri alikuwa ni Mchungaji na alifanya hivyo kwa sababu alidai alikuwa safarini na mazingira yalikuwa magumu kwake. Na kupitia kofia hiyo ya Utumishi alitumia muda na mbinu za kiroho ili kuondoa na mathara hayo na hatimaye kufanikiwa.

Wapo watu wanaojikuta wakiwa na hali ya mapooza kiroho, yaani hawawezi kuomba, kuimba, ama kusoma Neno kama hapo awali huku sababu ikiwa ni hii hali ya kubugia bugia. Mtu mmoja akaniambia; “lakini uji wao ni mtamu”. Ila kila akila anajikuta nakosa amani gafula na huzuni huingia ndani yake.

Mimi nilimjuza kuwa kukosa huko amani ni ishara ya kuingia kwa roho ya kigeni ndani yake na roho hiyo inamfanya Roho Mtakatifu kuugua kwani humuhatarishia nafasi yake kwako.
Tudhibitishe athari hizi kimaandiko. Ninakupa nukuu ya makala yangu itakayokujia kesho, yenye dhima ya kukujuza ama kuwakomboa watu wanaoota ndoto za kula vyakula, tuoe kipengele hiki cha Mithali hapo:
Mithali 23: 6 Usile mkate wa mtu mwenye husuda; Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa; 7 Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. Akuambia, Haya, kula, kunywa; Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.
AwazavyoNafsini mwake, kwa hiyo muda unakula au kabla yeye huwana na mawazo mabay ama ya hila dhidi yako na hukudhuru. Nimetumia neno kukuwazia maana bibilia ya kingereza haijatumia aonavyo bali imetumia neno afikirivyo ama awazavyo;
(7 For as he thinketh in his heart, so is he: Eat and drink, saith he to thee; but his heart is not with thee. ) Hiyo ni ya King James Version,
Tuone ya Basic English; (Proverbs 23:7 For as the thoughts of his heart are, so is he: Take food and drink, he says to you;but his heart is not with you.{Ni kama yalivyo mawazo ya moyo wake}

Mathara hayo tunayaona kwenye msatari wa 8 ambapo hudhiirika mwilini pia; (8 Tonge lile ulilokula utalitapika, Na maneno yako matamu yatakupotea. )
Mstari wa 6, anataja chakula cha mtu huyu mwenye husuda, kisha msitari wa 7, Tunayaona mahusiano hayo, kwani mtu huyu anakupa chakula kwenye mstari wa 6, ila wa saba, anakinenea ama anakiwazia nafsini mwake na jambo hilo huwa na mathara kwako.

Ninachotaka ukione hapa ni kwamba, mtu huweza kukupa chakula na moyoni ama nafsini mwake akakuwazia vibaya ama anakunenea vibaya na chakula hicho kukudhuru ndiposa mstari wa 8 ukasema utakitapika, na hautaishilia tu hapo bali na maneno matamu yatakutoka.

Kwa mantiki hiyo ni kwamba, punde ulapo chakula cha kidini ama kisicho salama kiroho yale maneno yaliyonenwa ama ile roho iliyobebwa na hicho chakula huambatana nawe.

Kuwa makini sana na swala hili. Pia kama upo mazingira hatarishi kima hayo na huna uwakika na kile unachokula hata kama ni hotelini, maana zipo hoteli ambazo hupika kishirikina kiasi ambacho hukifanya chakula hicho kuwa hatari kiroho yakupasa kukiombea na kuvunja roho zilizopo ndani ya hicho chakula. Ila njia hii isikuhalalishie kula chakula ovyo ama kula vile vya ibada ya sanamu, kumbuka hata Paulo ameonya jambo hilo. Pia epuka vyakula vyote vinavyoambatana na sherehe za dini isiyo salama kiroho, pamoja na vile vya sherehe za kipepo.

Mfano wapo watu wanopewa mashariti na waganga hususani wanaofanya biashara za kipepo, mashariti hayo huwa ni kuandaa sherehe ili kuwalisha watu. KWEPA HAYO ILI UWE SALAMA.
Ilikuwa nikuage hapa ila ninaguswa kuwapa njia za kuwakomboa wale ambao wameadhirika na jambo hilo.
NJIA ZA KUWAKOMBOA WALIOATHIRIKA NA VYAKULA HIVI.
1. Omba rehema yaani fanya maombi ya toba kwa Mungu kwa kula vyakula hivyo
2. Fanya maombi ya kuondoa hayo mathara, omba huku ukifanya ishara ya kuyaondoa kwa jina na Damu ya Yesu kivitendo.
3. Rejesha kila kilichoibiwa ama kilichodhurika kutoka na athari hizo, waweza tumia hili andiko. Yoeli 2: 25 Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu.

4. Mfukuze Shetani kwa maombi ya vita na ikiwezekana njia hii itumiye kabla ya ile ya nne kadri Roho atakavyokupa kibali.
Ninakutakia kila la heri katika kuyaishi masomo haya, usikubali kupitwa na ujumbe wa kesho.
Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigospel.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              
Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa
2 DAY SKY: https://www.2daysky.com/home


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni