Jumamosi, 27 Mei 2017

BONDE LA KUKATA MANENO.

Na Mwalimu Oscar Samba #Ug Ministry 
Kwa furaha isiyo na kifani wala uzani ninakukaribisha ndugu yangu katika Bwana wetu Kristo kwenye safu hii ya makala za kiroho zenye dhima ya kukuinua kiroho, langu jina ni Mwalimu Oscar mwana wa Flora Samba kipenzi cha Mzee Prospa.

Katika makala hii sehemu ya kwanza nitakujuza athari ya maneno huku sehemu ya pili nikikupa mbinu za kupambambana na silaha hii ya maneno yenye nguvu kuliko bunduki ama mabomu yatengenezwayo na wanadamu.

Awali ya kukuletea uhodo huo natamani nikujuze maana ya bonde la kukata maneno. Huu ni ufunuo nilioupata na unamaanisha ya kwamba mtu yupo kwenye mazingira magumu ya kiroho kivita huku hali hiyo ikiwa ni matokeo ya maneno mabaya anayosemwanayo kutoka kwa watesi wake na nguvu ya vita hivyo ni ukaribu wa watu hao aidha kimwili au kiroho.


Katika kitabu changu cha NAMNA YA KUSIHI WAKATI WA MAJARIBU AU MAPITO nimelielezea kwa kina jambo hili na mathara pamoja na Suluhu lake husani kwenye kipengele chenye mukutadha wa kuchoka kiroho na maneno yakiwa ni kisababishi moja wapo.
Ninataka ujione pamoja nami kipengele hicho;
Tutazame maneno kama slaha ya uongo, Zaburi 144:8 Vinywa vyao vya sema visivyofaa, na mkono wao wakuume ni mkono wa uongo.
Kwa hiyo mtu asemapo au anenapo kusingizia jambo la uongo kwenye ulimwengu wa roho anapigana na wewe kutumia mkono na kama ujuavyo mkono hukunja na kurusha ngumi, kofi hata kwenzi pamoja na kushika silaha yoyote ile kwa hiyo usikubali kuchoshwa na jambo kama hili bali wewe tumia Upanga wa Roho Mtakatifu ambao ni Neno la Mungu kuukata huo mkono wa uongo na kukifunga hicho kinywa huku ukiomba kwa kutumia pia andiko lile la Isaya 54:17. Ambalo hubatilisha kila silaha iliyokuinukia na kuvihukumu hivyo vinywa vya uovu kuwa mkosa.

Kabla ya kutazama mifano ya watu kwenye bibilia waliochoka kutokana na maneno, nataka ufahamu rasimi ya kwamba maneno yanauwezo wa kupiga au kufanya kazi kama silaha, ndio maana likanenwa hili;
Ayubu 5:21a Utafichwa na mapigo ya ulimi..,Kwa hiyo Ulimu hupiga na ukikupiga usipopambana au kuuzuia unakuchosha, ndiposa utamsikia mtu akisema, sifanyi tena huduma au siendi tena kanisani maana wamenisema eti najipendea kwa Mchungaji, wamesema mimi sijui kuimba?, siimbi tena, wamenijerui sana Kama Nafsi yako imejeruhiwa kwa njia hiyo, omba uponyaji kama Daudi, Zaburi 22:20a Uniponye nafsi yangu na upanga

Tutazame adhari zake kwa mifano ndani ya Bibilia,Tumuone Daudi ambaye Nafsi yake inachoka kwa kuinama ikiwa ni matokeo ya kusemwa na adui au watesi wake,
Zaburi 42:3 Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, pindi wanaponiambia mchanakutwa, “Yuko wapi Mungu wako?”. Umeyaona hayo maneno? (Yuko wapi Mungu wako?”)


Tutazame kinachofwata,
4 Nayakumbuka hayo nikiweka wazi nafsi yangu ndani yangu, jinsi nilivyokuwa nikienda na mkutano, na kuwaongoza nyumbani kwa Mungu, kwa sauti ya furaha na kusifu, mkutano wa sikukuu.
Kwa hiyo hayo maneno yalikuja kama silaha na kuipiga nafsi kama nilivyo kujuza hapo juu kwamba hupenda sana kushambulia nafsi na Daudi mwanzoni mwamsitari huu analidhibitisha hili anaposema,
Nayakumbuka hayo nikiweka wazi nafsi yangu ndani yangu” Sasa tutizame kilichotokea mara baada ya nafsi yake kushambuliwa au kupigwa na maneno hayo yaliyonenwa Yuko wapi Mungu wako?” Mstari wa 5a Nafsi yangu kwa nini kuinama, na kufadhaika ndani yangu? Kwa hiyo Nafsi inainama sababu kubwa ikiwa ni Maneno ya watu ila Daudi anatafuta dawa yake na kujitaidi kujiponya kwa maneno ya tumaini na faraja ambayo pia ni dawa sahihi na sala,
 5b.Umtumaini Mungu kwa maana nitakuja kumsifu, aliye afya ya uso wangu, na Mungu wangu.
Fahamu kuwa anaposema uso anawakilisha moyo wake. Ka hiyo ukiondoa neno hilo na kuweka hapo moyo mstari huo utasomeka hivi; “Umtumaini Mungu kwa maana nitakuja kumsifu, aliye afya ya moyo wangu, na Mungu wangu.

Pia maneno yakikujia katika mfumo wa Laumu, Laumu huja pale unapotenda kosa na watu kuishia kukulalamikia au kukusema vibaya kutokana na kosa ulilolitenda huku dhamira yao ikishindwa kukusaidia, na hujeruhi zaidi pale kosa linapokuwa dogo na kisha mashutumu yakawa makubwa zaidi.Ama unapowaomba msamaha na kuitaji matengenezo, kisha baada ya hapo wewe unasamehe kama nao walikutenda na unasahamu kosa ulilotendewa maana pia umeshatengeneza na Mungu, kisha baada ya muda unawasikia wakitumia jambo lile lile na kulifanya kama fimbo ya kukuchapia au kama silaha ya kukudhoofisha ili uonekane una hatia au wao wapate ushindi kwa hatia ambayo ulishaitubia ingawaje na wao ni wakosa katika hilo.


Ama pia mashutumu au laumu hiyo yaweza kuelekezwa kwako pasipo kuwa na hatia, jambo hili huuvunja moyo na nafsi pia na tiba yake ina muhitaji Yesu, hali hii huwa na maumivu zaidi kama wakulaumuo ndio uliowategemea wangekuwa msaada kwako. Tumtazame tena Daudi yalivyo msibu;
Zaburi 69:20 Laumu imenivunja moyo, nami ninaugua sana, Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna; na wakunifariji, wala sikumuona mtu.

Ni vyema kuifuta kumbukumbu ya dhambi uliyoitenda kwenye ulimwengu wa roho, na kama ni masingizio, futa pia kwa Damu ya Yesu.


Tumtazame Yeremia alivyodhurika na silaha hii ya maneno, Yeremia 18:18 Hapo ndipo waliposema , “Njooni na tufanye mashauri juu ya Yeremia,…..Njoni, natumpige kwa ndimi zetu, wala tusiyaangaliye maneno yake yoyote.
Kwa hiyo adui zake kwa makusudi waliamua kuitumia silaha hii ili kujaribu kumdhofisha maana wanasema na tumpige kwa ndimi yaani kwa maneno.

Tutazame kilichotokea mara badaa ya mishale kurushwa: pinde hizo kupindwa na panga kutumika yaani maneno kama silaha ya adui; Mstari wa 19. Niangaliye, Ee Bwana, ukasikilize sauti ya wanao shidana nami. 20 Je, mabaya yalipwe badala ya mema? Mana wameichimbia nafsi yangu shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele yako ili niseme mema kwa ajili yao, nikaigeuza gadhabu yako isiwapate.

Pigo hilo linamfanya kulia, ila uzuri wake alimlilia Mungu hakulia kama Daudi ambaye machozi yaligeuka kuwa chakula chake mchana kwa usiku, hapo tunaona uwepo wa silaha nyingine ambayo ni maneno kama shimo, kwa hiyo maneno pia huweza kukuchimbia shimo kwenye ulimwengu wa roho hususani watakaposema “natuone sasa kama atafanikiwa” au “hapa atoboi” wakiwa na maana haufanikiwa ukifika hatua fulani.

Ndio maana ipo haja kubwa ya kubatilisha au kufuta maneno ya adui zako kwa Damu ya Yesu, na maandiko mfano Isaya 54:17Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa, na kila ulimi utakaokuinukia juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa…;

Na kama yana uhalali kwa dhambi uliyoitenda au yoyote ile omba kwanza rehema kwa damu ya Yesu kisha yafute na utayarike hizo silaha na kuhukumu vinywa vyao kuwa mkosa pamoja na kuondo madhara yake rohoni.

Tunamuona Yeremia akiwa wazi ya kwamba maneno hayo yameiadhiri nafsi yake kama nilivyokujuza hapo awali, anaposema Maana wameichimbia nafsi yangu shimo”. Pia anaumizwa na yeye kutenda mema ikiwemo kuwaombea rehema adui zake na badala yake kulipwa mabaya jambo ambalo hata Daudi kwenye hiyo Zaburi ya 42:4 analiliamikia.

Yamkini hata mimi na wewe tunaposemwa na mtu ambaye tulimsaidia au kumuonyesha fadhili huwa tunaumia sana ila mtazame Mungu na muone kama aliyetumumika na adui na pambanae rohoni maana ukiziruhusu fikra kama hizo huta pambana na hatimaye nafsi yako italemewa kwa majeraha na kuchoka hatimaye kuchukua maamuzi yasiyo sahihi.
Kumsema Mtumishi wa Mungu au Mchungaji wako vibaya ni jambo la hatari sana maana wakati wowote hata bila kujua anaweza kuomba ya kwamba Bwana apigane na wanaopiga naye na huenda hajui uliwai kumsema, ukashangaa unakumbwa na mabaya bila kufahamu yalipotoka, na wapendwa wengi wa leo hatujui kumuliza Mungu kwa nini hili limetokea; bali likija baya sisi ni kukemea tukidhani limetoka kwa Shetani maana ndiko kutokako kila lililo baya na likija jema hushangilia kwa mtazamo kwamba kila jema hutoka kwa Mungu bila kufahamu ya kwamba ipo njia ionekanayo kuwa njema machoni petu bali kwa Mungu ni laa!.

Pia kwa kufahamu anaweza akaamua kuomba Maombi kama ya Yeremia hususa au kama jeraha lake ni kubwa na uchungu ungali mifupani mwake au moyoni mwake na maombi hayo yakakupata bila kujali Mungu alisema ombea mema adui zako na wale wanaokuudhi, tuone maombi hayo ya Yeremia dhidi ya adui zake mara baada ya kuumizwa na maneno yao.

Tuendelee na kitabu hiki sura hiyo ya 18: 21 Kwa sababu hiyo, watoe watoto wao waone njaa, uwatoe nguvu za upanga ziwapige; wake zao wafiwe na watoto wao, na kufiwa na waume zao, wanaume zao wauwawe, na vijana wao wapigwe kwa upanga vitani.
22 Kilio na kisiwe kitokacho katika nyumba zao, hapo utakapo leta kikosi juu yao kwa ghafula; kwa maana wamenichimbia shimo waninase, nao wameifichia miguu yangu mitego.
23 Lakini wewe Bwana, unajua mashauri yao yote juu yangu, yakuniua; usiwasamehe uovu wao, wala usifute dhambi yao mbele ya macho yao .Bali wakwaze mbele zako; uwatende mambo wakati wa hasira yako.

Kwa muombezi hayo sio maombi sahihi sana ila wewe epuka kusengenya ili usipatwe na hayo, maana hata Musa aliposemwa hakuomba ila Mungu alishuka na kumuadhibu Haruni na Miriamu, pia jiuluze kama Musa asinge waombea rehema au angeamua naye kuomba kama Yeremia, nini kingalitokea? Ukitaka kupata picha ya kile ambacho kingetokea nenda kasome kisa cha Korana, Dathani na Abiramu, Hesabu sura 16 hadi sura ya 17 (Hes 16-17), (Kwa kifupi walilambwa na moto baathi, na wengine Mungu alipasua aridhi ikawameza na ikajifunga). Tusonge mbele na sababu nyingine.
Hiyo sababu nyingine sitakuletea maana hiyo ilikuwa ni nukuu kutoka hapo kitabuni na nililenga tu kipengele cha Maneno, kwa zaidi kitabu kikitoka kitafute sokoni. Na ni yangu imani kuwa ujumbe huu umekupa nguvu na fahamu zaidi katika safari hii ya kiroho. Ninakuaga katika jina la Bwana huku nikikutaka kuendelea kufwatilia makala zangu.


Usikose makala murwa na Mubashara kutoka hapa UG MINISTRY kesho itwayo, MAJIRA YA FARAO ASIYEMJUA YUSUFU.

Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundila Fb, ili kuupta habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni