Ijumaa, 9 Juni 2017

TUMAINI KWA ALIYEKATALIWA AU KUACHWA.

Na Mwalimu Oscar Samba wa Ug Ministry.
Haijalishi umeachwa ama kukataliwa kwenye Ndoa, Mwenzako amekuacha ama ni Mchumba amekusaliti, Umekataliwa kazini  na hatimaye kufukuzwa. Ama umekosa kibali mbele ya wapendwa kanisani kwako au viongozi wako wa kiroho wamekukataa na kukutelekeza na imefika hatua ya wewe kujiona kama mtu aliyeachwa.

NISIKILIZE, Leo nimekuletea TUMAINI na TUMAINI hili ni YESU KRISTO aliye Bingwa wakuwakumbatia waliokataliwa na kuachwa. Ni kweli jambo ama mambo hayo yanaumiza na mimi katika uzoefu wangu wa miaka isiyofika Theladhini hapa Duniani kwani umri wanguni ni miaka 28 na siku tatu, nimebaini kwamba kama kuna mambo ambayo huujerui moyo; Kukataliwa ni miongoni mwayo.
 Ukitaka kuamini, jaribu kumwambia mtoto mdogo asiyejua hata kunena ya kwamba unampenda atatabasamu na hata kuachia kicheko, ila punde umamwambiapo kwamba haumpendi, ama unamchukia tabasamu lile hugeuka kuwa simanzi. Ndio maana mtu anapokuwa kwenye tatizo ama uhitaji na kisha kuwaona watu hawaguswi na tatizo lake ni rahisi sana kuumia zaidi.

Ndiposa kwenye misiba wafiwa mara nyingi huzungukwa na watu, huku wakiwafariji na wengine huacha shuhuli zao na kuamua hata kulala kwao ama kujumuika nao kwa muda mrefu. Hiyo yote ni kuwaondolea upweke.
Jambo hili liliwai kumsumbua Mfalume Daudi, Zaburi  69: 20 Laumu imenivunja moyo, Nami ninaugua sana. Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna; Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu.

Nifika kwamba alitamani mtu wakumfariji ila alimkosa. Na wewe kama umefika hapo Usijali wala usiumize Kichwa maana Yesu yupo tayari kufanyika Faraja yako leo.


Kitabu kile cha Zaburi kina chambua jambo hili na tunapata TUMAINI la ajabu sana hapa, kwani  unapopapitia pia Mtumishi huyu aliwai kupapitia na alitambu haya kwamba ni Mungu mwenyewe pekee ndiye awezaye kumpa Faraja hiyo. Fungua nami kitabu hicho;  Zaburi 27:10 Baba yangu na mama yangu wameniacha, Bali Bwana atanikaribisha kwake.

Umeona Mukutadha wa hilo andiko? Anasema kuwa wazazi wake wamemuacha ila Mungu atamkaribisha kwake. Kwa hiyo kwako wewe kilicho cha Msingi ni kuhakikisha ya kwamba unasimama katika mstari wa Mungu majira kama haya ili Mungu akukaribishe kwake.
Tatizo kubwa kwa watu wengi leo wanapojikuta wamekwaruzana ama kuachwa au kukataliwa hujikuta wanatupa maneno, kujibu hoja kwa njia za “mipasho,” kukasirika ama kuweka kinyongo au kushindwa kusamehe walio wa udhi.

Shetani akifanikiwa kukuumbia vitu hivyo basi jua hali yako itakuwa ngumu maana MUNGU hata kukaribisha kwake, maana tayari umeshajitengenezea Mazingira ya wewe  kujitetea ama kujipigania.

Kuna kisa kimoja kilichozaa chanzo cha wimbo wa Baba na Mama wakiniacha sitarudi kwamwe, sitarudi;
Kisa hicho ni hiki hapa. Ilikuwa ni nchini India, ambapo kulikuwa na binti mmoja aliyeamua kuokoka na wazazi wake wakamuonya ila alikataa kumuacha Yesu, kisha wakampeleka ufukweni mwa bahari kwa ajili ya adhabu ama kumuacha au kumtenga kabisa na familia yao maana wao waliamini miungu ila binti bado aliendelea na msimamo wake.

Wakiwa ufukweni tayari kwa ajli ya jambo hilo, Ndipo walipoanza kujitenga, Upako wa Mungu ulitiririka na kisha mtoto huyu kujikuta akijawa na nguvu za Mungu na kuimba huo wimbo. Kwa upako huo wazazi wake walishindwa kuvumilia na kuhairisha jambo lile. Leo hii wimbo huo umekuwa ni wabaraka kwa watu wengi mno.

Ilitokea India na hata leo inatokea kwa wengi wanaoamua kuokoka katika familia zenye mazingira magumu kama hayo, wewe ikikutokea fahamu kama mtunga Zaburi anavyo Nena “Baba yangu na mama yangu wameniacha, Bali Bwana atanikaribisha kwake. Zaburi 27:10 .
Kila la heri; Cha msingi hapa usikubali kumuacha Yesu kwa sababu ya kuachwa ama kukataliwa na wanadamu maana kwa ndiko liliko TUMAINI la kweli; kwani ukimkimbilia Yeye hutaaibika.
Yule mama aliyetokwa na Damu kwa muda ule wa miaka 12, alitengwa na kukataliwa na jamii yake kwa kuonekana kuwa ni najisi na hali ile ilikuwa ni kama msiba kwake ila alitambua ya kwamba msaada na TUMAINI lake ni kwa YESU pekee.

Alipomkimbilia tu, Punde misiba yake ikakoma hapo hapo, aliyeitwa najisi, akapata kibali na kuwa maarufu mbele ya maelufi ya watu katika makutano na hadi leo tanasoma habari zake.

Huyo Binti wa India alimkimbilia Yesu akijua kuwa ndiye TUMAINI lake na amekuwa maarufu hadi leo, mimi na wewe tunaimba wimbo huo. Na wewe hakikisha unamkimbilia Yesu ili siku moja vizazi vijavyo vikukumbuke kwa tendo hilo la Ujasiri huku maelufu kwa mabilioni na hata matrilioni ya watu wakitiwa moyo na jambo hilo.
Ninakutakia maisha mema ya ushindi katika Kristo Yesu huku nikikusihi kuendelea kufanya maombi ya vita ili kuoma kibali kwa wanaokupinga na pia kumuomba MUNGU akutiye nguvu katika majira hayo huku nawe ukijilinda ili usijibize neno kwa neno wala usitende lililobaya ama kujiwekea kisasi au kukasirika, vitu ambavyo vinaweza kukutenga na YESU na kumfanya asikukaribishe kwake.  

Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigospel.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              
Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa
2 DAY SKY: https://www.2daysky.com/home



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni