Jumatano, 17 Mei 2017

MAREHEMU WALIOGEUKA JESHI KUBWA, (MIFUPA MIKAVU).

 Na Mwalimu Oscar Samba Ug Ministry
Nabii Ezekieli alionyeshwa bonge lilojaa mifupa ya wafu na aliitabiria mara mifupa ikageuka na kuwa maremu, kisha marehemu wakapata uhai kwa kufufuka. Na wewe leo hicho kilichokufa maishani mwako na kusaulika, kitafufuka kwa JINA LA YESU na kisha kuwa hai tena.

Kama ile maiti ilivyogusana na mifupa ya Nabii Elisha ndivyo itakavyokuwa kwako leo, kwa hicho kilicho kufa kugusana na YESU KRISTO MTENDA MIUJIZA. Aliyemfufua Lazaro, Binti wa mama yule mjane wa mji wa Naini, Kijana aliyekuwa amekufa na Yesu kusema amelala, kisha watu kumcheka. Ila punde si punde, maiti alifufuka. Yamkini na wewe unapowambia nitaolewa, wanakucheka sana, kwani umri umesonga, ama unapowaambia ya kwamba, utasoma, utajenga, utamiliki magari na hata majumba, hucheka sana. Wewe endelea kumuamini Yesu aliyemfufua huyu mfu sanjari na mifupa ile mikavu, ikawa mibichi, marehemu na kisha WALIO HAI.


Kumbuka kisa cha waliokuwa wanaenda kuzika kile cha Mifupa ya Elisha, watu hawa hawakuwa na tumaini la marehemu wao kufufuka ila kwa kuwa alikwepo Nabii wa Mungu aliyeupendeza uso wa Mungu, Mungu aliliheshimisha jina lake. Na kwa kuwa nipo Nabii, Mtume na Mwalimu wa Mungu mbele yako leo, Mungu lazima aliheshimishe jina lake. Wewe Muone Elisha wako na maiti ama marehemu wako ambaye yamkini ni Ndoa, Uchumi, ama mifupa hiyo ni Elimu au Afya, ITAPATA UHAI LEO. Sio UHAI tu, bali itakuwa JESHI, Naam sio JESHI tu, Bali ni JESHI KUBWA, litakalo pigana na adui zako wote.

Mimi nawe tuangaziye macho yetu kwenye maandiko haya ili kujirithisha na niyasemayo kwa kuanza na mujiza ule wa Bwana Mkubwa YESU,
Mathayo 9:24 akawaambia, “Ondokeni, kwa maana kijana hakufa, amelala tu.” Waka mcheka sana.
Ona hapo, walimcheka Yesu, tena sio kumcheka tu, bali sana. Sasa wewe una ona nini aibu kuchekwa unapo waambia nitaolewa, na wakiatama umri umeenda, nitasoma, wakiatzama, fedha hakuna, nitajenga, ndoa yangu itapata amani, na wakitazama hivi  leo ni kama maisha yap aka na panya?
Kama Yesu aliye Mungu alichekwa, itakuwaje kwako wewe? Tuendelee na ona kilichotendeka hku andiko hilo likianza na neno, “Lakini,” Amablo kisarufi linaamana ya ama dhima ya kuonyesha ukinyume ama utofauti na fkra fulani. Na hapa utofauti huo ni wa wale waliomcheka Yesu, ambapo kwako ni kwa hao wanaokusagia meno na kujaribu kukukwamisha kwa kukucheka.

25 Lakini makutano walipoondoshwa, akamshika mkono; yule kijana akasimama. (Ndugu yangu hapa ni kwamba, Marehemu kawa hai. Tazama kilichoendelea) 26 Zika enea habari hizi katika nchi ile yote. Nawe ziamini habari hizi ili mujiza wako uenee katika nchi yote wakisema, huyu si yule aliyekuwa omba, omba pale mtaani, mbna leo anamiliki HAMA. “Eti, Yule aliyepakata mapacha ni yule aliyekuwa maepitiliza umri wa kuolewa?” Huku na wewe ukiwafinya watoto kidogo kwa makusudi ili wasikie wakilia, alafu unawabembeleza kwa kuwainu inua na kuwaambia kwa sauti ya upole ila watakayoisikia, “Pole, pole wanagu, pole , nawapenda.” Wakijifanya hawakuoni unawapungia na kuwaambia, “Watoto jamani wanadeka hawa.” Ni ili Mungu wao atukuzwe na vinywa vyo vimgeukie Bwana kama laa aibu ya kushindwa iwafunike usoni huku wewe ukipeta katika YESU WANGU.

Kama Nabii wa Bwana ninakwmabia tena leo kwa mara nyingine ya Kwama, Yaliyoshdikana kwa madakitari Bingwa, wanajimu, wachawi na walozi kwa Yesu yote yanawezekana, Iwe ni UKIMWI,UKOMA, MALERIA SUGU, TAIFODI, KASWENDE, UPOFU, UKIZIWI, UBUBU, UPOFU, na hata EBOLA, KANSA ama Kukataiw ana ndugu YESU anaweza yote hayo.

Kama alivyofufua mifupa mikavu na hayo yaliyoshindik kwako na kwa kila hosipitali kwake yanawezekana. Tuangaziye kwa pamoja kisa hiki chenye kuinua IMANI sana. Kwa mwendo wa poe fungua nami kitabu kile cha Nabii Ezekieli.
Ezekieli 37:4 Akaniambia tena, “Toa unabii juu ya mifupa hii, uiambiae, Enyi mifupa mikavu, sikieni neno la Bwana. 5 Bwana Mungu aiambia mifupa hii amneno haya, Tazama, nitatia pumi ndani yenu, anyi mataishi. 6 Nami nitatia mishipa juu yenu, nami nitaleta nyama iwe juu yenu, na kuwafunika ngozi, na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana
Hayo ni maneno ya Mungu kwa Nabii Ezekieli, na mimi leo ninataka yawe maneno yako ili kitokee kama kilichotokea, tukione hapo mbeleni.
7Basi nikatoa unabii kama nilivyo amriwa; hata nilipokuwa nikitoa unabii, palikuwa na mshindo mkuu; na tazama, tetemeko la nchi, na ilemifupa ikasogeleana, mfupa kwa mfupa mwenziwe.  8 Nikatazama, kumbe! Kulikuwa na mshiapa juu yake, nyama ikatokea juu yake, ngozi ikaifunika juu yake, lakini haikuwamo pumzi ndani yake.
Huyu tarari ameshatoka kwenye hatua ya kuwa mifupa mikavu na kuitwa marehemu, sasa kinachohitajika ni pumzi ili awe hai yani afufuke. Na wewe hilo teso lako limesha fikia hatua hii, kwa mifupa kusogeleana, mishipa juu yake, nyama na hatimaye ngozi kuifunika. Na wale walikuwa awaambni waanza kuwa na imani ingawaje ni haba kwa kuona dalili za kutokewa na Mungu wako.

Kwa hiyo vuta pumzi, kidogo kwa kuhewa alafu chukua hatua ya kuongeza IMANI yako ili marehemu awe hai. Tuendelee;

9 Ndipo akaniambia, “Tabiri, utabiriye upepo, mwanadamau, ukauambiye upepo, Bwana Mungu asema hivi, Njoo kutoka pande za pepo nne, ee pumzi, ukawapuliziye hawa waliouawa, wapate kuishi” Nami ninayatabiria masha yako sasa, “KWA JINA LA YESU KILA KILICHOKUFA MAISHANI MWA HUYU MTU, KIPOKEE UHAI SASA, IWE NI NDOA, UCHUMI, ELIMU, AFYA, KIBALI KWA NDUGU AMA HUDUMA, UPAKO AU AMANI, KWA JILA LA YESU NATMA PUMZI YA UHAI,AMENI”
10  Basi nikatabiri kama alivyoniamuru; pumzi ikawaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno.

Sio kikosi, bali ni jeshi kubwa, sio kubwa tu, bali ni kubwa mno. Na walisimama kwa miguu yao wala sio ya jirani zao ama kwa msaada wa magongo bali ni yao. Naiwe kwa hivyo leo, kama mifupa mikavu/wafu walikwa marehemu na ksha kuwa hai, hakika kila kilichokufa kwako kinawezekana. Usiniambiye ama kuniuliza na hili Mtumishi linawezekanaje,? Mimi niachojua hakuna lisilowezekana kwa Mngu, kama Sara wa maika tisini na Ibrahimu wa maika mia waliapata mwana. Je, kwako itakuwaje? Waliokuwa viikongwe kupakata mwana. Huku mzee wa wa miaka tisini akienda Leba, Je kwako?
Tukutane kisho mpebdwa wangu katika safu hii ya makala, nan i hakika MANA niliyoiandaa kesho, iatakuacha ukiwa kinywa wazi kwa kutirika mate kama mtu alaye asali, kwani ni tamu nan i yenye Afya, ithili ya Alwaa ileya Zenji. Langu jina nililopewa na wazazi ni Oscar, na Mungu kunipa wito wa huduma ya Ualimu kwa hiyo wa weza niita Mwalimu Oscar aliyezaliwa kwene ukoo wa Samba mwana wa Flora katika familia teule ya Mzee Prospa, waliokoka.
Nawe kama hujaokoka fanya hima leo uokoke ili uwe na uwalali wakupokea huo mujiza huku ukiuutunza kama mwana wa Mungu, Kama upo tayari kuokoka sema nami maneno haya hapa.
BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KAUMINI KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapa.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba


Maoni 1 :

  1. ninaomba tafsiri ya neno la kwa msaada wa Mungu nafuatia jeshi

    JibuFuta