Jumatatu, 15 Mei 2017

KWA NINI UJINYONGE, KWA NINI UJIUWE, KWA NINI UKATE TAMAA? WAKATI YESU ANAWEZA.

 Na Mwalimu Oscar Samba #UgMinistry
Ipo nguvu ya ajabu ipatikanayo katika msalaba wa Yesu Kristo iwezayo kukupa majibu ya masumbuko unayoyahitaji. Na kama msaada upo basi haipaswi kukata tamaa ama kuendelea kufadhaika bali wewe uhitaji huu msaada ili uwe salama.

Kuna kisa kimoja kwenye Bibilia nacho ni cha Petro ambaye alitembea juu ya maji, ila punde mara baada ya kuanza tendo hili la Imani alianza kuzama. Petro hakunyamza, wala hakufikiria kuzijizamisha kama wengine hivi leo wanavyofikiria kujiua, kwa kujinyonga ama kunywa sumu. Bali rafiki yangu huyu alimuita Yesu. Na Yesu alimsaidia.


Kitu cha ajabu ambacho nimejifunza hapa kwa Petro ni hiki, Alikuwa akizama na Yesu alimuona, ila hakumsaidia hadi pale Petro alipohitaji msaada. Na wewe ni kweli unazama ama umechoka kiroho ama kimaisha na umefikia hatua yakutamani hata kuacha Wokovu ama kunywa sumu au kujinyonga na hata kujitupa gorofani kwa sababu ya ugumu wa maisha ama jambo fulani.

Ukikaa na hali hiyo ni hakika dhamira hiyo itatimia kama ilivyokuwa kwa Yuda aliyetembea na Yesu na kuwa mwanafunzi wake kisha kujinyonga. Nataka ujifunze nami hapa kwa Petro, alianza kuzama ila Yesu hakumsaidia hadi alipoita na kuomba msaada na wewe yamkini unajiuliza mbona unateseka hivyo na Mungu unaye, ama na Yesu unampenda au kumuamini?

Jibu ni kwamba bado hujahitaji msaada na ukihitaji Yeye ni mwaminifu atakujibu punde kama ilivyokuwa kwa Petro. Mathayo 14:25-33, 30 Lakini alipoona upepo, akaogopa, akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, “Bwana niokoe.” 31 Mara Yesu akanyoosha mkono wake, akamshika, akamwambia, “Ewe mwenye imani haba mbona uliona shaka?” 
Ni baada ya Perto kupiga YOWE kwa kuomba msaada na wewe piga YOWE mbele za Yesu leo kwa kufanya maombi ya kumuita ili akuokowe katika pito hilo ama teso hilo. Hata kama hujaokoka wewe piga YOWE Yesu hakuja kwa ajili ya waliokoka tu bali ni kwa kila mtu aliye wa uzao wa Ibrahimu ama uzao ule wa Ishmaeli na hata wa Esau na wale wengine wa mataifa. Wote ni wake kwani aliwafia wenye dhambi wala sio wenye haki. Walio wazima hawakuwa na haja na tabibu ndio maana wagonjwa ndio waendao hosipitalini na wazima ni wasindikizaji. Kwa hyo wewe ni mlengwa mkuu wa ujumbe huu.

Ukisha piga Yowe hakika upepo unaokuzamisha utakoma kama ilivyokuwa kwa Petro mara baada ya kushikwa mkono, na atapanda na wewe chomboni wala hutatembea tena juu ya hayo maji yaliyokuzamisha. Tuendelee na msatari unaofwata.

Mathayo 14:32 Na walipopanda chomboni upepo ulikoma.
Siku moja niliota ndoto iliyonishangaza sana, siku hiyo sio mbali sana bali ni wiki kama mbili zilizopita. Niliota nikiwa na malaika aliyekuwa na umbo kama la kibinadamu. Alikuwa akinipitisha msituni na pembezoni kwenye majabli makubwa, kuna mahali alikuwa akinifikisha. Ila aliniacha nyuma mita kadhaa huku akigeuka kila mara ili kuniangalia nilipo fika.

Ilifika wakati nikashindwa kuvumilia kuachwa nyuma na kumuita huku nikimfahamisha kwamba nashindwa kutembea sambamba naye kutokana na mguu wangu wa kushoto kuwa na jeraha kwenye unyayo. Alikuja kwa haraka na kunitoa kijiti kirefu kilichokuwa kimenichoma na  pia alitoa kipande cha jani la aina ya “Isaale” (Ni mmea unaopatika na sana kanda ya kasikarini hususani Maeneo ya Uchagani na Arusha).
Nilishangaa sana, kilicho nishangaza ni; Ni kwamba nilitembea naye kwa muda mrefu na huku nikichechemea ama nikishindwa kutembea sawa ila hakunisaidia hadi pale nilipohitaji msaada. Jambo hili lilinipa kujiuliza na kuhitaji kupata ufumbuzi wa kina kuhusu kanuni hii.

Ndiposa nilipokumbuka lile andiko lisemalo ya kwamba, “Aliwaponya wale waliokuwa na haja ya kuponywa” Andiko hilo lipo kwenye kitabu cha Luka. Ni kweli Yesu alikutana na watu wengi wenye uhitaji ama wenye matatizo ila hakumponya kila mtu bali ni yule aliyeonyesha kuhitaji msaada wake. Hakika kipofu Baltomayo angeomba fedha angepewa fedha ila aliomba uponyaji na kupewa uponyaji.

Tazama kisa hiki, Kulikwepo na mama mmoja aliyetokwa na damu kwa muda wa miaka 12, ila siku moja aliamua kushika pindo la Yesu ndipo alipopokea mujiza wake. Ni kweli kwamba Yesu toka juu mbinguni aliona teso la mama huyu tangu mwaka na siku ya kwanza na hata kabla halijamkumba ila aliachilia uponyaji pundea mara baada ya mtu huyu kuhitaji msaada kutoka kwake.

Alipoenda kwa wagaga Yesu alikaa kimwia, alipowaendea matabibu alijifanya kama vile amuoni ila alipoamua kushika upindo wa vazi lake mara Yesu alishindwa kujizuia na cha ajabu  hata Yesu hakujua kuwa nguvu zimemtoka na Yesu anakuja kugundua kuwa kuna mtu amepona baada ya mtu kuponywa na nguvu zake.

Ona kitu hapo, Kumbe Nguvu za majibu zilizopo kwa Yesu huweza kufanya kazi bila hata Yesu mwenyewe kuziamuru  kujua kama utafwata kanuni.

Katika uzuri huu kweli ipo haja ya wewe kuendelea kufikiria kujinyonga? Kujiua? Ama kuwaza kujitupa baharini ama juu ya Ghorofa ili ufe?

Hapa, Mshike Yesu, mwite kwa YOE kama Petro, Naye atakujibu tena wala sio kesho bali ni leo. Hata kama hujui kuomba wewe, Sema tu, “YESU, NIOKOWE, YESU NINAKUHITAJI”
Maneno hayo kama yameambatana na imani kama kwa Petro aliyetamka maneno mawili na Yesu kumsaidia, (Bwana, niokoe), itakuwa hivyo kwako leo.
Kama hujaokoka, na unamuhitaji huyu YESU ili akusaidiye, ama ulirudi nyuma kiroho kwa sababu kadhaa, tamka sala hii ya toba kwa imani na utakuwa umeunganishwa na nguvu za Yesu Kristo. Sema.

“Bwana Yesu, NIMEKUJA KWAKO, MIMI NI MWENYE DHAMBI, NINAKUAMINI, NINAKUPENDA NA KUKUPOKEA MOYONI MWANGU LEO. TAFADHALI FANYIKA BWANA NA MWOKOZI WANGU. AMENI”

Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa lolote la kiroho ama la watu waliokoka ukasali hapo. Na umtafute Mchungaji umuelezee kilichotokea ili awe karibu na wewe kiroho zaidi. Ameni.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple #MwalimuOscarSamba


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni