Ijumaa, 5 Mei 2017

Wasifu, Mjuwe Mwalimu Oscar Samba.

Mwalimu Oscar Samba
Ni Mwalimu wa Neno la Mungu na Muasisi wa Huduma ya Ug, yenye kirefu cha UKOMBOZI GOSPLE. Na yenye tafsiri ya Injili ya Ukombozi.

Pia ni mwandishi wa vitabu vya Neno la Mungu, na kitaaluma ni mwandishi wa habari mwenye elimu ya ngazi ya Diploma/Stashahada na ngazi ya Cheti cha Juu. Amesomea kwenye chuo cha AJTC kilichopo mkoani Arusha.

Ana elimu ya Thielojia ngazi ya cheti aliyoipata kwenye chuo cha kupanda makanisa Makuyuni mkoani Arusha kikiwa ni tawi la chuo cha TAG cha BIBILIA ARUSHA, kwa hivi sasa ni Chuo cha Bibilia Kanda ya Kasikazini.

Pia amehitimu shule ya Msingi Maharo na ya sekondari ngareni zilizopo mkoni Kilimanjaro. Kabila lake ni mchaga wa maeneno ya Rombo. Na Dini yake ni Mlokole.

Baba yake ni Prospa, Mama yake ni Flora. Na Ukoo wake ni Samba.  Ni mtoto wa pili katika familia ya Mzee Prospa.
Kuzaliwa ni 6/6/1989,
Anaishi mkoani Arusha na kiasili ni mtu wa mkoani Kilimnjaro.

Pia Kabla ya kuingia kwenye wito wa kitumishi aliwai kufanya Siasa na alikuwa mwanachama wa vyama viwili ambapo chama cha kwanza alikitumikia kwa muda mrefu zaidi na hatimaye kuhamia kingine kutoka na masilai ya kisiasa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni