Jumanne, 23 Mei 2017

NGAMBO YA YORIDANI Sehemu ya 1

                Na Mwalimu Oscar Samba #Ug Ministry 
Ni kweli Maziwa na Asali ni Ahadi ya Mungu maishani mwako, lakini kabla ya kuuvuka mto Yoridani, nilazima ukutane na bahari ya Shamu, Kisha ugumu wa jangwa.

Yesu aliwaambia wanafunzi wake na tuvupe mpaka ng’ambo, lakini kabla ay kuvuka walikumbana na dhoruba kali baharini, Upepo ambao uliwapa hofu kuu. Petro alitamani kutembea juu ya maji ili  amfike alipo Yesu. Ila kabla ya kumkaribia wimbi lilifanyika kikwazo kwake.


Nawe ni kweli Mungu amekuaidia kukupa Mume/Mke, Nyumba, Kiwanja, Biashara nzuri, Huduma yenye ukubwa wa matendo ya miujiza na ishara, Kibali cha huduma, Maisha bora ya kiuchumi na Upako kwa ajili ya kazi yake. Na dalili ya kwamba amekupa ni ndoto unazoota ukiwa unachuma matunda, za mafanikio kihuduma na zile za mapesa mengi.
Lakini  kwa kweli maisha unayoishi ni kama hayasadifu hayo uliyoaidiwa, kwani kila sehemu kumejaa vikwazo, Uchumi mgumu, milango ya Baraka ni kama imefungwa, Ndoa imepoteza tumaini, Furaha maishani imepotea, kila ndugu wa kiroho na kimwili ni kama vile amekusahau. Watoto wanasoma na kula kwa shida yamkini hata kodi ya nyumba kulipa ni matatizo.

Nisikilize nikumegee siri ya hayo: Ahadi ya MUNGU maishani ni lazima itimiye, ila kabla haijatimia hunabudi kuandaliwa kwa ajili ya kukuwezesha kuimudu  hiyo ahadi, yaani Mungu hukupa maarifa katika hilo jambo na akili ili mafanikio hayo yasije kukutoa kwa Mungu.

Kwa lugha rahisi ni kwamba mapito unayoyapitia ni shule na majaribu hayo ni mtihani na punde utakapo faulu ndiposa utakapopewa hiyo ahadi. Ndio maana kuna wakati unaota ndoto upo darasani ikiwa ni ishara ya kwamba MUNGU anakufundisha. Kwa hiyo usikimbiye hayo mapito kwani kama wanafunzi wa Yesu wangali kimbia kwenye boti wasingeweza kufika ng’ambo. Na wana wa Iziraeli wale waliyoyachukiwa maisha ya jangwani walifia hapo na kushindwa kuifikia Kanani yao.

Pia wakati mwingine maisha hayo huwa ni matokeo ya vita kutoka kwa Shetani ambaye huviachilia kwa shabaha ya kukukwamisha. Katika hali hii yakupasa sana kuwa muombaji na sio mnung’unikaji. Unatakiwa kuhakikisha unafanya maombi ya vita, na ya ulinzi pamoja na yale ya kuondoa vikwazo barabarani ili kumshinda adui aliyepanga kukumeza.

Pia unatakapo kutana na ugumu wo wote ule unatatikana kuwa mwepesi wa kumwendea YESU na sio wanadamu ama kunung’unika kama baathi ya wana wa Iziraeli. Iga sana tabia za Musa, Yoshua na Kelebu katika safari yako ya kuivuka Yoridani na hatimaye kuingia ng’ambo ya pili. Kumbuka ng’ambo uliyopo ni ya Misiri ama jangwani na kiu yako ni ukiingia ile ya Kanani.

Usikubali kuacha hata ukwato Misiri ama jangwani, bali nenda na kila kilicho chako. Wengine wanaacha vitu vyao. Kwa mfano, unakuta mtu ana mafanikio kiuchumi na kiriho, maana yake katika hiyo yupo Kanani ya kiuchumi na kiroho ila ndoa yake ina migogoro toka awali ile isiyoisha. Maana yake ameenda kanani na kufika akiwa na uchumi na kiroho ila ameacha ndoa yake Misiri ama imekwama jangwani.

Nina maana wakati unaombea maisha yako, usibaguwe baathi ya vitu na kuviona hivyo vina dhamani zaidi ama kuona matatizo mengine ni kama vile hayana tiba, bali ombea yote na beba vyote ili ufike ng’ambo ya Yoridani salama.
Tutafiti maandiko haya ili kujionea tabia ile ya Musa ya kumlilia Mungu kwa haraka anapokuwa na matatizo. Tuanze kwa kuchunguza mawazo au mtazamo ambao unapaswa kuuepuka.
Kutoka 14:11 Wakamwambia Musa, “Je, kwa sababu hapakuwa na makaburi katika Misiri umetutoa huko ili tufe jangwani? Mbona umetutenda haya, kututoa katika nchi ya Misiri? 12 Neno hili silo tulilokwambia huko Misiri, tukisema ‘Tuache tuwatumikiye wamisiri?’ Maana ni afadhali kuwatumikia Wamisiri kuliko kufa jangwani
Na yakupasa uwe na mtazamo huu, ambao unaona njia pasipokuwa na njia.
Kutoka 14:13 Musa akawaambia watu, “Msiogope! Simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakao wafanyia leo; kwa maana hao Wamisiri mliowaona leo hamtawaona tena milele.14 Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimiya

Ndivyo unavyopaswa kutazama vikwazo vilivyopo mbele yako katika safari yako ya Maziwa na Asali. Kwani wasomaji wa maandiko wanafahamu mara baada ya mtazamo huo wa Musa Mungu alimtumia kuigawa Bahabari ya Shamu nayo ilitii na kuwagwanyika kisha wana wa Iziraeli wakavuka na mbele wanaanza kuimba wimbo wa Musa uliojawa na Ushindi tele.

Unaonaje kama Musa angalikuwa na matazamo kama huo wa wana wa Waebrania?  .. Na wewe ukiendelea kutazama vikwazo kwa namna hiyo ya kushindwa, je, wanao ama washirika wako au jamaa yako itaishi maisha gani baadae? Ni kweli mtafika ng’ambo ya Yorida?
Mtazamo mwingine, Ni pale Masa walipokosa maji. Kutoa 17:2 Kwa hiyo hao watu wakateta na Musa, wakasema “Tupe maji tunywe!” Musa akawaambia kwanini kuteta na mimi ? Mbona mnanijaribu ? 3 Watu wakawa na kiu huko; nao wakamnung’unikia Musa, wakisema, “Mbona umetupandisha kutoka Misiri ili kutuua sisi na watoto wetu na wanyama wetu kwa kiu?” 
Musa kama kawaida yake alimlilia Mungu na Mungu ukimlilia huwa hanyamazi kimia bali hufanya jambo.
Songa nami hadi mstari wa 6, Tazama, nitasimama mbele yako huko, juu ya lile jabali katika Horebu; nawe utalipiga jabali, na maji yatatoka, watu wapate kunywa.” Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Isiraeli.
Baada ya hapo Mungu aliufanya mwamba kutoa maji, kumbuka sio udongo wala changarawe bali ni mwaba ama jabali lilitoa maji, Mungu hakutaka kutoa maji chini ya mti ama kando ya jiwe kubwa bali alitaka jiwe gumu liwatolee maji ili wajuwe ya kwamba Mungu huyu ni Mungu wa mambo makubwa. Na wewe hayo mapito yaliyokuwa magumu ni mahali ambapo Mungu anataka ajitwaliye Utukufu ili kila mwenye mwili ajuwe ya kwamba Mungu wako ni Mungu wa mambo magumu, ila wewe uwe na mtazamo kama wa Musa. 
Wakati wengine wanasema ya kwamba hapana njia wewe ona njia, wakati wengine wanaona ni mwamba wewe ona maji ndani yake.
Nina kiu na shauku yakuendelea nawe kama Ayala anavyoyaonea shahuku maji ya mtoa, ambaye wanatheolojia wanasema ni aina ya mnyama aliyeishi zamani na alikuwa na tatizo la kiu ama alikuwa ni mwenye kiu isiyoisha na akiyapata maji huyabugia kwa kiwango kikubwa ila punde kiu ile humrejea akitoka majini.

Nami ndivyo ninavyowiwa ndani mwangu kushinda nawe nikikujuza siri zilizopo ndani ya Biblia ila sina budi kuishia hapa, tukutane tena kesho panapo majaliwa ya MOLA, nitakapo kuwa nikiendelea na makala hii katika sehemu ya pili na hapo nitaanza na mfano wa Dhoruba ziwani kwa wanafunzi wa Yesu na kukupa mbinu teule zitakazo kuwezesha kuvuka jangwani ama kwenye mawimbi salama huku kesho kutwa nikikupa KIGONGO ama MANA nyingine itwayo, YESU KAMA MTULIZA MAWIMBI AU DHORUBA. Ni kweli mapito magumu yapo ila yupo Mwanamume aliyelala kwenye Sherti na wewe muendee Yeye ukimwamsha kama wanafunzi wake ili atulize hayo mawimbi makali kwenye ndoa yako ama kwenye uchumia au kwenye hiyo huduma. Pia hata upepo anatuliza huyu MWANAMUME WA AJABU KWELI KWELI.Langu jina ni OSCAR PROSPA mwana wa Flora na Mzee SAMBA. Mutu ya MUNGU kutoka Arusha Tanzania.

Kama hujaokoka na unataka kuokoa tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KAUMINI KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapa.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundila Fb, ili kuupta habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                      PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                               

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni