Alhamisi, 18 Desemba 2025

Mfululizo wa 1 wa Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UNAOOKUWA NJIA PANDA

Tunaanza na Utangulizi (kinapatikana Google Bure)

 Na Mwl. Oscar Samba

 Utangulizi

Kitabu hiki kimenuia kumsaidia mtu ambaye yupo katika mazingira

magumu ya kimaamuzi, na mbele yake kuna aina zaidi ya moja ya

maamuzi ambayo anahatarishwa kuyachukuwa au yanayomkabili,

inawezekana lililo hatari ni moja, au salama ni moja ila kuna zaidi ya

aina mbili au moja na kadhalika.

Kitabu hiki ni matokeo ya sehemu ninayopitia sasa kuhusu ndoa yangu.

Ikumbukwe sasa ni mwaka unaokaribia wa nane toka mwenzangu

tuoane na kujikuta ananiacha kwa talaka mahakamani hali inayonipa au

kunipelekea kuwa njia panda. Njia panda yangu inaweza isiwe na tija

sana kwako ila la muhimu ni wewe kufahamu mazingira ya kitabu

hiki ili kikusaidia. (Wakati nakitoa, imetimia miaka 10/11, “2015-

2015”.)

Unaweza usione umuhimu wake kwa leo ila nikuhakikishie kuwa

chakula hiki ni kama akiba, kuna muda tunakula leo lakini chakula

hicho kinatusaidia kesho; sio kwamba tuliingia kwenye mfungo la! Bali

homa ya ghafula imetukuta na kutunyima hamu au uwezo wa kula. Ila

kwa akiba ya jana ambayo hatukuwa hata na wazo la kula tumevuka leo

salama!

….Nikikuongezea ni kwamba, mara baada ya kuandika

utangulizi huu, na nikiwa tayari nimeshaanza kukiandika hiki

kitabu, njia panda nyingine ilijitokeza kama sio moja basi ni

zaidi, licha ya swala la ndoa, lakini pia limeibuka swala la

kusimamishwa masomo chuoni. Kumbuka nipo katika chuo cha

Biblia Dodoma cha CBC; mara baada ya kutofautiana na

kiongozi wangu mmoja wapo katika swala fulani, nilijikuta

nikipewa adhabu ya kusimamishwa masomo mwaka mmoja.

Nikiwa tu nimetoka kuchukuwa barua zangu, (ikiwa moja yangu na ya

mchungaji wangu kingozi,) ndipo nilipokutana na mchungaji mmoja wa

dhehebu jingine akiniambia kuwa nihamie kwake. Maana huku

kumekuwa kugumu kwangu na katoa sababu kadhaa: zingeweza

kuonekana ni zenye mashiko maana nyuma ya pazia jambo langu

limeonekana ni matokeo ya mimi kuwa na tabia ya kutetea na kudai haki. Pamoja na kusema ukweli pale ambapo ninapoona mambo

hayajaka sawa.

Wazo hili halikwepo kabisa kichwani mwangu, maana nilishapitia

mahali kama hapa mara baada ya uongozi wangu wa sehemu huko

Arusha kutofautina nami na kunichukulia mamuzi ambayo sikuyapenda

maana sikusikilizwa kimapana!

Japo mara baada ya taarifa za kusimamishwa kwangu, wenzangu

niliokuwa nao chumba kimoja miongoni mwa ushauri wao wa kwanza,

ni ule wa kunitaka nisihame dhehebu, sikuwa nimewaelewa maana

wazo hili halikwepo. Sasa baada ya ushauri wa kuhama niliokuja

kuupata baadae, na hususani nikiwa kwenye gari wakati narudi

nyumbani; ndipo wazo hili la ile mbegu ya yule mtumishi likataka

kumea au kukua ndani yangu. Niliing’oa kwa haraka kwenye mawazo

yangu! Maana nilijua kitu adui anachokitafuta.

Japo kulizaliwa nyingine ya je, nikimaliza adhabu nirudi tena hapo

chuoni au nihame! Maana mazingira yaliyonipelekea hapo ninafahamu

fika bado yangalipo! Nafika nyumbani nako nakuta mradi wa kuku

niliouanzisha kuku wamekufa kama asilimia 75 hivi!

Njia panda nyingine inazaliwa ya kukata tamaa; kuuendeleza au

kuupatia nguvu tena! Ila baada ya imizo kubwa moyoni mwangu

nikajisema kuwa; ukiniuliza swali kwamba kwa nini Oscar nafanikiwa

nitakujibu kuwa, nilifeli somo la kukata tamaa!

Mimi sijui njia panda yako ni ipi! Ila unatakiwa kuwa makini na aina ya

maamuzi unayofanya hususani ukiwa katika nyakati ngumu! Utulivu ni

muhimu sana. Utanielewa katika kipengele cha utulivu.

Ngoja nikuongezee jambo jingine!

Niongeza hii inakuja mara baada ya kukikamilisha kitabu hiki kabisa,

na ninaiongezea mwaka huu wa 3/2025, maana nilikianza na

kukikamilisha mwaka huo wa 2022 kwenye mwezi wa 3.

Kwanza mara baada ya mkasa huo wa kusimamishwa masomo,

nilijikita katika maombi ya siku 21, ghafula nikagundua dozi haitoshi. 

Nikaendeleza megine ya siku 40, jumla yakawa siku kama 61 hivi. 

Katika maombi hayo ndipo nilipopokea agizo na imizo moyoni

mwangu la kuanza mikutano ya injili. Na nilimwambia Shetani wazi ya

kuwa umenipiga chuoni, mimi ninakupiga mtaani. 

Nilifanikiwa kufanya mikutano ya injili kama 24 ndani ya miezi 7.

Ukifanya idadi ya wiki kwa kufanya 7x4=28 ukitoa hiyo mikutano 24

utapata ni wiki 4 tu ambazo siku hubiri.

Idadi hiyo ya mikutano iliwapa hofu sana wachungaji wenzangu wa

dhehebu langu. Kukainuka vita vikubwa sana. ikaenea propaganda ya

kuwa nina mpango wa kufungua kanisa huko Rombo, kwa hiyo

nikifungua nitachukuwa washirika wao wote. Maana pia nilikuwa

nafanya na mikesha ya maombi nyumbani kwangu, na kwenye baadhi

ya makanisa yaliyotupa kibali. Sanjari na hayo tulikuwa tukifanya

mikesha kama hiyo kwenye nyumba za watu wenye mahitaji

mbalimbali, kundi lilikuwa ni kubwa.

Mikesha hiyo ilikuwa ikiudhuriwa na baadhi ya wachungaji, wake zao,

na familia zao. Lakini pia na wazee wa kanisa kutoka makanisa

mbalimbali ya dhehebu langu huko Rombo.

Nilipofikia mkutano wa 14, nilikutana na upinzani mkali uliotishia

kuendelea kwangu na mikutano hiyo; ulitoka kwa mlezi wangu kiroho

ya kuwa niache kuendelea na mikutano hiyo. Japo, toka mwanzoni

kabisa mara baada ya mikutano kadhaa, niliona hali ya kunyimwa

ushirikiano. Upinzani huo ulipanuka hadi ngazi ya sehemu na kiongozi

mmoja wapo wa jimboni kuwa sehemu ya swala hilo. 

Wachungaji kadhaa ambao nilipaswa kuhitaji ushirikiano nao,

walijikuta wakipewa taarifa mbaya kuhusu mimi; hali iliyotishia

ufanyikaji wa mikutano yangu. Kwa hiyo, dehebu langu la nyumbani

likanisusa kabisa. Watu wengine wakajitokeza na kunipa ushirikiano.

Wakati nikipambana katika kipindi hicho hicho, sasa nikiwa ninaelekea

mkutano wa 15; ndipo nilipopokea ujumbe wa simu ya mkononi kutoka

kwa mlezi wangu kiroho wa kunifukuza kanisani. Sababu ni kwamba

ninafanya mikutano kwa kiburi. Nilipokonywa na spika. Nikasalia na

spika zile za juu “horn speaker” na baadhi ya vyombo. 

Sikuacha, nikahubiria kuzipitia hizo hizo. Ila Mungu akanipatia “midi

speaker” kipindi cha muda mchache mbeleni. Watu wa madhebu

mengine wakaibuka, wakitaka nijiunge nao. Kiukweli walinipa

ushirikiano mkubwa sana, japo nia ya kunivutia kwao ilikuwa ni kubwa

pia.

Kama hilo halitoshi, ngazi ya sehemu bila kunisikiliza, au kujitetea,

nayo ikatangaza kunifukuza. Na wakasema nimefukuzwa katika kanisa

la nchi nzima. Kumbuka hapo nimesimamishwa masomo, na huku

ninafukuzwa. 

Nilikuwa, katika hati-hati ya kuendelea na mikutano au la! Nilijisemea

moyoni ya kuwa, sitarudi nyuma. Nitaendelea na mikutano hadi

mwisho, kisha nitaona atakalolitenda Bwana. Mara baada ya juhudi za

kuhitaji suluhu, nilijibiwa ya kwamba labla niache kuhubiri; ndipo

tutakaa na kuzungumza. Niliwajibu, kama kuhubiri ni kiburi basi

amueni wenyewe. Japo jibu hilo nililitoa moyoni; sio mbele zao moja

kwa moja. Nikajisemea tena, kama kuhubiri ni kiburi, basi hiki ni kiburi

kizuri Zaidi.

Niliijua hofu yao, walisema ya kuwa hii ni “movement.” Na

wanamashaka itachukuwa washirika wao wote, wakidai nina kibali sana

kwao. Kwa hiyo, makakati wao ulikuwa ni kunizima! Matunda ya watu

kuokoka, ilikuwa ni nguvu yangu.

Wakati huu, hali ilikuwa ngumu kidogo. Maana tangazo la sehemu

lilipiga marufuku hata washirika wa kawaida kuwa pamoja nami,

wakionekana tu na mimi wao nao watafukuzwa. Kwa hiyo,

wakalazimika kutuma tu watoto wao kuja kunisaidia kuimba pamoja

nami kwenye mikutano. Wao wakaishilia kunichangia na kuniombea. 

Wachache sana walidiriki kuja na kunisaidia majukumu moja kwa

moja.

Nilikabiliwa na njia panda nzito ya kuendelea kusalia na dhehebu langu

au la. Tofauti na kipindi nilichofukuzwa Arusha, kipindi hiki sikuwa na

shida sana kuhusu kutaka kuhama mwamvuli wa dhehebu. Ila washirika

baadhi yao walinishindikiza, wakisema muulize Mungu uwenda wakati

huu anataka uhame, tofauti na ule wa Arusha aliokuzuilia.

Mchungaji mmoja rafiki yangu akaniambia, labbla niache kwanza

kuhubiri niingie maombi ya siku 40. Nikamuuliza ya nini? Akanijibu ni

ili nimulize Mungu ni kwa nini ninapigwa vita? Nikamjibu, maombi

nilishaomba. Maana ule ulikuwa ni muda wa kazi. Nikamwambia Roho

alishanijibu. Akaniuliza, amenijibuje? Nikamwabia ameniambia;

“kanyaga twende; kanyaga twende.” Tukaishilia kucheka, ila huo ndio

uhalisia.

Nilipokaribia na mwisho, nikapokea ufunuo kutoka kwenye Zaburi, ya

kwamba nimetengwa na mpenzi wangu, waliopaswa kunisaidia

nimetengwa nao. Nikajikita katika maombi ya siku 4. Bwana

kanipatanisha na adui zangu, nikaandikiwa barua mbili. Moja ya

kunirudisha katika ushirika, na pili ilikuwa ni ya kunirudisha chuoni.

Na kipindi hicho cha kufukuzwa, ashukuriwe Mungu aliniinulia

mhazini wa Jimbo, ambaye alinipokea kwa nguvu. Kinyume na taratibu

maana nilipofukuzwa sikupewa mahali pa kusali; nikawa chini yake

nikaabudu kwake.

Leo ninavyoongea yaani 2025 hii ni miongoni mwa watumishi muhimu

katika dhehebu hili hili. Kwa hiyo, adui aliijua kesho yangu, na akataka

kunizuilia. Jiulize, ni wangapi wanaopitia katika nyakati kama hizo na

kujikuta wanafanya maamuzi ya kuhama katika makanisa, au madehenu

yao? Hapana shaka ni wengi, kwa hiyo adui ameua kesho za watu

wengi kwa kupitia njia panda kadha, wa kadha alizozileta mbele yao!

Ukiamua vyema leo, utaifikilia ndoto yao. Usibadili urai wa uzao wa

Yakobo, kisa ndugu zako wamekuchukia na kukuuza. Salia nyumbani.

Maana wewe ndiwe msaada wao miaka kadhaa ijayo.

 Tafadhali Usikose Sehemu Ijayo (2)

Km Hujaokoka Okoka Sasa...Sema: *BWANA YESU, MIMI NI MWENYE DHAMBI, NAKUOMBA UNISAMEHE; Ameni* 

...Tafuta Kanisa la Watu Waliokoka Ukaabudu Hapo...Nimekuombea

Karibu Sana Katika Channel Yetu Hii

Tafadhali Tembelea na Hufuma Zetu Nyingine 

 Ni Maalumu kwa Ajili ya Mafundisho ya Neno la Mungu.

Kwa Maombi: +255759859287 

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Tumeunda Channel ya WhatApp, Tufolo; https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Kwa Maombi +255759859287 

Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL


 *UWE NA AMANI*

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni