Jumanne, 23 Mei 2017

BELIVE ON YOUR DREAMS, AMINI KATIKA NDOTO ZAKO.

Na Mwalimu Oscar Samba #Ug Ministry
Ni nani unataka kuwa, Dakitari, Mwanasiasa, Mwimbaji wa Nyimbo za Injili, Muhubiri fulani mwenye Upako wa hali ya Juu? Whom one you what to be, a Doctor, A Singer, Politician or a Preacher. God Never lie. Mungu kamwe hasemi uongo.
AMINI KATIKA NDOTO ZAKO, Usiruhusu Mtu mwingine yeyote akwambiye kuwa hauwezi, wala mazingira yasikuaminishe hiyvo. Wewe amini tu ya kwamba inawezekana kuwa unayehitaji kuwa kesho bila kutazama wewe wa leo. Belive on You are Dreams.

Tumtizame Yusufu kijana wa Mzee Yakobo, aliamini kuwa ipo siku anachokiona kitageuka uhalisia. Mwanzo 37:7 Tazama sisi tulikuwa tukifunga miganda shambani, kumbe! Mganda wangu ukaondoka ukasimama, na tazama, miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu.
Hiyo ndiyo iliyokuwa ndoto yake, ambayo ilibeba ukuu katika maisha yake, na wewe tazama ndoto yako kisha, amini katika hiyo wala sio katika kitu kinginecho.

VIKWAZO KWA YUSUFU. 1. Ndugu kumchukia, 2. Kutupwa Gerezani.
Mwanzo 37:5 Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia. Mstari wa 8 unaonyesha kauli za kumchukia huyu kijana. 8 Ndugu zake wakamwambia, “Je, kweli wewe utatumili sisi? Nawe utatutawala,” Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake na maneno yake.
Bila kosa Yusufu alitupwa Gerezani mara baada ya kukataa kutenda dhambi ya kulala na mke wa bwana ama mwajiri wake Potifa. Mwanzo 39:20-23. Cha ajabu hapo ukisoma hayo maandiko utakuta kuwa Yusufu alipata kibali hata huko gerezani na mkuu wa gereza hakutazama maneno ama mashitaka dhidi yake.
#Usitazame vikwazo, tazama Furusa, na geuza matatizo ama changamoto kuwa furusa kama Yusufu. Kijana huyu alikuwa gerezani na mazingira ya gereza yangeweza kuwa kikwazo tosha katika safari ya ndoto zake ila aliyageuza matatizo na vikwazo hivyo kuwa furusa kwani humo gerezani ndiko alikotafsiri ndoto hali iliyomfanya kutambulika kwa Farao na kisha Farao kumtoa na kumfanya kuwa mkuu sana hali iliyompa Mwanya wa kutimia kwa maono yake.
Fungua nami kwa mwendo wa pole kama twiga nyikani kitabu kile cha Mwanzo ili ujione ujasiri huu wakuyafanya mazingira yasiyowezekana kuwa mtaji ama daraja la kufika ng’ambo.
Mwanzo 40:1-22, 12 Yusufu akamwambia tafsiri yake ndiyo hii, “Matawi matatu ni siku tatu. 13 Baada ya siku tatu Farao atakiinua kichwa chako, atakurudisha katika kazi yako; nawe utampa Farao kikombe mkononi mwake, kama desturi ya kwanza, ulipokuwa mwenyeshaji wake
Baada ya hapo huyu Mweshaji kwa mikono yake mwenyewe anatengeneza daraja ili Kijana Mbeba maono apite. Mwanzo 41 Sura yote. Ila miye nitakupitisha katika maandiko kadhaa.
Mwanzo 41:12 Na huko pamoja nasi palikuwa na kijana Mwebrania, mtumishi wa mkuu wa askari, tukamhadithia, naye akatutafsiria ndoto zetu; akamtafsiri kila mtu kama ilivyokuwa ndoto yake.
Baada ya daraja kujengwa Farao hakuweza kunyamaza bali alihitaji daraja kuzinduliwa na uzinduzi huo ni kwa Yusufu kutoka Gerezani, Tazama nami.
Mwanzo 41:14 Ndipo Farao akapeleka watu, wakamwita Yusufu, wakamtoa haraka kutoka gerezani. Akanyoa, akabadili nguo zake, na kuingia kwa Farao.
Kijana aliingia kazini, na Mungu akiwa pamoja naye. Kama alivyofanya Mwebrania huyu kwa kumshika Mungu na kuendelea kuamini katika ndoto zake nawe fanya hivyo kwani ukiyumba kwa kupoteza mwelekeo utakwama mahali. Tuendelee ili kutazama kilichotokea. Utaona aliyekuwa Mfungwa namna anavyopewa heshika kubwa kama mwana wa kifalume.
Mwanzo 41:41 Farao akamwambia Yusufu, “Tazama, nimekuweka juu ya nchi yote ya Misiri.” 42 Farao akavua pete yake ya mhuri mkononi mwake, akaitiya mikononi mwa  Yusufu; akamvika mavazi ya kitani kizuri, na kumtia mkufu wa dhahabu shingoni mwake. (Unafikiri Mungu huyu wa Yusufu amekufa? Jibu ni laa, yaani Yungali hai na atatenda hivyo kwako ila wewe amini tu katika ndoto zako ya kwamba ipo siku utakuwa unayetaka kuwa hata kama huko kwako ama katika taifa hili hajawai kutokea mtu kama wewe. Wewe amini tu, ipo siku You will become Some One as You Wish.)

Mpendwa! Na wewe Geuza gereza ulilonalo kuwa mtaji  ama njia ya kutokea kama Yusufu. Ni jambo gani linalofanyika kikwazo kwako? Je, Unaona Bahari ya Shamu mbele yako? Kulia na kusho milima? Nyuma Jeshi kubwa la Farao?

Lisikiye Neno la Bwana, Kutoka 14:13 Musa akawaambia watu, “Msiogope! Simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakao wafanyia leo; kwa maana hao Wamisiri mliowaona leo hamtawaona tena milele.14 Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimiya”

Ni jambo gani la kumshinda Yesu?  Halipo. Tukutane kesho kwenye somo la SHINDA VIKWAZO TUKUTANE NG’AMBO YA YORIDANI. Ulikuwa na Mwalimu mwana wa Flora Samba, katika familia ya Mzee wa Hekima Mzee Prospa. Kwa Busu takatifu lenye upako wa kutimiza maono ninakuaga.

Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI. Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.
Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundila Fb, ili kuupta habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                      PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni