Jumatatu, 15 Mei 2017

MUNGU ANAPOKUWA KIMYA FANYA YA FWATAYO. Sehe. 2.

Inaumiza kuwa katika pito gumu na unamtumaini Mungu kisha kumuona Yupo kimya, Ingawaje wakati mwingine huongea ila hatuelewi ila kiukweli upo wakati anakuwa kimya kama wakati ule wa Yesu pale msalabani.

Wengine hujifariji kuwa alinyamza kwa sababu Yesu alikuwa amebeba dhambi na Mungu hachangamani na wenye dhambi. Hoja hii kwangu ni dhaifu kwani kama aliweza kuzungumza na Petro katikati ya dhambi yake ya kumkana Yesu kwa ishara ya jogoo kuwika huku Yesu akimgeuki na kumkumbusha moyoni maneno yale ya kwamba kabla ya jimbi kuwika atamkana, alishindwaje kunena na mwanaye aliyemtuma kwa kusui hilo?

Ila katika yote hayo haipaswi kukata tamaa ama kutafuta njia za mkato kama wengine wafanyavyo baada ya hali kama hii.
Wapo walioamua kuolewa nje ya utaratibu wakibibilia ama wengine kwenda kwa waganga kama Sauli ili kusaka utajiri ama majibu fulani.
Nataka ujifunze uvumilivu aliokuwa nao Ayubu, hakika mwanume huyu aliyeishi miaka kadhaa iliyopia alikumbana na majaribu ya ajabu na kinachonipa kumshangaa Ayubu ni pale alipoweza kustaimili ukimia wa Mungu kuanzia sura ya kwanza anapoanza kupatwa na majaribu, Mungu hakunena lolote hadi sura ya 38. Na hapo anaanza na kumuhoji maswali ila majibu yake yanatokea sura ya mwisho ya 42. Kisha Bwana akageuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; Bwana akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza. Ayubu 42:10.
16 Kisha baada ya mambo hayo Ayubu akaishi miaka mia na arubaini, naye akawaona wanawe, na wana wa wanawe, hata vizazi vinne. 17 Basi Ayubu akafa, mzee sana mwenye kujawa siku.
Kumbe hata Mungu akiwa kimya kwa kiasi gani inafika wakati anatujibu, ni kweli kwa Ayubu ukimia huu haukuwa mwepesi kwake kwani ulimtesa kama anenavyo hapa. Ayubu 312:35 Laiti ningekuwa na mtu wakunisikia! –Tazama sahihi yangu ni hii! Mwenyezi na anijibu!-Laiti ningekuwa na hayo mashitaka yaliyoandikwa na adui yangu! 36 Hakika ningeyachukuwa mabegani ningejifunga mfano wa kilemba; 37 ninge mwambia hesabu ya hatua zangu, ningemkaribia kama vile mkuu.
Lakini katika yote hayo Ayubu hakumtenda Mungu dhambi bali alimngoja yeye kwa saburi, nataka kukuonyesha siri iliyopo kwenye saburi kama nilivyoifafanua kwenye kitabu changu cha Namna ya kuishi wakati wa majaribu au mapito.

Yakobo 1:2 Ndugu zangu hesabuni ya kuwa ni furaha tupu mkiangukia katika majaribu mbalimbali. 3 mkifahamau ya kwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.

Yamkini ulijiuliza kama mimi saburi ni nini? 4 Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno.

Ona neno hili Saburi kwenye kitabu kile cha Warumi 5:3 Wala sii hivyo tu, ila na tufurai katika dhiki pia; tukijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi; 4 na kazi ya saburi ni udhabiti ya moyo; na kazi ya udhabiti wa moyo ni tumaini.

Saburi, inazaa, udhabiti wa moyo ikiwa na maana ya uhodari au ushujaa ulio jawa na uvumilivu pamoja na ujasiri, kisha inazaa tumaini. Na kitabu hiki cha
warumi kimelielezea kama dhiki ila ufahamu dhiki ni aina ya pito au jaribu lenye makali mno na mara nyingi huwakuta watumishi wa madhabauni na huwa ni jaribu la muda mrefu huku likiwa na sifa ya upweke kijamii.”

Hiyo ni nukuu iliyopo kwenye hicho kitabu, natumai imeona dhamani ya Uvumilivu aina ya Saburi ambayo hukuwezesha kuvuka mahali pa gumu kama ilivyokuwa kwa Ayubu.
Ninakuletea somo hili nikiwa ni shuhuda wa wahanga waliowai kukwama mahali kama hapa, Yupo mtu mmoja ambaye alikuwa ni mtumishi wa Mungu na alilazwa hosipitalini kwa muda fulani, aliombea wagonjwa wengine pale hosipitalini na walipona ila yeye bado alikuwa amelazwa. Aliumia sana kwa Mungu kuponya wengine ila kumuacha yeye.

Mie mwenyewe ni shuhuda miongoni mwa huu ushuhuda. Kuna kipindi nilikuwa kwenye hali ngumu sana ya hitaji la fedha na cha ajabu nilikuwa nikiwaombea wengine ikiwemo ndugu zangu walikuwa wakifanikiwa angali nikijiombea mimi ni kama Mungu anijibu na alikuwa kimiya hadi kulazimika kuomba msaada kwao.

Nkimuliza Mungu kuhusu mambo mengine hunijibu kwa haraka ila kuhusu uchumi yupo kimya. Na hili limewakuta wapendwa wengi sana, kwani unakuta anahitaji fulani na ameliombea kwa muda mrefu sana hadi kufikia hatua ya kuishiwa nguvu za kusonga mbele na inafika wakati anajikaza tena na kuinuka kiroho ila bado Mungu Yu kimya.

Akiombea mengine anajibiwa ila katika hilo ni kama Mungu amsikii. Inafika hatua mtu anahitaji hata jibu la njia ya ndoto ila na hapo tena Mungu Yu kimiya. Baada ya Ibrahimu kumpata Ishmaeli Mungu alikaa kimya bila kuzungumza nae kuhusu kumpatia majibu yake kwa kipindi cha miaka 14, Alimpata Ishmaeli akiwa na miaka 86, Mwa16:15-15, na malaika walipomletea majibu ya Isaka alikuwa na miaka 100, Mwa 17:17
Hakikuwa kipindi cha kawaida, bali ni kigumu, Yusufu mwana wa mzee Yakobo mara baada ya kutafsiri zile ndoto mbili za mwokaji na mwenyeshaji mkuu alikaa gerezani tena miaka 2 na hapo hatuoni mahali Mungu akizungumza naye. Fahamu bado hakikuwa kipindi kizuri ama rahisi kwake.

Ila mara baada ya majira ya watu hao kupita, Ibrahimu alimpokea Isaka wake na hatimaye kuwa ni nderemo na kicheko, Yusufu alipokea mujiza wake na hatimaye kuwa ni mwingi wa furaha kwa kutimiza maono.

Huo ndio wakati ninaotaka uangaliye wewe kama mpendwa. Ni kweli leo upo gerezani ila tazama wakati Farao akisema, Mwanzo 41:38 Frao akawaambia watumwa wake, “Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake?” 39 Farao akamwambia Yusufu, “Kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote, hapana mwenye akili na hekima kama wewe. 40 Basi wewe utakuwa
juu ya nyumba yangu, kwa neno lako watu wangu watatawaliwa…”

Huo ndio wakati wa kuutazama, usitazame wakati wa mke wa Potifa wakukusingizia na kutupwa gerezani ama wakati wa mkuu wa wanyweshaji kukusahau angali ulimtedea mema na amefanikiwa kwa mema yako.
Yamkini kuna watu uliwasaidia maishani nao wamefanikiwa na kukuacha wewe ungali unatafuta mpenyo, wewe mtazame Yesu atakuinulia Samweli wako atakayekupaka mafuta ama Barinaba wako atakayekutambulisha kama ilivyokuwa kwa Paulo. Cha msingi ni Uvumilivu wenye Saburi.

Baada ya uvumilivu tuangaziye njia nyingine, Na hii ni ya maombi na utoaji sadaka. Usikubali kukaa kimiya wakati ambao unamuona Mungu ni kama hakujibu ama asemi na wewe na unauwakika ya kwamba haujatenda dhambi. Na kama ni dhambi rejea pale awali kwenye sehemu ya kwanza ya makala hii, niliokutaka kumuomba Mungu rehema na kufanya mengineyo kama ukimya huo ni matokeo ya dhambi.
Hana mara baada ya kugundua kuwa Mungu alikuwa kimiya aliamua kumtolea Mungu sadaka ya Nadhiri kwa mtoto wake. Kumbuka ukimya huu haumaanishi kuwa Mungu akusikii, hapana! Anasikia maana Yeye sio kiziwi wala mtu ama mwadamu ndo asinziye. Ila kuna jambo anataka ujifunze, Ufanye ama anakufundisha Saburi kwa kukutaka kuwa nayo.
Fungua nami kitabu kile cha 1 Samweli, 1Samweli 1:11 Akaweka nadhiri, akasema “Ee Bwana wa majeshi, ikiwa wewe utaliangalia teso la mjakazi wako, nakunikumbuka, wala usinisahau mimi mjakazi wako, na kunipa mimi mjakazi wako mtoto mume, ndipo mimi nitakapo mpa Bwana huyo mtoto siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita kichwani mwake
Mungu hakuweza kunyamaza hata kidogo,kwani mstari wa 20, Hana anapokea muujiza wake na kusema “Ikawa, wakati ulipowadia, Hana akachukuwa mimba na kuzaa mtoto mwanamume; akamwita jina lake Samweli, akisema “Kwa kuwa nimemuomba kwa Bwana”  

Maombi na Sadaka ya Nadhiri yalimfanya Mungu kunena na hatimaye kumpatia majibu yake Hana. Na wewe usipoteze muda kwa kufadhaika bali hakikisha una mtafuta Mungu kwa viwango hivyo vya maombi kwa kushinda hekaluni na kisha kumuwekea Mungu Sadaka ya Nadhiri ama kutoa Sadaka nyingineyo ili kumfanya Mungu kushindwa kuendelea kukaa kimya na kukutokea katika kona iliyo sahihi.
Natamani kuendelea kunena nawe kuhusu jambo hili ila Muda wangu umekuwa kama ukuta nami naogopo kushindana nao kwani wahenga walishanena kuwa nikifanya hivyo nitaumia. Nakusihi niombee ili nipate kibali cha kuendelea na somo hili katika sehemu ya tatu.
Pia usikose somo jingine lenye mukutadha kama huu liitwalo, EPUKA KUYAFANYA HAYA PUNDE UMUONAPO MUNGU YUPO KIMYA. Ni miye Mwalimu wako Osar Samba

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple#MwalimuOscarSamba


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni