Jumamosi, 27 Aprili 2019

KUNA MTU MMOJA MWENYE KESI AMENIOMBA NIMFUNZE NAMNA YA KUOMBA, NAMI NAKUMEGEA:

1. Omba Rehema, tubu bila kujihesabia haki, tumia Danieli 9, pia Warumi 3:25 ukiitaka Damu ya Yesu ifanye rehema, na Mathayo 26:28 kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.

2. Ifute hiyo Kesi kwa Damu ya Yesu, Waebr 9:22, futa hizo nakala/kopy za kesi ama mashitaka.

3. Gongomelea hzo hati za Mashitaka Msalabani, Wakolosai 2:14 akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;


4. Hukumu kila kinywa kuwa mkosa, ukianzia cha mshitaki wako hadi mashahidi, ukifanya hivi maana yake unaviondolea haki na kuvitisha hatia au makosa; Isaya 54:17

5 Itakae Damu ya Yesu Inene mema, juu yako,  Waebrania 12:24.

6. Pia Usikubali kuwa na Woga, (fahamu hofu ni lango la adui kukushinda, ikija ikemee,) huku ukimtaka Yesu ama Roho wake akutangukie na tegemea hekima yake wakati wa kunena; Mathayo 10:19 Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.
:20 Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.

NB: Ukiguswa kuambatanisha maombi haya na sadaka ni vyema zaidi, hujaguswa endelea kuamini Mungu yu nawe !
Kwa Ushauri na Maombi: 0759859287, baruapepe: ukombozigospel@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni