Jumatano, 21 Julai 2021

KAWIA UFIKE

 Na Mwalimu Oscar Samba

Ni kweli ngoja ngoja huumiza matumbo, au fahamu pia simba mwendapole ndie mla nyama! Maana mtaka yote kwapupa hukosa yote! Hawakuwahi kukosea waliosema kuwa subra yavuta heri!

 Ni hakika haraka haraka haina baraka! Maana hata waingereza ama wenye kingereza chao husema kuwa, njia ya kato siku zote ni njia isiyo sahihi.

 Kuna watu wengi wamjejikuta wakiingia hasara maishani mara baada ya kutaka mafanikio kwa haraka! Wamejikuta wakipoteza ama wakiharibikiwa kimaisha, ni kweli ni tajiri ila kapoteza mke na woto kwa sababu ya mashariti ya mganga! Ni kweli ana fedha sawa na elimu sawa ila ni muadhirika wa UKIMWI! Kapenda chipsi hatimae ni mjamzito na ndoto za kusoma zimakomea hapo!

 Ni heri ukawie lakini ufike uendako, kuliko kukimbia ukajikuta unakimbia hadi unasahau nyumbani ama unashindwa kuangalia taadhari ya alama za barabarani na hatimae ukaingia katika kusababisha ama kujisababishia ajali!

Narudia tena na tena kuwa kawia ufike, pole pole ndio mwendo! Unaonaje mkulima akapanda mbegu leo na kutaka kuvuna siku hiyo hiyo! Kama kwa mkulima haiwezekani uwe na uwakika kuwa na katika safari ya mafanikio ndivyo ilivyo.   

Embu tujionee jinsi maandiko mtakatifu ya Biblia yanavyotufunza katika kitabu kile cha Yakobo: 5:5 Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.

8 Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia.9 Ndugu, msinung'unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.

 

Mafanikio ya mtu yapo mwishoni, kama ilivyo kwa mkulima! Sasa mbona wewe unataka mafanikio mwanzoni! Huvuni hujapanda, na ukipanda lazama ulimie, ama upalilie!

Unaonaje mtoto ama mwanafunzi wa darasa la kwanza akatamani kwenda hosipitalini na kuanza kufanyia watu upasuaji akiulizwa ajisemee kuwa mimi ni daktari!

Kuwa na ndoto ama kipawa cha udakitari haikufanyi kuwa dakitari! Kama inavyompasa kuingia darasani na amalize shule ya msingi, kisha sekondari, na hatimae chuo tena akae huko muda wa kutosha, basi na ndivyo ilivyo kwa mtu mwenye ndoto ya mafanikio!

Maisha hayaitaji njia ya mkato! Yanahitaji kanuni! Unaonaje mpishi akitaka kupika ugali achukue maji ya baridi na kuchanganya na unga na kuanza kusonga akiwa na nia ya kupata ugali! Hakika atapata kituko, maana kitakachotoka hapo hakitakuwa hata na sifa ya kuitwa uji!

 

Ukitaka ugali, ama wali, kuna kanuni zake! Alikadhalika mafanikio ya kiroho, ama kimaisha ndivyo yalivyo! Haraka ya mafanikio kwenye huduma, utajiri wa haraka na kadhalika! Kitabu cha Mithali chenyewe kina onyo katika hili!

Mithali 20: 21 Urithi uliopatikana mwanzo kwa haraka, Mwisho wake, lakini, hautabarikiwa.

 

Pupa ni hatari, fanya kazi kwa malengo, panga mpango, nenda hatua kwa hatua, acha kurukia ngazi,usitake kuiona kesho kutwa ungali leo! Maandiko katika Mithali yanatupa mambo muhimu hapa, ama kuna taadhari kama sio onyo toka hapa! Jionee; Mithali 21:5 Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu; Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.

Mali iliyopatikana kwa haraka au utajiri hauwezi kudumu, maana muhuska hakupitia shule ya Mungu ambayo ni mapito, kibiblia hii ipo ili ikujengee nidhamu ya fedha ili kukuwezesha kuwa na uwezo wa kutambua nafasi ya Mungu katika mafanikio yako, 1 Thimotheo 6, inakupa mambo muhimu ya kuzingatia kwa anayetaka kuwa tajiri!

 Hayo hujifunza katika shule ya Mungu! Haipatikani ukiwa na fedha, hupatikana ukiwa huna! Ile sura ya tano inaeleza jinsi ambavyo fedha huweza kuwa ni shina la mabaya yote!

Fedha ikikosa nidhamu ni hatari na adui! Maana mafanikio ya mpumbavu ni kwa uharibifwa nafs yake! Acha Pupa, Kawia Ufike!

Nikuhitimishie na andiko hii la Ayubu inalonena kuhusu mwanzo mdogo ambao ungeongeeka tu kama muhusika angalikaa kwenye kanuni! …..

Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, Lakini mwisho wako ungeongezeka sana. Ayubu 8:7 SRUV.

Kama hujaokoka na umesoma ujumbe huu na unataka kuokoka, (maana ni fika huwezi kunufaika na msaada wa Kiungu maishani mwako kama hujaamua kumruhusu Yesu aingie kwenye maisha yako.) kwa hiyo fuatisha Sala hii ya Toba kwa Imani.

Sema; MUNGU BABA, NINAKUJA KWAKO, NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, TAFATHALI FUTA JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, LIANDIKE SASA KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MIELE: Ameni.

 

Hongera kwa kuokoka, tafathali tafuta kanisa la watu waliokoka, usisite kuwasiliana nasi kwa maombi, ushauri, na hata kwa msaada wa kitabu cha Kuukulia wokovu.

 

Simu, WhatsApp au Telegram: +255759859287, Baruapeoep: ukombozigospel@gmail.com, Web: www.ukombozigospel.blogspot.com, Facebook page: @mafundishoyanenolamungunamwalimuoscarsamba, (Mafundisho ya Neno la Mungu na Mwalimu Oscar Samba)

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni