Jumatatu, 15 Mei 2017

EPUKA KUYAFANYA HAYA PUNDE UMUONAPO MUNGU YUPO KIMYA.

Kijana mmoja akasema, “Sitowi tena sadaka maana kila nikitoa ndo kama matatizo yanaongezeka”
Wengine wameanguka kwenye uzizi na uasherati huku sababu ikiwa ni kumuona Mungu kama awasikii ama amechelewa kuwaletea majibu yao, aidha ya kuolewa ama mtoto.
Sarai akamwambia Abrahamu/Ibrahimu, “Basi sasa, Bwana amenifunga tumbo nisizae, umwingiliye mjakazi wangu, labla nitapata uzao kwa yeye.” Abrahamu akaisikiliza Sauti ya Sarai. Mwanzo 16:2.

Baada ya hapo kilichofwata ni Ibrahimu kuzaa na kijakazi huyo wa bibi Sarai na hatimaye kumpata Ishmaeli ambaye
kimaandiko hakuwa mrithi maana mrithi alipaswa kuwa Isaka. Kumuona Mungu amechelewa ama yupo kimya kulimfanya Sarai kuchukuwa maamuzi yasio sahihi na kumshawishi mumewe kutenda jambo ambalo halikuwa mapezi makamilifu ya Mungu.

Nawe nakutaka kuwa mwenye subira wala usikubli kutenda kama hayo maana utendaji huo utakufanya kuziepuka Baraka za Mungu wako ama kukupa mathara makubwa sana kiroho. Kumbuka ukimya wa Mungu sio wa milele ama wa kudumu, ama unapomuona Mungu amekawia haimaanishi kuwa hatakujibu, Bali fahamu kuwa atakujibu na majira yake yamkini yamekaribia na ulipotoka ni mbali kuliko unakotazamia kwenda. Wakati Ibrahimu anampata Ishmaeli alikuwa na mika 86, ikiwa bado miaka 14 ili ampate Isaka. Jaribu kufikiria ya kwamba amevumilia miaka mingapi ? na imesalia miaka mingapi mbeleni?

Nani ajuaye ya kwamba kwako zimebaki siku chache, ama masaa machache ilikuifikia mema yako. Yesu pale msalabani wakati analalama ya kwamba Mungu wake mbona amemwacha, alikuwa amebakisha dakika ama sekunde chache akaketi na baba yake katika mkono waka wa kuume. Na kwako yamkini ni sekunde zimesalia ama hata sekunde hazifiki.
Kitu kingine, Epuka kunena maneno ya kufurua ama ya kwazayo au yasiyofaa mbele za Bwana au Wivu. Tuone kisa hiki kimaandiko. Mwanzo 30:1 Naye Raheli alipoona ya kuwa hamzalii Yakobo mwana, Raheli alimwonea ndugu yake wivu. Akamwambia Yakobo, “Nipe wana; kama sivyo, nitakufa mimi.” Jambo hili halikuwa jema machono pa Yakobo, 2 Yakobo akamgadhabikia Raeli. Akasema, “Je, mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia uzao wa mimba?
Hii yote ilikuwa ni matokeo ya yeye kukosa majibu yake kutoka kwa Mungu kwa muda mrefu. Unaweza kuniuliza, Mwalimu angalifanyaje? Rejea makala zangu mwenza za “MUNGU ANAPOKUWA KIMYA FANYA YA FWATAYO”.
Lakini pia tuangaziye alichokifanya baba mkwe wake na mama mkwe wake walipokosa nao mtoto, ambapo njia hii ndiyo iliyomfanya Mungu kumpatia Yakobo mumewe anayemnenea yasiofaa kutokana na uvumilivu kupungua ama waswahili husema kuwa “ziro (0)”.
Walifanya hivi, Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukuwa mimba. Mwanzo 25:21.
Kumbuka walikosa watoto kwa muda wa miaka takiribani 20, Maana walioana na Isaka akiwa na mika 40, Na Kujibiwa, Isaka akiwa na miaka 60. Nawe fanya hivyo na usichoke kumlilia Bwana.

Jambo jingine la kuepuka ni Manung’uniko, hali hii ni hatari sana katika maisha ya kiroho maana humfanya Mungu kugadhabika na kukuathibu. Katika kitabu kile cha Hesabu 11, Wana wa Iziraeli walifanya kosa hili na Mungu aliwaadhibu kwa kuwapa nyama za kware zilizowatokea puani. Katika Hesabu pia 13, na 14 Mungu aliwakasirikia baada ya kuzikubali taarifa za kukatisha tamaa na kuingiwa na roho hii ya manung’uniko hali iliyowafanya kushindwa kuifikia Kanani yao.

Ni kweli waliiona safari ni ndefu ya kufika kanani ila hawakupaswa kunung’unika. Pia katika kitabu hicho cha Hesabu 21, utaona jinsi Mungu alivyowaangamiza kwa nyoka ya moto kwa sababu ya jambo hili.

Hesabu 21:4 Wakasafiri kutoka mlima wa Hori kwa njia ya Bahari ya Shamu, ili kuizunguka nchi ya Edomu; watu wakafa Moyo kwa sababu ya ile Njia.
5 Watu wakamnung’unkia Mungu na Musa “mbona mmetupandisha kutoka nchi ya Misiri, ili tufe jangwani? Maana hapa hakuna chakula, wala maji na roho zetu zinakinai chakula hiki dhaifu”

6 Bwana akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma watu wengi wakafa.

Epuka jambo hili la manung’uniko ili kuwa salama. Wakati Mungu ananipitisha katika maandiko haya nilimuliza jambo la ajabu sana na kumshangaa maana nilitazamia kuwahurumia kwa kuto kuwaadhibu kwa makali haya kwani walikuwa katika hali ya kuchoka kiroho.
 Ila Mungu huwa na desturi ya kutoa adhabu kwa dhambi kama hii na haijalishi unapitia ugumu mkubwa kiasi gani bali hawezi kukuacha salama kama utafanya kosa hili. Soma kuanzia mwanzo hadi Ufunuo ukitafuta madhara ya kosa hili na mtaji wako mkubwa uwe ni safari ya wana wa Iziraeli.

Usiache kutenda mema, Wagalatia 6: 9 Tena tusichoke katika kutena mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho..

Kuna watu wameacha kabisa kutoa sadaka kwa madai ya kwamba Mungu amechelewa kuwabariki ama amekaa kimya, na wanapotoa wanaona ni kama hali ndo inazidi kuwa ngumu zaidi kimaisha. Mtazamo huu huwafanya kuacha kutenda mema na badala yake huleta kuzimia roho na mathara yake ni kutokuvuna kwa wakati na mara nyingine kuto kuvuna kabisa.

Unapofanya maombi ama kusoma Neno au kujisogeza mbele za Mungu kwa kuutafuta uso wake na kisha kuona kama Mungu hakujibu, fahamu fika ya kwamba hupaswi kuacha kutenda hilo jambo jema kwa kuwa na matazamo ya kwamba Mungu yupo kimya au kumuona kama hana dhamira ya kukupa majibu yako.

Mungu wetu husikia yale tumuombayo kwani ni Mungu aliyekaribu sana nasi. Yeremia 23:23 “Mimi ni Mungu niliyekaribu, asema Bwana, mimi si Mungu aliye mbali.

Na kukumbusha tena ya kwamba ukimya wa Mungu sio kwamba hakusikii bali anasubiri majira yake ya kunena kama ilivyokuwa kwa Ayubu, ama anakuhitaji ufanye jambo fulani kama kwa Hana aliyeomba na kutoa na Sadaka ya Nadhiri. Ama ni Ishara ya kukuandalia mapokezi mema kama ilivyokuwa kwa Yesu.

Mungu akitujalia tutaendelea na makala hii siku yoyote ile panapo majaliwa yake, Miye ni mwalimu wa Neno la Mungu; Mwalimu Oscar Samba.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple#MwalimuOscarSamba


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni