Jumatano, 14 Januari 2026

Karibu Katika Mfululizo wa 8 wa Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UKIWA NJIA PANDA, Pointi ya 5.

 Na Mwl. Oscar Samba

 5. Omba Mpenzi ya Mungu Yatimie.* Unajua maana yake ni nini?

Ni kwamba, umefikia mahali ambapo kwa akili na fahamu zako, 

hujui mpango wa Mungu, ama unajua lakini huna ujasiri na uwezo 

wakuukukabili! Sasa mwambie Mungu sio kama mimi nitakavyo bali 

mapenzi au mpango wako, ama njia yako ndiyo niiendee, sio njia 

nyingine. Yaombe haya kwa mzigo mkubwa sana, na kwa kumaanisha 

kwa viwango vikubwa mno.

22:41 Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba, 

42 akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; 

walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. 

43 Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.

Tunaona baada ya kuomba au kuyataka mapenzi ya Mungu, ndipo 

malaika wa Bwana anamtokea na kumtia nguvu! Wakati mwingine 

nguvu zinakuja pale unapokuwa tayari, kutoka ndani ya moyo wako 

kuya kubali mapenzi yake! Maana anajua akikupa nguvu za maombi 

kiholela; unaweza jikuta unazitumia kinyume: kwa kuombea mipango 

ambayo siyo yake.

Kuna kisa cha mtu mmoja aliyekuwa na njaa sana, naye alikaribia kufa. 

Akaja mtu akamletea biskuti, alipoiona alicheka kwa furaha; na ghafula 

akadondoka na kufa! Kwa nini? Alikuwa na nguvu ndogo, alisalia na 

nguvu kidogo sana. Ambazo alitakiwa kuzitumia kwenye kula chakula, 

ila akazitumia kwenye kucheka!

Unapaswa kuwa makini sana unaposalia na nguvu ndogo za maombi! 

Usizitumie kumlaumu, au kumlalamikia Mungu, ama kuombea 

mipango mingine. Bali zielekeze moja kwa moja kwenye kumtukuza   Mungu. Kuonyesha uku wake, kumuonyesha kuwa bila Yeye wewe 

huwezi lolote. Kumuonyesha kwa hata hapo ulipofika sio kwa uweza au 

nguvu zako; bali kuna mkono wake Mungu nyuma yake. Na hata unako 

kwenda Yeye bado anakujua. Onyesha kuwa Yeye anakuwazia mema, 

maana anayajua mawazo anayokuwazi; kwani ni ya mema siku zote.


Baada ya hapo sasa penyeza wazo la kumtaka akupiganie. Akupe 

kutembea kwenye mapenzi yake, mueleze ukweli kuwa mwili na fikra 

na nafsi yako ni dhaifu. Ila akutie nguvu na uyakubali na kuyatimiza 

mapenzi yake. Kama huyajua anza na wewe kuyajua, kisha uyakubali 

na hatimaye kuyatimiza.

Kumbuka sana hili; kuwa Mungu ni Mungu na atabaki 

kuwa Mungu hata kama hujamuelewa. Hata kama unaona 

amekupitisha mahali pa gumu sana; haimbadilishi kuwa Mungu: 

kwa kuwa wewe umekwama au unataka kukwama! 

Ukibisha kawaulize wakina Meshaki, Shedraka na Abernego 

watakusimulia. Haikumbadilisha kuwa Mungu kwa waokuwa kwenye tanuru la moto! 

Wakati hao wanaokolewa wengine walikufa kwa kuawa. Stefano, na 

Agripa Shaihidi wake na msashujaa wa Agano la Kale waliifia imnai. 

Na hiyo haikumbadilisha hata kidogo; kuwa Mungu: kwa sababu tu hakuwaokoa! 

Mungu ni Mungu hata kama humuelewi, atabaki kuwa Mungu! Hawi 

Mungu kwa sababu amekujibu, wala haibadilishi Uungu wake kwa 

kuwa unamuona amekaa kimya! Ukifa kwa kuungua moto, bado ni 

Mungu, na ukiokolewa kwenye huo moto kama hao mashujaa hapo pia 

ni Mungu.

Kutokujibiwa kwako, au kuchelewa kujibiwa; ama kupokea majibu 

ambayo hujayatarajia, hakumbadilishi Mungu. Yesu hakuokolewa 

msalabani; wala hakujiokoa, na hiyo haikumbadilisha MUNGU AMA 

KUATHIRI Ungu wao. Uungu na uweza wake ulisalia pale plale, 

maana hivyo ndivyo ilivyoupendeza Uungu. 

Epuka kuona kwamba Mungu anakuonea. Au kuzikubalia akili 

na fahamu zako, kukosa sababu za kuelewa ni kwa nini 

anakupitisha hapo. Madhara yake ni kuzaliwa na kukua kwa hali 

ya kutokumuelewa Mungu!

Usipomuelewa Mungu! Hutaona thamani ya kuendelea kuvumilia 

kuwepo hapo! Thamani ya kupitia hapo ikitoweka au 

kupungua, uwe na uhakika sababu za wewe kuvumilia 

zitakosekana. Hali itakayokufanya kuona kuendea 

kuvumilia hakuna faida yoyote. Ni sawa na kujiumiza na 

kupoteza muda bure. Linda sana sababu yoyote inayonuia 

kukufanya kutokumuelewa Mungu isikukaribie. 

Waliokwama jangwani ni matokeo ya kutokumuelewa Mungu!

Walifikia hatua ya kuona ni kama vile aliwatoa Misri ili aje awaulie 

jangwani!

Sasa nawiwa kukujuza jambo hili, katika ile mistari ambayo 

tuliitazama pale, kuna mstari huu muhimu sana, “kuwa Yesu alijitenga 

na wanafunzi wake..kisha akasogea mbele kidogo akaomba..”

Luka 22.41 Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, 

akapiga magoti akaomba, 

42 akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; 

walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke.

Ukitazama kwa makini na kwa jicho nililo nalo. Ndipo utakapokuja 

kugundua kuwa; aina ya ajenda aliyokuwa nayo Yesu ingeweza kupata 

upinzani mkubwa: kutoka kwa wana timu wenzake! 

Na kabla sijafika huko, ngoja ni kwambie kuwa; hitajio kubwa kwa 

Yesu kutoka kwa wanafunzi wake ni wamuombee. Hali aliyokuwa 

nayo kwenye nafsi yake, hakunuia sana mapenzi ya Mungu kutoka 

kwao, bali ile hali ya kusumbuka ndani. hali iliyompelekea kuwa na 

huzuni iliyopitiliza.

Sasa ngoja nikujuze, aina ya ajenda ya Yesu ilimfanya kujitenga kidogo 

na wanafunzi wake. Yesu moyoni mwake alikuwa na nia kabisa ya 

kupita msalabani! Ila mwili ulikuwa ukimpigia kelele au kumzuia. Na 

alifahamu fika kuwa akiwaeleza wanafunzi wake moja kwa moja, kuwa 

anataka kupita hapo, upinzani lazima ungekwepo. Maana hawakuwa 

wameuelewa mslaba, kwa namna ambavyo Yesu alikwa amefahamu.

Ukija kule awali kwenye kitabu cha Mtahato ile 16, utafahamu kuwa

Petro alikuwa amemgomea kwa kupinga kufa kwake. Ukija hata baada 

ya hayo maombi; kipindi hicho cha kukamatwa kwa Yesu, Petro alitwa upanga na kumkata mtumwa wa kuhani mkuu sikio (akipinga kufa kwa 

Yesu)! 

Yesu alifahamu kuwa, wakimsikia moja kwa moja, ya kuwa anaomba 

apite hapo; kuna hatari ya kukabiliana na upinzani mwingine. Najua 

walijua kuna kitu mbele, ndio maana na wao walipaswa kumuombea. 

Ila sio kwa namna ambavyo Yesu pia angeomba, maana hata baada na 

hata wakati wa kufa kwake, namna walivyokabiliana na matokeo yale 

pale awali inasadifu jambo hili sana.

Nataka kukujuza au kukufunza nini hapa? Kuna aina ya maombi ya 

mapenzi ya Mungu, unaweza omba mbele ya watu na wao wasikuelewe 

kabisa. Hata kama una timu ya maombi, uwe na hakika kuwa kuna 

majira ya kujitenga na kuzama kwenye kunena kwa lugha ili kuepuka 

aina ya upinzani. Wanaweza wasikwambie, ila na wao kujikuta 

wanaomba kinyume na wewe. Hali itakayokuletea vita vipya kwenye 

ulimwengu wa roho. Maana kuna muda inakuwa ni mwenye nguvu 

mpishe. Nikimanisha maombi megine yasiyo sahihi yanaweza 

kufanyika zuio. 

Ndio maana Mungu alimuonya Balaamu na kumkamata kinywa maana 

kungekuwa na athari kama angeachiwa kufanya hivyo. Unajua kama 

kungekuwa na uwezekano wa kutokuwa na madhara; basi kusingekuwa 

na umuhimu kwa Mungu kutumia nguvu kubwa kwa kiasi hicho 

kumdhibiti! 

Na wewe ukabili ushirikina wa kimaombi wenye kutumia jina la 

Yesu; kwa kutumia hekima! Maana maombi hata yakiombwa kinyume 

huwa yanaweza kukudhuru. Maana hapa inawezekana nia yao ni njema, 

ila katika hili la mapenzi ya Mungu; ambayo yapo mbele yako; wao 

hawaja yafahamu wala kuyaelewa. Kama ilivyokuwa kwa wanafunzi 

wa Yesu. Japo ujuzo huu haupaswi kukupa moyo wa kugomea 

mashauri yao; au kujisemea kuwa hawatakuelewa. Au hatanielewa 

maana hata Mwalimu Oscar alishawazungumzia watu kama hawa! 

Hapa usinisingizie, huko ni kukosa maarifa, Roho wa Bwana 

anapaswa kukuongoza. Na fahamu kuwa kuna muda hutumia watu 

kukujulisha aina ya mapenzi yake. Ni kazi kwako kuwa na uwezo wa 

kujua hapa ni wapi. Na huyu ni adui ama ni Roho Mtakatifu ndani 

yake! 

Na Wiwa Kukuongea na Pointi ya 6:

 6. Washirikishe ama Omba Msaada kwa Wapendwa; Ni muhimu kujifunza kuunganisha nguvu, Esta alipokuwa katika hali ya 

njia panda; maana Modekai alimuleza wazi mara baada ya kujaribu 

kulikwepa shauri la Bwana: ilimbidi aombe msaada wa maombi ya 

kufunga na kuomba kwa muda wa siku tatu.

Yesu mwenyewe aliyekuwa ni Mungu, aliomba msaada; Akawajia wale 

wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza 

kukesha pamoja nami hata saa moja? Mathayo 26:40

Ni kweli maombi haya yalikuwa na umuhimu kwa wanafunzi pia, ili 

wasije kuingia majaribuni, ila kiukweli na kihalisia Yesu alihitaji 

waombaji pamoja naye! Na wewe usiendelee kukomaa wewe 

mwenyewe. Vita nyingine inahitaji msaada. Hata kama ukiona huwezi 

kujielezea mbell yao moja kwa moja, wewe waambie tu niombeni. 

Maana kuna mahali napitia, kwa kweli pananiweka njia panda ya 

kiroho, ninasueni kwa kuniombea nipata nguvu za kiroho. Na naniweze 

kuyafuata mapenzi ya Mungu maana kwa kweli inatishia kiroho 

changu.

Usipitwe na Mfululizo wa 9, wenye pointi ya 7. Kama Hujui Chakufanya Usifanye Chochote.....

Km Bado Hujaokoka, Nikutie Moyo Kufanya Hivyo Sasa...

Sema; BWANA YESU, MIMI NI MWENYE DHAMBI, NAKUOMBA UNISAMEHE SASA: Amen.

Tafuta Kanisa la Watu Waliokoka Ukasali Hapo 

Usiache Kufolo Channel Hii ya Wasapu 

Tumeunda Channel ya WhatApp, Tufolo; https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h 

Ni Maalumu kwa Ajili ya Mafundisho ya Neno la Mungu.

Kwa Maombi: +255759859287 

http://www.ukombozigospel.blogspot.com


Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Kwa Maombi +255759859287 

Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL


UWE NA AMANI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni