Jumanne, 23 Mei 2017

YATOSHA.

 
   Na Mwalimu Oscar Samba #UgMinistry 
Ni fika na bayana ya kwamba mapito yapo, mateso, dhiki na taabu, kulala njaa na kutengwa ama kukataliwa na ndugu ama wapendwa.
Ila yapo majira ya mambo hayo kukoma, na ndiposa Yesu pale msalabani akasema IMEKWISHA, na Mungu akawaambia wana wa Iziraeli wakati wanazunguka ile milima ya Seiri yakwamba YATOSHA.  “Mlivyouzunguka mlima huu yatosha; geukeni upande wa kasikazini.”  Ni Torati 1:2.
Na wewe imetosha sasa kuteseka kulala njaa, Nasema imetosha kulialia kwani majira ya furaha yako yamekwisha kutimia. Kwa waliyokosa watoto kwa muda mrefu ninaachilia Neno la kinabii kwao ya kwamba majira kama haya mwakani watapakata wana na kama ilivyokuwa mwisho wa machozi ya Hana kwa kumpata Samweli na kwao itoshe hivyo.


Hana aliteseka ila mateso yake yalikoma kwa Bwana kumpatia kitulizo cha moyo wake. Umechumbiwa na kuachwa kila uchwao ila wakati huu pokea neno hili litokalo katika kinywa na kudhibitishwa na mikono ya Mtumishi wa Mungu aliye hai ya kwamba majira ya kuowa ama kuolewa kwako yamekaribia na punde BWANA atakutokea wewe anza kuanda rangi ya nguo ya “Send-off” na arusi bila kusahau pozi la siku ya pete.

Wewe ni mwana wa Mfalume tena atawalaye kwa haki na kwa mamlaka, kwa hiyo huna tena haja ya kuishi kama jogoo wa mjini aliyenyeshewa na mvua kwa kujikunyata ama kujiona huu mnyonge kifikra bali anza kuruka ruka kama ndama wa mazizini kwani IMETOSHA KWA KUSOTA KWAKO BILA KAZI.

Mungu wetu anasema ya kwamba imetosha. Mwanaume Yesu walimkamata kwa dharau na kuvunjiwa heshima kama mwivi ama mnyanganyi katika majira ya kuteseka kwake, wakamtesa kwa kumpiga mijeleji, mate akatemewa, mavazi ya aibu na kejeli akavikwa, Alidhiakiwa Yesu, alipigwa bila hatia.
Alibaguliwa, walimuona Banaba mwizi na jambazi kuwa na haki kuliko huyu Mwebrania aliyekuwa mpole uso na mnyenyekevu wa moyo, mweye fikra za utulivu  kama mwanakondoo apelekwaye machinjoni ama atuliavyo wakati wa kukatwa manyoya.

Maneno ya kebei ndiyo yaliyokuwa chakula chake, hata mwizi aliyesulubiwa naye alimnenea mabaya.

Ila atukuzwe Mungu BABA Duniani na juu mbinguni ajuaye kuyapitisha majira ya uaribifu na mateso kwa kasi ya ajabu. Kwani kufumba na kufumbua KIDUME Huyu anayeukosha moyo wangu alishida na hatimaye kuketi mahali pa juu palipo inuka sana horofa za wanadamu.
Kubwa yake ni KITIMU TIMU siku ile ya tatu pale mjini Galilaya alipowatangulia, Sio hapo tuu bali katika Iziraeli yote na Ulimwengu, zilivuma habari na sio zile za mateso na aibu bali ni zile za USHINDI.

Aliteseka kweli ila majira yalipofika, alisema;  “IMEKWISHA,” Na kuanzia hapo kila mwenye mwili alitambua kuwa mtu huyu alikuwa ni mwenye haki, na mimi na wewe tuseme wote kwa IMNAI iliyo KUU ya kwamba;  “IMEKWISHA.” Maana yake YATOSHA sasa, Neno hilo linakaribisha ukurasa mpya wa Mafanikio na Ushindi uliyopo kwenye kitabu cha FANIKIWA KIMUNGU huku mwandishi wake akiwa ni YESU mwenyewe na amekuandikia yaliyo mema sasa kazi ni kwako kuamini pamoja nami ya kwamba. Kuzunguka mlima ama milima ya Seiri kumefika mwisho ama kulizunguka jangwa kwa Muda wa miaka arobaini kumekoma kwani mwaka huu ndio wa kuivuka Yoridani na kuingia Kanani.

Ninakutakia kila la heri katika maisha hayo mapya ya Kanani mpendwa mwenzangu katika Bwna Yesu ila taadhari yangu ni kukutaka usisahau yale uliyofundishwa na kuonywa na Bwana katika jangwa kwenye kitabu kile cha Torati wala usilialifu Agano lake ili yasije kukupata mabaya na wala usiseme ya kwamba ni akili zako ndizo zimekupatia utajiri huo.
Kumbukumbu la Torati 8:17 Hapo usiseme moyoni mwako, ‘Nguvu zangu na uwezo wa mikono yangu ndivyo vilivyonipatia utajiri huo.’ 18 Bali utamkumbuka Bwana Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri, ili alifanye imara agano lake alilowapa baba  zako,  kama hivi leo.
Ona lakini hii, Tujongee hadi mstari ule wa kumi na  tisa. 19 Lakini itakuwa, kama ukimsahau Bwana, Mungu wako, na kuiandama miungu mingine, na kuitumikia na kuiabudu, nawashuhudia leo yakuwa mtaangamia bila shaka.

Kila la heri na Mola wangu akuepushie kila la Shari na Fanikiwa kama Mtende uliopandwa kando ya Mto. Miye ni Mwalimu wa Neno la Mungu Mwl. Oscar Samba wa Huduma ya Ug.

Kama hujaokoka na unataka kuokoa ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KAUMINI KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundila Fb, ili kuupta habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni