Jumanne, 16 Mei 2017

LAZARO HAJAFA, AMELAA NA WEWE AMINI TU.


 Na Mwalimu Oscar Samba Ug Ministry
Wakati Dada yake  Lazaro anasema, Lazaro amekufa na ni siku ya nne sasa, na kunuka ananuka, Jemedari YESU anasema, “Lazaro ajafa bali amelala.” Na kumtaka dada huyu amini tu, ili mujiza utendeke.

Na kwako wakati wanasema kuwa, ndoa yako, imekufa,Uchumi wako umedidimia, Eti ndoto zako za kuwa mbunge, kiongozi, msomi ama dakitari na hata zile za kuwa na huduma kubwa zimekufa, mimi ninakwambia kwa jina la Yesu aliye hai hazijafa bali zimelala tu, na siku ya leo zitaamka kama Lazaro na kijana walivyo fufuliwa.


Ni kweli katika macho ya nyama Lazaro na kijana walikuwa wamekufa, ila YESU aliye bingwa wakufufua vitu vilivyokufa kwa kuvipa uhai alitazama kwa macho ya ndani na aliona uhai wa watu hawa, kama alivyotazama mifupa ile mikavu kipindi kile cha Nabii Ezekieli.
Yamkini bado tatizo lako halijaonja mauti ila linaumwa, Nina kuhakikishia kuwa ugonjwa huo sio wa mauti bali ni ili Mungu atukuzwe kwa mgogoro huo wa ndoa, ama uchumi wako kuporomoka ama wewe kusimamishwa kazi, ili baadaye wamtukuze Mungu wako.
Yohana 11:Naye Yesu aliposikia, alisema “Ugonjwa huu sio wa mauti, bali ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu, ili mwana wa Mungu atukuzwe kwa huo

Na yamkini unasema moyoni mwako ya kwamba Mwalimu Oscar ni mwezi wa tatu saa ama miaka toka mume/mke wangu aondoke nyumbani, au toka nifukuzwe kazi ama biashara yangu idode. Ninakwambia kama Yesu,
Yohana 11:11 Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha
Usiwe kama wanafunzi wa Yesu waliotazama mambo kimwili kwa kuzania ya kwamba amelala kweli kimwili ila Yesu alinena kuhusu kufa kimwili na kwa macho ya rohoni aliona kulala. Ikiwa ni kauli dhabiti ya Imani yake.
Tudodose kwenye mstari unaofwatia jambo hili, 12 Basi wale wanafunzi wakamwambia, “Bwana , ikiwa amelala, atapona” 13 Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walizani amenena habari ya kulala usingizi. Mstari wa 14 aliwaambia wazi wazi kuwa Lazaro amekufa.
Pia usiwe na mtazamo kama huu wakutaka kufa na Lazaro, nikiwa na maana kama ndoa ama uchumi au hilo jambo lako limekufa na wewe unataka ufe kiro, yaani kukata tamaa kuacha kabisa wokovu kwa sababu ya pito lako. Usikubali kuwa kama waliopoteza tumaini maana unapaswa kuamini tu.
Msikilize Tomaso wakati anawakilisha fikra za wenzake, “16 Basi, Tomaso aitwaye pacha, akawaambia wanafunzi wenzake, ‘twendeni na sisi ili tufe pamoja naye.”
Baada ya Yesu kwenda kwa Marehemu Lazaro dada yake aitwaye Martha alianza kumlaumu Yesu ya kwamba kama angalikuwapo kaka yake asingali kufa. Dada huyu alitambua na kuamini uweza wa Yesu wa kumponya Lazaro kwa haraka  ila imani hiyo haikwenda hadi kwenye kuweza kumfufua nduguye. Ndiposa Yesu analazimika kuanza kumjengea Imani ili mujiza utendeke.
Ila dada huyu hakuwapungukiwa kiasi cha kutokuamini kabisa, bali aliamini Yesu bado anaweza yote, na kabla ya kuona jitiada za Yesu za kumjengea imani tuone kwanza kiwango cha imani yake na uwelewa wake kuhusu uwezo wa ufufuo wa Yesu.
22 Lakini hata sasa najua ya kwamba yoyote utakayomuomba Mungu, Mungu atakupa.
Yesu akasonga mbele zaidi kwa kumwambia habri za kufufuka kwa nduguye na ona hapa fikra zake. 24 Matha akamwambia, “Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.”
Mawazo kama hayo nataka yakutoke kwenye fikra zako maana siku ya mujiza wako ni leo, na hapa sineni habari za kutajirishwa mbinguni wala kupewa afya peponi ila ninanena habari za kupokea ufufuo kwenye tatizo lako majira haya. Na kama ni mtoto mwakani majira kama haya upakate mwana. Alikadhalika kama ni ndoa ama kuolewa ama kuoa majira kama haya mwakani uitwe bibi ama bwana fulani.
Nimekwisha kukujengea imani na wewe sasa amini tu, na tuone jinsi Yesu alivyoanza kumjengea Martha imani mpya kuhusu ufufuo maana alimwamini Yesu kweli ila sio katika jambo kama hii, Na wewe ni kweli yamkini unamwamini Yesu lakini sio katika jambo kama hilo.

25 Yesu akamwambia, “Mimi ndimi huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa atakuwa anaishi”
 Baada ya msingi huo unaonyesha pia asiyeamini atakufa kwa mstari wa mbele yake, Yesu anataka kujua kama somo lake limeingia kichwani kwa kumuliza hili swali.
26… Je, unayasadiki hayo?
Na mimi ni swali langu kwako leo, Je, unayaamini haya ninayo kwambia kuwa majira kama haya mwakani utapakata mwana? Ya kwamba mume/mkeo atarejea nyumani tena mwenyewe bila kuitwa? Au walio kufukuza kazi watakutafuta siku chache zijazo na kukuri kuwa bila wewe ofisi haiendi?
Je, Unasadiki pamoja nami kuwa waliokudharau na kukutenga kihuduma kanisani kwako dakika chache zijazo watakutafuta nakukwambia tumpate wapi mtu kama wewe ambaye roho ya miungu watakatifu wanakaa ndani yako, ama kwa kuwa Mungu amekupa akili na maarifa na hekima namna hii basi utakuwa mkuu katika Misiri yote kama Farao kwa Yusufu ama Nebukadreza kwa Belteshaza?
Tuendelee, na Ujenzi wa Imani wa Yesu kwa Martha, Baada ya hapo Yesu aliwataka waliondowe jiwe kaburini; (kwa lugha ya leo wafukuwe kaburi), ila dada huyu alisema ya kwamba amekufa na ananuka ni siku ya nne sasa, ndiposa Yesu akamjibu,
40 Yesu akamwambia, “Mimi sikukuambia ukiamini utauona utukufu wa Mungu?
Usifeli mtihani kwa kupungukiwa na imani, kumbuka mimi ni Mwalimu na hapa ninakujengea imani na wakati wa “Pratical” yaani vitendo vya kudhibitisha imani yako unakuja, na hapo amini tuu, ili nisije kukuhoji kama Yesu;

Mimi ninakwambia kama Yesu, amini ili uone Utukufu wa Mungu, mara badaa ya Yesu kujenga imani hiyo kwa Martha dadaye na Marehemu Lazaro, kilichotokea ni mujiza kwa Lazaro aliyeitwa Marehemu kuwa mzima na jina marehemu kufutika.

Na wewe itakuwa hivyo kwako leo, waliokuita aliyaechika, masikini, hohehaye, fukara wa kwanza, na hata asiye na mbele wala nyuma. Watakuita mbarikwa, tajiri wa matajiri, mama/baba wa mataifa mengi na hutaitwa tasa tena kwani vinywa vya wakina Penina vinakwenda kukoma sasa. Ila wewe amini tu. Ili uone Utukufu wa BWANA, Kwani wamisiri yaani watesi unaowaona leo hautawaona tena na BWANA atakupigania na wewe utanyamaza kimia.

(Kutoka 14:13 Musa akawaambia watu, “Msiogope! Simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana
atakao wafanyia leo; kwa maana hao Wamisiri mliowaona leo hamtawaona tena milele.14 Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimiya) Kwa Neno hilo mashujaa walivuka bahari ya Shamu. Na kwa neno hilo nawe vuka.

Lazaro hayupo tena kaburini, Yohana 11:43 Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, “Lazaro njoo huku nje.” 44 Akatoka nje yule aliyekufa, .. Na wewe utoke nje ule uchumi wako uliokufa, Ndoa ama Elimu yako, Huduma ama Afya yako, ninaiita sasa nawe kwa imani itapamoja nami kwa sauti iliyo kuu. Njoo Ndoa kwa Jina la Yesu, njoo Uchumi, Elimu, Afya, Huduma, Upendo, Kibali, Upako, Karama kwa Jina la YESU KRISTO MNAZARETI NJOO NJE NAWE UFUFUKE KATIKA WAFU. Ameni na hongera kwa Mujiza wako.
Kabla sija kuaga kwa busu takatifu, nataka kukujuza jambo jingine muhimu hapo ikiwa ni kanuni za kufufua kila kilichokwama maishani mwako na wewe kuwasaidai wengine,
 1. Imani, 2. Ita kwa sauti iliyo kuu kamaYesu alivyoita ama aliyo omba.
3. Kaa karibu a Yesu, na umalaki kama Martha.
        Na 4. Hakikasha unaomba kwa huzuni ya roho yenye dhima ama taswira ya kumaanisha na yenye kumfadhaisha Yesu kama Mariamu dadaye mwingne wa Lazaro ili Yesu naye aguswe na tatizo lako na hatimaye kukutendea mujiza.
Usikubali kuomba kwa mazoea ama kibosi, hakuna ubosi mbele ya kufufua kilichokufa. Ukiweza kugaragara , garagara na ukiweza kulia lia haswa bila woga.

Yohana 11:32 Basi Mariamu alipofika pale alipokuwapo Yesu na kumuona, alianguka miguuni pake, akamwambia, “Bwana, kama ungalikwepo hapa ndugu yangu asingali kufa” 33 Basi Yesu alipomwona analia, na wale wayahudi waliofwatana naye, aliugua rohoni, akafadhaika roho yake, 34 akasema, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, Bwana njoo utazame.

Anauliza alipowekwa  Lazaro baada ya kuugua na kufadhaika rohoni pamoja na Mariamu na wafariji wake, na wewe mfanye Yesu afadhaike kwa kuugua pamoja naye kimaombi, sio kuugua mwilini na kulia sana! Hapana!! Bali ni kuugua kwa kuomba ama kuanguka miguuni pa Yesu. Nao bila kupoteza muda walimjibu, “Bwana njoo utazame

Na wewe Yesu akikuhoji, mwanagu nikutende nini, ama yupo wapi mwenzi wako, mwambiye kwa haraka na weka mambo bayana. Achana na hadidhi za kukosa mtu wakukusaidia punde maji yatibuliwapo , “Oho, mara wenzangu wananipita na kutangulia birikani punde malaika atibuapo maji”, wewe mwambiye Yesu nataka ufufuwe ndoa yangu, mwenzangu kaondoka, ama nataka kusoma sina ada mdhamini wangu kafarikia na kagoma, au mwambiye nimefukuzwa kazi au biashara imedodo. Pia waweza weka bayana bila woga ya kwamba, nina miaka kadhaa kwenye ndoa nami sina mwana, ama kiu yangu niolewe.
Nii Mwingi wa tabasamu, lisilo pimika kwa uzani wala futi, ninakupongeza kwa ujasiri na umahiri wako kama mtu apigaye mbiyo mashindanoni ya kufwatilia makala zangu bila kuchoka, ni hakika ujumbe huu umefanyika msaada kwako, usisite kuwadokezea ma kuwamegea  wengine uzuri wa ujumbe huu, na kama huja penda/kulike page/ukurasa wetu wa Facebook fanya hima kufanya hivyo ili upate jumbe hizi kwa haraka na waalike na wengine pia. Ukurasa wetu una jina la UG UKOMBOZI GOSPLE Pamoja na kundi letu.
Tukutane tena kesho panapo majali ya Mwenyezi MUNGU, na kama hujasoma makala za nyuma zitafute hapa uzisome.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni