Jumanne, 23 Mei 2017

NYUMA YA MLIMA.

Na Mwalimu Oscar Samba #Ug Ministry 
Baraka zako ama majibu ya maombi  yapo nyuma ya mlima mpendwa kwa hiyo usichoke kuupanda huo mlima kwani ukiumaliza  utakutana na majibu yako.

Ninakuhakikishia ya kwamba PITO hilo ulilonalo ni kama mlima maishani mwako na uhakikisho ni huu; Ukilimaliza salama utakumbana na majibu ya maombi yako.

Wana wa Izirali waliizunguka milima ya Seiri siku za kutosha ila mara baada ya kumaliza kuizunguka nyuma yake walikutana na majibu yao yaliyolenga kuwapitisha salama na Mungu kufungua ukurasa wa kanuni za kuishi nchi ya ahadi sanjari na kuwawezesha kuifikia Kanani yao kwa wepesi zaidi.
kumbukumbu la Torati  2:1 “Ndiposa tukageuka, tukashika safari yetu kwenda jangwani kwa njia ya Bahari ya Shamu, kama alivyoniambia Bwana; tukawa tukiizunguka milima ya Seiri siku nyingi. 2Bwana akanena akaniambia                             3 Mlivyouzunguka mlima huu yatosha; geukeni upande wa kasikazini.


Usichoke kuupanda huo mlima bali endelea kukaza mwendo ndugu yangu kipenzi, Kuna mwimbaji mmoja wa nyimbo za Yesu aitwaye Jenifa Mgendi katika wimbo wake ameimba na kusema ya kwamba mbele yake kwa macho ya nyama anaona mlima ila kwa macho ya ndani anayaona majibu yake yakiwa nyuma ya mlima. Kwa hiyo anaupanda huo mlima ili ayapate hayo majibu.

Na wewe nakutaka kufanya hivyo kwa Imani na bidii iliyokuu, Usikubali mtu wa ndani ama wewe wandani kuona mlima ila wewe ona majibu nyuma ya mlima na mtu wa nje mtiye moyo kwa kumuonyesha dhamani ya majibu hayo ili asikate tamaa.

Wana  wa Iziraeli wengi walikata tamaa kwa sababu hawakuwa na taswira kama hii kwani mtu wa nje hakuona dhamani ya majibu yale bali alikuwa mwepesi wa kutazama ugumu wa mlima ule ikiwemo, kukosa maji, chakula, na wakati mwingne kukinai chakula na kujikuta wakikiita kidhaifu sanjari na umbali wa safari. Ila wachache kama wakina Yoshua na Kalebu walitazama sana nyuma ya mlima.

Rafiki yangu katika BWANA na Mpendwa mwenzangu, Usichoke kuuzunguka ama kuupanda mlima kwani Mungu yu karibu kukujibu kama ilivyokuwa kwa hao wana wa Waebrania alipojitokeza kwenye mstari ule wa tatu na kuwaambia, Mlivyouzunguka mlima huu yatosha; geukeni upande wa kasikazini.”
Na kwako Itakuwa hivyo karibuni. Wewe mtazame YESU aliyekuaidia Baraka tele. Usikubali kukwama hadi umsikiye BWANA akikwambia yakuwa “YATOSHA.” Na hakika akinena hivyo sikiliza maelekezo atakayokupa na yamkini yakawa ya kuchuma matunda yako ama kuelekea njia nyepesi na isiyo na mlima ya upande wa Kasikazini kama ilivyokuwa enzi zile za Musa pale Seiri.

Wakati huu ninapokuandikia makala hii Roho Mtakatifu ndani yangu anaimba wimbo huu.
Usichokee kuubeba Masalabaa,
Katika huoo Mujiza wako upoooo, X Rudia zaidi kuimba.

Ninakutakia majira yenye Fanaka na Mubashara katika safari hii ya kwenda mbinguni, Usikose makala ya Kesho itwayo, YATOSHA. Ni fika na bayana ya kwamba mapito yapo, mateso, dhiki na taabu, kulala njaa na kutengwa ama kukataliwa na ndugu au wapendwa.
Ila yapo majira ya mambo hayo kukoma, na ndiposa Yesu pale msalabani akasema IMEKWISHA, na Mungu akawaambia wana wa Iziraeli wakati wanazunguka ile milima ya Seiri; YATOSHA.  “Mlivyouzunguka mlima huu yatosha; geukeni upande wa kasikazini.” Na wewe imetosha sasa kuteseka…. Tafadhali ni kesho maana upako nilionao naweza maliza mboga jikoni kwa kukuonjesha.

Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundila Fb, ili kuupta habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni