Jumatatu, 15 Mei 2017

USITISHWE NA MAZINGIRA, MUNGU AKISEMA AMINI TU.

Na Mwalimu Oscar Samba #UgMinistry
Kuna wakati ukitazama mazingira uliyonayo na kulinganisha na ahadi ya Mungu maishani mwako, unapata vitu tofauti ama visivyowezekana. Mungu alimuaidia Ibrahimu na Mkewe Sara kuwafanya taifa kubwa, cha ajabu aliwapa mtoto mmoja.  Kimazingira ilikuwa ngumu kwani tungalitarajia kupewa watoto wengi.

Isaya 51:2 Mwangaliye Ibrahimu, baba yenu, na Sara aliyewazaa; kwa maana alipokuwa mmoja tu nalimwita, nikambariki, nikamfanya kuwa wengi.
Mazingira haya yalikuwa hayasadifu ahadi hii ya Mungu ila Ibrahimu na mkewe waliishika kwa Imani iliyo kuu kwani licha ya kupewa mtoto mmoja pia walikuwa hawajapata mtoto huyo hadi kufikia uzeeni ambapo Ibrahimu alimpata Isaka akiwa ni mtu wa miaka mia na ushee, jambo hili halikuwa dogo kwake maana yeye na mkewe walicheka wakati ahadi hii inatokea kwa kudhibitishwa.


Mwanzo 17:17 Ndipo Ibrahimu akaanguka kifudufudi akacheka, akasema moyoni, “Je, mtu wa umri wa miaka mia, kwake atazaliwa mtoto? Naye Sara mwenye umri wa miaka tisini atazaa?”
Mwanzo 18:12 Kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake, akisema, “Niwapo mkongwe, nitapata furaha na, na bwana wangu mzee?”
Ukitazama mstari huu kwa Sara utadhania ya kwamba kicheko hicho ni cha furaha kwa kumpata mtoto uzeeni na furaha kuzaliwa hapo, ila mistarii inayofwata malaika wa Bwana anadhiriisha kuwa kicheko hicho kilikuwa ni cha kuonyesha shaka iliyotokana na mazingira ya umri wao ama uzee kusema haliwezekani ingawaje Mungu hatazami hayo mazingira kwani anasema inawezekana.

Mwanzo 18:13 Bwana akamwambia Ibrahimu, “Mbona Sara amecheka akisema, ‘Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee?’ 14 Kuna neno gani lilogumu la kumshinda Bwana? Kwa muhula wake nitarudia, wakati uu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume.”

Ni kweli na pasina shaka mazingira yalikuwa magumu kwa watu hawa wa Mungu, ila ahadi ya Mungu ilitimia na wao walijilazimisha kumuamini Mungu katika ugumu wa hayo mazingira na Imani ndicho kitu pekee kilichowawezesha kulitimiza hili Neno, ingawaje hali hii iliwapa ugumu.
Waebrahia 11:8-12, 11 Kwa imani hata Sara mwenyewe alipokea uwezo wa kuwa na mimba, alipokuwa amepita wakati wake; kwa kuwa alimhesabu yeye aliyeaidi kuwa mwaminifu.
Nataka ujifunze kitu hapo, katika mazingira haya magumu Ibrahimu na Sara mkewe walimwamini Mungu, na hapo tunamuona Sara akionyesha Imani ya utofauti inayomuhesabu Mungu kama au kuwa ni mwaminifu. “kwa kuwa alimhesabu yeye aliyeaidi kuwa mwaminifu” Licha mukutadha huo, pia linabainisha kuwa hata umri wake ulikuwa umepita, “alipokuwa amepita wakati wake” Na wewe haijalishi wakati wako wa kupata mtoto kibaolojia umepita, ama wakati wako wakuolewa ama kuoa ukiutazama ni kama vile umesonga, yamkini ulitarajia kuwa umesha jenga ama kusoma au kufikia ngazi fulani ya elimu na ukitazama mazingira ya fedha ni magumu na umri wako umesogea kwani uzee ama utu uzima unakaribi au majukumu kuongezeka.

Lisikiye Neno la Bwana linalotoka kwenye kinywa changu na kudhibitishwa na vidole vyangu vikuandikiavyo makala hii. “YASIOWEZEKANA KWA WANADAMU KWA MUNGU YANAWEZEKANA, JE, NI JAMBO GANI LA KUMSHINDA MUNGU?”
Jibu Iake, hakuna lolote lilo gumu kwa huyu Jemedari Yesu, bali wewe amini tu na uwe na imani iliyo kamilifu kama wakina Ibrahimu na Sara kwani mara baada ya Imani yao kilitokea hiki;
Waebrania 11:12 Na kwa ajili ya hayo kazaliwa mtu moja, naye alikuwa ni kama mfu, watu wengi kama nyota za mbinguni wingi wao ni kama mchanga ulio ufuoni, usioweza kuhesabika.
Mtu moja anayetajwa hapo ni Isaka, ambaye alimzaa Yakobo na Yakobo kuzaa watoto kumi na wawili, waliogeuka kuwa kabila kumi na mbili za Iziraeli ambazo ziliujaza ulimwengu kwa wingi wake kama nyota za angania ama wingi wa idadi ya mavumbi ya aridhi au mchanga wa baharini.

Mpendwa kwa imani watu hawa waliyafilia mema yao maishani, na wewe kwa imani utayafikilia yale ambayo Mungu amekuaidia, haijalishi leo unalala njaa, unashinda bila chakula na kuamkia vyakula vilivyo lala ama dhaifu. Tazama ahadi ya Bwana maishani mwako wala usitazame hapo ulipo hivi leo, macho yako ya ndani yaone mafanikio makubwa.

Yamkini leo wanakuita majina yaliyodharauliwa, “Kilaza, Kishoiya, Fukara, Ohehaye, Masikini wa kutupwa.”  Lakini wewe tazama majira watakayokuita, “Mbarikiwa,” Watakapo imba Hosana na kutandika kanga zao ama mashuka yao barabarani ili punda uliyempanda asikanyage mavumbi, hayo ndiyo majira ya kuyatazama kiimani.

(Daudi alidharauliwa kiasi cha kusaulika katika idadi ya watoto wa mzee Yese walioitajika kupakwa mafuta, na wakati ule anataka kumwendea Goliati kaka yake alimdaharu na kumwambia kuwa anajua kiburi chake, wakati kijana huyu alikuwa hana kosa. Ila Daudi hakutishwa na mazingira ya kunukiwa kinyesi cha kondoo na harufu ya mazizini wala kule kudharauliwa na nduguze ama kuonekana duni machoni pa familia ya mzeee Yese, Bali aliyatazama majira haya hapa:
 1 Samweli Nao wale wanawake wakaitikiana wakicheza, wakasema
“Sauli amewaua elufu zake,
na Daudi makumi elufu yake
Hakutazama majira ya nyimbo na miluzi ya kumkatisha tamaa bali ni majira ya wanawake waliopita na kuimba sifa zake njema ikiwa ni ishara ya kuinuliwa na Bwana. Na wewe tazama majira ya kuinuliwa na JEHOVA na achana na majira ya kupakwa kinyesi na wanadamu wenye mwili wasioshiriki hata kwa harufu kikao cha kuitwa kwako.)

Leo hii wakifanya vikao vya maamuzi hawakuiti, wala hawakukumbuki, usitazame huko wewe mtazame Yesu na yapo majira watakusanyika na kusema bila fulani yaani wewe hakuna kitakacho amulika hapa. Yusufu huyu huyu aliyekaa gerezani ndiye aliyekuja kufanyika msaada mkubwa kwa ndugu zake walio mdharau na kumchukia na taifa la wamisiri liliomtia gerezani.

Mwanzo, 37:8…Wakazidi kumchkia kwa sababu ya ndoto yake, na kwa maneno yake.  Ukiedelea utaoana jinsi walivyo muuza na hatimaye kutupwa gerezani.
Yamkini umechukiwa na ndugu zako, kiasi cha kutokukudhamini na hukunenea maneno ya hadaha na kejeli. Na kinachokumiza zaidi ni kwamba umejitaidi kuwatendea yaliyomema ila malipo yake yamegeuka kuwa kejeli na dharau na kutegwa. Wewe sio wa kwanza bali Yusufu na Yesu walipitia huko ila baadaye waliimba Hosana ni Mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana. Ndugu wa Yesu waliwai kumwambia kuwa maerukwa na akili.
Kwa Yusufu hali ilikuwa ngumu ila baadaye nduguze walisujudu kama andiko lilivyosema, na Farao kukiri ukuu wa Mungu ndani yake hadi kusema haya:

Mwanzo 41:Frao akawaambia watumwa wake, “Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake?” 39 Farao akamwambia Yusufu, “Kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote, hapana mwenye akili na hekima kama wewe. 40 Basi wewe utakuwa
juu ya nyumba yangu, kwa neno lako watu wangu watatawaliwa…”

Hayo ndiyo majira ambayo imani isiyotishwa na mazingira inatazama, Yamkini ni kweli ndoa yako imekufa, uchumi wako umekufa, afya yako imedhoofu, ukitazama ndoto zako zakuwa dakitari ama mwanasiasa au kiongozi fulani ni kama zimefifia kabisa.
Usikubali kutishwa na hayo mazingira, wewe mwamini Mungu kama Sara na mumewe. Ni kweli Lazaro amekufa na ananuka. Ila Yesu anasema ugonjwa huo sio wa mauti angali ni mgonjwa. Na sasa kafa, Yesu anasema kuwa Hajafa ila amelala.
Ni kiu yangu kuendelea na makala hii murwa ila kwa kweli kengele ya muda inalia, ila usikose kufwatilia makala mwenza hiyo kesho, itwayao, “LAZAZO HAJAFA, AMELAA NA WEWE AMINI TU” Kumbuka pia Yesu alisema kijana hajafa ila amelala watu wale wakamcheka. Na wewe hiyo ndoa yako yaijafa bali imelala na mkeo/mumeo atarejea wakati Yesu anatakaposema kijana “Tabitha”

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni