Jumamosi, 27 Aprili 2019

Upole wako na ujulikane na kila mtu !

Bwana Yesu asifiwe,
Kuna Mtu aliniambia niseme Neno, nami nilisema ! Sasa nakumegea nilichomfunza !

    Upole ni Tunda la Roho, ambalo linadhima ya unyenyekevu ndani yake.

  Kazi na faida moja wapo ya upole ni kukupa majibu ya busara hata katika nyakati ngumu, haijalishi ni zenye kuuthi au kujeruhi, utajifunza kwa Yesu, na Yeremia pia, ila ona hapa;Mithali 15:1 Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.

Upole unakuwezesha kuepukana na mitego ya adui, inauonuia kukuyumbisha, ama kukukwamisha, au kukuvurugia masiha, maana upole umebeba unyenyekevu ndani yake ! Yeremia 11:19 Lakini mimi nalikuwa kama mwana-kondoo mpole, achukuliwaye kwenda kuchinjwa; wala sikujua ya kuwa wamefanya mashauri kinyume changu, wakisema, Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake, na tumkatilie mbali atoke katika nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.
Upole huu ndio uliomvusha Yesu ! Isaya 53:7 Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake.

Kuna wakati adui ananuia kabisa kukukwamisha mahali kwa kuibua changamoto, ama vikwazo, ila ukiwa nao huo upole, utanyamaza kimywa na adui anakosa mwanya wa kukudhuru au kukuangamiza !
Sasa sababu ya maandiko kututaka upole wetu ujulikane na kila mtu ni ili kuwa na maisha ambayo Tunda hili litakuwa active au hai, ili kutuwezesha kunufaika nalo, usisahau kuwa anamalizia nakusema Bwan yu karibu, ikiwa na maana kuwa unapokaribia mafanikio kama Yesu, au kukutana na majibu yako, adui haachi kuleta vikwazo, iwe kwa ndugu, marafiki, muajiri wako, wafanyakazi wenzako,walezi na kadhalika akinui kukuzuilia kukutana na Bwana, sasa upole utakuvusha kama Yesu na Yeremia ! Ona haya maandiko :
Anaanza na kututaka tufurai, akiwa na maana upole umebeba ama hukuwezesha kufurahi, maana mazingira ya huzuni, na uchungu hayawezi kuzaliwa penye upole ! Alafu amani huyoke, kumbuja amani pia ni Tunda la Roho !, pamoja na Furaha ! Sasa ukipata upole, hayo mengine ni rahisi sana kuchipuza !
Wafilipi 4:4 Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
:5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.

Katika somo hilo, tuna au una jigunza nini hapo ?

Natumai somo kuu, ni kwamba ukiwa mahali pagumu, huna majibu ya maswali yako, mazingira yanakuzalia ama hukutishia kukuzalia huzuni, au kukunyima amani, na furaha, masononeko na ukiwa zinakunyemelea! Basi upole ni dawa ! Ambapo utazaa Amani, na Furaha ! By Mwalimu Oscar Samba. Simu: +255759859287

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni