Watu wengi wamejikuta wakiwa katika njia isiyo sahihi mara baada ya kupitia
kipindi cha ukimya wa Mungu. Kuna kipindi Mungu huwa kimya kama
sehemu ya jaribu kwetu. Ikiwa imani yetu kwake inapimwa, jambo la
sabra na hata nidhamu, utii na hofu kwake; ni kwamba ni kweli
tunamtegema na kumtumaini Yeye!
Japo wakati mwingine anaongea lakini hatuelewi, na pia kuna muda
anaona hata akiongea hatutamuelewa. Usisau pia ukimya wake, huweza
kuwa ni matoke ya hasira yake juu yetu. Maana hata mfalme Sauli kuna
wakati Mungu hakusema naye; baada ya kukorofishana naye, na
kujikuta akigeukia msaada kwa mganga wa kienyeji. Na alilalamika
kuwa Mungu hasemi naye hata kwa ndoto.
Sasa, Nisikilize; Mungu anapokua kimya, au unapofikia katika hatua
ama “point” ya kutokuelewa cha kufanya: ni sawa na mtu aliyeko njia
panda. Njia ziko nyingi, na hajui anaelekee wapi! Wewe tulia, usiwe na
haraka.
Wakati ufunuo hu unanijia, ulinijia na kujikuta najiambia kuwa; njia
panda nyingi zinakuwaga na eneo la kupumzikia, au lililotengwa na
kuwekwa vitu fulani, fulani: kama mau au bustani. Nyingine zinakuwa
na eneo la duara na katikati kuna kuwa na mnara au nembo au alama
fulani. Aidha kiwakilishi cha maji na kadhalika. Ya pale Moshi Mjini
Kilimanjrao Tanzania; kwa sasa moja wapo ina “kichuguu” cha mlima
Kilimanjro. Nyingine sanamu ya mwanajeshi mwenye sila, ile ya
Ufaransa ina mnara mkubwa tu. Huku ya Mwanza ikiwa na Samaki. Pia
ya Arusha mjini nayo ina mnara wa Mwenge ile iliyopo mkaba na
Azimio la Arusha. Nyinge ina mnara wa Saa ile iliyopo karibu na ofisi
ya mkuu wa Mkoa au tawi la Benki Kuu ya Tanzania.
Kwa hiyo, kama upo katika njia panda kama hiyo, kuliko
uamuwe kufuata njia ni njia, utapotea! Na gharama ya kupotea
ni kubwa: na kurudi huwa gharama kubwa sana: na kuna kuwa
na kutokurudi kabisa; kwa hiyo, ni bora upumzike kwenye hilo
eneo lenye nafas tajwa hapo juu. Jifanye hata kama unangolea
majani au muhudumuwa bustani ama maua yaliyopo hapo.
Hata kama hakuna maua, au mnara, basi kuna uwezekana kukawa na
eneo la kusimama; hapo simama!
Kama hakuna, simama katikati kabisa, na magari yatakupisha tu maana
hapo katikati huwa hayapiti!
Epuka kuendea njia ni njia! Nimewaona wengi wakisema
kuwa nimesubira mume vyakutosha, mwezi hu ukipita, asipokukuja
mtu kunichumbia aliyeokoka; basi. Nimevumilia vyakutosha, akija hata
mlevi nitaoana naye! Hata mwisilamu maadamu ni mwanaume nitaona
naye! Huku ni kuhatarisha maisha kwa viwango vikubwa sana! Wengi
tumewapoteza na hakuja tena kuirudia njia ya wokovu, waliziendea njia
nyingine moja kwa moja.
Unakuta mtu katafuta kazi muda wa kutosha, na baada ya muda,
anavunjika moyo. Anakata tamaa, hajui mbele yake kuna njia panda.
Anafika hapo, kuna njia ya kwanza imeandikwa au inatwa; vumilia
utapata kazi katika mpango wa Mungu: japo utakawia kulingana na
mtazamo wako. Ingawa mimi Mungu sikawii maana ni na muda
nilioupnga. Ya pili inatwa, kubali kutoa rushwa ya ngono, yaani weke
wokovu pembeni alafu upate kazi na utaanza kesho. Na utapewa na
kiasi fulani cha fedha cha kuanzia maisha, ila uwe na uhakika uwokovu ndo umeuacha hivyo.
Nyingine ya tatu inatwai, kubali kusilimu, yaani uwe mwisilamu, au
kuolewa kama mke wa pili alafu nitakupatia maisha mauzri. Lakini
huyo Yesu wako muweka pembeni.
Mtu kwa kuwa amechoka kiroho, na amemuona Mungu kama
hajamjibu, anajikuta anaangukia katika njia ambayo si sahihi! Maamuzi
kama haya huwa hayafanywi ghafula. Ila ni jambo ambalo linakuwa
katika hali ya mgogoro kwenye nafsi ya mtu kwa muda kitambo!
Fahamu kuwa maamuzi hufanywa kwenye nafsi. Ndiposa
unampoyasikia maneno ya mtu aliyevunjika moyo; au kukata tamaa
unapaswa kuwa makini sana.
Jifunze kuisemesha nafsi yako, na kujiambia kuwa, muamini
Mungu. Kama wakina Kalebu, Musa na Yoshua walivyozungumza na
ndugu zao. Wakiwambia kuwa msimwasi Bwana: nawe ongea na nafsi
yako, iambie; Ee nafsi yangu; usimwasi Bwana. Maana atabaki kuwa
Mungu hata kama hakujibu; ni bora kufia au kuzalilika kwenye mikono
ya Bwana kuliko nje ya hapo.
Huwezi kumuelewa Musa, kama hukuwahi kupitia hapo. Mungu alikuja
na pendekezo la njia, ambayo Musa alilikataa; kwamba niwauwe hawa
watu wote alafu wewe uwe taifa kubwa. Musa aliipangua hoja ile, kisha
Mungu akakubali waende, ila Yeye hatakuwa pamoja nao! Napenda
sana maneno haya kuwa, “kama hutaenda pamoja nasi, nasi hatatoka
hapa!” Ifike mahali na wewe, kaa pembeni kwenye eneo la njia panda;
alafu mwabie Mungu, sichukui maamuzi yoyote yale kama
hutaninyesha njia sahhi!
Unajua kilicho waangusha wana wa Israeli na kujikuta
wanajitengenezea ndama ya kuyayusha na kuiabudu kama Mungu! Ni
pale walipoona Musa amekawia sana mlimani! Adui akawafikisha njia
panda ya kimawazo! Kisha akawaonyesha njia isiyo ya kweli
aliyoikusudia, Haruni naye akajikuta anawasikiliza wale watu!
Nakujulisha hili maana eneo la kumngoja Bwana, limefanyika kuwa
gumu sana kwenye maisha ya watu wengi; Hata watu walipoona ya
kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana
wakamwendea Haruni, wakamwambia, Haya! Katufanyizie miungu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika
nchi ya Misri hatujui yaliyompata. Kutoka 32:1
Sijui kwako ni jibu lako lipi lililokawia kuja! Ila kumbuka na
fahamu sana hata Mithali husema; kuwa jambo likikawia moyo
huugua! Usipojifunza kuongeza imani yako; ya kumngoja
Bwana kwa Saburi, uwe na hakika unakabiliwa na hatari ya kuwa njia panda.
Musa alionekana amekawia machoni pao! Na wao kujikuta wakichukua
maamuzi yasiyo sahihi! Sio hao tu, kuna makosa pia kwa mfalme
Sauli. Hapa ni mwanzoni tu mwa ufame wake, alikwena kutoa sadaka,
na watu walijikusanya kwa ajili ya jambo hili, ila Samweli alikawia, na
alipokawia, watu waanza kuondoka. Alipoona wanaondoka naye moyo
wake ukavunjika. Kwa jeuri na kiburi akaisongeza yeye ile sadaka.
Ile amemaliza tu, Samweli kuhani huyo mbele yake! Sijui kama
unajifunza kitu hapo, unapokuwa unasoma haya maandiko! Ni kwamba
ile mtu amenaguka au kuiendea njia nyinge, tu, hukumu ya Mungu
inamjili punde. Mungu ambaye alifikiri yupo mbali, anamuona sasa
anamjilia ila sio katika kumpatia, majibu bali ni katika kumpatia hukumu!
Hali kama hii utaiona pia kwa Adamu na mkewe. Wakati wakiwa njia
panda ya mamuzi ya kwamba wakubaliane na onyo la Mungu au
waambatane na ushawishi wa Shetani Mungu alikuwa kimya. Alitulia
kama vile hayupo, ila walipoanguka tu! Ndipo walipomuona huyo
ajitokeza, na uwepo wake walianza kuuhisi, baada ya anguko: ndiposa
uliwapatia hukumu na kujificha!
Mungu sio kwamba yupo mbali, yupo karibu, ila njia
panda wakati mwingine zipo ili kutupima kama kweli
tunampenda, au kumtegemea Mungu!
Mfano hapa kwa mfalme Sauli, vumilvu ulikuwa ukipimwa, na utii pia.
Kumbuka kinyume cha utii ni kiburi! Na hapo kilijidhiirsha. Yamkini
alijisemea moyoni, mwake kukwa ba Samweli ni nani! Hata mimi
naweza kutoa sadaka hii, mimi ni mfalme, nami ni mpakwa mafuta wa
Bwana! Watu wengi Mungu anazungumza nao, kuhusu jambo fulani,
ila kuhusu utekelezaji wake anakawia kusema. Hapo wengi huanza
kulitekleza, baada ya muda wanakuja kugundua kuwa wakati wa
Mungu ulikwa bado. Hapo ni baada ya maumivu mengi! Fahamu, hata wachezaji na waimbiji, hawaanzi bila kusikia kipenda au filimbi ama
mlio fulani !
Na sisi tunapswa kujifunza pia. Jionee maandiko haya kisha ujifunze
jambo hapa. 1 Samweli 13:
8 Akangoja siku saba, kwa kadiri ya muhula uliowekwa na Samweli
lakini Samweli hakuja Gilgali; na hao watu wakatawanyika mbali naye.
9 Sauli akasema, Nileteeni hapa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za
amani. Akaitoa sadaka ya kuteketezwa.
10 Hata mara alipokwisha kuitoa hiyo sadaka ya kuteketezwa, kumbe!
Samweli akatokea. Naye Sauli akatoka kwenda kumlaki na kumsalimu.
11 Samweli akasema, Umefanya nini? Naye Sauli akasema, Ni kwa
sababu naliona ya kuwa watu wanatawanyika mbali nami, na wewe
hukuja siku zile zilizonenwa; nao Wafilisti wamekusanyika pamoja
huko Mikmashi;
12 basi nikasema, Wafilisti watanishukia sasa mpaka Gilgali, kabla
sijaomba fadhili za Bwana; kwa hiyo nalijishurutisha, nikatoa sadaka ya
kuteketezwa.
13 Naye Samweli akamwambia Sauli, Umefanya upumbavu;
hukuishika amri ya Bwana, Mungu wako, aliyokuamuru; kwa maana
Bwana angaliufanya ufalme wako kuwa imara juu ya Israeli milele.
14 Lakini sasa ufalme wako hautadumu; Bwana amejitafutia mtu
aupendezaye moyo wake, naye Bwana amemwamuru yeye kuwa mkuu
juu ya watu wake, kwa sababu wewe hukulishika neno lile Bwana
alilokuamuru. 1 Samweli 13:8-14.
{Mstari wa 13 na 14, unalenga kutujulisha ya kuwa, kuna jambo jaribu
hili lililenga. Nyuma yake anatujulisha kuhusu yeye Sauli kupimwa na
kukutwa na hatia/kosa la kukosa utii. Lakini; kitu Mungu alikusudia ni
kwamba, ufalme wake udumu milele. Na hauwezi kudumu, kama
hatashinda mtihani. Tazama mara baada ya kufeli; utakuta
anapokonywa ufalme!}
Tuendelee: Kama Samweli angetokea siku ya kwanza, lisingekuwa
jaribu kwa mfalme Sauli, lakini hata ya pili, tatu na ya sita mfalme bado
moyo wake ungeweza kuimili. Ila zaidi ya hapo uvumilivu ulimshnda!
Matokeo yake namabiw ana samweli kuhani kuwa hajaitii sauti au mari
ya Bwana! Na kwkao inawezekana kuw amajib yangekukuta mwaka wa kwanza, wa pli au awatat, bado isingekuw ajaribu kwkao, ilalimekaa
hadi sasa kwawa nee ayua wa sita, limeanza kufanyiajaribu kwkao.
Kitendo cha wengine kuole, au kufanikiwa a kukuacha kinakuumiza
kama ilivyokwa kwa Sauli mfalme ilehali yawat kundkana
kumuachahuku kukiw ana shindikiz la Waflisi! Nikwmabie tu kwmaba,
majira ya Mungu ni ya thamani kulko harakaharaka zako. Na ni nnai
amekwmabia kwua umeitiwa kfanaikwia katika mda unaofanna na
wenzako! Ibrahimualipata mdtoto Isaka katika muda ulikinza na watu
wengi!
Fahamu : Shindikizo, ni njia ya adui ya kukusukuma au
kukuharakisha. “Presha” kutoka nje, au msukumo fulani; Shetani
huutumia sana kukuharakisha. Vitu kama umri umeenda, tazama jinsi
wenzako wanavyofanikiwa na kukuacha. Na kadhalika.
Kuna sentesi moja muhimu sana kutoka kwa mfalme Sauli tunapaswa
kuidodosa kwa kina hapo juu. Na kabla ya kukupatia hiyo, nataka uione
hali ya watu kuanza kuondoka! Watu walipoanza kutawanyika, au
kurudi majumbani kwao katika ile siku ya saba; ndipo na moyo wa
mfalme ulipoanza kutetereka.
Maana yangu ni nini? Adui akiona umeweza kuliimili jaribu, atatumia
kelele za wana wa Israeli; ili kukushindikiza wewe Haruni uwachongee
ndama. Maana ameshajua, ameshindwa kukupigia kelele nafsini
mwako; sasa anatumia kelele za watu wengine.
Kitendo hicho, kiliuteteresha moyo wa mfalme. Lakini pia; hofu ya ujio
wa adui ambao ni Wafilisti; ilimteteresha mara dufu. Lazima ujifunze
namna ambavyo adui hufanya kazi. Tazama sentesi hii kutoka kwa
Sauli; mara baada ya kuulizwa na Samweli: basi nikasema, Wafilisti
watanishukia sasa mpaka Gilgali, kabla sijaomba fadhili za Bwana;
kwa hiyo nalijishurutisha, nikatoa sadaka ya kuteketezwa. 1 Samweli 13:12.
Tafadhali Usikose Sehemu Ijayo, inayobeba pointi ya 8 isemayo UWE NA UTULIVU MOYONI...
Kama Bado Hujaokoka na unaguswa kufanya hivyo, Fuatisha Pamoja Nami Sala Hii ya Toba.
Sema ; MUNGU BABA, NINAKUJA MBELE ZAKO, MIMI NI MWENYE DHAMBI, NAKUOMBA UNISAMEHE: AMENI.
Hakikisha unatafuta kanisa la Watu Waliokoka Ukaabudu Hapo.
Tumeunda Channel ya WhatApp, Tufolo; https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h
Kwa Maombi: +255759859287
http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL
UWE NA AMANI
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni