Jumamosi, 6 Juni 2026

#MILANGO au #MAMBO 5 AMBAYO ADUI SHETANI HUYATUMIA KUVURUGA NDOA au AMANI KATIKA NYUMBA

1. #Hasira ...ni Mlango Hatari sana Pamoja na Uchungu...Vikikaa muda mrefu...Shetani Hupata Nafasi..(hugeuka na kuwandhambi)...Waefeso 4:26 Mwe na hasira, #lila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; 27 *wala msimpe Ibilisi nafasi . 2. #Kuzira au Kununa ...Wanawake wengi (wanaume pia wapo ila wachache) huwa na tabia ya kununa muda mrefu na hata wiki na wengine mwezi...Biblia huita ni upumbavu na kila penye upumbavu Shetani hupata mlango..Mithali 19:3 Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake; Na moyo wake hununa juu ya BWANA. Ambapo hukupotosha njia zako...kwa wanawake wengi hufanya njia hii kama fimbo ya kumchapia mwanaume...lakini Mithali pia huita ni fimbo ya Kiburi...kila anayezira ana kiburi...(Huu ni Utafiti Nilioufanya wa Kisomi na Kitaaluma Kabisa...na katika Roho Mtakatifu...ukiendelea hivyo baada ya muda utajikuta mwenzako anapunguza upendo nawe...maana hali hii humuathiri katika nafsi yake...) Mithali 14:3 Katika kinywa cha mpumbavu mna fimbo ya kiburi, Bali midomo ya wenye hekima huwahifadhi. (Unamsemesha aongei...na wengine wanaweka mgomo hadi kwenye haki za msingi...UJINGA Kabisa huo). 3. #Kunyima au Kunyimana Haki ya Tendo la Ndoa ...tendo hili limewekwa na Mungu kama kiunganishi...maana kama anayeungana na kahaba anakuwa mwili mmoja naye...uwe na hakika anayeungana na mke au mume wake huwa kitu kimoja pia...sasa adui akifanikiwa kuwavuruga hapo ujue kashafanikiwa kuwatenganisha tayari...Paulo alishaonya hili...1 Wakorintho 7:5 Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu. Adui Shetani Anapata Nafasi ya Kuwajaribu... 4. #Migogoro au Malumbano... Magomvi huondoa uwepo wa Mungu ...maana Roho wake ni wa Amani...Amani ni Tunda la Roho lakini Amani ni Yesu mwenyewe maana ni mfalme wa Amani yaani Salemu...Salemu ni Yerusalemu...ambapo hubeba pia Yerusalemu Mapya kama Mji na Nchi Mpya...Ufalme wa Mbinguni ni Sasa na Utimilifu wake ni Baada ya Unyakuo...kwa hiyo Utawala wa Kristo wa Amani Upo Sasa Kati Yetu...Ndoa ni Sehemu ya Kristo Yesu Kutawala...(Ni Kibiblia Kabisa). Fujo ni tunda la Shetani yaani tabia zake. 5. #Kukosa au Kukosekana kwa Ibda ya Pamoja ...umoja wa Roho ni Ulinzi...kumbuka ndoa ni wito...katika kila wito kuna kifungo cha amani...na Roho Mtakatifu ndiye msimamizi mkuu wa kifungo hiki...ndio maana kanisa au dhehebu likipoteza kifungo hiki...kuna namna umoja utatoweka tu...Soma maneno haya kwa sura ya ndoa kama wito...fahamu kabla ya dhambi kuingia ulimwengu ndoa ndilo kanisa la kwanza...mifumo mingine ya kikanisa ni matokeo ya dhambi kutuviruga....lazima ndoa ibebebkitu cha kikanisa kwanza ndipo iweze kufanikiwa...Soma; Waefeso 4:1 Kwa hiyo nawasihi, mimi niliye mfungwa katika Bwana, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa; 2 kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; 3 na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani. 4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu. #Tutaendelea Wakati Mwingine Tukipata Neema .. _Imeandikwa na Mwl Oscar Samba Mwanza Tz Kama Bado Hujaokoka na unaguswa kufanya hivyo, Fuatisha Pamoja Nami Sala Hii ya Toba. #Sema ; MUNGU BABA, NINAKUJA MBELE ZAKO, MIMI NI MWENYE DHAMBI, NAKUOMBA UNISAMEHE: AMENI. Hakikisha unatafuta kanisa la Watu Waliokoka Ukaabudu Hapo. Tumeunda Channel ya WhatApp, Tufolo; https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h Kwa Maombi: +255759859287 http://www.ukombozigospel.blogspot.com Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv Kwa Maombi +255759859287 Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL UWE NA AMANI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni