Jumatatu, 19 Juni 2017

Mwalimu Oscar Samba: MBINU TEULE ZA KUTOKA KWENYE UMASIKINI KWA WATU WALIOKOKA.

Na Mwandishi wetu, Ug Ministry.

Hakika kwetu Jehova Jire ni Ebeneza maana sio kwa uweza wetu bali ni kwa nguvu zake ndiposa tunayanena hayo. Jana tulifanikiwa kuhitimisha semina yetu huku nguvu za Mungu zikishuka mahali pale, watu wakifunguliwa na hakika semina ilikuwa ya Baraka maana licha ya watu kunufaika na mafundisho pia wapo waliookoka.

Kama ilivyo ada Mwalimu jana alianza kwa kuwaimiza wakristo kumtafuta Mungu kwanza na haki yake kisha hayo mengine yote wanayoyahitaji kutoka kwake Yeye atawajaza.

Siku ya jana Mwalimu alihitimisha kwa Mbinu ya 9, nayo ni ; Kufahamu athari za kuwa na Mali isiyo na Yesu. Katika hili alisisitiza mathara yanayoweza kujitokeza kwa mtu mwenye mali kisha akamkosa Yesu kwenye Uchumi wake.
Alinza na andiko lile la Ufunuo wa Yohana 3: 17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.

Maandiko hayo yanamzungumzia mtu mwenye kiburi cha fedha, na yanamtaka aje kwa Mungu maana yu Uchu avikwe vazi jeupe ambalo ni wokovu, na anajiona ni tajiri ila Bibilia inamuona kuwa ni mnyonge, masikini na kipofu, mwisho anatakiwa kutubu maana maandiko yanasema anampenda ndio maana anamuonya au kumkemea. Andiko hili liwe lako wewe mwenye hali hiyo, uliyepandisha mabega kwa sababu ya mali yako.
Tutazame kitabu cha Yeremia 17: 11 Kama kware akusanyaye makinda asiyoyazaa, ndivyo alivyo mtu ajipatiaye mali, wala si kwa haki, katikati ya siku zake zitaachana naye, na mwisho wake atakuwa mpumbavu.
Hapa Yesu anawazungumzia wale wanaojipatia mali kwa njia ya udhalimu, wanataka rushwa, utapeli ama njia zilizo za hila, na anawaita ni wapumbavu kisha hufanana na kware ambaye ni ndege anayekusaya watoto asiyowazaa, maana yake mtu kama huyu anafanya kazi bure kwani watoto wasio wako hawawezi kukuita baba ama mama, labla udogoni ila wakikua watagundua wewe sio mzazi wao, alikadhalika hiyo mali haitakuwa ya kwako.
Tugeukiye kitabu kile cha Mithali 15: 16 Kuwa na mali chache pamoja na kumcha Bwana; Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.

Andiko hilo linatutaka tumche Bwana katika chumi zetu hata kama uchaji huo utatupelekea kuwa na mali chache kwani ni heri zaidi, kuliko kuwa na mali nyingi kisha ukakosa kwenda kanisani, ukashindwa kuudhuria maombi na mbaya zaidi hali yako ya kiroho ikafa, mwishowe ukaenda jehanamu ya moto.
Tuone tena jambo hilo katika Mithali 16: 8 Afadhali mali kidogo pamoja na haki, Kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.
Ni afadhali kutenda haki ile ya kibibilia katika kuitafuta mali kuliko njia haramu kama za hongo ili kuipata mali nyingi.
Ona tena hapa; Zaburi 37: 16 Kidogo alicho nacho mwenye haki ni bora Kuliko wingi wa mali wa wasio haki wengi.

Dhima ya andiko hili ni kukutaka kutokuwa na tamaa katika kuitafuta mali, pia sio kusudio lake kukutaka kuwa masikini au mwenye mali chache bali yakupasa kuitafuta mali au kuwa na bidii katika Kriso Yesu na sio tamaa ya mali ama mali bila Yesu.
Turejee tena kwenye Mithali, Mithali 30: 8 Uniondolee ubatili na uongo; Usinipe umaskini wala utajiri; Unilishe chakula kilicho kadiri yangu.
9 Nisije nikashiba nikakukana, Nikasema, Bwana ni nani? Wala nisiwe maskini sana nikaiba, Na kulitaja bure jina la Mungu wangu.


Maandiko haya ni ya ajabu sana kwani yana upekee wake, muombaji anaukataa umasikini, kwani athari zake ni mbaya mno, maana huweza kumpelekea kuiba, pia anaukataa utajiri usio na Yesu ndani yake kwani huweza kumpelekea kumkana ama kumkufuru Mungu ama kutokumcha Yeye maana huweza kujikuta anaota kiburi ambacho kitamfanya hadi kusema kwa kejeli kuwa Mungu ni nani?

Ndiposa na Mwalimu akakutaka kuwa na kiu ya kuwa tajiri ila hakikisha katika mali zako unakuwa na Yesu, kumbuka Mwalimu siku za nyuma aliwai kutoa mfano wa kijana yule tajiri jinsi mali yake ilivyomzuia kumtumikia Mungu.

Na jana alisema kuwa ukimuona Mpendwa ambaye yupo tayari kutoa laki moja kwenye harusi ila mchago wa ujenzi wa kanisa anatoa elufu tano jua mali yake inampeleka au imeshamfikisha pa baya, na hiyo ni dalili ya mali isiyo na Yesu kikamilifu, au kabisa.

Nikutakiye siku njema na majira mazuri na hari kuukatika kumfwatilia Mwalimu wetu kwenye masomo mengine na huenda kesho tukaendelea na sehemu ya 4, ya ile makala yetu ya NGUVU YA AGANO, Ikiwa ni sehemu ya kitabu chetu cha TAJIRIKA KIBIBILIA. Pia usiache kutazama video ya mafundisho yote ikiwemo ya somo ili kwenye Channel yetu ya Youtubu hiyo hapo chini. Hapo pia utanufaika na maombezi maalumu ya Uchumi ya jana na siku nyinginezo.

Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigospel.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,  
 PAGE: https://www.facebook.com/ugukombozigospel/
Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa
2 DAY SKY: https://www.2daysky.com/home               

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni