Ijumaa, 5 Mei 2017

KUTOA MIMBA NI DHAMBI

Na Mwalimu Oscar Samba
Kumekuwa na matukio mengi ya watu kutoa mimba huku baathi yao wakijifariji kuwa kufanya hivyo sio mauaji.

Ninataka kukufahamisha bayana ya kwamba utoaji wa mimba ni mauaji, na kibibilia hakuna muuaji mwenye uzito zaidi ila ukubwa ama kipimo cha kosa hilo la umwagaji damu ni sawa.

Yaani aliyeua mtoto aliyetumboni na aliyeumuua mtu wa miaka kumi ama zaidi wote hukumu yao inalingana.

Kwa kifupi aliyetoa mimba na aliyeshiriki wote ni kundi la wakina kaini.

Ikumbukwe kuwa kibibilia mtoto ama mtu hutambulika toka tumboni, Na hapo Mungu umuhesabu sawa na aliyezaliwa.

Ndio maana akamwambia Yeremia kuwa "Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa..." Yeremia 1:5

Yohana mbatizaji alicheza akiwa tumboni mara baada ya mama yake kukutana na mama yake na Yesu. Hii ni ishara kwamba kusudi la Mungu lilidhirishwa ndani yake angali tumboni mwa mamaye, sanjari na hapo kwaYeremia.

Kwa hiyo epuka kushiriki dhambi hii kwa namna ya aina yoyote ile na kama ulishashiriki tubu haraka.

Maoni 1 :