Jumatatu, 15 Mei 2017

MUNGU ANAPOKUWA KIMYA FANYA YA FWATAYO. Seh. 1


Ni rahisi kunena kinyume na mtazamo huu ya kwamba Mungu hawezi kunyamaza ila wasomaji wa maandiko na watu wanaopitia mapito magumu na ya muda mrefu ni wepesi wa kukubaliana na Falisafa hii.

Ila kumbuka hali hii ilimkuta hata Yesu, “Mungu wangu, Mungu wangu mbona umeniacha?”, Mathayo 27:46. Kiukweli Mungu alikuwa Kimya. Hatumuoni akiongea naye wala kumjibu lolote baada ya kukamatwa kwa Yesu.
Kuna taswra kuu mbili za Mungu kunyamaza kimya, ya kwanza ni ile ya mtu kutenda dhambi na Mungu kumuacha, na ya pili ni ile ya mtu kuwa katika hali ya pito huku Mungu akipima subira yake iliyondani ya Saburi ya Kimungu ama Mungu akimsubiria achukuwe hatua fulani ndipo amjibu.


Tuanze kuidodosa ile ya kwanza ya mtu kutenda dhambi, Mfalume Sauli alikuwa kipenzi cha Mungu, ila alipotenda dhambi ya kukataa kufwata maelekezo ya Mungu; Mungu alimwacha na hakumjibu ama hakuzungumza naye kwa njia yoyote ile hata ile ya kinabii mara baada ya kifo cha Kuhani na Nabii Samweli.

Alikadhalika Yuda Iskariote, mara baada ya kumtenda Yesu, Matokeo yake yalikuwa ni mabaya na hii ilikuja baada ya kuachwa na Mungu.  Yuda alihitaji msaada ili kumzuilia kujinyonga, Kumbuka Mungu husema kuwa hapendi kuinona nafsi ya mwenye dhambi ikipotea.

Silengi tuu kuwasaidia wakina Yuda na Sauli bali hata wakina Petro, Petro alipata msaada wa karibu sana kutoka kwa Yesu na Roho Mtakatifu alimsaidia kwa haraka sana kwa ishara ya Kengele ya Jogoo kuwika. Na mimi ninaguswa na wakina Yuda ambao hawaijui ama huipuzia ishara ya jogoo kuwika.

Sauli mara baada ya kumuasi Mungu na mbele yake kulikuwa na mtihani mgumu sana wakupigana na wafilisti, kabla ya mtihani huo hakuona umuhimu sana wakutafuta msaada na kwa bahati mbaya sana alikuwa akitegemea nguvu za Nabii Samweli na hakujua dhamani na umuhimu wa kwenda mbele za Mungu.

Bali alijikuta akitafuta msaada kwa waganga wakienyeji, 1 Samweli 28:3-25,7Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwenye pepo wa utambuzi nipate kwenda kuuliza kwake.” Watumishi wake wakamwambia “Tazama, yuko mwanamke mwenye pepo wa utambuizi huko Endori.” 
Matokeo yake yalikuwa ni Sauli kupata adhabu ya kimungu hali iliyopelekea mauti yake na kwa watu wa nyumbani kwake huku Wafilisti wakijipiga kifua mbele ya taifa la Mungu wetu Iziraeli.

1Mambo ya Nyakati 10: 13 Basi Sauli alikufa kwa sababu ya kosa lake alilomkosa Bwana, kwa sababu ya neno la Bwana, asilolishika; na tena kwa kutaka shauri kwa mwenye pepo wa utambuzi, aulize kwake, 14 asiulize kwa Bwana; kwa hiyo akamua na ufalume akamgeuzia Daudi, mwana wa Yese.
Sio yeye tu bali na watu wa nyumbani mwake, 1Mambo ya Nyakati 10:6 Hivyo sauli akafa na wanaye watatu, na nyumba yake yote wakafa pamoja.

Kiu yangu hapo ilikuwa ni kuona madhara ya kutokutenda vyema punde Mungu anapokuacha kutokana na dhambi uliyoitenda, Kumbuka Sauli aliangukia Upanga, na Yuda alijinyonga. Hayo ni matokeo yakutokuamua vyema. Na nimekuandalia chakufanya ili usikumbwe na hayo.

Unapotenda dhambi hakikisha unaomba rehema kwa Mungu na wala usiruhusu kiburi kuinuka ndani yako kwa kukataa maonyo kwani hali hii ni hatari sana na kitabu cha Mithali kimeonya kiundani jambo hili la kukataa maonyo.
 Pili hakikisha hurudii kosa lilokufanya kukorofishana na Mungu.

Kama dhambi yako ama kosa lako limfikia lile la Sauli la kuachwa na Mungu kiasi ambacho hata maombi ya Rehema ya Samweli juu yako hayajibiwi, Hakkisha utafuta nalohiji Mungu juu yako nawe ulifanye na sio kumwinda Daudi kwani kufanya hivyo ni kuchochea hasira na gadhabu ya Mungu juu yako.

Sauli alipogundua kuwa Mungu amemwacha hakutafuta kuupendezesha uso wa Mungu badala yake aliaza kupanga mipango na kuitekeleza ile ya kumua Daudi. Cha kufanya kama Mungu ameshaurarua ufalume wako na kumpa jirani yako hakikisha unaukabithi kwa aliyepewa lli wewe uwe salama usijiuwe wala wakina Yonathani wasife na Mefiboshethi kuwa kilema.

Matokeo ya kuvaa miwani nyeusi kwa kujifanya haujali eti una kiburi ama kumuona Mungu kama ni mdogo wako na anapaswa kujinyenyekeza mbele yako ni mabaya sana. Kumbuka huwezi kujifanya wakiroho kuliko Sauli ama Yuda aliyeonana na Yesu ana kwa ana. Cha msingi ni wewe kujishusha na kupondeka kifudifudi mbele zake kama Petro. Luka 22:60-62, 62 Akatoka nje akalia kwa majonzi.
Nimewaona watu wengi walioanguka kwenye uzinzi na kujikuta wameacha wokovu kabisa na mwisho wao kuwa mbaya kabisa kiimani na hatimaye kufa kifo cha aibu.

Kulikuwa na Mtumishi mmoja wa Mungu natumai ni kule mkoani Morogoro, Mtumishi huyu aliifanya kazi ya Mungu katika viwango vikubwa sana, Alitumiwa katika ishara na miujiza ya hali ya juu. Ikafika kipindi akaanguka kiroho na hatimaye kuoa wanawake wa wili kisha mwanaye alijitaidi sana kumuombea.
Siku moja Mungu akamuotesha ndoto ya kuwa anaitafuta silingi iliyodumbukia kwenye tundu la shimo la choo. Ndoto iliyokuwa na tafsiri ya kwamba ache kumuombe baba yake kwani tayari amekwisha fikia kiwango cha kuachwa na Mungu, na hali hii ndiyo iliyokuwa kwa Samweli dhidi ya Sauli.
1Samweli 16:1 Bwana akamwambia Samweli, “Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asimiliki Iziraeli?..”

Mara bada ya ujumbe huo siku chache mbeleni mtu huyu aliyekuwa mtumishi alivamiwa na majambazi na kuuwawa. Tazama kifo chake! na kosa lake.
Tugeukiye taswira ya pili ambayo ni ya Mungu kukaa kimnya angali ujatenda dhambi bali upo kwenye pito fulani. Kumbuka kuwa hata kwa Ayubu Mungu alinyamaza na kuja kumjibu mwishoni kabisa.
Tafadhali ungana nami tena kesho ili kusoma sehemu ya pili ya makala hii…

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni